KERO Mwanza: Soko la Buhongwa, upande ni Soko, upande ni Dampo ndani ya fensi moja. RC Said Mtanda na Waziri Mchengerwa ingilia kati

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

hijacker

New Member
Jan 25, 2018
2
2
Viongozi wa Serikali Mkoa wa Mwanza ebu angalieni Afya na utu wa wananchi wenu. Hivi kweli Wilaya ya Nyamagana tena Jiji kabisa mmekosa sehemu nzuri ya kuwaweka wafanyabiashara wadogo wadogo na machinga wa Buhongwa, hadi mkaamua kuwapeleka kwenye dampo la kumwaga uchafu na taka mlilojenga Buhongwa ??

Hili jambo linashangaza sana kuona binadamu wenzenu wanatafuta riziki yao kwenye eneo ambalo upande mmoja panamwagwa taka taka na kipande kingine ndani ya fensi moja ni shughuli za biashara!!.

Viongozi, ebu angalieni hata hayo mabanda ya hao wafanyabiashara ambayo wamejengwa bila usimamizi na mpangilio, mabanda yanachafua pia taswira ya jiji kwani yamejengwa kwa bati chakavu na kuezekwa kwa magunia! Hivi kweli tunasubili majanga ya moto yatokee ndio tuchukue hatua ?

Kwa kuwa mbunge Stanslausi Mabula wa jimbo la Nyamagana ameshindwa kuwasemea na kuwatetea wananchi wake na Halmashauri ya Jiji la Nyamagana Meya na Mkurugenzi wapo kimya, basi tunaomba Mkuu wa Mkoa Said Mtanda na Waziri TAMISEMI muingilie kati suala hili kwani halijakaa vizuri kabisa na madhara yake ni makubwa mno.

Mamlaka ebu amueni kati ya dampo na soko ni kipi kitoke na kingine kibaki, na kama litabaki soko basi watengenezee wafanyabiashara hao Mazingira mazuri ya biashara ili Serikali pia iweze kuingiza mapato na wao waweze kunufaika na biashara zao wanazofanya.
 
Hivi kumbe dampo halikuondolewa pale baada ya Soko kuhamia ? Pananuka sana watu wanawezaje kushinda hapo siku nzima miezi na miezi wakifanya biashara ? Duuh wapiga kura wa CCM tuna kazi kweli kweli
 
Viongozi wa Serikali Mkoa wa Mwanza ebu angalieni Afya na utu wa wananchi wenu. Hivi kweli Wilaya ya Nyamagana tena Jiji kabisa mmekosa sehemu nzuri ya kuwaweka wafanyabiashara wadogo wadogo na machinga wa Buhongwa, hadi mkaamua kuwapeleka kwenye dampo la kumwaga uchafu na taka mlilojenga Buhongwa ??

Hili jambo linashangaza sana kuona binadamu wenzenu wanatafuta riziki yao kwenye eneo ambalo upande mmoja panamwagwa taka taka na kipande kingine ndani ya fensi moja ni shughuli za biashara!!.

Viongozi, ebu angalieni hata hayo mabanda ya hao wafanyabiashara ambayo wamejengwa bila usimamizi na mpangilio, mabanda yanachafua pia taswira ya jiji kwani yamejengwa kwa bati chakavu na kuezekwa kwa magunia! Hivi kweli tunasubili majanga ya moto yatokee ndio tuchukue hatua ?

Kwa kuwa mbunge Stanslausi Mabula wa jimbo la Nyamagana ameshindwa kuwasemea na kuwatetea wananchi wake na Halmashauri ya Jiji la Nyamagana Meya na Mkurugenzi wapo kimya, basi tunaomba Mkuu wa Mkoa Said Mtanda na Waziri TAMISEMI muingilie kati suala hili kwani halijakaa vizuri kabisa na madhara yake ni makubwa mno.

Mamlaka ebu amueni kati ya dampo na soko ni kipi kitoke na kingine kibaki, na kama litabaki soko basi watengenezee wafanyabiashara hao Mazingira mazuri ya biashara ili Serikali pia iweze kuingiza mapato na wao waweze kunufaika na biashara zao wanazofanya.
Picha au video tafadhali
 
Huyo mjenzi alipatia sana kusevu eneo na kuweka ubunifu huo wa dampo na soko kutochukua nafasi kubwa.
HEKO KWAKE

MIKOA MINGINE IGENI UBUNIFU HUU
 
Back
Top Bottom