Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,801
- 11,961
Katika muendelezo wa Rais Samia kukutana na kuongea na Makundi mbalimbali nchini, leo ataongea na Vijana wa Tanzania kupitia vijana wa mkoa wa Mwanza katika Uwanja wa Michezo wa Nyamagana.
Taarifa zaidi zinafuata:
Mkuu wa mkoa wa Mwanza ameanza kwa kuwatambulisha watu mbalimbali kwa makundi yao mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan. Uwanja wa Nyamagana ukiwa umefurika vijana wengi sana kutoka sehemu Mbalimali Jijini Mwanza na mikoa ya Jirani. Salamu kutoka kwa wakuu wa mikoa mbalimbali zinaendelea.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassani akabidhiwa zawadi ya Ng'ombe dume na jike. Zawadi hiyo imetolewa na vijana wa mkoa wa Mwanza ikiwa ni shukrani kwake kwa kuendelea kusikiliza mahitaji ya vijana na kuyafanyia kazi.
Hasrat Hanje apendekeza Rais aanzishe baraza la vijana ambalo litakalounganisha vijana wote ili kuwasememea vijana changamoto zao, vijana hao ni kama mama lishe, bodaboda, watu wa migodi, wanafunzi nk.
Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan, akizungumza na vijana Mwanza
Kusema kweli sikutaraji Umma mkubwa kiasi hiki kusema kweli hii inaonyesha mnajali serikali yenu, kwakweli mmetia fora vijana.
Vijana na watanzania mnaonisikiliza Vijana ni ni kundi muhimu katika Taifa lolote hiyo inatokana na takwimu kuwa vijana ni kundi kubwa kitakwimu, angalau katika nchi zetu za kiafrika ila kwa wale waliozuiliwa kupata watoto wao wana tatizo la vijana ila kwetu vijana ni kundi kubwa.
Na kwa hapa Kwetu Tanzania kwa mujibu wa sensa ya ya watu na makazi 2012 kila kundi la watu 10 basi 4 vijana ni watu wenye umri miaka 15 hadi 35 lakini hii ni tafsiri ya kisera na sheria ya vijana lakini tukihesabiana vijana hapa wanakwend ampaka miaka 40, 50 bado ni vijana, hivyo hii inafanya vijana wawe kundi kubwa.
Lakini kwa tawimu za sasa nchi yetu inakadiriwa kuwana vijana milioni 20 na laki saba, karibu milioni 21. Ukiachilia mbali na takwimu hizo vijana ndio wenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi na ndio maana wanaitwa nguvu kazi ya Taifa.
Ni walinzi wa Taifa ni watu wenye ubunifu watu wenye uthubutu ni wajasiri na ndio waliobeba maono na na matarajio ya Taifa kwa sasa na siku zijazo. Kwa maneno mengine uhai, maendeleo na ustawi wa taifa unategemea vijana hakuna taifa lisilotegemea uwepo wa vijana katika ukuaji wake.
Lakini kundi hili linakabiliwa na changamoto nyingi kama mlivyozisikia hapa nami nazitaja na hatua tulizochukua ,
Mfano, Hivi karibuni tumetoa ajira za walimu nafasi elfu sita mia sita na sitini naaa..lakini maombi ni zaidi ya vijana elfu ishirini wameomba nafasi hizo vilevile tumetangaza ajira kutoka kada ya afya vijana wengi sana wamejitokeza kuomba ajira hizo watachukuliwa lakini ni uhakika wengine watabaki na ajira katika sekta za umma huendana na ukuaji wa kiuchumi ili kuwa uwezo wa kulipa mishahara.
Lakini kwa upande mwingine serikali hutekeleza miradi mikubwa ya kitaifa ili iweze kutoa ajira za moja kwa moja na isiyo ya moja kwa moja miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati inayotoa ajira ni kama hiyo ya ujenzi wa reli bwawa la kufua umeme, barabara miradi ya madaraja ambayo iko nchi nzima yanapishana tu kwa ukubwa lakini yote hiyo hutoa ajira na hii ni baadhi tu ya miradi ambayo serikali inafanya.
Hivi karibuni tutaanza kutekeleza bomba la mafuta kutoka Hoima Uganda kuja Tanga na mradi huu kwa sehemu kubwa upo ndani ya Tanzania na hapo vijana wengi watapata ajira, Tanzania yote ina fursa za ajira kupitia miradi ya aina hii.
Pia Tanzania kuna fursa ya ajira kupitia sekta binafsi hapa serikali hujenga mazingira ili wenye mitaji waweze kuwekeza katika viwanda na kufungua biashara mbalimbali ili waweze kuwekeza na kutoa ajira kwa vijana.
Pia tutofautisha kati ya ajira na kazi, hapa ni pale kijana hajaajiriwa ila kuna sehemu anafanya shughuli zake ili kuweza kujipatia kipato chake hili ni eneo ambalo serikali hujenga mazingira kwa vijana kujiajiri wenyewe mmoja mmoja au katika makundi yao.
Serikali katika kutengeneza mazingira ya kukuza ajira katika sekta binafsi na kuwezesh awananchi kujiajiri imefanya mambo kadhaa ikiwemo kufuta tozo kwenye kilimo, mifugo na uvuvi. Pia imerahisisha upatikani wa leseni ili vijana waombe leseni za biashara kupitia mitandao pia tumefuta tozo au kodi kero za osha, zimamoto na na kodi za aina hiyo ili kuwapa vijana fursa za kuweza kujiajiri
Kwenye madini tumefuta tozo na kodi mbalimbali na kutenga maoneo mbalimbali ya wachimbaji wadogo yenye ukubwa wa hekta Thelathini na nane elfu mia tano na sitini na saba. Maeneo mengine ambayo tumeboresha mazingira ili kuweka mazingira ya vijana kujiajiri ni katika sekta ya utalii ambapo tumeongeza mbuga tano mpya za kitaifa na kununua ndge 11 na kupunguza ada ya leseni ya kusafirisha watalii kwa wakala mwenye magari chini ya manne kutoka dola za kimarekani 2000 hadi dola 500.
Kwenye tehama serikali imejenga data center yaani kituo cha taarifa Dar ili kuwekeza kwenye mambo ya kidijitali, hii ni fursa kwa watanzania kuwekeza kwenye mambo ya mtandao. Pia serikali imewekeza kwenye kuzalisha umeme na watu watumie umeme kwenye kukuza uchumi.
Sanaa na Utamaduni ni eneo lingine la Ajira, kama mnavyofahamu hivi karibuni sanaa imekuwa ikitoa ajira kwa vijana katina muziki, filamu na michezo na wasanii wataanza kulipwa miongoni mwa hatua tulizochukua ili sekta hii iendelee kukuza ajira ni kusimamia haki miliki ya wasanii. Na napenda kuwaarifu wasanii kuwa kuwa mwaka huu Desemba 2021 wasanii wataanza kulipwa mirahaba ya kazi zao zinapotumiwa na redio, televisheni na mitandao.
Na katika Michezo tumeanzisha mfuko wa maendeleo ya michezo ili kuvisaidia au kuziandaa timu zetu za taifa na pia kama mlivyosikia kwenye bajeti ijayo tumefuta kodi ya nyasi bandia ili viwanja viweze kuwekwa nyasi bandia. Na pia niseme na chama changu cha mapinduzi viwanja vingi vinamilikiwa na chama cha mapinduzi ila hali yake hairidhishi, tafute program ya kuviboresha viwanja hivyo na kama hamna uwezo tafuteni namna na pia kila anaye tumia viwanja hivyo alaipe pesa inayostahili.
Kuhusu ujuzi tumeanzisha vyuo mbalimbali vyaufundi na umahiri ili vijana waweze kupata ujuzi. Kuanzishwa kwa vyuo vya umahiri ikiwemo na chuo cha teknolojia Dar, chuo cha umahiri Mwanza kitabobea kwenye ngozi na chuo Cha Arusha kitaboboa kwenye mambo ya anga. Pia kwenye mabo ya sanaa na michezo chuo cha Bagamoyo kitapewa hadhi stahiki. Pia waziri wa michezo waanze kufikiria kujenga academy za michezo mikoni.
Kutenga maeneo ya kuweka wajasiriamali wadogowadogo ili wajasiriamali waende wakafanye biashara zao kule bila kubughudhiwa.
Niliona Morogoro watu wametengewa maeneo mbali wakafanyie biashara zao na kwa sababu hawauzi wakarudi maeneo ya awali na baada ya hapo miga,mbo wakawapiga kuwafukuza na kuharibu bidhaa zao. Niseme tu kuwa tukio lile lilinisikitisha na kuniudhi sana na niseme tu kuwa mkurugrnzi na mkuu wa wilaya ya eneo lile hawana kazi kwakuwa kulikuwa na njia nyingine ya kufanya na sio vile.
Vitambulisho vya ujasiliamali vinatakiwa kufanyiwa marekebosho, ili viwe na taarifa ya mjasiriamali na aweze kufanya kazi zake bila bughudha. Pia mnatumika vibaya na wenye maduka kwa kupewa bidhaa na wenye maduka ili muwauzie na wao kukwepa kodi hivyo mnaturudisha nyumba kwenye kufanya maendeleo, sitarajii tena mtumike vibaya. Lakini hatutarajii muendelee kuwa wajasiriamali wadogo tunataka kuweka mpango wa kuwatambua na mkue kutoa wadogo wa kati na wakubwa.
Vijana tunaomba mjitambue kuwa nyiyi vijana ndio wenye maoni ya taifa hili kwa sasa na vijana na karibu wateuliwa wote ni vijana na kuna mkeka wa maDC utakaotoka hivi karibuni nataka kuwaambia kuwa wote ni vijana lakini vijana baadhi mnapopata fursa hizi mnatuangusha napenda kuwaambia kuwa mkipata fursa hizi mkafanye kama ilivyotarajiwa.
Vijana waliopata nafasi wajiulize je wana ufanisi wa kutosha, wana uzalendo wa kutosha na mambo kama hayo nakumbuka hayati Magufuli alisema kuwa hawa vijana wa 80 wananiendesha sana na zile tumbua tumbua zote ni vijana wa 80 ila bado kuna vijana wa 80 wanafanya vizuri. Nakumbushwa kuwa kunamkeka wa wakurugenzi bado haujatoka.
Kama vijana mnakutana wapi kuweka ajenda za taifa bila kujali itikadi ? Muweze kuongea bila itikadi zenu na hii inanikumbusha jambo alilosema bintiyangu juu ya jukwaa la vijana. Na hii tutakwenda kuwaandalia jukwaa la vijana tutajadili kwa nini halikuanzishwa shida nini na nk likianzishwa muweke ajenda za kitaifa.
Rais Samia Suluhu Hassan amesema "Vijana mnatumia Mitandao vibaya, kama una mawazo toa mapendekezo sio kulaumu, kushutumu haina faida. Tumieni Mitandao vizuri”
Ameongeza "Kama una jambo la kulaumu, laumu na toa ushauri, kama unakosoa kosoa na toa mapendekezo nini kifanyike. Amewataka Vijana kushirikiana, akisema wakati mwingine malengo hayafikiwi kwasababu kila mmoja kazi anafanya peke yake.
Asema ushirikiano ukiwepo itakuwa rahisi hata kwa Serikali kuwasaidia na kuwawezesha
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewataka Vijana kushirikiana, akisema wakati mwingine malengo hayafikiwi kwasababu kila mmoja kazi anafanya peke yake.
Asema ushirikiano ukiwepo itakuwa rahisi hata kwa Serikali kuwasaidia na kuwawezesha, amewataka Vijana kushirikiana, akisema wakati mwingine malengo hayafikiwi kwasababu kila mmoja kazi anafanya peke yake. Asema ushirikiano ukiwepo itakuwa rahisi hata kwa Serikali kuwasaidia na kuwawezesha.
======
Uzinduzi wa Chelezo( meli mbili zilizokarabatiwa) na uwekaji saini wa mikataba mitano ya ujenzi meli
Lakini nduguzangu leo tena tumeshuhudia uwekaji wa kuweka saini mikata ya kujenga meli tano na moja itakwenda kufanya kazi bahari ya hindi na hii ni kuendelea kuenzi kazi za Hayati Magufuli na dhamira yeti ni kuendelea kuifanya Mwanza kuwa kituo kikubwa cha biashara kati ya nchi za maziwa makuu.
Na ndio maana tunajitahidi kujenga bandari , meli, reli, barabara na pia kujenga kiwanja kikubwa cha ndege, Mwazna Mungu ameiweka sehemu nzuri na inazalisha mazao ya kibiashara kama pamba pia chakula mazao ya ziwani hivyo ndio maana serikali ina dhamira na Mwanza.
Serikali kuiwezesha Mwanza kimtandao ili biashara ziweze kufanyanyika kimtandao na wataokaokuja kukaa Mwanza waweze kuja kufanya biashara kimtandao.
Nishukuru sana wafanyakazi wa bandari na wafanyakazi wa meli na makontrakta na wale wote tuliowekekeana sahihi nasi kama serikali tutaisimamia vyema miradi. Na pia meli hizi zitunzwe na wote wanaohusika ili ziweze kukuza uchumi wetu.
Taarifa zaidi zinafuata:
Mkuu wa mkoa wa Mwanza ameanza kwa kuwatambulisha watu mbalimbali kwa makundi yao mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan. Uwanja wa Nyamagana ukiwa umefurika vijana wengi sana kutoka sehemu Mbalimali Jijini Mwanza na mikoa ya Jirani. Salamu kutoka kwa wakuu wa mikoa mbalimbali zinaendelea.
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassani akabidhiwa zawadi ya Ng'ombe dume na jike. Zawadi hiyo imetolewa na vijana wa mkoa wa Mwanza ikiwa ni shukrani kwake kwa kuendelea kusikiliza mahitaji ya vijana na kuyafanyia kazi.
Hasrat Hanje apendekeza Rais aanzishe baraza la vijana ambalo litakalounganisha vijana wote ili kuwasememea vijana changamoto zao, vijana hao ni kama mama lishe, bodaboda, watu wa migodi, wanafunzi nk.
Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan, akizungumza na vijana Mwanza
Kusema kweli sikutaraji Umma mkubwa kiasi hiki kusema kweli hii inaonyesha mnajali serikali yenu, kwakweli mmetia fora vijana.
Vijana na watanzania mnaonisikiliza Vijana ni ni kundi muhimu katika Taifa lolote hiyo inatokana na takwimu kuwa vijana ni kundi kubwa kitakwimu, angalau katika nchi zetu za kiafrika ila kwa wale waliozuiliwa kupata watoto wao wana tatizo la vijana ila kwetu vijana ni kundi kubwa.
Na kwa hapa Kwetu Tanzania kwa mujibu wa sensa ya ya watu na makazi 2012 kila kundi la watu 10 basi 4 vijana ni watu wenye umri miaka 15 hadi 35 lakini hii ni tafsiri ya kisera na sheria ya vijana lakini tukihesabiana vijana hapa wanakwend ampaka miaka 40, 50 bado ni vijana, hivyo hii inafanya vijana wawe kundi kubwa.
Lakini kwa tawimu za sasa nchi yetu inakadiriwa kuwana vijana milioni 20 na laki saba, karibu milioni 21. Ukiachilia mbali na takwimu hizo vijana ndio wenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi na ndio maana wanaitwa nguvu kazi ya Taifa.
Ni walinzi wa Taifa ni watu wenye ubunifu watu wenye uthubutu ni wajasiri na ndio waliobeba maono na na matarajio ya Taifa kwa sasa na siku zijazo. Kwa maneno mengine uhai, maendeleo na ustawi wa taifa unategemea vijana hakuna taifa lisilotegemea uwepo wa vijana katika ukuaji wake.
Lakini kundi hili linakabiliwa na changamoto nyingi kama mlivyozisikia hapa nami nazitaja na hatua tulizochukua ,
- Tatizo la Ajira
Mfano, Hivi karibuni tumetoa ajira za walimu nafasi elfu sita mia sita na sitini naaa..lakini maombi ni zaidi ya vijana elfu ishirini wameomba nafasi hizo vilevile tumetangaza ajira kutoka kada ya afya vijana wengi sana wamejitokeza kuomba ajira hizo watachukuliwa lakini ni uhakika wengine watabaki na ajira katika sekta za umma huendana na ukuaji wa kiuchumi ili kuwa uwezo wa kulipa mishahara.
Lakini kwa upande mwingine serikali hutekeleza miradi mikubwa ya kitaifa ili iweze kutoa ajira za moja kwa moja na isiyo ya moja kwa moja miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati inayotoa ajira ni kama hiyo ya ujenzi wa reli bwawa la kufua umeme, barabara miradi ya madaraja ambayo iko nchi nzima yanapishana tu kwa ukubwa lakini yote hiyo hutoa ajira na hii ni baadhi tu ya miradi ambayo serikali inafanya.
Hivi karibuni tutaanza kutekeleza bomba la mafuta kutoka Hoima Uganda kuja Tanga na mradi huu kwa sehemu kubwa upo ndani ya Tanzania na hapo vijana wengi watapata ajira, Tanzania yote ina fursa za ajira kupitia miradi ya aina hii.
Pia Tanzania kuna fursa ya ajira kupitia sekta binafsi hapa serikali hujenga mazingira ili wenye mitaji waweze kuwekeza katika viwanda na kufungua biashara mbalimbali ili waweze kuwekeza na kutoa ajira kwa vijana.
Pia tutofautisha kati ya ajira na kazi, hapa ni pale kijana hajaajiriwa ila kuna sehemu anafanya shughuli zake ili kuweza kujipatia kipato chake hili ni eneo ambalo serikali hujenga mazingira kwa vijana kujiajiri wenyewe mmoja mmoja au katika makundi yao.
Serikali katika kutengeneza mazingira ya kukuza ajira katika sekta binafsi na kuwezesh awananchi kujiajiri imefanya mambo kadhaa ikiwemo kufuta tozo kwenye kilimo, mifugo na uvuvi. Pia imerahisisha upatikani wa leseni ili vijana waombe leseni za biashara kupitia mitandao pia tumefuta tozo au kodi kero za osha, zimamoto na na kodi za aina hiyo ili kuwapa vijana fursa za kuweza kujiajiri
Kwenye madini tumefuta tozo na kodi mbalimbali na kutenga maoneo mbalimbali ya wachimbaji wadogo yenye ukubwa wa hekta Thelathini na nane elfu mia tano na sitini na saba. Maeneo mengine ambayo tumeboresha mazingira ili kuweka mazingira ya vijana kujiajiri ni katika sekta ya utalii ambapo tumeongeza mbuga tano mpya za kitaifa na kununua ndge 11 na kupunguza ada ya leseni ya kusafirisha watalii kwa wakala mwenye magari chini ya manne kutoka dola za kimarekani 2000 hadi dola 500.
Kwenye tehama serikali imejenga data center yaani kituo cha taarifa Dar ili kuwekeza kwenye mambo ya kidijitali, hii ni fursa kwa watanzania kuwekeza kwenye mambo ya mtandao. Pia serikali imewekeza kwenye kuzalisha umeme na watu watumie umeme kwenye kukuza uchumi.
Sanaa na Utamaduni ni eneo lingine la Ajira, kama mnavyofahamu hivi karibuni sanaa imekuwa ikitoa ajira kwa vijana katina muziki, filamu na michezo na wasanii wataanza kulipwa miongoni mwa hatua tulizochukua ili sekta hii iendelee kukuza ajira ni kusimamia haki miliki ya wasanii. Na napenda kuwaarifu wasanii kuwa kuwa mwaka huu Desemba 2021 wasanii wataanza kulipwa mirahaba ya kazi zao zinapotumiwa na redio, televisheni na mitandao.
Na katika Michezo tumeanzisha mfuko wa maendeleo ya michezo ili kuvisaidia au kuziandaa timu zetu za taifa na pia kama mlivyosikia kwenye bajeti ijayo tumefuta kodi ya nyasi bandia ili viwanja viweze kuwekwa nyasi bandia. Na pia niseme na chama changu cha mapinduzi viwanja vingi vinamilikiwa na chama cha mapinduzi ila hali yake hairidhishi, tafute program ya kuviboresha viwanja hivyo na kama hamna uwezo tafuteni namna na pia kila anaye tumia viwanja hivyo alaipe pesa inayostahili.
- Elimu na ukosefu wa ujuzi
Kuhusu ujuzi tumeanzisha vyuo mbalimbali vyaufundi na umahiri ili vijana waweze kupata ujuzi. Kuanzishwa kwa vyuo vya umahiri ikiwemo na chuo cha teknolojia Dar, chuo cha umahiri Mwanza kitabobea kwenye ngozi na chuo Cha Arusha kitaboboa kwenye mambo ya anga. Pia kwenye mabo ya sanaa na michezo chuo cha Bagamoyo kitapewa hadhi stahiki. Pia waziri wa michezo waanze kufikiria kujenga academy za michezo mikoni.
- Ukosefu wa mitaji
Kutenga maeneo ya kuweka wajasiriamali wadogowadogo ili wajasiriamali waende wakafanye biashara zao kule bila kubughudhiwa.
Niliona Morogoro watu wametengewa maeneo mbali wakafanyie biashara zao na kwa sababu hawauzi wakarudi maeneo ya awali na baada ya hapo miga,mbo wakawapiga kuwafukuza na kuharibu bidhaa zao. Niseme tu kuwa tukio lile lilinisikitisha na kuniudhi sana na niseme tu kuwa mkurugrnzi na mkuu wa wilaya ya eneo lile hawana kazi kwakuwa kulikuwa na njia nyingine ya kufanya na sio vile.
Vitambulisho vya ujasiliamali vinatakiwa kufanyiwa marekebosho, ili viwe na taarifa ya mjasiriamali na aweze kufanya kazi zake bila bughudha. Pia mnatumika vibaya na wenye maduka kwa kupewa bidhaa na wenye maduka ili muwauzie na wao kukwepa kodi hivyo mnaturudisha nyumba kwenye kufanya maendeleo, sitarajii tena mtumike vibaya. Lakini hatutarajii muendelee kuwa wajasiriamali wadogo tunataka kuweka mpango wa kuwatambua na mkue kutoa wadogo wa kati na wakubwa.
Vijana tunaomba mjitambue kuwa nyiyi vijana ndio wenye maoni ya taifa hili kwa sasa na vijana na karibu wateuliwa wote ni vijana na kuna mkeka wa maDC utakaotoka hivi karibuni nataka kuwaambia kuwa wote ni vijana lakini vijana baadhi mnapopata fursa hizi mnatuangusha napenda kuwaambia kuwa mkipata fursa hizi mkafanye kama ilivyotarajiwa.
Vijana waliopata nafasi wajiulize je wana ufanisi wa kutosha, wana uzalendo wa kutosha na mambo kama hayo nakumbuka hayati Magufuli alisema kuwa hawa vijana wa 80 wananiendesha sana na zile tumbua tumbua zote ni vijana wa 80 ila bado kuna vijana wa 80 wanafanya vizuri. Nakumbushwa kuwa kunamkeka wa wakurugenzi bado haujatoka.
Kama vijana mnakutana wapi kuweka ajenda za taifa bila kujali itikadi ? Muweze kuongea bila itikadi zenu na hii inanikumbusha jambo alilosema bintiyangu juu ya jukwaa la vijana. Na hii tutakwenda kuwaandalia jukwaa la vijana tutajadili kwa nini halikuanzishwa shida nini na nk likianzishwa muweke ajenda za kitaifa.
Rais Samia Suluhu Hassan amesema "Vijana mnatumia Mitandao vibaya, kama una mawazo toa mapendekezo sio kulaumu, kushutumu haina faida. Tumieni Mitandao vizuri”
Ameongeza "Kama una jambo la kulaumu, laumu na toa ushauri, kama unakosoa kosoa na toa mapendekezo nini kifanyike. Amewataka Vijana kushirikiana, akisema wakati mwingine malengo hayafikiwi kwasababu kila mmoja kazi anafanya peke yake.
Asema ushirikiano ukiwepo itakuwa rahisi hata kwa Serikali kuwasaidia na kuwawezesha
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewataka Vijana kushirikiana, akisema wakati mwingine malengo hayafikiwi kwasababu kila mmoja kazi anafanya peke yake.
Asema ushirikiano ukiwepo itakuwa rahisi hata kwa Serikali kuwasaidia na kuwawezesha, amewataka Vijana kushirikiana, akisema wakati mwingine malengo hayafikiwi kwasababu kila mmoja kazi anafanya peke yake. Asema ushirikiano ukiwepo itakuwa rahisi hata kwa Serikali kuwasaidia na kuwawezesha.
======
Uzinduzi wa Chelezo( meli mbili zilizokarabatiwa) na uwekaji saini wa mikataba mitano ya ujenzi meli
Lakini nduguzangu leo tena tumeshuhudia uwekaji wa kuweka saini mikata ya kujenga meli tano na moja itakwenda kufanya kazi bahari ya hindi na hii ni kuendelea kuenzi kazi za Hayati Magufuli na dhamira yeti ni kuendelea kuifanya Mwanza kuwa kituo kikubwa cha biashara kati ya nchi za maziwa makuu.
Na ndio maana tunajitahidi kujenga bandari , meli, reli, barabara na pia kujenga kiwanja kikubwa cha ndege, Mwazna Mungu ameiweka sehemu nzuri na inazalisha mazao ya kibiashara kama pamba pia chakula mazao ya ziwani hivyo ndio maana serikali ina dhamira na Mwanza.
Serikali kuiwezesha Mwanza kimtandao ili biashara ziweze kufanyanyika kimtandao na wataokaokuja kukaa Mwanza waweze kuja kufanya biashara kimtandao.
Nishukuru sana wafanyakazi wa bandari na wafanyakazi wa meli na makontrakta na wale wote tuliowekekeana sahihi nasi kama serikali tutaisimamia vyema miradi. Na pia meli hizi zitunzwe na wote wanaohusika ili ziweze kukuza uchumi wetu.