Behaviourist
JF-Expert Member
- Apr 8, 2016
- 39,901
- 95,402
Labda ngoja nikusaidie kwa manufaa ya wengi.Haki huwa haiombwi bali huchukuliwa kwa nguvu kwa sababu anaepaswa kutoa haki huwa hayupo tayari kutoa haki hiyo.Kweli kabisa, hski haipaswi kuombwa,, Mpaka hapo nimekuelewa mkuu,
Anaepaswa kutoa haki huwa hayupo tayari kutoa haki kwa sababu kitendo hicho huwa kinamuumiza yeye.Mfano Samia akiruhusu mikutano ya kisiasa ambayo ni haki ya kikatiba ya vyama vya kisiasa maana yake anajenga upinzani kitendo ambacho kitakiondoa chama chake madarakani.
Kwa kuwa hayupo tayari kuona chama chake cha kisiasa ambacho ndicho kimwemwajiri na kinampa ugali yeye pamoja na familia yake kinatoka madarakani basi anakuwa hayupo tayari kutoa haki hiyo kwa vyama vya kisiasa.
Kwa hiyo katika mazingira kama haya ni lazima utumie nguvu kudai haki yako kwa sababu Samia hayupo tayari kutoa haki hiyo kwa sababu ataumia yeye.Sasa katika mazingira kama haya ukimwendea Mama kwa upole kama wewe ulivyokuwa unadai huwezi kufanikiwa.Umeelewa sasa?