Mwanza hapakutosha, maandamano ya amani zaidi ya saa moja katikati ya Jiji

Hakutaja aina ya madini yaliyomo kwenye vilima, bali ame-generalize hivyo kwa mantiki hiyo huwezi ku-rule out kwamba hivyo vilima havina madini, unless una ripoti ya utafiti wa vilima vyote vya Mwanza.

Hivi milima yenye utajiri wa madini inaweza kuwa mawe ya kujengea nyumba?
 
Mkuu tupia amo vijipicha basi vishamishe Thread siunajua matamaso kama kina Ritz,Rejao,na magamba wengine wote thread ikiwa kavu hivi hawaamini!
 
Mkuu kufuru ni nini? Halafu nashangaa sana wewe ndio kiongozi wa Chadema unanipa wasiwasi na ufahamu wako wa mambo ya kitaifa.

Unasema Jiji la Mwanza linazungukwa na madhari milima yenye utajiri wa madini.

Navyoijua Mwanza sijui ni mlima gani wenye madini kwenye hivi vilima vya Nyashana, Bugarika, Machemba, Bwiru, Kawekamo, Bungado, Nyegezi, kabuoro, Nyakato, Pasiansi, Ibanda.

Hayo ndio majina ya vilima vya Mwanza tufahamishe hayo madini yapo kwenye mlima gani.


Pole kamanda. Soma katikati ya misitari unless utajikuta unaniuliza kujibu kitu/vitu ambavyo sijakiandika au sijaviandika. Ukisoma vyema na ukaniambia nitakujibu mkuu Ritz. Pole.
 
wa jamii sijui ni great thinkers wa aina gani hamjui kuwa ritz nia yake ni kudisturb threads zinazo waeleza ukweli magamba sasa mnavyo kazania kumjibu mnatimiza lengo lake muo mnafikiri jamani dawa yake ni kumpotezea.
kurudi kwenye point huyo slaa jamani aende maeneo ya kusini, pwani na magharibi huko mwanza hakuna shida tena magamba on their knees
 
Yaan Ritz hoja ulichoona wewe katika Thread yote hiyo ni "Vilima vyenye Madini"?mbona unajaribu kupoteza maana na ujumbe tarajiwa wa thread hii!Wacha kudilute thread magamba wewe!Bosi wako naona siku ni Mwendo wa FB tu!na ndiyo kunamfaa!

Mytake: Ritz CCM siyo Kabila wa Ukoo useme uwezi kubadili!
 
Wakuu

Leo CHADEMA imefanya kufuru nyingine katika Jiji la Mwanza. Umefanyika mkutano mkubwa katika Uwanja wa Sahara ambao uko maeneo ya katikati kabisa ya Jiji hili lililozungukwa na madhari ya milima yenye utajiri wa madini na Ziwa Viktoria lenye utajiri wa samaki, uliofuatiwa na maandamano makubwa ya amani yaliyodumu kwa saa nzima na zaidi.

Siku ya leo wananchi wa Mwanza wamepeleka ujumbe mkubwa sana kwa watawala. Kwanza kwa namna isiyokuwa ya moja kwa moja, wame-challenge umuhimu wa ile sheria inayohitaji wananchi 'kuomba' (au kutoa ripoti?) kibali cha kuomba kuandamana.

Pili wametuma ujumbe tena kwa mara nyingine kuwa maandamano ya CHADEMA yasipoingiliwa na polisi, hayawezi kuwa na vurugu hata kidogo. Watu mbalimbali, wanaume kwa wanawake, watoto kwa wakubwa, vijana kwa wazee, wameandamana na msafara wa Katibu Mkuu, Dkt. Slaa kutoka eneo la mkutano mpaka Hotel aliyokwenda kupumzika.

Hakuna namna nyingine ya kuweza kuita hali hiyo isipokuwa kusema wazi kuwa yalikuwa maandamano ya amani kwa takriban saa 1 na kitu. Jiji la Mwanza kwa muda wote huo hasa maeneo ya katikati hadi maeneo ya Bwiru shughuli zilisimama kwa muda. Jiji lili-paralyze kwa muda.

Vijana wanaimba "mafisadi wajiuzulu, mafisadi wajiuzulu". Ilikuwa ni baada ya nondo za uhakika kupigwa pale uwanjani, kuhamasisha masuala mbalimbali ikiwemo vita takatifu dhidi ya UFISADI na MAFISADI.

Mkutano wa leo Mwanza umehitimisha ziara ya siku 10 ya Dkt. Slaa kukagua uhai wa chama katika mikoa 5 ya Tabora, Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza ambayo ilikuwa ni mwendo wa vikao vya ndani asubuhi, mchana, jioni mikutano ya hadhara kisha vikao vya ndani tena usiku.

Maandamano yalikuwa makubwa kwa kweli. Watu wamehamasika. Rebellion dhidi ya CCM na utawala mbovu unaoandamwa na kashafa moja baada ya nyingine uko wazi sana wakuu.Umati wa watu wamelazimika kukimbia umbali wa takriban kilometa 5, kutoka Sahara pale mpaka maeneo ya Bwiru,

Kama ilivyo ada, maelefu ya watu wa Mwanza waliitikia wito kisha wakakubaliana na nondo zilizokuwa zikipigwa na makamanda tangu majira ya saa 9 mpaka saa 12, bila ulinzi wa polisi. CHADEMA wanajilinda wenyewe katika mikutano na maandamano. Wakiachiwa, wanaweza.

Makamanda, wakiongozwa na Katibu Mkuu, Dkt. Slaa, Godbless Lema, Mwita Mwikabe Waitara na wengine kibao, waliwakoga wananchi kwa hoja zinazozungumzia namna ya kutafakari mstakabali wa taifa.

Nondo za leo zilikuwa ni;

Kamanda mie tatizo langu hapo kwenye vilima vilivyozunguka Jiji la Mwanza kuwa na utajiri wa Madini.
 
Tumaini uwe unatupia picha kamanda wengine ni matomaso lakini pia picha zinatuma ujumbe wa kutosha kwa kina ritz na wengine wengi
 
Na wewe unakubali tu kila kitu utakachaambiwa na Chadema mwenzako, kweli Jiji la Mwanza limezungukwa na milima ya madini?


Tuna mtazamo mgando kwamba madini ni almasi, dhahabu na tanzanite tu? Siku hazigandi wajumbe. This is a problem kwani tunaishi kwa mazoea kiasi cha kushindwa kuona hata kama mtu anakushika katika mboni ya jicho lako. Tuamke kwani wakati ni ukuta. Isije tokea siku zijazo wajukuu wetu wakayachapa bakora makaburi yetu kwa kutowaachia lolote lililo la msingi.
 
Mkuu kufuru ni nini? Halafu nashangaa sana wewe ndio kiongozi wa Chadema unanipa wasiwasi na ufahamu wako wa mambo ya kitaifa.

Unasema Jiji la Mwanza linazungukwa na madhari milima yenye utajiri wa madini.

Navyoijua Mwanza sijui ni mlima gani wenye madini kwenye hivi vilima vya Nyashana, Bugarika, Machemba, Bwiru, Kawekamo, Bungado, Nyegezi, kabuoro, Nyakato, Pasiansi, Ibanda.

Hayo ndio majina ya vilima vya Mwanza tufahamishe hayo madini yapo kwenye mlima gani.

Ritz jifungue hyo mimba ya magamba inayokusumbua!,pumba tupu.Hv wewe huna jpya?.Ccm kwa sasa hamna chenu hapa tz! Subirini hukumu ya watz hapo 2015 kwa sasa ni m4c inawatosha watu vilaza kama wewe.
 
Mkuu kufuru ni nini? Halafu nashangaa sana wewe ndio kiongozi wa Chadema unanipa wasiwasi na ufahamu wako wa mambo ya kitaifa.

Unasema Jiji la Mwanza linazungukwa na madhari milima yenye utajiri wa madini.

Navyoijua Mwanza sijui ni mlima gani wenye madini kwenye hivi vilima vya Nyashana, Bugarika, Machemba, Bwiru, Kawekamo, Bungado, Nyegezi, kabuoro, Nyakato, Pasiansi, Ibanda.

Hayo ndio majina ya vilima vya Mwanza tufahamishe hayo madini yapo kwenye mlima gani.

Duh! ninawasiwasi na elimu yako, hata walio shule za kata wanatambua kuwa mawe ni madini, sasa huoni milima yote ya mwaza ina mawe? hayo ndiyo madini ya kufikia bila kufanya uchunguzi wa kina. We gamba kabisa walaumu serikali yako kwa kukupa elimu ya darasa la pili (kusoma na kuandika)
 
Naweka kwanza ili suala sawa kupinga huu upotoshaji kuwa Jiji la Mwanza limezungukwa na vilima vya madini.

RITZ KWANI MADINI NI NINI? nADHANI HUJUI AINA ZA MADINI, MAANA HATA MCHANGA PIA NI MADINI SIYO LAZIMA IWE DHAHABU AU ALMASI
 
nikisikia ma tu anaongelea TBC nataka kutapika hivi TBC ina sera gani kwenye uandishi wa habari?
 
Back
Top Bottom