Ngalikihinja
JF-Expert Member
- Sep 1, 2009
- 31,272
- 31,395
Chukulia mahakama ya kadhi imeanza na hii kesi imepelekwa huko...Hivi sasa ktk ya jiji la Mwanza kuna tahaluki kubwa, watu,magari yanakimbia ovyo,shughuli karibu zote zimefungwa. Kama mtakumbuka wana JF hapa Mwanza kumekuwa na mvutano wa kiiman kati ya waislam na wakristo uliopelekea kuchomwa moto kwa kitabu kitakatifu (kuruan) na kuchomwa moto kwa kanisa.
Leo ndo ilikuwa siku ambayo kesi ilikuwa inasikilizwa mahakaman na ndo vurugi hii ilipoanzia, hadi napost habari hii sijapata kujua ni nini chanzo hasa cha vurugu hizi kutokea hapo mahakaman na kusambaa hadi ktk ya jiji.