Mwanza: CUF waungana na CCM kwenye uchaguzi wa Meya

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
KUGAWANYIKA kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuundwa kwa Halmashauri mpya ya Wilaya ya Ilemela kumekirejeshea Chama Cha Mapinduzi (CCM) matumaini ya kuongoza tena jiji hilo, huku Chama cha Wananchi (CUF) ndicho kikiwa na kura ya kuamua nani anakuwa Meya.

Taarifa kutoka ndani ya CCM hapa Mwanza zinaeleza kuwa tayari vikao vya mikakati vimeanza ili kufanikisha mipango ya kuongoza Jiji hili kwa kuwashirikisha madiwani wawili wa CUF ili waweze kuungana na chama hicho dhidi ya CHADEMA katika uchaguzi wa meya.Taarifa kutoka ndani ya vikao hivyo zinaeleza kuwa mlengwa katika mikakati hiyo ni Diwani wa CUF wa Kata ya Mirongo, Daud Mkama, ambaye ataungwa mkono na CCM katika umeya ili nacho kiungwe mkono na CUF kwenye unaibu meya.

Hata hivyo, inasemekana ahadi hiyo inaweza ikawa inatumika kumvuta diwani huyo na chama chake kuwaunga mkono tu kwa kuwa CCM wana hofu kuwa CHADEMA wana uwezekano mkubwa wa kumfanya awe naibu meya hivyo CCM imemuahidi umeya ili kukichanganya CHADEMA.

“Mheshimiwa (Mkama) anashawishiwa kwa kuwa kuna taarifa kuwa CHADEMA wameahidi kumuunga mkono kama naibu meya. Wanachofanya CCM ni kumvuta aamini kuwa anaweza kuwa meya, lakini kwa uhakika uko mkakati mwingine ambao haujui utaibuliwa dakika za mwisho ili malengo ya CCM kunyakua umeya yatimie na yeye ataambulia unaibu meya,” kinaeleza chanzo chetu toka ndani ya vikao hivyo.

Tayari ziko dalili kuwa CUF wanaweza kuwa wamekubaliana kuwaunga mkono CCM na kuwaacha wapinzani wenzao CHADEMA kwa kuwa juhudi za CHADEMA kumshawishi diwani huyo zinaeelekea kukwama.

Habari hizi zimekasirisha wananchi wengi wa Jiji la Mwanza na kuhoji endapo kama kweli chama cha CUF ni wapinzani wa kweli au ni vibaraka wa CCM.

Source:Raia mwema.
 
Jamani haya ni mambo serious lazima tuyaangalie vizuri kwenye katiba mpya.

Kama CDM ina madiwani 9, CCM 9 na CUF 2. Maana yake ni kwamba chaguo la wana Mwanza ni vyama vya CDM na CCM. Kama kweli tunafuata demokrasia ya kweli basi nilitegemea MEYA NA NAIBU MEYA watoke either CDM or CCM. Naibu meya kutoka CUF chenye madiwani 2 tu huu ni ubakaji wa DEMOKRASIA mchana kweupe.

Mapendekezo yangu, ili kuondokana na hii mizengwe, kwenye KATIBA MPYA tupendekeza ma-MEYA wae wanapigiwa kura direct na wananchi kwenye uchaguzi mkuu. Sio Ma-meya kuchaguliwa na madiwani.

Ndvyo MAMEYA wanavyopatikana katika nchi za wenzetu mfano MAMEYA wa London, Paris, NY etc.

Tuondokane na katiba hii ya mizengwe iliyowekwa na CCM.
 
point. Cuf wangefanya toafauti ndio ungeitwa usaliti.

na cuf angefanya usaliti angepewa talaka tatu mara moja.. Au kuitwa kwa wazee wa baraza kuhojiwa kwanini anakuwa kiugeugeu na kutamani wanaume wengine... Na atapaswa kutamka mmoja tu ni yupi anampenda kwa dhati yake (fisadi-nyinyiemu) au mtetea wanyonge cdm.. Chezea miiko ya ndoa yeye alahaaaaaa
 
Mkuu Molemo ni lini halmashauri ya jiji la mwanza inatarajiwa kuvunjwa rasmi ili kupisha uanzishwaji wa halmashauri za Ilemela na Nyamagana?
Katika mgawanyo huo wa Ilemela na Nyamagana kwa kuangalia uwiano wa madiwani ni chama kipi kitakuwa na uwezo wa kushinda umeya katika halmashauri hizo mpya?
Na je uchaguzi wa meya wa jiji la mwanza umepangwa kufanyika lini?
 
Last edited by a moderator:
Hapo ndipo faida ya kuoa inapoonekana. Kwa hiyo saa hizi Mzee CCM amejifunga taulo lake tu anangoja kuhudumiwa na Mamaa.

Mimi sijui zogo liko wapi? CDM walishapiga kelele na kufanya watu waamini kama CUF wameolewa na CCM sasa nashangaa leo wanalalama kwa nini CUF hawataki kuwaunga mkono kwenye umeya.

Ushauri wangu CUF waendelee na msimamo wao huo huo na CDM wazidi kueneza propaganda za hiyo ndoa, until such a time CDM wakagundua kama mbinu zao chafu za kuipakazia ubaya CUF ina gharama yake.

Kudos CUF.
 
Chadema bana juzi humu si mlikuwa mnawasifia madiwani wa Chadema Mwanza kwa kupiga kura ya kutokuwa na imani naye leo tena mnalia lia nini...huyu diwani wa Miringo Daud Mkama, wa kata ya mjini kabisa ya wazawa wa mji wa Mwanza ni kipenzi cha wana Mwanza ni diwani wa muda mrefu taingia mwaka 2000...tatizo kina Wenje walikuwa wanamdharau sana leo tena kawa lulu.

Tatizo la Chadema walivyopata mafanikio kwenye uchaguzi uliopita wakajikuta wakihodhi wajibu wa jamii kisiasa kwa niaba ya vyama vingine wakihisi kwamba wao ni bora zaidi mbele ya jamii kuliko vyama vingine vyote nchini..

Chadema wanasema wao ndio wapinzani Chadema peke yao hawawezi kuing'oa CCM sababu wanakopita kisiasa tayari wenzao CCM walishatoka.
 
Chadema kilipotoa Meya hapo Mwanza alileta tija gani, na ni madhara gani itakayoyapata Chadema kama haitakuwa na Meya hapo Mwanza?
 
Mkuu Molemo ni lini halmashauri ya jiji la mwanza inatarajiwa kuvunjwa rasmi ili kupisha uanzishwaji wa halmashauri za Ilemela na Nyamagana?
Katika mgawanyo huo wa Ilemela na Nyamagana kwa kuangalia uwiano wa madiwani ni chama kipi kitakuwa na uwezo wa kushinda umeya katika halmashauri hizo mpya?
Na je uchaguzi wa meya wa jiji la mwanza umepangwa kufanyika lini?

Tena umeuliza vizuri sana ! natamani kuona majibu yake.
 
Huyo diwani wa cafu anawajua magamba wanavyobadilika kama kinyonga?hata huo u kaim ataukosa.shauri yake atadondokea pua na imani kwa wananchi kushney.
 
Kuna possibility meya tuliye mwondosha aka mpigia kura mgombea wa CCM, kwa hivi sasa haeleweki eleweki
 
Jamani haya ni mambo serious lazima tuyaangalie vizuri kwenye katiba mpya.

Kama CDM ina madiwani 9, CCM 9 na CUF 2. Maana yake ni kwamba chaguo la wana Mwanza ni vyama vya CDM na CCM. Kama kweli tunafuata demokrasia ya kweli basi nilitegemea MEYA NA NAIBU MEYA watoke either CDM or CCM. Naibu meya kutoka CUF chenye madiwani 2 tu huu ni ubakaji wa DEMOKRASIA mchana kweupe.

Mapendekezo yangu, ili kuondokana na hii mizengwe, kwenye KATIBA MPYA tupendekeza ma-MEYA wae wanapigiwa kura direct na wananchi kwenye uchaguzi mkuu. Sio Ma-meya kuchaguliwa na madiwani.

Ndvyo MAMEYA wanavyopatikana katika nchi za wenzetu mfano MAMEYA wa London, Paris, NY etc.

Tuondokane na katiba hii ya mizengwe iliyowekwa na CCM.

mkuu mbona cuf waliungana na ccm katika uchaguzi wa meya uliopita. cuf ijiangalie upya ktk hili swala.. la sivyo 2015 madiwani wao wote 2 hawatarudi c'se wananchi hawakutegemea iwapo madiwani wao wangefanya kitendo kile ktk uchaguzi wa meya. Hapa haiangaliwi sifa ya mgombea bali ni UCHU WA MADARAKA.. nitalaani sana cuf kupewa hongo ya unaibu meya pasipokuzingatia uwezo wa diwani mwenyewe.

HII NI RUSHWA YA MADARAKA.. sijui takukuru wapo wapi
 
Kwa mlio mbali hamjui kilichotokea.Hali halisi ni kwamba ktk uchaguzi wa udiwani kata ya mirongo chadema hawakusimamisha mgombea, cuf waliwaomba cdm wawaunge mkono na cdm wakakubali.mgombea wa ccm yahya nyahonge alikua na nguvu na anakubalika kuliko wa cuf, lakini cdm ndio waliowabeba na hata matokeo yalipokuwa yakitangazwa katani cdm ndio waliokuwa wengi wakiongozwa na wenje ktk kushangilia ushindi huo wa cuf.Bika cdm, cuf hicho kiti wangekisikia tu
 
Narubongo samahani ndugu yangu, hivi hiyo picha unayotumia kama Avatar ni ya nani, maana kwa muda mrefu nimeshindwa hata kukuelewa maana upo kama popo si ndege wala si mnyama. ni hilo tu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom