Mwanyika aongea...

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
EPA.JPG

EPA%202.JPG

EPA%203.JPG

EPA%204.JPG


Haya kazi kwenu!
 
Huyo ni mwanasheria mkuu wa serikali.....? kwani kutuambia mwizi wetu ni huyu ni kuwafedhehesha jamani? kwani kwa wao kuwaibia hawajawafedhehesha watanzania kibao ambao wanakosa huduma za afya, kama kina mama, kwa sababu ya ukosefu wa fedha za kuwalipa wataalam na vitendea kazi?

Tukisema ni kulindana tutakuwa tumekosea?
 

Nawa hili naamini hakuna hata mhariri mmoja aliyeuliza swali!!!Wangemuuliza hivi inakuwaje mhalifu wa kuku anapokamatwa anaadhibiwa na kutangazwa papo hapo pasi na kusubiri matokeo ya uchunguzi?Je kwa Mahalau na mwenzake mbona walitangazwa na kisha uchunguzi wa kipolisi na mshitaka tayari yapo mahakamani na kesi inaungurma?Kuna utofauti wowote wa kesi hizi mbili?EPA sio uhujumu uchumi pia?

Je Mwanyika hajataka kukubali kuwa hao mafisadi sio watuhumiwa?Na kama ni watuhumiwa si wapelekwe polisi kisha uchunguzi uendelee huku sheria ikijiandaa kuchukua mkondo wake (kama kweli tachukua)?Duh Mwanyika once again proves how bogus he is!!I cannot believe seeing him advancing such premitive and unfounded legal arguments and worse still he is our chief of the law!!
 
Jamani Jamani kusema huyu hapa katuibia ni kumfeedhesha MWIZI?????????? MWIZI??????????????. Asituambie mbinu wanazotumia sawa kabisa lakini atuambie ni nani kaiba huenda tukamsadia zaidi jinsi ya kupata hizo hela na mali zao ziko wapi. Si waliomba wenyewe kuwa mtu mwenye taarifa apeleke?
 
BIG NO..............Mr Mwanyika

............awali ya yote wewe tayari una madoa mengi na hivyo hatuna imani na wewe katika uchunguzi huu.........please step down from kamati

......pili.......kama mtu alichukua pesa kihalali kwanini arudishe??, JK mwenyewe alisema wale wote waliochukua pesa isivyo halali warudishe na wachukuliwe hatua....PERIOD...... in short ni wahujumu UCHUMI!! hawa.......wananchi tumehujumiwa.......sasa usianze kutafuta namna ya KUREMBA lugha ili kuwafanya waonekane ni watu innocent...............kwanini unatumia eti neno.............."tutawafedhehesha"!!!!!................no way wao wamekwisha tufedhehesha sisi wananchi and now its their turn kuona mlango wa sheria without delay.

.........mbinu za kurudisha pesa ni zipi na zina usiri gani na kwanini ziwe siri kwa watu ambao tayari wanajulikana na makampuni yao yanajulikana?.....freeze their damn assets........damn it!!!.............watu wanahujumu uchumi mnataka kuwageuzia makosa kama mlivyofanya kwa rafiki yenu Ditto!!............hakuna cha jinai hapa.........hawa ni wahujumu uchumi!!
 
Changa la Macho .... Hapa tayari wanaanza kuweka mazingira maalum ya kuzima Ripoti ya EPA isijadiliwe Bungeni kwenye kikao kijacho cha mwezi April kwa kuwa Tume ya Mwanyika itakuwa bado inaendelea kufanya kazi na haijakamilisha uchunguzi wake na hivyo haitakuwa vyema kuanza kuijadili report ya EPA wakati Tume ya Mwanyika haijakamilisha uchunguzi wake. Baada ya hapo kikao cha Bajeti cha Juni tutaambiwa ratiba iko tight sana na hivyo hakuna nafasi ya kuipenyeza hiyo report, hatimaye itabaki Ikulu kwa JK na hatutajua kilicho ndani ya hiyo report.

Hii ndiyo Bongo na hii ndiyo serikali ya JK! Tukisema JK na Tume yake ya EPA wanawalinda mafisadi wanalalamika kwamba tunawaonea/tunawasingizia, lakini sasa naona kuna juhudi zote za kuficha report ya EPA na majina ya mafisadi tena kwa makusudi kabisa.
 
Sasa kama makampuni yanafahamika kwanini asiseme ni kampuni gani imerudisha pesa????? Ukisikia kamati iliyo-fail kabla ya kazi ni hii ya wajinga watupu--Mwanyika-Hosea- kwanza wote inabidi waachie ngazi na wanaendelea kuonyesha uwezo wao mdogo.
 
EPA.JPG

EPA%202.JPG

EPA%203.JPG

EPA%204.JPG


Haya kazi kwenu!

Amebwabwaja tu! tangu lini kuwataja wezi au mafisadi hadharani kukawa na kuwafedhehesha? Kwani wao walipokuwa wakifanya ufisadi wao hawakujua kama wakigundulika watafedheheka kwa lile walilolifanya? Kwa hiyi Mwanyika anaendlea kuwakingia kifua eti mafisadi wasitajwe ili wasifedheshwe hadharani! Huyu Mwanyika hajui kama akiwataja hadharani inaweza kusaidia kupata ushahidi zaidi na ushirikiano mkubwa toka kwa wananchi wanaowafahamu mafisadi hawa? Acha usanii Mwanyika! wataje mafisadi hadharani ili Watanzania wote tuwajue.
 
BABA HUMU KUMBE SISI NI WAPANGAJI!!! DUH! KUMBE HII NCHI NI YA WACHACHE DUH!! BORA HATA NIMEJUA ......

MMMH HAWA WATU MBONA NIWAJASIRI MPAKA NAOGOPA AU NI MKWARA NINI.YAANI UNAIBIWA NA UNAPEWA MASHART NA MWIZI.

SASA KAMA MLINZI AKIZUBAA MALI IKAIBWA JE SI NIYEYE ANAYE TURUDISHIA. SO TUNASUBIRI NINI MAANA HAWA JAMAA TUNA WAGHARIMIA KILA KITU IWEJE WASIFANYE MAJUKUMU YAO MPAKA TUNAIBIWA!!
MIMI NINGEPENDA TU WAZIDI KUJIWAJIBISHA NA ADHABU JUU NA KUTURUDISHIA FADHILA MAANA TUMEWATUNZA ILI MAMBO YAENDE ILA TUMEAMBULIA MAMBO KUTO KWENDA NA ASARA JUU.SASA TUNASUBILI NINI????
 
Kuyataja majina makampuni anapatwa na kigugumizi seuze kuyashughulikia.

I banked alot on this gentleman but not anymore...
 
I bank alot on this gentleman but not at more...
Mkuu Masatu umesahau hii kitu "Confidential"? Naona bado anafuata "Protocol".

Anyway, labda itawezekana... Tusubiri tuone lakini kikitokea kimya kidogo tu ujue itakuwa ndio imetoka!
 
bado nastaajabu namna serikali yetu inavyozidi kutoa majibu ya kitoto kuhusu wizi mkubwa kama huu.Hata hivyo tokea mwanzo nilijua hakuna hatua zozote kubwa zitakazochukuliwa.

UNAJUA KWA NINI?
MAFISADI NDO HAOHAO WALIOPO KWENYE HIYO TASK FORCE[/SIZE]
 
Wameshatuangalia na kugundua kuwa watanzania wote ni watiifu kwa viongozi wao ndio maana wanatuchezea kama mpira,unyonge wetu ndio uliotufikisha hapa,na ipo siku watakuja kutushika hata naniliu zetu na tutabaki kuwasujudia tu. na huku tukiimba mapambio ya kuwasifu,lakini wakitoka tu tunarudi kwenye ile korasi ya ufisadi,ufisadi ufisadi oye oye oye,na mwisho usiku tunalala,kesho yake tena mwimbo ni ule ule.
 
Watanzania kwa mara nyingine tumepigwa bao la kisigino
Nina mashaka sana na shule ya sheria aliyosoma mwanyika,
nina mashaka sana na mwalimu aliyemfundisha mwayika masuala ya sheria.
ni mashaka hayo yananipelekea kuamini kuwa, zitafika siku ambapo mahakama zitaendesha kesi za kifisadi ktk sebule za mafisadi, Wanaogopwa hawa..... kama hawaogopwi ni kwa nini wanafichwa identity zao??
Au CCM inahusika?????? Hili sipendi kuamini ila nashawishika kuamini hivyo endapo akina mwanyika na wenzake wataendelea kuficha ukweli.

Na ni kwa nini hawajafutwa kazi hawa wazee wawili?? kipi kinaogopwa? au ndo kudharauliwa kwa maamuzi ya Bunge??

Tanzania ni miracle country
 
Wameshatuangalia na kugundua kuwa watanzania wote ni watiifu kwa viongozi wao ndio maana wanatuchezea kama mpira,unyonge wetu ndio uliotufikisha hapa,na ipo siku watakuja kutushika hata naniliu zetu na tutabaki kuwasujudia tu. na huku tukiimba mapambio ya kuwasifu,lakini wakitoka tu tunarudi kwenye ile korasi ya ufisadi,ufisadi ufisadi oye oye oye,na mwisho usiku tunalala,kesho yake tena mwimbo ni ule ule.

Katika siku zote wandugu leo it has been more serious na sina hata la kusema .Nakaa kimya tuna angalia matunda ya CCM na JK wanakutelea maendeleo .
 
Nimebahatika kuisikia press conference ya Mwanyika na Mwema sioni nia ya dhati ya hii kamati katika kupambana na ufisadi.
Ni longo longo nyingi katika kuupaka rangi ufisadi ili upendeze
 
Kwa waliokuwepo na kumwelewa mwema alivyozungumza, ingawa ameingiza politics nyingi, lakini anatia moyo kuwa kinachofanyika kitazaa matunda hapo baadaye. nadhani wanapaswa kufahamu kuwa watanzania wengi wamefikia hatua mbaya sana ya kukata tamaa hivyi wanapaswa kulishughulikia suala hili kwa uharaka sana.

Kimsingi mwema alisema kuwa kuna aproach kadhaa za upelelezi, moja ikihusisha kukamata kwanza na baadaye kuchunguza (kama ilivyotokea kwa Ditopile) na nyingine inayohusisha kuchunguza kwanza na kukamata baadaye, ambayo ndiyo wanaitumia katika uchunguzi huu. Lengo anasema ni kuua ndege wawili kwa jiwe moja, kurudisha fedha na kuwabana mafisadi.

Nilivyomsikiliza inaonekana ana point fulani (kama si politics). nampa benefit of doubt kwanza kabla sijamhukumu
 
source: mzee wa sumo (Mpoki Bukuku)

Mwenyekiti wa Timu Maalumu (Task Force) ya Rais ya kuchunguza wizi wa mabilioni ya shilingi Benki Kuu katika kashfa ya ufisadi, Johnson Mwanyika (kushoto), ameshindwa kutoa hesabu kamili ya pesa wanayodai kukusanya na hakuwa na jipya la kueleza badala yake alishindwa kutoa majibu ya msingi ya maswali ambayo yamekuwa yakiulizwa.

Mwanyika akionekana dhahiri kushindwa kujieleza huku akijikanyaga katika kauli zake, alisema hadi sasa fedha hizo zinarejeshwa katika akaunti maalumu ambayo alisita kusema imefunguliwa katika benki gani na mafisadi wanaorejesha pesa wameijuaje?

Huku akionekana kukosa taarifa mpya za kutoa kwa vyombo vya habari, Mwanyika alishindwa kueleza kwa dhati kiasi cha fedha kilichokusanywa hadi jana badala yake alikisia kwamba ilitarajiwa kuwa sh 60 bilioni hadi asubuhi alipoondioka kazini.

Kwa kuonyesha Mwanyika hakuwa amejiandaa vya kutosha kuzungumza na vyombo vya habari, taarifa yake imepingana na taarifa yya maandishi iliyotolewa jana na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambayo ilimukuu taarifa ya timu hiyo na kusema zilikuwa zimekusanywa sh 64 bilioni.

Alirudia maeneo yake ya kusihi Watanzania kuwa na subira huku akishindwa kueleza pia kwamba, katika fedha hizo thamani ya mali ni kiasi gani na fedha taslimu.

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali (IGP) Said Mwema akizungumza katika mkutano huo amewafafanisha watuhumiwa wa ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), sawa na watuhumiwa wa ugaidi ambao wanaweza kuilipua nchi.

alisema mchakato unaondelea katika urejeshaji wa fedha za umma zaidi ya sh 133 bilioni zilizoibwa EPA, alisema watu hao wanaweza kuilipua nchi iwapo watatafutwa kwa pupa.

IGP Mwema alisema timu inafahamu kwa kina jinsi Watanzania wanavyokerwa na kuhoji vipi, watuhumiwa hawakamatwi kitu ambacho hata wao (timu) kinawaumiza roho.

Alisema kuna mashaka makubwa miongoni mwa Watanzania kwamba, watu waliotajwa katika ufisadi huo wanapita mijini huku wakitamba lakini hawakamatwi hali ambayo inawafanya wananchi wahoji kazi ya timu hiyo.

"Kuna mashaka makubwa, watu waliotajwa wanaonekana kupita mijini, wanatamba, watu sasa wanaohoji hii timu kazi yake nini, hili jambo linawakera wengi na sisi pia tunajisikia hivyo hivyo," alisema IGP Mwema na kuongeza:,

"Tunaulizwa tunawaogopa, hata sisi inatusikitisha kwanini hatuwakamati, kila mtu anajua na kila mtu anataka wakamatwe, lakini hili suala linahitaji upepelezi mtambuka."

"Suala hili si dogo, linagusa watu wengi na maeneo mengi, tunachofanya ni kulishughulikia kwa umakini, watuhumiwa waliochukua fedha ni sawa na magaidi, tukiwafuata kwa pupa wanaweza kuilipua nchi
.
 
source: mzee wa sumo (Mpoki Bukuku)

Mwenyekiti wa Timu Maalumu (Task Force) ya Rais ya kuchunguza wizi wa mabilioni ya shilingi Benki Kuu katika kashfa ya ufisadi, Johnson Mwanyika (kushoto), ameshindwa kutoa hesabu kamili ya pesa wanayodai kukusanya na hakuwa na jipya la kueleza badala yake alishindwa kutoa majibu ya msingi ya maswali ambayo yamekuwa yakiulizwa.

Mwanyika akionekana dhahiri kushindwa kujieleza huku akijikanyaga katika kauli zake, alisema hadi sasa fedha hizo zinarejeshwa katika akaunti maalumu ambayo alisita kusema imefunguliwa katika benki gani na mafisadi wanaorejesha pesa wameijuaje?

Huku akionekana kukosa taarifa mpya za kutoa kwa vyombo vya habari, Mwanyika alishindwa kueleza kwa dhati kiasi cha fedha kilichokusanywa hadi jana badala yake alikisia kwamba ilitarajiwa kuwa sh 60 bilioni hadi asubuhi alipoondioka kazini.

Kwa kuonyesha Mwanyika hakuwa amejiandaa vya kutosha kuzungumza na vyombo vya habari, taarifa yake imepingana na taarifa yya maandishi iliyotolewa jana na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), ambayo ilimukuu taarifa ya timu hiyo na kusema zilikuwa zimekusanywa sh 64 bilioni.

Alirudia maeneo yake ya kusihi Watanzania kuwa na subira huku akishindwa kueleza pia kwamba, katika fedha hizo thamani ya mali ni kiasi gani na fedha taslimu.

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali (IGP) Said Mwema akizungumza katika mkutano huo amewafafanisha watuhumiwa wa ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), sawa na watuhumiwa wa ugaidi ambao wanaweza kuilipua nchi.

alisema mchakato unaondelea katika urejeshaji wa fedha za umma zaidi ya sh 133 bilioni zilizoibwa EPA, alisema watu hao wanaweza kuilipua nchi iwapo watatafutwa kwa pupa.

IGP Mwema alisema timu inafahamu kwa kina jinsi Watanzania wanavyokerwa na kuhoji vipi, watuhumiwa hawakamatwi kitu ambacho hata wao (timu) kinawaumiza roho.

Alisema kuna mashaka makubwa miongoni mwa Watanzania kwamba, watu waliotajwa katika ufisadi huo wanapita mijini huku wakitamba lakini hawakamatwi hali ambayo inawafanya wananchi wahoji kazi ya timu hiyo.

"Kuna mashaka makubwa, watu waliotajwa wanaonekana kupita mijini, wanatamba, watu sasa wanaohoji hii timu kazi yake nini, hili jambo linawakera wengi na sisi pia tunajisikia hivyo hivyo," alisema IGP Mwema na kuongeza:,

"Tunaulizwa tunawaogopa, hata sisi inatusikitisha kwanini hatuwakamati, kila mtu anajua na kila mtu anataka wakamatwe, lakini hili suala linahitaji upepelezi mtambuka."

"Suala hili si dogo, linagusa watu wengi na maeneo mengi, tunachofanya ni kulishughulikia kwa umakini, watuhumiwa waliochukua fedha ni sawa na magaidi, tukiwafuata kwa pupa wanaweza kuilipua nchi
.

Bonge ta Drama . Polisi ni wepesei kumkamata mwenyikiti wa tawi wa Chadema kwa maelekezo ya CCM kuliko Fisadi ambaye kwanza CC ya CCM inajadili ndiyo Kamati leo inaenda kusema kulemba na kuunga mkono.Yaani watu wako mitaani walipue Nchi ?Na Mwema anajua hili ? Wako wangapi na silaha zao ziko wapi ? Kuna utani mwingi sana hapa .
 
Back
Top Bottom