Mwanguko wa kura za Kikwete (2005 to 2010) ni ashirio mbaya kwa Magufuli!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
JK mwaka wa 2005 alipata karibu 82% lakini mwaka 2010 alipata karibu 61% likiwa ni anguko la 21%.

JPM mwaka 2015 alipata takribani 56% kwa kuangaliza anguko la JK kwa 21% basi JPM uchaguzi ujao yaani 2020 kuambulia 35%.

Kama upinzani kura zao zote wataziweka kapu moja basi hakuna jinsi mgombea wao wa UKAWA ataibuka kidedea kwa 65%.


Na jinsi uchumi unavyozidi kudorora na wapigakura wengi kuisoma namba vilivyo huku watawala hawana majibu zaidi ya kudai tunaolalama ni wapiga dili wakati kama dili zilikuwepo wachoraji ni wao basi tegemea hata hiyo 35% kushuka chini ya 30%.

Nyerere mwaka 1981 baada ya kuona kila mtu analia na ugumu wa maisha hakutulaumu bali alikuja na kauli za matumaini akiwa Kigoma alisema yafuatayo......" ....tusikubali kugeuka kuwa jiwe....na tufunge mikanda kwa miezi kumi na nane."

Ulikuwa ni utapeli wa kisiasa lakini ulimsaidia kumaliza ngwe yake ya mwisho bila vurugu na akasoma alama za wakati na kubwaga manyanga hapo 1985.

Kuwalaumu wapigakura na kuwaita wapiga dili ni kuwatusi na kukosa majibu ya kero za kiuchumi ni kuwafyagilia wapinzani wako na kujiandaa kisaikolojia kuwakabidhi dola kiulaini kabisa.
 
CCM na serikali yake is a sinking boat! No wonder hivi viashiria vya ubabe na kusigina sheria ni dalili za "panic in the palace"! Afterall no situation is parmanent, vinginevyo Sadam Hussein na Mobutu na Ghadafi wangekuwa bado wanatesa ulingoni! Muda utaongea
 
JK mwaka wa 2005 alipata karibu 82% lakini mwaka 2010 alipata karibu 61% likiwa ni anguko la 21%.

JPM mwaka 2015 alipata takribani 56% kwa kuangaliza anguko la JK kwa 21% basi JPM uchaguzi ujao yaani 2020 kuambulia 35%.

Kama upinzani kura zao zote wataziweka kapu moja basi hakuna jinsi mgombea wao wa UKAWA ataibuka kidedea kwa 65%.


Na jinsi uchumi unavyozidi kudorora na wapigakura wengi kuisoma namba vilivyo huku watawala hawana majibu zaidi ya kudai tunaolalama ni wapiga dili wakati kama dili zilikuwepo wachoraji ni wao basi tegemea hata hiyo 35% kushuka chini ya 30%.

Nyerere mwaka 1981 baada ya kuona kila mtu analia na ugumu wa maisha hakutulaumu bali alikuja na kauli za matumaini akiwa Kigoma alisema yafuatayo......" ....tusikubali kugeuka kuwa jiwe....na tufunge mikanda kwa miezi kumi na nane."

Ulikuwa ni utapeli wa kisiasa lakini ulimsaidia kumaliza ngwe yake ya mwisho bila vurugu na akasoma alama za wakati na kubwaga manyanga hapo 1985.

Kuwalaumu wapigakura na kuwaita wapiga dili ni kuwatusi na kukosa majibu ya kero za kiuchumi ni kuwafyagilia wapinzani wako na kujiandaa kisaikolojia kuwakabidhi dola kiulaini kabisa.
  • We mpiga dili huna hoja ya maana, Yupo kiongozi ambaye awamu ya kwanza alipata kura chache na ilipo fika awamu ya pili zikaongezeka
  • Mkapa 1995 alipata 61.82% na mwaka 2000 ziliongezeka mpaka 71.74%
 
  • We mpiga dili huna hoja ya maana, Yupo kiongozi ambaye awamu ya kwanza alipata kura chache na ilipo fika awamu ya pili zikaongezeka
  • Mkapa 1995 alipata 61.82% na mwaka 2000 ziliongezeka mpaka 71.74%
Sasa mkapa si alileta unafuu wa maisha kwanini watu wasimchague? Halafu mkapa alikuwa anashindana na nani? Hapa upinzani wanatakiwa wajipange hasa kwenye kumsimamisha mtu .babu kipara hana ujanja atakula jeuri yake
 
CCM mwisho ni 2020 tukishindwa hapo bora wote tuhamie CCM itakua haina maana
 
Upinzani nao unakufa taratibu. Kura zitashuka CCM ziende kwa nani??

Labda Joka la mdimu kupitia ACT kama unamfutilia Zitto.
 
CCM na serikali yake is a sinking boat! No wonder hivi viashiria vya ubabe na kusigina sheria ni dalili za "panic in the palace"! Afterall no situation is parmanent, vinginevyo Sadam Hussein na Mobutu na Ghadafi wangekuwa bado wanatesa ulingoni! Muda utaongea
Labda wajirekebisha ingawaje sioni hata mwelekeo
 
  • We mpiga dili huna hoja ya maana, Yupo kiongozi ambaye awamu ya kwanza alipata kura chache na ilipo fika awamu ya pili zikaongezeka
  • Mkapa 1995 alipata 61.82% na mwaka 2000 ziliongezeka mpaka 71.74%
Unachosahau Mkapa alikumbana na mood ipi ya wapigakura na hapakuwepo UKAWA mwaka 2000!
 
Back
Top Bottom