Mark Mwandosya akanusha uvumi kuhusu kutoa tamko kwa waraka wa maaskofu KKKT

JMWAKA

JF-Expert Member
Jun 18, 2012
694
574
Ndugu marafiki na watanzania wenzangu, taarifa zinasambaa kwenye mitandao mbalimbali za kijamii zikilenga kuaminisha umma kwamba nimetoa tamko kuhusu lile linaloelezwa kama "shambulizi" dhidi ya Maaskofu wa Kanisa. Ujumbe huo sio wa kweli, ni wa uzushi na ni wakugushi. Hivyo basi ni ujumbe wa kupuuzwa. Nikiwa Mwalimu, Mbunge, na Waziri mstaafu nina nafasi pekee ya mawasiliano na viongozi wa Serikali, Waheshimiwa Masheikh na Maaskofu, na Taasisi nyingine kwa njia zinazoweza kuleta matokeo chanya.

Mimi ni muumini wa uhuru wa kujieleza na kutoa mawazo. Huu umekuwa msingi wa maendeleo na kukua kwa uelewa kwa karne nyingi. Hata hivyo kusambaza taarifa za uongo sio tu ni dhambi bali ni kosa la jinai, na bila shaka kitendo hicho kina madhumuni hasi.

Mark Mwandosya,
Lufilyo
Busokelo
8 Juni 2018

Ameyaandika hayo kwenye mtandao wa twitter.
 
Umefanya vizuri kupinga mapema kabla hatujakuelewa vibaya. Polisi wakusaidie uujue mwanzo wa uongo huo.
 
“Nina nafasi pekee za mawasiliano na viongozi wa serikali kwa njia zinazoweza kuleta matokeo chanya.”

Njia za mitandao ya kijamii haziwezi kuleta matokeo chanya?

Mbona alitumia mitandao kutoa maoni kuhusu Sugu?

Old servant is going senile, ugonjwa wa wazee.
 
Prof kaogopa,ila Jiwe ni mwanaume namkubari sana uwa ayumbishwi akiamua kaamua, Siku ile kwenye kikao cha Chama chao Mfu anamwita Kinana "Sasa huyu aliomba kupumzika muda mrefu tukawa tunamkatalia" bonge ya zarau.
 
Nguvu ya chama ccm sijui ni mdudu gani ukiwa huko hata mwanao unaweza kumkana
 
Ndugu marafiki na watanzania wenzangu, taarifa zinasambaa kwenye mitandao mbalimbali za kijamii zikilenga kuaminisha umma kwamba nimetoa tamko kuhusu lile linaloelezwa kama "shambulizi" dhidi ya Maaskofu wa Kanisa. Ujumbe huo sio wa kweli, ni wa uzushi na ni wakugushi. Hivyo basi ni ujumbe wa kupuuzwa. Nikiwa Mwalimu, Mbunge, na Waziri mstaafu nina nafasi pekee ya mawasiliano na viongozi wa Serikali, Waheshimiwa Masheikh na Maaskofu, na Taasisi nyingine kwa njia zinazoweza kuleta matokeo chanya.

Mimi ni muumini wa uhuru wa kujieleza na kutoa mawazo. Huu umekuwa msingi wa maendeleo na kukua kwa uelewa kwa karne nyingi. Hata hivyo kusambaza taarifa za uongo sio tu ni dhambi bali ni kosa la jinai, na bila shaka kitendo hicho kina madhumuni hasi.

Mark Mwandosya,
Lufilyo
Busokelo
8 Juni 2018

Kanusho kama hili kama ulivyo ujumbe wa awali hauwezi kupewa uzito wa kuaminika isipokuwa kama Mwandosya mwenyewe anarekodiwa akizungumza (kukana au kuthibitisha). Watanzania wanazidi kuwa wahanga wa habari feki (fake news).
 
Kanusho kama hili kama ulivyo ujumbe wa awali hauwezi kupewa uzito wa kuaminika isipokuwa kama Mwandosya mwenyewe anarekodiwa akizungumza (kukana au kuthibitisha). Watanzania wanazidi kuwa wahanga wa habari feki (fake news).

Umeniwahi! Nami nilitaka kusema hivyo hivyo! Kwamba hata hili kanusho laweza kuwa ni la kizushi vilevile!
 
Watu tukisema chadema wana pull strings za Askofu Shoo mnabisha, sasa nani anaeneza haya mambo na kwa nini?

Chadema= evil!
Wewe jamaa na Chadema!!! Hivi inaweza kupita simu bila kuiparamia Chadema? Tatizo ni nini huwa inakupa ndoto za jinamizi nini?
 
Mwandosya tumekuelewa! Siku hizi unaitwanga ukweli serikali kisha ujumbe ukifika unaukana kuwa wamegushi, ila message delivered
 
Back
Top Bottom