Mwandishi ZNZ akamatwa kwa 'Uchochezi!!!'!

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Kuna habari kwamba Mwandishi wa Habari wa IPP wa PST, Nipashe na Guardian amekamatwa kwa uchochezi Zanzibar. na pia kuna habari kwamba waandishi wa TVT na RTD wamepata ajali Korogwe wakiwa njiani kwenda Moshi kumzika Salome Mbatia. Habari zaidi baadaye
 
Kuna habari kwamba Mwandishi wa Habari wa IPP wa PST, Nipashe na Guardian amekamatwa kwa uchochezi Zanzibar. na pia kuna habari kwamba waandishi wa TVT na RTD wamepata ajali Korogwe wakiwa njiani kwenda Moshi kumzika Salome Mbatia. Habari zaidi baadaye

Duuh...!
Makubwa haya
 
Kuna habari kwamba Mwandishi wa Habari wa IPP wa PST, Nipashe na Guardian amekamatwa kwa uchochezi Zanzibar. na pia kuna habari kwamba waandishi wa TVT na RTD wamepata ajali Korogwe wakiwa njiani kwenda Moshi kumzika Salome Mbatia. Habari zaidi baadaye

Hizi ajali naona zitawafanya waweke umuhimu unaotakiwa katika sekta ya barabara na usafirishaji.

Je, ni uchochezi wa namna gani ambao huyo mwandishi ameshikiliwa?
 
Naomba radhi jana kwa kupotea kutokana na matatizo ya kiufundi. Hii ndio habari kamili kama ilivyosambazwa na mwandishi mwingine wa habari wa Zanzibar, Jabir Idrissa.


Na Jabir Idrissa, Zanzibar

Mwandishi wa habari wa kampuni ya The Guardian Limited, Mwinyi Sadallah amekamatwa na kufunguliwa mashitaka ya uchochezi kutokana na habari alizowahi kuandika hivi karibuni.



Mwandishi huyo anayeiwakilisha kampuni hiyo upande wa Zanzibar , alikamatwa kiasi cha saa 3.30 asubuhi jana na kupelekwa moja kwa moja kituo cha Polisi cha Mwembemadema, yalipo makao makuu ya Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi.



Baada ya hatua mbalimbali zilizofuatia zikisimamiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa, SSP Said Malekano, mwandishi huyo aliachiwa saa 8.30 mchana baada ya kuwa amewekwa ndani pia katika kituo cha polisi cha Mazizini.



Mara baada ya kuachiwa, mwandishi huyo aliwaeleza waandishi wa habari waliofuatilia kwa karibu tukio hilo , kwamba ameachiwa kwa dhamana ya Sh. Milioni 2 kupitia mdhamini mmoja pamoja naye binafsi.



Sadallah alisema katika kuachiwa kwake huko, ametakiwa Jumanne ijayo apige ripoti ofisini kwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa aliyepo Mwembemadema.



Kamanda wa Polisi wa Mkoa, ACP Bakari Khatib Shaaban hakupatikana jana kwa vile kwa muda mwingi simu yake ilikuwa haipokewi ingawa wakati mmoja alijibu kuwa amepumzika kwa homa.



Waandishi wa habari waliokuwa wanafuatilia kukamatwa kwa Sadallah, walipofika Mwembemadema na kuulizia, walijibiwa kuwa alikuwa ameachiliwa tayari na ameondoka.



Hata hivyo, waandishi hao walilazimika kupiga kambi hapo baada ya kubaini utata wa taarifa hizo, hasa kwa kuwa mwandishi huyo alikuwa hayuko ofisini mtaa wa Weles, Kikwajuni, wala nyumbani kwake Mazizini.



Alipopigiwa simu Kamanda Bakari na kuelezwa kuna utata huo, alimuelekeza askari mmoja kufuatilia kaunta, aliporudi aliwataka waandishi wasubiri kidogo wafahamishwa aliko.



Baadaye, Sadallah aliwapigia simu waandishi waliokuwa wakimfuatilia na kuwaambia kuwa wasiondoke maana alikuwa anakuja kituoni hapo.



Dakika tano kupita, alifika akishuka kwenye gari aliyokuwemo na RCO na kueleza kuwa alikuwa amewekwa ndani kituo cha Polisi cha Mazizini.



Wakati RCO akipita kaunta kupanda juu ofisini kwake, alisikika akimtaka Sadallah awe na mdhamini mmoja ambaye alifuatana naye.



Akieleza zaidi mkasa huo, Sadallah alisema askari watatu wa upelelezi waliomfuata ofisini asubuhi walimtamkia kuwa yuko chini ya ulinzi na aondoke wafuatane hadi kutoni.



"Hawakuniambia kosa langu nini walisisitiza tu twende nitafahamishwa kituoni," alisema. Alipinga walipotaka kumfunga pingu mikononi baada ya kumwambia kuwa amekuwa mbishi.



"Nilipofika Madema walinipandisha juu kwa RCO na kuniambia kuwa nimeandika habari za uchochezi na kunitaka niweke saini kwenye hati ya maelezo waliyokuwa wameiandaa, lakini niliwakatilia siwezi kusaini maelezo yasiyo ya kwangu na nahitaji mwanasheria," alisema.



Sadallah hakuelezwa ni nani aliyekwenda kulalamika Polisi hata ikalazimu akamatwe, lakini alielezwa kuwa kuwa ameandika habari zisemazo kuwa Rais amepora kiwanja na kuwapatia wawekezaji kujenga kituo cha mafuta.



"Mimi sijafanya uchochezi wowote nimeandika habari kwa mujibu maadili. Lakini iwapo wana matatizo yao , basi tusubiri mahakama ndiyo itaamua maana ndiyo yenye kazi ya kutafsiri sheria," alisema.



Sadallah alisema hakupata kipigo chochote akiwa vituo hivyo viwili ingawa alitakataliwa kutoka alipotaka kwenda kujisaidia choo kidogo.



"Sikupigwa lakini walikuwa wakituma askari wao kujaribu kunitafuta maoni yangu wakijifanya nao wamewekwa ndani. Niliwafahamu kwa hivyo sikuwashughulikia," alisema.



Mazingira yalivyo, inaonyesha Polisi watamfikisha mahakamani mwandishi huyo kwani wamemwambia amefanya kosa kinyume na Sheria ya Magazeti ya Zanzibar ya mwaka 1988.



Habari inayotajwa na Polisi kuwa ni ya uchochezi inahusu malalamiko ya mkazi wa Chwaka, Ramadhan Mohamed Vuai ambaye amefungua kesi Mahakama ya Ardhi ya Zanzibar kudai kurejeshewa kiwanja alichokipata kwa njia ya urithi na akiwa na hati halali za serikali.



Vuai anamshitaki Mkurugenzi wa Idara ya Ardhi na Usajili anayedaiwa kupima kiwanja kwenye eneo la mlalamikaji na kuwapatia kampuni ya Gapco waliojenga kituo cha mafuta hapo.

Mdaiwa mwingine ni Meneja wa Gapco aliyepo Zanzibar .



Miongoni mwa vielelezo vya mlalamikaji huyo ambaye kesi yake imekwama mara mbili kusikilizwa kutokana na dharura ya Mwenyekiti wa Mahakama ya Ardhi, ni barua aliyomuandikia Rais Amani Abeid Karume kumtaka amgawie sehemu ya hisa 30 alizopewa na Gapco baada ya kutoa kiwanja hicho.



Maelezo ya hati hiyo yanaonyesha kuwa mdai huyo alielezwa taarifa za kuwa Rais Karume ndiye aliyekitoa.



"Kwa masikitiko makubwa ninaandika barua hii ili kuomba sehemu ya hisa ambayo unayoipata kutoka katika sheli hiyo ya Chwaka, ukizingatia mimi ndiye niliyekuwa nikiendesha maisha yangu hapo kwa ajili ya kilimo.



"Hisa hiyo niliidai hapo mwanzo nilipovamiwa kwa ujenzi wa sheli hiyo, nikaambiwa siwezi kuipata hisa hiyo kwa sababu wewe unapata sehemu fulani ya hisa."



Mdai huyo ametaja majina ya watu aliodai walimpa taarifa hizo: Ali Sadi wa Gapco na mwenzake aitwaye January, Mwalim Talib ambaye ni Ofisa Tawala Wilaya ya Kati na Nassor (NICO) ambaye ni Ofisa Mipango, Wilaya ya Kati.



Kukamatwa kwa mwandishi huyo ni mfululizo wa vitendo vya vitisho vinavyotokea hapa dhidi ya waandishi wa habari wa vyombo binafsi. Waandishi kadhaa wamewahi kukamatwa, wengine wakifunguliwa mashitaka yakiwemo ya kuteka nyara mwanamke wakati wa harakati za uchaguzi wa 2000. aliachiwa baada ya Hakimu kuikataa kesi hiyo mara baada ya kufikishwa mahakamani. Mwandishi wa habari hizi aliwahi kufungiwa kufanya kazi Mei 2005 kwa kukosa kitambulisho kinachotolewa na Idara ya Habari (Maelezo) ya Zanzibar .



Mwandishi mwingine, Salma Said Humoud wa Mwananchi Communication, aliwahi kufuatwafuatwa mara kadhaa na maofisa Usalama wa Taifa na Idara ya Uhamiaji akidaiwa si raia.



Mwandishi wa siku nyingi aliyewahi kuwa Katibu wa Waziri Kiongozi na baadaye Katibu wa Makamu wa Rais, Ali Mohamed Nabwa, aliwahi kuvuliwa uraia wake na alikuwa hajarejeshewa mpaka alipofariki dunia Februari mwaka jana.



Alifariki dunia baada ya kuugua kwa muda na aliwahi kusema kwamba kadhia hiyo ilichangia kudhoofisha afya yake. Alikuwa Mhariri Mtendaji wa Dira aliloanza kulifanyia kazi baada ya kustaafu serikalini.



Magazeti kadhaa yanayochapishwa na kampuni zilizosajiliwa Tanzania Bara, yamewahi kufungiwa kusambazwa hapa. Mwaka 2004 Sserikali ililifungia gazeti pekee binafsi, Dira na baadaye likakataliwa kusajiliwa upya licha ya Mahakama Kuu kuamuru hivyo katika hukumu ya kesi iliyofunguliwa na kampuni miliki ya gazeti hilo ya kupinga kufungiwa.



Hukumu ya Mahakama Kuu haikusema kuwa gazeti limekosea chochote katika kazi yake, bali halikuwa limesajiliwa kihalali. Mahakama ilitaka wamiliki wakate rufani au waombe upya kusajili gazeti hilo .



Wakati maombi ya usajili mpya yakiwa serikalini, Waziri wa Habari, Ali Juma Shamhuna alisema ndani ya Baraza la Wawakilishi kwamba gazeti hilo si tu limefungiwa, "limezikwa kabisa."

Ends.
 
Na jabir idrissa, Zanzibar

Jeshi la Polisi limeshindwa kumfungulia mashitaka mwandishi wa habari wa kampuni ya The Guardian Limited, Mwinyi Sadallah, na badala yake ametakiwa kuripoti kituo kikuu cha polisi kila Jumatatu asubuhi.

Hakuna muda maalum uliowekwa wa mwandishi huyo kuwa anaripoti kituoni Mwembemadema yalipo makao makuu ya Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi.

Sadallah ambaye amekuwepo hapa kwa miaka 11 sasa akifanya kazi ya uandishi wa habari chini ya kampuni hiyo, alipewa amri hiyo jana baada ya kufika kituoni hapo saa 3 asubuhi kama alivyotakiwa Ijumaa ya wiki iliyopita alipoachiwa kwa dhamana ya wadhamini wawili, akiwemo binafsi, kila mmoja akisaini dhamana ya maandishi ya sh milioni moja.

Alikamatwa Oktoba 26 akiwa ofisini kwake Weles, Kikwajuni, na kufikishwa Mwembemadema alikotakiwa kusaini hati ya mashitaka akidaiwa kuwa amefanya uchochezi kwa kuandika habari zilizomhusu Rais Amani Abeid Karume zikisema kuwa ameuza kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mafuta kinachomilikiwa na kampuni ya Gapco.

Alipofika jana alitakiwa tena kusaini hati hiyo, lakini aliposhikilia kukataa, safari hii akiwa na wakili Hamidu Mbwezeleni wa mjini hapa, alichukuliwa alama za vidole na kujazwa kwenye fomu nne tofauti kabla ya kuamriwa kutoka na kufuatana na maofisa wa Idara ya Upelelezi ya Mkoa hadi Makao Makuu ya Polisi Kilimani.

Wakili huyo alisisitiza kuwa raia ana haki ya kukataa kusaini hati ya Polisi na kutoa maelezo yoyote na kwamba ni sheria kusema kuwa atafanya hivyo mbele ya Mahakama.

Kutoka Mwembemadema, Sadallah alipelekwa kitengo cha picha na kupigwa picha mara mbili ambazo hakuelezwa zinatumika kwa ajili ya kitu gani.

Baada ya kitendo hicho, alielezwa kwamba yuko huru isipokuwa atahitajika kuripoti kituoni Mwembemadema, kila Jumatatu saa 3 asubuhi. Atakapofika, aonane na ofisa upelelezi aitwaye Khatib Juma na asipokuwepo amuone Koplo Abbas au Mwita.

Wiki iliyopita, Sadallah baada ya kufika kituoni, aliambiwa kuwa atashitakiwa chini ya Sheria ya Magazeti ya mwaka 1988 ya Zanzibar . Kifungu kinachozungumzia habari za uchochezi, kinasema mtu akitiwa hatiani kwa kosa hilo , anaweza kuhukumiwa kifungo cha hadi miaka mitatu jela.

Habari alizoandika mwandishi huyo na kuchapishwa kwenye toleo la Nipashe la Septemba 24, mwaka huu, zilitokana na malalamiko ya mwananchi mkazi wa Chwaka, Ramadhan Mohamed Vuai, dhidi ya kuporwa kiwanja chake cha urithi kilichopo eneo la Kipilipilini ambacho sasa pana kituo cha mafuta cha Gapco.

Kwa mujibu wa habari hizo, mwananchi huyo alieleza kuwa amelazimika kufungua kesi kwenye Mahakama ya Ardhi ya Zanzibar kudai haki yake ya kumiliki ardhi ambayo imeporwa bila ya idhini yake, hatua iliyokwenda kinyume na sheria.

Katika malalamiko hayo, Vuai anadai kuwa alipofuatilia kiwanja chake kwa kampuni ya Gapco, walimweleza kwamba wao hawawezi kumsaidia kwa lolote kati ya madai yake, kwa kuwa wamepata eneo hilo kwa idhini ya Rais Karume ambaye walidai ananufaika na asilimia 30 ya biashara.

Mwananchi huyo aliamua kumuandikia Rais Karume binafsi, akimuomba amgawie sehemu ya asilimia hiyo ili naye anufaike na eneo hilo ambalo amekuwa akilitegemea kwa maisha yake.

Hakupata majibu ya barua hiyo na badala yake baadhi ya maofisa wa Ikulu walimtaka asifuatilie tena hapo kwa kumueleza kuwa Rais hahusiki na suala hilo .

Barua aliyomuandikia Rais Karume, ni moja ya vielelezo vyake katika kesi aliyofungua akiomba mahakama ibatilishe umiliki wa kiwanja hicho na kumrudishia kwa sababu ana hati halali za kukimiliki.

Ametaka kituo hicho kivunjwe kwa amri ya mahakama hiyo, alipwe fidia ya asilimia 30 ya mauzo yaliyokwishafanyika hapo, tangu kituo kilipoanza kutoa huduma. Kesi hiyo namba 67 ya mwaka 2007, haijaanza kusikilizwa.
Ends
 
Duh wapendwa huu Uzi ulikuwa kwenye kapu la Nani?? .... Watu kwa kufufua nyuzi zilizokufa hamfai
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom