Rejao
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 9,220
- 4,056
POLISI katika Kanda Maalumu ya Tarime-Rorya, wamemkamata raia wa Marekani kwa tuhuma za kupiga picha maiti za mauaji ya mgodini Tarime na kuzituma nje ya nchi bila kibali.
Joyceline Tembi anayehisiwa kutumiwa na wafadhili wa nje wa vyama vya upinzani nchini, anadaiwa kuingia nchini kama mtalii akitoka Uganda.
Alikutwa akiongozana na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika vurugu zilizotokana na mauaji ya watu hao yaliyofanywa na polisi baada ya kuvamia Mgodi wa North Mara Barrick.
Kamanda wa Polisi wa Tarime na Rorya, Costantine Massawe alisema jana kuwa Joyceline alikutwa akipiga picha za matukio ya vurugu zikiwemo miili ya watu wanne kati ya watano waliouawa wakati kundi la watu zaidi ya 800 walipovamia mgodi huo wa Nyamongo.
Ameonekana akiongozana na wafuasi wa Chadema kila mahali, hali inayofanya tumtilie mashaka, iweje huyu mtalii aongozane na wafuasi wa Chadema? alihoji Kamanda Massawe.
Kwa mujibu wa Kamanda Massawe, Joyceline ambaye baada ya kuhojiwa, alidai kuwa yeye ni mwandishi wa habari anayefanya kazi nchini Uganda na Marekani, alipiga picha hizo katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Tarime.
Marehemu hao ni Chacha Ngoka wa Kewanja, Nyamongo, Emmanuel Magige wa Nyakunguru, Mwikwabe Marwa na Chawali Bhoke; wote wa Mugumu Serengeti.
Mbali na picha za maiti hao, Joyceline pia anadaiwa kufika katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime juzi na kupiga picha watuhumiwa wa uchochezi akiwemo Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) na watuhumiwa wenzake saba.
Washitakiwa wengine katika kesi hiyo iliyofikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Mei 24 ni Mwita Waitara (36), Mwita Maswi (48), Abdalah Suleman Sauti (31), Stanslaus Nyembea (33) na Underson Chacha (35) ambao ni wakazi wa Tarime.
Wengine ni Andrew Andalunyandu (63) na Irahim Juma (27) ambao ni wakazi wa Singida. Baadaye Joyceline anadaiwa alipiga picha baadhi ya majengo ya Serikali ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Tarime na kutuma baadhi ya picha hizo nje ya nchi.
Kamanda Massawe alisema Joyceline mwenye hati ya kusafiria ya Marekani iliyoandikishwa Aprili mwaka huu, anaendelea kuhojiwa na polisi pamoja na maofisa uhamiaji wilayani hapa kutokana na ujio wake huo wenye utata.
Kamanda Massawe alisema hati ya kusafiria ya Joyceline namba 7100566100, inaonesha aliingia nchini Mei mosi mwaka huu 2011 na kuondoka na baadaye akarudi tena Mei 22 na kuanza kupiga picha za matukio hayo ya vurugu na maiti.
Ofisa Uhamiaji wa Wilaya ya Tarime, Isack Mayeka amethibitisha kukamatwa na kuhojiwa kwa Joyceline na kuongeza kuwa hata kama ni Mwandishi wa Habari, hakupaswa kufanya kazi ya uandishi katika nchi nyingine kabla hajajulisha vyombo vya usalama.
Mayeka alisema Joyceline pia alitakiwa kutoa taarifa kwa Idara ya Habari (MAELEZO) au Baraza la Habari Tanzania (MCT) na kufuata utaratibu wa nchi husika.
Alisema kwa kitendo hicho cha Joyceline kuingia nchini na kuanza kupiga picha za matukio hayo bila kutaarifu idara na mamlaka husika, kinatia shaka ujio wake hapa nchini.
Mayeka alisema yeye na maofisa wengine wa Polisi wanaendelea kumhoji zaidi mwanamke huyo kuhusu ujio wake nchini kwa kuwa anatia shaka huenda anatumiwa na vyama vya upinzani na wafadhili wa baadhi ya vyama hivyo.
Wakati huo huo, Mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwine (CCM) amewapiga marufuku wanasiasa wachochezi kufika jimboni humo kwa sababu wanazorotesha kasi ya maendeleo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Nyangwine alisema hawezi kuwavumilia wanasiasa wa aina hiyo na kuwataka wakae kwenye maeneo yao ili walete maendeleo.
Alisema, muda wa kampeni na ushindani wa kisiasa umekwisha hivyo kila mmoja aelekeze nguvu zake kwenye shughuli za maendeleo na kutekeleza ahadi walizotoa.
Wilaya ya Tarime inayo mamlaka kamili ya kujitegemea kama serikali, sasa nawataka wanasiasa na wabunge wa upinzani watuache, matatizo ya Tarime tunayatatua wenyewe hatutaki kuingiliwa.
Naomba wananchi wa Tarime waniunge mkono katika hili nataka tukae tushikamane kuleta maendeleo na kutekeleza ahadi nilizotoa wakati naomba ridhaa yenu.
Sitakubali kuwaona watu wanakuja kutuvuruga kama wanataka kuja kwetu waje kwa shughuli za maendeleo na sio vinginevyo, alisema Mbunge huyo ambaye hivi karibuni msafara wake ulishambuliwa kwa mawe na wanachi aliodai kwamba wameshawishiwa na wanasiasa wengine.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa wazee wa mila wilayani humo, Enock Chambiri alisema wanalaani kitendo cha baadhi ya wananchi kuushambulia kwa mawe msafara wa mbunge wao.
Alisema wananchi wa Tarime hawana desturi ya kuwapiga viongozi wao na kubainisha kwamba kilichotokea ni ushawishi na msukumo wa kisiasa.
Kwa niaba ya wazee 26 wanaowakilisha koo 13 kule Tarime na serikali kwa upande mwingine, tunalaani kitendo cha baadhi ya wanasiasa kutumia muda wao kulivuruga jimbo letu, alisema Chambiri.
Katika hatua nyingine, CCM imeitaka Serikali kufanya uchunguzi wa kina wa vifo na mazingira ya vifo hivyo vya Tarime na pia itafute ufumbuzi wa kudumu wa migogoro inayotokea mara kwa mara kati ya wananchi wanaozunguka migodi na wawekezaji.
Hata hivyo, Chama Cha Mapinduzi kilaani vikali tabia iliyojionyesha dhahiri kwa baadhi ya wanasiasa nchini kuvifanya vifo vya Watanzania wenzetu kuwa mtaji wa kisiasa, ilieleza taarifa ya Idara ya Itikadi na Uenezi Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM jana.
SOURCE: HABARI LEO 27/05/2011
Joyceline Tembi anayehisiwa kutumiwa na wafadhili wa nje wa vyama vya upinzani nchini, anadaiwa kuingia nchini kama mtalii akitoka Uganda.
Alikutwa akiongozana na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika vurugu zilizotokana na mauaji ya watu hao yaliyofanywa na polisi baada ya kuvamia Mgodi wa North Mara Barrick.
Kamanda wa Polisi wa Tarime na Rorya, Costantine Massawe alisema jana kuwa Joyceline alikutwa akipiga picha za matukio ya vurugu zikiwemo miili ya watu wanne kati ya watano waliouawa wakati kundi la watu zaidi ya 800 walipovamia mgodi huo wa Nyamongo.
Ameonekana akiongozana na wafuasi wa Chadema kila mahali, hali inayofanya tumtilie mashaka, iweje huyu mtalii aongozane na wafuasi wa Chadema? alihoji Kamanda Massawe.
Kwa mujibu wa Kamanda Massawe, Joyceline ambaye baada ya kuhojiwa, alidai kuwa yeye ni mwandishi wa habari anayefanya kazi nchini Uganda na Marekani, alipiga picha hizo katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Tarime.
Marehemu hao ni Chacha Ngoka wa Kewanja, Nyamongo, Emmanuel Magige wa Nyakunguru, Mwikwabe Marwa na Chawali Bhoke; wote wa Mugumu Serengeti.
Mbali na picha za maiti hao, Joyceline pia anadaiwa kufika katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime juzi na kupiga picha watuhumiwa wa uchochezi akiwemo Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) na watuhumiwa wenzake saba.
Washitakiwa wengine katika kesi hiyo iliyofikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Mei 24 ni Mwita Waitara (36), Mwita Maswi (48), Abdalah Suleman Sauti (31), Stanslaus Nyembea (33) na Underson Chacha (35) ambao ni wakazi wa Tarime.
Wengine ni Andrew Andalunyandu (63) na Irahim Juma (27) ambao ni wakazi wa Singida. Baadaye Joyceline anadaiwa alipiga picha baadhi ya majengo ya Serikali ikiwemo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Tarime na kutuma baadhi ya picha hizo nje ya nchi.
Kamanda Massawe alisema Joyceline mwenye hati ya kusafiria ya Marekani iliyoandikishwa Aprili mwaka huu, anaendelea kuhojiwa na polisi pamoja na maofisa uhamiaji wilayani hapa kutokana na ujio wake huo wenye utata.
Kamanda Massawe alisema hati ya kusafiria ya Joyceline namba 7100566100, inaonesha aliingia nchini Mei mosi mwaka huu 2011 na kuondoka na baadaye akarudi tena Mei 22 na kuanza kupiga picha za matukio hayo ya vurugu na maiti.
Ofisa Uhamiaji wa Wilaya ya Tarime, Isack Mayeka amethibitisha kukamatwa na kuhojiwa kwa Joyceline na kuongeza kuwa hata kama ni Mwandishi wa Habari, hakupaswa kufanya kazi ya uandishi katika nchi nyingine kabla hajajulisha vyombo vya usalama.
Mayeka alisema Joyceline pia alitakiwa kutoa taarifa kwa Idara ya Habari (MAELEZO) au Baraza la Habari Tanzania (MCT) na kufuata utaratibu wa nchi husika.
Alisema kwa kitendo hicho cha Joyceline kuingia nchini na kuanza kupiga picha za matukio hayo bila kutaarifu idara na mamlaka husika, kinatia shaka ujio wake hapa nchini.
Mayeka alisema yeye na maofisa wengine wa Polisi wanaendelea kumhoji zaidi mwanamke huyo kuhusu ujio wake nchini kwa kuwa anatia shaka huenda anatumiwa na vyama vya upinzani na wafadhili wa baadhi ya vyama hivyo.
Wakati huo huo, Mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwine (CCM) amewapiga marufuku wanasiasa wachochezi kufika jimboni humo kwa sababu wanazorotesha kasi ya maendeleo.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Nyangwine alisema hawezi kuwavumilia wanasiasa wa aina hiyo na kuwataka wakae kwenye maeneo yao ili walete maendeleo.
Alisema, muda wa kampeni na ushindani wa kisiasa umekwisha hivyo kila mmoja aelekeze nguvu zake kwenye shughuli za maendeleo na kutekeleza ahadi walizotoa.
Wilaya ya Tarime inayo mamlaka kamili ya kujitegemea kama serikali, sasa nawataka wanasiasa na wabunge wa upinzani watuache, matatizo ya Tarime tunayatatua wenyewe hatutaki kuingiliwa.
Naomba wananchi wa Tarime waniunge mkono katika hili nataka tukae tushikamane kuleta maendeleo na kutekeleza ahadi nilizotoa wakati naomba ridhaa yenu.
Sitakubali kuwaona watu wanakuja kutuvuruga kama wanataka kuja kwetu waje kwa shughuli za maendeleo na sio vinginevyo, alisema Mbunge huyo ambaye hivi karibuni msafara wake ulishambuliwa kwa mawe na wanachi aliodai kwamba wameshawishiwa na wanasiasa wengine.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa wazee wa mila wilayani humo, Enock Chambiri alisema wanalaani kitendo cha baadhi ya wananchi kuushambulia kwa mawe msafara wa mbunge wao.
Alisema wananchi wa Tarime hawana desturi ya kuwapiga viongozi wao na kubainisha kwamba kilichotokea ni ushawishi na msukumo wa kisiasa.
Kwa niaba ya wazee 26 wanaowakilisha koo 13 kule Tarime na serikali kwa upande mwingine, tunalaani kitendo cha baadhi ya wanasiasa kutumia muda wao kulivuruga jimbo letu, alisema Chambiri.
Katika hatua nyingine, CCM imeitaka Serikali kufanya uchunguzi wa kina wa vifo na mazingira ya vifo hivyo vya Tarime na pia itafute ufumbuzi wa kudumu wa migogoro inayotokea mara kwa mara kati ya wananchi wanaozunguka migodi na wawekezaji.
Hata hivyo, Chama Cha Mapinduzi kilaani vikali tabia iliyojionyesha dhahiri kwa baadhi ya wanasiasa nchini kuvifanya vifo vya Watanzania wenzetu kuwa mtaji wa kisiasa, ilieleza taarifa ya Idara ya Itikadi na Uenezi Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM jana.
SOURCE: HABARI LEO 27/05/2011