mzee naona unazinduka baada ya viroba vya janaNalipa pongezi gazeti la Majira kwa kuandika habari za ukweli na uhakika.
Ni kweli wahuni wa CDM wanataka kuleta machafuko nchini wananchi wapenda amani hatuwezi kukubaliana na huo upuuzi
<br />Nalipa pongezi gazeti la Majira kwa kuandika habari za ukweli na uhakika.<br />
Ni kweli wahuni wa CDM wanataka kuleta machafuko nchini wananchi wapenda amani hatuwezi kukubaliana na huo upuuzi
.Mwandishi kazungumza ukweli kabisa.Kama uko mpinzan ukikosea nawe ukubali kukosolewa.Watz hawapaswi kusamehe upuuzi wa CDM wa kujichukulia sheria mkononi hasa vijana wa kiume kumshambulia na kumkamata mama wa kike.Chama cha siasa tangu lini kikawa na makamanda?,hapo mwandishi ndio anasema CDM mnakoelekea ni kubaya.Kumvua mama hijabu mmedhihirisha kuwa padre anachuki na uislam na waislam hatutawasamehe kamwe labda mtuombe radhi.
<br /><b>CHADEMA kwa hili mmechemka</b><br /><br /><br />
<br />
Na Gladness Mboma<br />
<br />
ALHAMISI ya wiki iliyopita wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walimkamata Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bi. Fatma Kimario kwa<br />
madai kuwa walimkuta akifanya kikao na viongozi wa vijiji na kata ndani ya ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Isakamaliwa.<br />
<br />
Kwanza kabisa kwa mtazamo wangu CHADEMA walichofanya ni makosa lisha ya kwamba walimdhalilisha kiongozi wa wananchi kwa kumvuta huku na huko huku wakitambua wazi kwamba kufanya hivyo ni kosa la jinai.<br />
<br />
Kosa ambalo ama hakika bila ushabiki wowote wahusika wote wanapaswa kushtakiwa na kuchukuliwa hatua za kisheria haraka iwezekanavyo.<br />
<br />
Ni hoji kwanza, hivi hawa wahuni wanaojiita makomandoo wa CHADEMA wameenda Igunga kwa misingi ya kumnadi mgombea wao ama kumdhalilisha kiongozi aliyewekwa madarakani na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.<br />
<br />
Awali nilikuwa ninawakubali CHADEMA kutokana na sera zao za kuleta maendeleo lakini kwa uhuni huu uliofanywa na wanachama hao Igunga katu siwezi kusita kutamka kwamba wakipata nafasi ya kutawala nchi hii awachelewi kuwanyanyasa Watanzania kijinsia.<br />
<br />
Tuzingatie kwamba, Bi. Kimario ni kiongozi wa nchi hawakustahili kumdhalilisha kiasi hicho, tena kibaya zaidi wanaume ndio waliohusika kumvuta mama huyo huku na huko kama mwizi.<br />
<br />
Haiwezekani hizi ni vurugu ambazo zinatakiwa kupigwa vita na kukemewa kwa nguvu zote ina maana kiongozi ana mipaka ya kufanya mikutano?<br />
<br />
Huyu ni kiongozi ana haki ya kufanya kikao mahali popote muda wowote na wananchi wake bila kubuguziwa ili mradi asivunje sheria.<br />
<br />
Ina maana wakati huu kampeni za uchaguzi mdogo unaoendelea Igunga kiongozi yoyote wa serikali hatakiwa kufanya kikao na wananchi wake kwa kuhofia kuwa anapanga njama za ushindi wa chama fulani.<br />
<br />
CHADEMA sasa mnakoelekea ni kubaya mlikuwa mnakwenda vizuri sasa vurugu zenu na ubabe wenu ndio utakaowakosesha kura na wala si vinginevyo.<br />
<br />
Kwani mkifanya siasa na kampeni za ustaarabu hamtaonekana ndani ya jamii ama hadi kila siku muwe na jambo jipya linaloonesha udhalilishaji kwa ili nidhiriki kutamka kwamba wapumbavu siku zote huwa wanajitwalia makaa ya moto wenyewe hivyo siwafichi kwa stahili hii mnajiangusha wenyewe na mnajiua wenyewe.<br />
<br />
Vurugu hazipendezi hata kidogo, huyu Mkuu wa Wilaya ana haki ya kufanya mkutano au kikao na viongozi wake kwa sababu kwa ni haki yake ya msingi ili kuharakisha maendeleo ya wananchi.<br />
<br />
Katika suala hili hakuna ubishi ni lazima mchukuliwe hatua, watu waliomkamata na kumdhalilisha ni lazima sheria ichukue mkondo wake huu ni ukosefu wa nidhamu.<br />
<br />
Hii ni hatari kwa maana hiyo kiongozi yoyote wa serikali wa Wilaya ya Igunga asifanye chochote kwa kuhofia vyama vya upinzani, jamani tuacha mawazo mgando huu ni uhuni kama siyo ujinga katika vichwa vya watu walioelimika.<br />
<br />
Hata kama huyo mama alikwenda kinyume, lakini hakustahili kufanyiwa kitendo hicho hata kidogo ni udhalilishaji.
.Ni kweli mhalifu yeyote anastahili kuchukuliwa hatua. Ni kweli kila raia wa Tanzania anawajibu wa juzuia au kutoa taarifa pale anapoona kuwa jinai inataka kufanyika. lakini zipo taratibu za kumchukuliwa mhalifu na haufanani na utaratibu uliochukuliwa na makomandoo wa CHADEMA. Hivi kweli tunafika mahali tunashindwa kuwaheshimu viongozi wetu mpaka tunawavua nguo barabarani. mtu mwenye akili timamu akielezwa eti hizi ndizo taratibu za kumchukulia Mkuu wa wilaya wa kike atakuelewa kweli. pamoja na itikadi lazima tujenge utamaduni wa kukemea maovu hata kama yametendwa na sisi wenyewe. hebu tufundishane ustaarabu hapa. Ni rahisi sana kujisafisha katika hili kwa kiongozi wa kitaifa kusimama jukwaani na kuwaomba radhi. Watanzania ni waelewa sana badala ya kuendeleza ubabe.
nani kakwambia kama kavuliwa nguo? kuna mambo mengine unatakiwa upime kwa akili zako kichwa naz wewe,sio kila kitu upigie mstari pasipokutafakari,Ni kweli mhalifu yeyote anastahili kuchukuliwa hatua. Ni kweli kila raia wa Tanzania anawajibu wa juzuia au kutoa taarifa pale anapoona kuwa jinai inataka kufanyika. lakini zipo taratibu za kumchukuliwa mhalifu na haufanani na utaratibu uliochukuliwa na makomandoo wa CHADEMA. Hivi kweli tunafika mahali tunashindwa kuwaheshimu viongozi wetu mpaka tunawavua nguo barabarani. mtu mwenye akili timamu akielezwa eti hizi ndizo taratibu za kumchukulia Mkuu wa wilaya wa kike atakuelewa kweli. pamoja na itikadi lazima tujenge utamaduni wa kukemea maovu hata kama yametendwa na sisi wenyewe. hebu tufundishane ustaarabu hapa. Ni rahisi sana kujisafisha katika hili kwa kiongozi wa kitaifa kusimama jukwaani na kuwaomba radhi. Watanzania ni waelewa sana badala ya kuendeleza ubabe.
ukimaliza kachukue mgao wakoNaheshimu sana siasa za ushindani...hasa ushindani wa hoja. Nilishtuka sana kusikia yale wana CHADEMA waliyoyafanya kwa Mkuu wa Wilaya. Ni kitendo kibaya sana, na hasa ni picha mbaya sana kwa wale wapenda demokrasia ya ushindani. Hili ni kosa la jinai na waliohusika wote wanapaswa kushitakiwa bila kujali ni wafuasi wa CHADEMA au la. Kiungwana nilitegemea viongozi wa CHADEMA kuomba radhi kwa yale yaliyofanywa na wafuasi wao lakini kwa kuendelea kuwatetea wanaudhilishia umma wa watanzania kuwa wao sio wapenda amani na sio wastaarabu na hawana busara wapokuwa katika hali yenye changamoto kama ilivyo Igunga.
Ritz jaribu kuwa kama Ms si kila kitu kuponda pasipo kutafakari,mwangalie mwenzako maralia suguUjue tatizo ni hawa vijana wa CDM waliomwagwa jimboni Igunga, kutoka Kilimanjaro na Arusha, wamekwenda kuleta fujo.
Huko ni kujidanganya na sijui ni nani analipa gharama za chakula na malazi kwa vijana hawa zaidi ya 500 walioletwa na CDM
Nalipa pongezi gazeti la Majira kwa kuandika habari za ukweli na uhakika.
Ni kweli wahuni wa CDM wanataka kuleta machafuko nchini wananchi wapenda amani hatuwezi kukubaliana na huo upuuzi