Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Eric Nampesya, leo Ijumaa asubuhi alikamatwa na kuwekwa mbaroni baada ya kukorofishana na mkurugenzi wa jiji la Mwanza - kisa alienda kufuata reaction kwanini shule nyingi hazina vyoo vya kutosha?
Nampesya alifanya story iliyo-highlight watoto wa shule jijini Mwanza kujisaidia kwa shida kwasababu shule wanazosoma hazina mashimo ya kutosha ya vyoo. Story ya kwanza ilisikika Alhamisi na ya pili Ijumaa, lakini story hizo zenye kufichua uzembe, zimemponza.
Baadhi ya matatizo aliyoyaona ni shule tatu zilizo pamoja kuwa na jumla ya wanafunzi 3,680, lakini kuna mashimo ya vyoo 20 tu, kiasi kwamba watoto wanajisaidia kwa kushindwa kusubiri foleni ya kuingia kujisaidia.
Ingawa Nampesya ameachiwa jioni hii, ameshikiliwa na polisi kwa saa zaidi ya nne. Maelezo zaidi yatafuatia baadaye.
Nampesya alifanya story iliyo-highlight watoto wa shule jijini Mwanza kujisaidia kwa shida kwasababu shule wanazosoma hazina mashimo ya kutosha ya vyoo. Story ya kwanza ilisikika Alhamisi na ya pili Ijumaa, lakini story hizo zenye kufichua uzembe, zimemponza.
Baadhi ya matatizo aliyoyaona ni shule tatu zilizo pamoja kuwa na jumla ya wanafunzi 3,680, lakini kuna mashimo ya vyoo 20 tu, kiasi kwamba watoto wanajisaidia kwa kushindwa kusubiri foleni ya kuingia kujisaidia.
Ingawa Nampesya ameachiwa jioni hii, ameshikiliwa na polisi kwa saa zaidi ya nne. Maelezo zaidi yatafuatia baadaye.