Mwandishi Tanzania Daima atangaza kumng'oa Mramba

Tambara Bovu

JF-Expert Member
Dec 19, 2007
585
140
na Grace Macha, Rombo

MWANDISHI wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima, Edward Kinabo (29), ametangaza kuwania ubunge katika Jimbo la Rombo linaloshikiliwa na Basil Mramba.

Kinabo ambaye ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa, anawania kiti hicho kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Alitangaza azma hiyo jana alipokuwa akifanya mikutano ya hadhara kwenye tarafa za Tarakea, Useri na Mengwe akilenga kukiimarisha chama chake kuelekea uchaguzi mkuu.

Kinabo alisema amefikia uamuzi huo kuitikia wito wa wakazi wa kata mbalimbali za jimbo hilo waliomwomba agombee ubunge wakati akiwanadi wagombea wa CHADEMA walioshiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.

Mwanasiasa huyo kijana ambaye katika uchaguzi mkuu uliopita alikuwa meneja wa kampeni za mgombea ubunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA, John Mnyika, alisema ameamua kulikubali ombi hilo ili kutoa fursa kwa wananchi wa Rombo kupata mbunge kijana mwenye uwezo, unyenyekevu na usikivu wa kutosha kushughulikia matatizo na kero mbalimbali zinazowakabili vijana, wanawake na wazee wa jimbo hilo.

Akitangaza uamuzi wake huo aliouita kuwa ni zawadi ya mwaka mpya kwa wakazi wa Rombo, Kinabo alisema atatumia uzoefu wake wa kuwa mwanaharakati na kiongozi katika asasi zisizo za kiserikali (NGO’s), kushughulikia matatizo ya kijamii na kiuchumi likiwemo tatizo kubwa la umaskini wa kipato linalowakabili wakazi wengi wa jimbo hilo.

“Wazee wangu wa Mamsera, vijana wenzangu na mama zangu wa Mamsera, mimi Edward Edmund Kinabo leo natangaza rasmi kuwania ubunge wa Jimbo la Rombo, nimekubali kuwatumikia, uwezo huo ninao, msihofu nitawatumikia, endeleeni kuniunga mkono. Kwa pamoja tunaweza, kwa pamoja tutashinda,” alisema Kinabo huku akishangiliwa.

Aliyataja baadhi ya matatizo yaliyomsukuma kukubali ombi la kuwania kiti hicho kuwa ni pamoja na ukosefu wa ajira kwa vijana, uhaba wa huduma za maji, kudorora kwa kilimo cha kahawa, migogoro ya ardhi, uhaba wa shule bora na vifaa vya ufundishaji pamoja na tatizo la Halmashauri ya Wilaya ya Rombo kushindwa kutambua vipaumbele muhimu kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha, alisema ameamua kugombea ubunge kupitia CHADEMA ili kuongeza nguvu ya wabunge makini wa kambi ya upinzani katika kuwatetea wananchi wa Rombo na Watanzania wote kwa ujumla.

“Nimekuwa mwanachama wa CHADEMA kwa miaka sita sasa, nimelelewa na kujengwa kisiasa na chama hiki. Nimeiva kuwatumikia.

“Lakini wapo watu wanaojipitishapitisha wakisema Kinabo hafai ni mdogo. Hao ni washamba wa kisiasa, siasa za dunia zimebadilika…ni wakati wa Rombo kubadilisha historia na kujipatia mbunge kijana mwenye uwezo wa kuwatumikia. Kwa pamoja tutashinda,” alisema.

Katika mikutano hiyo, Kinabo alipokea wanachama wapya 150 na kuanzisha matawi mapya sita, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kukiimarisha chama hicho. ...


Kazi ipo kwa Mramba
 
Mhhhhh namtakia mafanikio mema kijana. Kweli ni wakati sasa watanzania tuangalie kushoto na kulia pia mbele na nyumaaaaaa.
Tumechoshwaaaaaaaa na MAFISADI!!!!!!!!!!
 
Kaka karibu...leta sera tusikie sie kule no longo longo. We are results oriented. Muulize mramba tulicho mfanya moja ya hizi chaguzi. Mwenyewe alikoma ndo maana akatoa machozi alipotetea hii lami tunayowekewa sasa.

Anyways karibu tuone utafanya nini!
 
Kaka karibu...leta sera tusikie sie kule no longo longo. We are results oriented. Muulize mramba tulicho mfanya moja ya hizi chaguzi. Mwenyewe alikoma ndo maana akatoa machozi alipotetea hii lami tunayowekewa sasa.

Anyways karibu tuone utafanya nini!

He!he!he!he!he!.....atawahakishia upatikanaji wa ndafu, mbege na kisusio....!
 
Mhhhhh namtakia mafanikio mema kijana. Kweli ni wakati sasa watanzania tuangalie kushoto na kulia pia mbele na nyumaaaaaa.
Tumechoshwaaaaaaaa na MAFISADI!!!!!!!!!!


Kwa kweli tumechoshwa na mafisadi.
 
Rombo CCM wataweka mtu atakewaletea uwaziri maendeleo yaje fasta, wafanyabiashara wao washamiri fasta.. Hakuna swala la CHADEMA rombo. They dont want to waste time alafu serikali ya JK iwawekee ngumu. CCM is the only thing in Rombo that can win. They operate in concert, wanakubaliana na mtu then wanampa kura. Mramba mwenyewe kidogo wamwage sema walijua ataleta uwaziri. CHADEMA no chance..sorry
 
mmh..ngoja tuyaoner ila where there is a will, the only limit is the sky!
 
Rombo CCM wataweka mtu atakewaletea uwaziri maendeleo yaje fasta, wafanyabiashara wao washamiri fasta.. Hakuna swala la CHADEMA rombo. They dont want to waste time alafu serikali ya JK iwawekee ngumu. CCM is the only thing in Rombo that can win. They operate in concert, wanakubaliana na mtu then wanampa kura. Mramba mwenyewe kidogo wamwage sema walijua ataleta uwaziri. CHADEMA no chance..sorry
Kwa mawazo haya kazi ya kuikomboa Tanzania safari bado ndefu, lakini ni kawaida kwenye vita no one to trust. Ukombozi wa kweli unahitaji kujituma na kuwa na mbinu mbalimbali na wanajeshi shupavu.
Pamoja tunaweza.
 
na Grace Macha, Rombo

MWANDISHI wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima, Edward Kinabo (29), ametangaza kuwania ubunge katika Jimbo la Rombo linaloshikiliwa na Basil Mramba.

Kinabo ambaye ni mchambuzi wa masuala ya kisiasa, anawania kiti hicho kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Alitangaza azma hiyo jana alipokuwa akifanya mikutano ya hadhara kwenye tarafa za Tarakea, Useri na Mengwe akilenga kukiimarisha chama chake kuelekea uchaguzi mkuu.

Kinabo alisema amefikia uamuzi huo kuitikia wito wa wakazi wa kata mbalimbali za jimbo hilo waliomwomba agombee ubunge wakati akiwanadi wagombea wa CHADEMA walioshiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.

Mwanasiasa huyo kijana ambaye katika uchaguzi mkuu uliopita alikuwa meneja wa kampeni za mgombea ubunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA, John Mnyika, alisema ameamua kulikubali ombi hilo ili kutoa fursa kwa wananchi wa Rombo kupata mbunge kijana mwenye uwezo, unyenyekevu na usikivu wa kutosha kushughulikia matatizo na kero mbalimbali zinazowakabili vijana, wanawake na wazee wa jimbo hilo.

Akitangaza uamuzi wake huo aliouita kuwa ni zawadi ya mwaka mpya kwa wakazi wa Rombo, Kinabo alisema atatumia uzoefu wake wa kuwa mwanaharakati na kiongozi katika asasi zisizo za kiserikali (NGO’s), kushughulikia matatizo ya kijamii na kiuchumi likiwemo tatizo kubwa la umaskini wa kipato linalowakabili wakazi wengi wa jimbo hilo.

“Wazee wangu wa Mamsera, vijana wenzangu na mama zangu wa Mamsera, mimi Edward Edmund Kinabo leo natangaza rasmi kuwania ubunge wa Jimbo la Rombo, nimekubali kuwatumikia, uwezo huo ninao, msihofu nitawatumikia, endeleeni kuniunga mkono. Kwa pamoja tunaweza, kwa pamoja tutashinda,” alisema Kinabo huku akishangiliwa.

Aliyataja baadhi ya matatizo yaliyomsukuma kukubali ombi la kuwania kiti hicho kuwa ni pamoja na ukosefu wa ajira kwa vijana, uhaba wa huduma za maji, kudorora kwa kilimo cha kahawa, migogoro ya ardhi, uhaba wa shule bora na vifaa vya ufundishaji pamoja na tatizo la Halmashauri ya Wilaya ya Rombo kushindwa kutambua vipaumbele muhimu kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha, alisema ameamua kugombea ubunge kupitia CHADEMA ili kuongeza nguvu ya wabunge makini wa kambi ya upinzani katika kuwatetea wananchi wa Rombo na Watanzania wote kwa ujumla.

“Nimekuwa mwanachama wa CHADEMA kwa miaka sita sasa, nimelelewa na kujengwa kisiasa na chama hiki. Nimeiva kuwatumikia.

“Lakini wapo watu wanaojipitishapitisha wakisema Kinabo hafai ni mdogo. Hao ni washamba wa kisiasa, siasa za dunia zimebadilika…ni wakati wa Rombo kubadilisha historia na kujipatia mbunge kijana mwenye uwezo wa kuwatumikia. Kwa pamoja tutashinda,” alisema.

Katika mikutano hiyo, Kinabo alipokea wanachama wapya 150 na kuanzisha matawi mapya sita, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kukiimarisha chama hicho. ...


Kazi ipo kwa Mramba
Huyo kijana amesha choka kuishi maisha ya Duniyani ,let wait and see I don`t want to cross the bridge before I get there .
 
- That is what we are talking about, ni vijana kujitokeza na kuingia in the game, saafi sana jamani mlio karibu naye tupeni kinachoendelea huyu kijana tumpe japo chochote katika kusaidia his dream, saafi sana Kinabo!

Respect.


FMEs!
 
Bwana Kinabo

Kila la kheri, lakini una mtihani mkubwa mbele yako. Pamoja na shutuma za Mramba yeye bado ana nafasi kule maana ana network ya watu wengi wakiwemo wa Dar ambao ndio huwa wanasupport wagombea. Pia una wakati mgumu wa kuwahamasisha wanarombo hasa ukuzingatia Mramba alivyokomaa mpaka barabara ikajengwa.

Kila la kheri ila utambue uzito wa kazi yako.
 
Bwana Kinabo

Kila la kheri, lakini una mtihani mkubwa mbele yako. Pamoja na shutuma za Mramba yeye bado ana nafasi kule maana ana network ya watu wengi wakiwemo wa Dar ambao ndio huwa wanasupport wagombea. Pia una wakati mgumu wa kuwahamasisha wanarombo hasa ukuzingatia Mramba alivyokomaa mpaka barabara ikajengwa.

Kila la kheri ila utambue uzito wa kazi yako.
Kha na kupulula kote kule bado ana nafasi? wajameni????
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom