Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mwandishi wa Habari na Mchambuzi wa michezo nchini wa kituo cha Radio EFM na TVE, Oscar Oscar leo Juni 9 2021 ameenda yalipo Makao Makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais katika Shirikisho hilo.
Mara baada ya kukabidhiwa fomu Oscar Oscar amesema baada ya kutoa maoni yake kwa muda mrefu ameona umefika wakati wa kuwania nafasi ya kuongoza Shirikisho la Mpira wa Miguu ili kuwa Mtendaji.
"Nimekuwa nikitoa maoni yangu kama Mwanahabari. Lakini sasa nimeona ni wakati mwafaka, kuwania nafasi hii ili kutekeleza mipango ambayo itaipeleka mbele soka letu la Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla". amesema Oscar.
Oscar Oscar amekuwa mgombea wa nne kuchukua fomu kwa ajili ya kuwania nafasi ya Urais katika Shirikisho hilo ambapo uchaguzi wa kikatiba unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi Agosti mwaka huu 2021.
Mara baada ya kukabidhiwa fomu Oscar Oscar amesema baada ya kutoa maoni yake kwa muda mrefu ameona umefika wakati wa kuwania nafasi ya kuongoza Shirikisho la Mpira wa Miguu ili kuwa Mtendaji.
"Nimekuwa nikitoa maoni yangu kama Mwanahabari. Lakini sasa nimeona ni wakati mwafaka, kuwania nafasi hii ili kutekeleza mipango ambayo itaipeleka mbele soka letu la Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla". amesema Oscar.
Oscar Oscar amekuwa mgombea wa nne kuchukua fomu kwa ajili ya kuwania nafasi ya Urais katika Shirikisho hilo ambapo uchaguzi wa kikatiba unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi Agosti mwaka huu 2021.