Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Saturday, 25 September 2010
MWANDISHI mwingine wa magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), amepata misukosuko kwenye kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mwandishi huyo Kwirinius Mapunda alipata mkasa huo, baada ya kuwekwa kizuizini mjini Songea, na walinzi wa CCM wakati wa ziara ya Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana (UVCCM) Ridhiwani Kikwete.
Ridhiwani alifika Songea mjini akitokea Namtumbo akifanya kazi ya kuomba kura kwa wagombea wa CCM.
Waandishi wengine wa Mwananchi ambao walishakumbwa na misukosuko katika kampeni za CCM ni Frederick Katulanda na Ray Naluyaga, wote wa Mwanza.
Katika tukio hilo Mapunda aliwekwa chini ya ulinzi na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya CCM mkoani Ruvuma, ambaye alimzuia kutekeleza majukumu yake
Mbali na kujitambulisha kuwa mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya mkoa, mtu huyo pia alidai kuwa ni mmoja wa mwanafamilia wa mgombea wa urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete.
Mara baada ya kuwasili kwa mgeni huyo wa UVCCM, mtu huyo alianza kumhoji mwandishi wa Mwananchi akitaka kujua ataandika nini kwenye ziara hiyo.
Mwandishi alimjibu kwamba ataandika atakayoyasikia na kuona na kwamba baada ya maelezo hayo , ofisa huyo alimtaka mwandishi wa habari apande gari alilokuwa akiliongoza yeye.
Msafara ulianzia ofisi ya CCM Mkoa wa Ruvuma na kwamba ulipofika ofisi ya CCM Wilaya ya Songea mjini, ofisa huyo alizidi kuwa karibu huku akimzonga wakati wa kupiga picha.
Ridhiwani Kikwete pamoja na wenyeji wake waliingia kwenye ukumbi ambapo, naye mwandishi aliingia.
Lakini ghafla baada ya muda mfupi kijana wa CCM aliyevalia mavazi yaliyoandikwa Green Guard, alifika na kumweleza mwandishi kwamba alikuwa akiitwa nje ya ukumbi.
Mwandishi alinyanyuka kwenda nje ambako hakumkuta mtu yeyote na kwamba alipochunguza zaidi aligundua kwamba gari alilopangiwa lilikuwa limeondoka likiwa na mfuko wake wa kamera na vifaa vingine.
Mapunda alianza kusaka namba ya simu ya ofisa wa CCM ambapo baadaye aliipata na kumpigia simu.
Ofisa wa CCM huyo alijibu kwamba gari analo na kwamba mzigo wake upo salama, lakini akasisitiza kwamba asubiri nje.
Mwandishi alipojaribu kuingia ndani , aliambiwa na vijana wa CCM kwamba haruhusiwi kuingia kwenye mkutano wa ndani jambo ambalo lilimshtua zaidi.
Lakini kibaya zaidi yule ofisa aliyetoweka na gari likiwa na mfuko wa mwandishi , naye hakurudi na baadaye alipiga simu kwamba mzigo wa mwandishi ulikuwa kwenye Hoteli Top In One iliyopo maeneo ya Msamala.
Kufuatia hali hiyo Mwandishi aligundua kwamba tukio lilikuwa la makusudi.
Katibu wa UVCCM wa Mkoa wa Ruvuma, Mwajuma Rashid, alipoulizwa kama anafahamu lolote juu ya tukiuo hilo alisema safari ya Ridhiwani Kikwete iliratibiwa na ofisi yake na kwamba aliyemsumbua mwandishi hakumuona.
http://joomladigger.com/
MWANDISHI mwingine wa magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), amepata misukosuko kwenye kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mwandishi huyo Kwirinius Mapunda alipata mkasa huo, baada ya kuwekwa kizuizini mjini Songea, na walinzi wa CCM wakati wa ziara ya Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza la Umoja wa Vijana (UVCCM) Ridhiwani Kikwete.
Ridhiwani alifika Songea mjini akitokea Namtumbo akifanya kazi ya kuomba kura kwa wagombea wa CCM.
Waandishi wengine wa Mwananchi ambao walishakumbwa na misukosuko katika kampeni za CCM ni Frederick Katulanda na Ray Naluyaga, wote wa Mwanza.
Katika tukio hilo Mapunda aliwekwa chini ya ulinzi na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya CCM mkoani Ruvuma, ambaye alimzuia kutekeleza majukumu yake
Mbali na kujitambulisha kuwa mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya mkoa, mtu huyo pia alidai kuwa ni mmoja wa mwanafamilia wa mgombea wa urais kupitia CCM, Jakaya Kikwete.
Mara baada ya kuwasili kwa mgeni huyo wa UVCCM, mtu huyo alianza kumhoji mwandishi wa Mwananchi akitaka kujua ataandika nini kwenye ziara hiyo.
Mwandishi alimjibu kwamba ataandika atakayoyasikia na kuona na kwamba baada ya maelezo hayo , ofisa huyo alimtaka mwandishi wa habari apande gari alilokuwa akiliongoza yeye.
Msafara ulianzia ofisi ya CCM Mkoa wa Ruvuma na kwamba ulipofika ofisi ya CCM Wilaya ya Songea mjini, ofisa huyo alizidi kuwa karibu huku akimzonga wakati wa kupiga picha.
Ridhiwani Kikwete pamoja na wenyeji wake waliingia kwenye ukumbi ambapo, naye mwandishi aliingia.
Lakini ghafla baada ya muda mfupi kijana wa CCM aliyevalia mavazi yaliyoandikwa Green Guard, alifika na kumweleza mwandishi kwamba alikuwa akiitwa nje ya ukumbi.
Mwandishi alinyanyuka kwenda nje ambako hakumkuta mtu yeyote na kwamba alipochunguza zaidi aligundua kwamba gari alilopangiwa lilikuwa limeondoka likiwa na mfuko wake wa kamera na vifaa vingine.
Mapunda alianza kusaka namba ya simu ya ofisa wa CCM ambapo baadaye aliipata na kumpigia simu.
Ofisa wa CCM huyo alijibu kwamba gari analo na kwamba mzigo wake upo salama, lakini akasisitiza kwamba asubiri nje.
Mwandishi alipojaribu kuingia ndani , aliambiwa na vijana wa CCM kwamba haruhusiwi kuingia kwenye mkutano wa ndani jambo ambalo lilimshtua zaidi.
Lakini kibaya zaidi yule ofisa aliyetoweka na gari likiwa na mfuko wa mwandishi , naye hakurudi na baadaye alipiga simu kwamba mzigo wa mwandishi ulikuwa kwenye Hoteli Top In One iliyopo maeneo ya Msamala.
Kufuatia hali hiyo Mwandishi aligundua kwamba tukio lilikuwa la makusudi.
Katibu wa UVCCM wa Mkoa wa Ruvuma, Mwajuma Rashid, alipoulizwa kama anafahamu lolote juu ya tukiuo hilo alisema safari ya Ridhiwani Kikwete iliratibiwa na ofisi yake na kwamba aliyemsumbua mwandishi hakumuona.
http://joomladigger.com/