Mwandishi Mbasha Assenga amnanga Anne Kilango na wenzake kwa kuitosa hoja ya ufisadi

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Katika gazatei la Mwanahalisi la leo, mwandishi Mbasha Asenga amewananga vilivyo wabunge wa CCM akina Anne Kilango, Ole Sendeka, James Lembeli na wengine ambao walijiweka mstari wa mbele katika hoja ya dhidi ya ufisadi – hoja ambayo waliipora kutoka Chadema.

Sasa hivi wabunge hao wameufyata na hoja hiyo ya ufisadi imebakia tena kwa Chadema.

Sehemu ya makala ya mwandishi huyo ni kama ifuatavyo:

"…Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 hoja ya vita dhidi ya ufisadi ilipoibuliwa na Chadema, wabunge wa CCM, akiwamo Anne Kilango wa Same Mashariki, walisimama na kuendesha kampeni ya kupora hoja hiyo.

"Walijitangaza kuwa ni makamanda wa kupambana dhidi ya ufisadi. Akizungumza bungeni kwa hisia kali, Kilango alisema hawezi kuwaachia wapinzani, akimtaja Zitto Kabwe (Chadema) kujitwalia umaarufu kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi.

"….walisimama kidete kupambana ukiwa ni mkakati wa kupiku Chadema ambao walionekana dhahiri kuungwa mkono na umma juu ya harakati zao za kupambana dhidi ya ufisadi. Umma kwa bahati mbaya ukaamini kundi hili la wanasiasa wa CCM, wakaaminika kuwa wanapambana kwa dhati ya mioyo yao. Lakini walikuja kushangazwa kundi hilo lilivyogeuka na kukimbia kabisa hoja walizokuwa wanasimamia."



My Take: Kwa ujumla makala ya mwandishi huyo ni 'must read.' Ni hakika akina Anne Kilango hawasikiki tena. Namkumbuka pale mama huyo alipotamka bungeni kwamba atahakikisha hela za EPA zinarudishwa kwa viroba, na siyo kwa karatasi. Jee 'viroba' hivyo aliviona na kujihakikishia? CCM bwana!
 
Katika gazatei la Mwanahalisi la leo, mwandishi Mbasha Asenga amewananga vilivyo wabunge wa CCM akina Anne Kilango, Ole Sendeka, James Lembeli na wengine ambao walijiweka mstari wa mbele katika hoja ya dhidi ya ufisadi – hoja ambayo waliipora kutoka Chadema.

Sasa hivi wabunge hao wameufyata na hoja hiyo ya ufisadi imebakia tena kwa Chadema.

Sehemu ya makala ya mwandishi huyo ni kama ifuatavyo:

“…Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 hoja ya vita dhidi ya ufisadi ilipoibuliwa na Chadema, wabunge wa CCM, akiwamo Anne Kilango wa Same Mashariki, walisimama na kuendesha kampeni ya kupora hoja hiyo.

“Walijitangaza kuwa ni makamanda wa kupambana dhidi ya ufisadi. Akizungumza bungeni kwa hisia kali, Kilango alisema hawezi kuwaachia wapinzani, akimtaja Zitto Kabwe (Chadema) kujitwalia umaarufu kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi.

“….walisimama kidete kupambana ukiwa ni mkakati wa kupiku Chadema ambao walionekana dhahiri kuungwa mkono na umma juu ya harakati zao za kupambana dhidi ya ufisadi. Umma kwa bahati mbaya ukaamini kundi hili la wanasiasa wa CCM, wakaaminika kuwa wanapambana kwa dhati ya mioyo yao. Lakini walikuja kushangazwa kundi hilo lilivyogeuka na kukimbia kabisa hoja walizokuwa wanasimamia.”



My Take: Kwa ujumla makala ya mwandishi huyo ni 'must read.' Ni hakika akina Anne Kilango hawasikiki tena. Namkumbuka pale mama huyo alipotamka bungeni kwamba atahakikisha hela za EPA zinarudishwa kwa viroba, na siyo kwa karatasi. Jee 'viroba' hivyo aliviona na kujihakikishia? CCM bwana!

Hakika makala hiyo ni superb. Mtazamo wangu ni kwamba Anne Kilango na wenzake walitishwa sana kukoseshwa Ubunge katika uchaguzi mwaka jana na wengi wa genge hilo laghai walipitishwa kugombea kwa hati hati tu. Usicheze na CCM. Chama hicho sasa kimefikia hatua ya kutumia ufisadi kama mtaji wao wa kisiasa (political capital) hasa katika kuwaweka mstarini wale ambao wanazidisha 'huu.'

Pia CCM imetumia ufisadi kuwanasa akina Mangula na Mkapa, na hata RA mwenyewe, kwenda Igunga kufanya kampeni. Hawa wametonywa kwamba wakikataa ufisadi wao utaweza kushughulikiwa na vyombo vya dola.
 
Nilijua tu walikuwa wanazungumza hayo with tongue in cheek. Ingefaa sasa waende tu Igunga wakawasaidie magamba wanaododa topeni.
 
Katika gazatei la Mwanahalisi la leo, mwandishi Mbasha Asenga amewananga vilivyo wabunge wa CCM akina Anne Kilango, Ole Sendeka, James Lembeli na wengine ambao walijiweka mstari wa mbele katika hoja ya dhidi ya ufisadi – hoja ambayo waliipora kutoka Chadema.

Sasa hivi wabunge hao wameufyata na hoja hiyo ya ufisadi imebakia tena kwa Chadema.

Sehemu ya makala ya mwandishi huyo ni kama ifuatavyo:

"…Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 hoja ya vita dhidi ya ufisadi ilipoibuliwa na Chadema, wabunge wa CCM, akiwamo Anne Kilango wa Same Mashariki, walisimama na kuendesha kampeni ya kupora hoja hiyo.

"Walijitangaza kuwa ni makamanda wa kupambana dhidi ya ufisadi. Akizungumza bungeni kwa hisia kali, Kilango alisema hawezi kuwaachia wapinzani, akimtaja Zitto Kabwe (Chadema) kujitwalia umaarufu kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi.

"….walisimama kidete kupambana ukiwa ni mkakati wa kupiku Chadema ambao walionekana dhahiri kuungwa mkono na umma juu ya harakati zao za kupambana dhidi ya ufisadi. Umma kwa bahati mbaya ukaamini kundi hili la wanasiasa wa CCM, wakaaminika kuwa wanapambana kwa dhati ya mioyo yao. Lakini walikuja kushangazwa kundi hilo lilivyogeuka na kukimbia kabisa hoja walizokuwa wanasimamia."



My Take: Kwa ujumla makala ya mwandishi huyo ni 'must read.' Ni hakika akina Anne Kilango hawasikiki tena. Namkumbuka pale mama huyo alipotamka bungeni kwamba atahakikisha hela za EPA zinarudishwa kwa viroba, na siyo kwa karatasi. Jee 'viroba' hivyo aliviona na kujihakikishia? CCM bwana!

Sitta kapewa uwaziri,mwakyembe kapewa uwaziri sasa unategemea nini?
 
Nadhani walitaka kupunguza kasi/popularity ya CDM walioasisi inshu hiyo. Hawakuwa na dhati mioyoni mwao thats why leo wako cool. Hata Shelukindo Beatrace inshu ya Jairo ni vile waliona Upinzani walishataka kuilipua so wakaiwahi otherwise utaratibu ule ndo wao miaka/bajeti zote
 
Kwenye CCM kuna upungufu mkubwa sana wa watu wenye kusimamia kweli, hapa mtu aweza kujitokeza akawa mbwabwajaji mkubwa na mwisho wa siku unamuona annywea kama puto lililotolewa hewa.

Unajua mtu kama Samweli sitta, Olesendeka, Mwakyembe, Anne Kilango, Beatrice Shelukindo, Job Ndugai, na wengine wengi tu hawana nia ya dhati bali ni unafiki tu wa kisiasa kwa manufaa yao binafsi. Kuitetea kweli kunahitaji dhamira ya kweli na si geresha.

Unajua kinachokosekana katika CCM ni watu wa aina ya Dk John Pombe Magufuli. Watu wa namna hii huwa hawapewi kabisa nafasi ya uongozi katika chama. Kwa kuwa wanahofiwa watakiweka chama kwa wananchi na hivyo kufanya mafisadi washindwe kukiteka. Kiukweli watu kama aina ya Dk Magufuli wapo wengi CCM lakini hawapewi nafasi.

CCM inahitaji sana uongozi thabiti na imara kwa sasa. Uongozi legelege kama wa sasa kwa kweli hatufiki popote. Hapa wanahitajika watu wenye mtazamo wa juu sana kuhusu kukijenga chama upya ili kiweze kukubalika kwa wananchi. Kujivua gamba peke yake hakutoshi kabisa.

Wakuu nawaacha na hii kuhusu uongozi
The mediocre teacher tells. The good teacher explain. The superior teacher demostrates. The great teacher inspires.
 
Katika gazatei la Mwanahalisi la leo, mwandishi Mbasha Asenga amewananga vilivyo wabunge wa CCM akina Anne Kilango, Ole Sendeka, James Lembeli na wengine ambao walijiweka mstari wa mbele katika hoja ya dhidi ya ufisadi – hoja ambayo waliipora kutoka Chadema.

Sasa hivi wabunge hao wameufyata na hoja hiyo ya ufisadi imebakia tena kwa Chadema.

Sehemu ya makala ya mwandishi huyo ni kama ifuatavyo:

“…Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 hoja ya vita dhidi ya ufisadi ilipoibuliwa na Chadema, wabunge wa CCM, akiwamo Anne Kilango wa Same Mashariki, walisimama na kuendesha kampeni ya kupora hoja hiyo.

“Walijitangaza kuwa ni makamanda wa kupambana dhidi ya ufisadi. Akizungumza bungeni kwa hisia kali, Kilango alisema hawezi kuwaachia wapinzani, akimtaja Zitto Kabwe (Chadema) kujitwalia umaarufu kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi.

“….walisimama kidete kupambana ukiwa ni mkakati wa kupiku Chadema ambao walionekana dhahiri kuungwa mkono na umma juu ya harakati zao za kupambana dhidi ya ufisadi. Umma kwa bahati mbaya ukaamini kundi hili la wanasiasa wa CCM, wakaaminika kuwa wanapambana kwa dhati ya mioyo yao. Lakini walikuja kushangazwa kundi hilo lilivyogeuka na kukimbia kabisa hoja walizokuwa wanasimamia.”



My Take: Kwa ujumla makala ya mwandishi huyo ni 'must read.' Ni hakika akina Anne Kilango hawasikiki tena. Namkumbuka pale mama huyo alipotamka bungeni kwamba atahakikisha hela za EPA zinarudishwa kwa viroba, na siyo kwa karatasi. Jee 'viroba' hivyo aliviona na kujihakikishia? CCM bwana!
Hili ni kundi la mitume kumi na mbili linaloongozwa na Mh.Samuel Sitta na privilage za cheo cha Nape na mission yao inajulikana ni kutwaa nafasi ya kumsimamisha mgombea wa mtandao wao kuwania urais. Ipo wazi waeanza kufurahiana na mafisadi kwa sababu historia zao na mwenendo wao unafanana na mafisadi na wamedhihirisha kuwa CCM bila mafisadi haiwezekani kwani bado wanashirikiana na mafisadi mfano mzuri ni Rostam ambaye ni fisadi na bado anatumiwa na ananyenyekewa na chama kupiga kampeni Igunga like Rostam alionewa. Na ile sera mama ya kujivua gamba imepotezewa kabisa. Tazama hapa:View attachment 37635
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom