Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Katika gazatei la Mwanahalisi la leo, mwandishi Mbasha Asenga amewananga vilivyo wabunge wa CCM akina Anne Kilango, Ole Sendeka, James Lembeli na wengine ambao walijiweka mstari wa mbele katika hoja ya dhidi ya ufisadi – hoja ambayo waliipora kutoka Chadema.
Sasa hivi wabunge hao wameufyata na hoja hiyo ya ufisadi imebakia tena kwa Chadema.
Sehemu ya makala ya mwandishi huyo ni kama ifuatavyo:
"…Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 hoja ya vita dhidi ya ufisadi ilipoibuliwa na Chadema, wabunge wa CCM, akiwamo Anne Kilango wa Same Mashariki, walisimama na kuendesha kampeni ya kupora hoja hiyo.
"Walijitangaza kuwa ni makamanda wa kupambana dhidi ya ufisadi. Akizungumza bungeni kwa hisia kali, Kilango alisema hawezi kuwaachia wapinzani, akimtaja Zitto Kabwe (Chadema) kujitwalia umaarufu kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi.
"….walisimama kidete kupambana ukiwa ni mkakati wa kupiku Chadema ambao walionekana dhahiri kuungwa mkono na umma juu ya harakati zao za kupambana dhidi ya ufisadi. Umma kwa bahati mbaya ukaamini kundi hili la wanasiasa wa CCM, wakaaminika kuwa wanapambana kwa dhati ya mioyo yao. Lakini walikuja kushangazwa kundi hilo lilivyogeuka na kukimbia kabisa hoja walizokuwa wanasimamia."
My Take: Kwa ujumla makala ya mwandishi huyo ni 'must read.' Ni hakika akina Anne Kilango hawasikiki tena. Namkumbuka pale mama huyo alipotamka bungeni kwamba atahakikisha hela za EPA zinarudishwa kwa viroba, na siyo kwa karatasi. Jee 'viroba' hivyo aliviona na kujihakikishia? CCM bwana!
Sasa hivi wabunge hao wameufyata na hoja hiyo ya ufisadi imebakia tena kwa Chadema.
Sehemu ya makala ya mwandishi huyo ni kama ifuatavyo:
"…Itakumbukwa kwamba mwaka 2007 hoja ya vita dhidi ya ufisadi ilipoibuliwa na Chadema, wabunge wa CCM, akiwamo Anne Kilango wa Same Mashariki, walisimama na kuendesha kampeni ya kupora hoja hiyo.
"Walijitangaza kuwa ni makamanda wa kupambana dhidi ya ufisadi. Akizungumza bungeni kwa hisia kali, Kilango alisema hawezi kuwaachia wapinzani, akimtaja Zitto Kabwe (Chadema) kujitwalia umaarufu kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi.
"….walisimama kidete kupambana ukiwa ni mkakati wa kupiku Chadema ambao walionekana dhahiri kuungwa mkono na umma juu ya harakati zao za kupambana dhidi ya ufisadi. Umma kwa bahati mbaya ukaamini kundi hili la wanasiasa wa CCM, wakaaminika kuwa wanapambana kwa dhati ya mioyo yao. Lakini walikuja kushangazwa kundi hilo lilivyogeuka na kukimbia kabisa hoja walizokuwa wanasimamia."
My Take: Kwa ujumla makala ya mwandishi huyo ni 'must read.' Ni hakika akina Anne Kilango hawasikiki tena. Namkumbuka pale mama huyo alipotamka bungeni kwamba atahakikisha hela za EPA zinarudishwa kwa viroba, na siyo kwa karatasi. Jee 'viroba' hivyo aliviona na kujihakikishia? CCM bwana!