Mentor
JF-Expert Member
- Oct 14, 2008
- 20,328
- 23,879
MWANAYUMBA (Inspired by Chege’s song – Mwanayumba)
Ilikuwa mwaka 2002 Desemba.
Nilikuwa kidato cha Sita katika shule moja ya kutwa huko Moshi mkoani Kilimanjaro. Nakumbuka tulivyokutana...nakumbuka kama ilikuwa jana.
Nakumbuka baba akiniambia nijiandae kumpeleka mdogo wangu hospitali KCMC kwa ajili ya kliniki ya ngozi. Ilikuwa ni siku yake ya kliniki. Kitengo hicho cha ngozi ndiyo kwanza kilikuwa kimeanzishwa na kilianza kuchukua umaarufu mkubwa hasa kwa wagonjwa waliokuwa wakitokea mikoa ya Karibu na Kilimanjaro. Ilikuwa ni ahueni kwa wagonjwa wengi kwani hawakuhitaji kwenda tena Muhimbili kwa ajili ya matibabu au kliniki tu ya ngozi.
Kesho yake tuliamka vizuri na tukiwa njiani mara akaanza kulalamika kwamba hatakutana na rafiki yake waliyekutana wakati wa kliniki iliyopita kwani hakuwa na uhakika kama walipangiwa tarehe moja ya kurudi. Nilipuuzia hilo na tukafika hospitali tukakuta foleni tayari hivyo kutufanya tuchukue namba 68.
Basi tukakaa kwenye mabenchi yale kila mtu na kitabu chake tunajisomea huku tukingoja zamu yake ifike. Mara ghafla nikamsikia mdogo wangu akiruka kwa furaha, "Yuleeee..." Sikumuelewa kwanza ila baada ya kutupa macho kuelekea mlango wa kuingilia ndipo nilipogundua kilichomtia mshawasha namna ile.
Ni binti mmoja mrembo, mchanganyiko wa kihabesh..si ndo Ethiopia huko??? sijui ila alikuwa binti mmoja mrembo, mwembamba kiasi, mrefu mwenye maumbile yenye kuelezeka. Binti kama kachorwa kisha kabanduliwa akapewa pumzi na uwezo wa kutembea. Kama picha ya darasani unayoweza kugusa na kusema hiki ni kiuno..na wanafunzi wakaelewa.
Walisalimiana kwa kukumbatiana kisha walikuja nilipokuwa nimeketi akanisalimia. Akajitambulisha, tabasamu lake...
Binti yule alienda kujiandikisha na kupewa namba 74 na kisha kuja kukaa na sisi. Tukaanza kuongea na kupiga hadithi za hapa na pale. Moyoni tayari nilishavutiwa na binti huyu ila sikuwa na jinsi hasa kwa sababu ya mdogo wangu lakini pia kwa sababu sikuwa namfahamu vilivyo. Nilikuwa mvumilivu nikiendelea kummezea mate bila utatuzi wa kiu yangu.
Ulifika muda wa mdogo wangu kwenda kumuona daktari kwani namba yake ilikuwa imefikiwa. Na hapo ndipo nilipouona muda wa wokovu wangu umefika. Nikajisogeza panapo kisima walau niweze kuchota maji kuridhisha kiu yangu ya kutaka kumfahamu binti huyu wa Kihabeshi.
Nilitoa kidaftari changu kidogo nikamwambia na tucheze mchezo. Aniambie kuhusu yeye "Tell me about you" ni kama mchezo mmoja marufu wa STOP ukishindwa kubuni neno nakuuliza swali lolote kukuhusu na unatakiwa unipe jibu sahihi. Kiufupi niliweza kufahamu alikuwa Akiitwa Mwanayumba Salum. Mkazi wa Arusha nimesahau mahali ila ni karibu na soko mjinga kama sikosei baada ya uwanja wa mpira. Jamani Mwanayumba wangu, nikipata nauli nitakuja kukuulizia.
Mdogo wangu alitoka kwa daktari na baada ya kwenda kuchukua dawa tulitakiwa kuondoka ila alituomba tumngoje maana angetakiwa kungoja peke yake angejisikia mpweke. Tulimpa sharti moja kuwa endapo tungemngoja basi asingekuwa na budi kuja nyumbanikwetu kwanza kabla ya kurejea kwao Arusha. Alikubali!
Nasi bila hiyana tulimngoja na alipotoka tukaondoka wote kuja nyumbani. Nakumbuka siku ile tulikula wote ugali nyumbani kwetu, tena kutoka kwenye sahani moja.
fast forward...
Katika mchezo ule nilifanikiwa kuchukua namba yake ya simu (ilikuwa namba ya mama yake kama tu ambavyo na mimi nilikuwa nikitumia simu na namba ya mama yangu). Tulikuwa tukiwasiliana usiku. Ilikuwa mbinu ya kujua kama si mama mwenye simu lazima u-beep na mimi ni-beep ndo tunaanza kuwasiliana kwa jumbe za simu!
Kidogo tukazoeana na hisia zikaanza kukua. Nakumbuka yeye ndo alikuwa wa kwanza kuniambia ananipenda. Nikamwambia amejuaje hayo na kuna mengi sana ambayo tunatofautiana?
Najua siku hizi dunia imeshanichakachua ila kipindi kile niliamini na nilijua ukimpenda mtu ni lazima aje kuwa mkeo. Tulikuwa na dini tofauti na hata katika maongezi niliweza kujua kuwa wazazi wake walimbania sana, hasa baba yake. Baba yake alikuwa mtu wa dini sana. Aliniambia ameshafikiria yote hayo na yuko tayari hata kubadili dini. Sikutaka kufanya haraka kukubali hilo ingawa na mimi moyoni tayari niishamkubalia nafasi siku nyingi.
Tulipanga siku tuonane na mimi nikaamua ningeenda Arusha. Nilienda mwaka uliofuata, 2003, na tulikutana kama sikosei maeneo ya stendi..majina ya yale majengo yamenitoka kiasi ila kuna "jogoo" na "sabasaba"!?? Tulielekea kwenye 'geto' la kaka yako hata sijui ni wapi tena maana tulipita vichochoroni, tukakatisha soko (soko mjinga?) tukakuta uwanja ukanionesha kwa mbaaali nyumba yenu. Tuliongea sana siku ile...tukapanga mambo mengi ambayo kwa utoto wetu tuliona ni sahihi. Tukakubaliana kuwa pamoja kama zaidi ya marafiki. Nilirudi nyumbani kama mtu aliyezaliwa upya.
Sikujali kuwa nilikuwa nasubiria mitihani ya mwisho ya kidato cha sita au la! Ila furaha tu ya kuwa ndani ya penzi ilinizidi, ilikuwa raha isiyo kifani. Ulikuwa ukija mara kwa mara hata siku ambazo hauna kliniki ila sasa ilikuwa rahisi kumdanganya baba...basi tulionana sana na tukazoeana.
Nilifanya mtihani wa kumaliza elimu yangu ya sekondari kidato cha sita na kuanza kutafuta kazi ‘tempo’ mtaani. Nikajitahidi nikanunua kamobiteli changu. nikakupa kale ka mama alikokuwa ameacha kukatumia. Tukawa tunawasiliana mpaka usiku wa manane...Kwa hakika penzi letu lilikuwa tamu.
September 2003
Ilifika kipindi nikatakiwa kwenda chuo kuendelea na masomo. Nakumbuka kipindi hicho ndo ulikuwa unamalizia kidato cha nne. Nilitakiwa kwenda kusoma nje ya nchi. Ukataka kujua mstakabali wa uhusiano wetu.
Nakumbuka nilienda kumuuliza mama kwa kutumia mwamvuli wa rafiki yangu, Salva. Nikamwambia mama, “Rafiki yangu Salva ana rafiki yake wa kike anampenda sana ila binti huyo ni muislamu na amesema yuko tayari kubadili dini ili tu wawe wote.”
Mama ni kama alikuwa akiongozwa na roho Mtakatifu kwani alinigeukia na kuniambia, "Mwanangu Mentor! angalia sana hao mabinti. Anaweza kusema lolote leo alimradi tu awe nawe. lakini mkishaoana akarudi kwenye dini yake utafanyaje? Utamuacha? Kumbuka haturuhusiwi kutalikiana!" Mh! maneno yale yaliniingia sana.
Kabla sijaondoka kwenda masomoni tulikutana Haria hotel Moshi pale double road nikamwambia, "Mwanayumba, mimi naenda kusoma lakini ukipata mwingine huku nyuma tafadhali endelea tu nisikuzuie!" Alilia sana Mwanayumba wangu siku ile. Hakujua kwanini nilimwambia vile ila ndo nilikuwa nampoteza Mwanayumba wangu. Sikujua! Alilia nikambembeleza ila sikutaka kumwambia nafanya vile kutokana na ushauri wa mama yangu.
Nilikwenda kusoma. Tuliwasiliana kwa muda mfupi baadaye gharama zikawa nyingi tukapunguza kuwasiliana. Mwanayumba ulinipa anuani yako ya barua pepe ila kila nikikutumia ujumbe haufiki. Huyu mjamaa anaitwa Mailer Daemon ananirudishia ujumbe wangu.
Mwanayumba nakumbuka tulikutana kipindi fulani pale Shoprite Arusha. Tuliongea sana Mwanayumba. Ukaniambia unafundisha sasa. Nadhani ilikuwa 2008. Ukanipa namba za simu. tukawasiliana kwa kipindi kile nilipokuwa nyumbani. Niliporudi shuleni tena nikapoteza line yangu ya Tanzania. Ndo ukawa mwisho wa mimi kukusikia na kuwasiliana na wewe.
Leo, December 10, 2012
Mwanayumba…umeenda wapi Mwanayumba? Mwanayumba ulikuwa binti niliyekupenda kuliko wote niliowahi kuwapenda. Mwanayumba, kila ninapokutana na vicheche vya jiji hili nakukumbuka binti wewe wa Kihabeshi. Popote mnioneapo Mwanayumba wangu mwambieni nampenda! Huenda alishaolewa sasa...ila atabaki kuwa Mwanayumba wangu, binti niliyempenda kuliko wote hadi sasa.
Wasalaam wapendwa,
Mentor.
MWANAYUMBA: PART II
Juni 2015
Ilikuwa siku ya Jumamosi, mwanzoni kabisa mwa mwezi huu wa sita. Nilikuwa nikiendesha gari kutokea baharini kwa kupitia njia hii ya kati ya Ikulu yetu ya Magogoni na Ikulu ndogo ya Zanzibar kama unaelekea hospitali ya Ocean Road. Safari yangu ilikuwa ikielekea Chuo cha Utalii. Nilipofika eneo la round about ile nikitaka kukunja kushoto kuendelea na safari yangu macho – yasiyo na pazia – yalielekea upande wa kulia ambapo kuna lango la kuingilia hospitali hiyo ya Ocean Road.
Niliiona sura ambayo ama kwa hakika haikuwa sura ngeni kabisa machoni pangu.
Itaendelea...
Ilikuwa mwaka 2002 Desemba.
Nilikuwa kidato cha Sita katika shule moja ya kutwa huko Moshi mkoani Kilimanjaro. Nakumbuka tulivyokutana...nakumbuka kama ilikuwa jana.
Nakumbuka baba akiniambia nijiandae kumpeleka mdogo wangu hospitali KCMC kwa ajili ya kliniki ya ngozi. Ilikuwa ni siku yake ya kliniki. Kitengo hicho cha ngozi ndiyo kwanza kilikuwa kimeanzishwa na kilianza kuchukua umaarufu mkubwa hasa kwa wagonjwa waliokuwa wakitokea mikoa ya Karibu na Kilimanjaro. Ilikuwa ni ahueni kwa wagonjwa wengi kwani hawakuhitaji kwenda tena Muhimbili kwa ajili ya matibabu au kliniki tu ya ngozi.
Kesho yake tuliamka vizuri na tukiwa njiani mara akaanza kulalamika kwamba hatakutana na rafiki yake waliyekutana wakati wa kliniki iliyopita kwani hakuwa na uhakika kama walipangiwa tarehe moja ya kurudi. Nilipuuzia hilo na tukafika hospitali tukakuta foleni tayari hivyo kutufanya tuchukue namba 68.
Basi tukakaa kwenye mabenchi yale kila mtu na kitabu chake tunajisomea huku tukingoja zamu yake ifike. Mara ghafla nikamsikia mdogo wangu akiruka kwa furaha, "Yuleeee..." Sikumuelewa kwanza ila baada ya kutupa macho kuelekea mlango wa kuingilia ndipo nilipogundua kilichomtia mshawasha namna ile.
Ni binti mmoja mrembo, mchanganyiko wa kihabesh..si ndo Ethiopia huko??? sijui ila alikuwa binti mmoja mrembo, mwembamba kiasi, mrefu mwenye maumbile yenye kuelezeka. Binti kama kachorwa kisha kabanduliwa akapewa pumzi na uwezo wa kutembea. Kama picha ya darasani unayoweza kugusa na kusema hiki ni kiuno..na wanafunzi wakaelewa.
Walisalimiana kwa kukumbatiana kisha walikuja nilipokuwa nimeketi akanisalimia. Akajitambulisha, tabasamu lake...
Binti yule alienda kujiandikisha na kupewa namba 74 na kisha kuja kukaa na sisi. Tukaanza kuongea na kupiga hadithi za hapa na pale. Moyoni tayari nilishavutiwa na binti huyu ila sikuwa na jinsi hasa kwa sababu ya mdogo wangu lakini pia kwa sababu sikuwa namfahamu vilivyo. Nilikuwa mvumilivu nikiendelea kummezea mate bila utatuzi wa kiu yangu.
Ulifika muda wa mdogo wangu kwenda kumuona daktari kwani namba yake ilikuwa imefikiwa. Na hapo ndipo nilipouona muda wa wokovu wangu umefika. Nikajisogeza panapo kisima walau niweze kuchota maji kuridhisha kiu yangu ya kutaka kumfahamu binti huyu wa Kihabeshi.
Nilitoa kidaftari changu kidogo nikamwambia na tucheze mchezo. Aniambie kuhusu yeye "Tell me about you" ni kama mchezo mmoja marufu wa STOP ukishindwa kubuni neno nakuuliza swali lolote kukuhusu na unatakiwa unipe jibu sahihi. Kiufupi niliweza kufahamu alikuwa Akiitwa Mwanayumba Salum. Mkazi wa Arusha nimesahau mahali ila ni karibu na soko mjinga kama sikosei baada ya uwanja wa mpira. Jamani Mwanayumba wangu, nikipata nauli nitakuja kukuulizia.
Mdogo wangu alitoka kwa daktari na baada ya kwenda kuchukua dawa tulitakiwa kuondoka ila alituomba tumngoje maana angetakiwa kungoja peke yake angejisikia mpweke. Tulimpa sharti moja kuwa endapo tungemngoja basi asingekuwa na budi kuja nyumbanikwetu kwanza kabla ya kurejea kwao Arusha. Alikubali!
Nasi bila hiyana tulimngoja na alipotoka tukaondoka wote kuja nyumbani. Nakumbuka siku ile tulikula wote ugali nyumbani kwetu, tena kutoka kwenye sahani moja.
fast forward...
Katika mchezo ule nilifanikiwa kuchukua namba yake ya simu (ilikuwa namba ya mama yake kama tu ambavyo na mimi nilikuwa nikitumia simu na namba ya mama yangu). Tulikuwa tukiwasiliana usiku. Ilikuwa mbinu ya kujua kama si mama mwenye simu lazima u-beep na mimi ni-beep ndo tunaanza kuwasiliana kwa jumbe za simu!
Kidogo tukazoeana na hisia zikaanza kukua. Nakumbuka yeye ndo alikuwa wa kwanza kuniambia ananipenda. Nikamwambia amejuaje hayo na kuna mengi sana ambayo tunatofautiana?
Najua siku hizi dunia imeshanichakachua ila kipindi kile niliamini na nilijua ukimpenda mtu ni lazima aje kuwa mkeo. Tulikuwa na dini tofauti na hata katika maongezi niliweza kujua kuwa wazazi wake walimbania sana, hasa baba yake. Baba yake alikuwa mtu wa dini sana. Aliniambia ameshafikiria yote hayo na yuko tayari hata kubadili dini. Sikutaka kufanya haraka kukubali hilo ingawa na mimi moyoni tayari niishamkubalia nafasi siku nyingi.
Tulipanga siku tuonane na mimi nikaamua ningeenda Arusha. Nilienda mwaka uliofuata, 2003, na tulikutana kama sikosei maeneo ya stendi..majina ya yale majengo yamenitoka kiasi ila kuna "jogoo" na "sabasaba"!?? Tulielekea kwenye 'geto' la kaka yako hata sijui ni wapi tena maana tulipita vichochoroni, tukakatisha soko (soko mjinga?) tukakuta uwanja ukanionesha kwa mbaaali nyumba yenu. Tuliongea sana siku ile...tukapanga mambo mengi ambayo kwa utoto wetu tuliona ni sahihi. Tukakubaliana kuwa pamoja kama zaidi ya marafiki. Nilirudi nyumbani kama mtu aliyezaliwa upya.
Sikujali kuwa nilikuwa nasubiria mitihani ya mwisho ya kidato cha sita au la! Ila furaha tu ya kuwa ndani ya penzi ilinizidi, ilikuwa raha isiyo kifani. Ulikuwa ukija mara kwa mara hata siku ambazo hauna kliniki ila sasa ilikuwa rahisi kumdanganya baba...basi tulionana sana na tukazoeana.
Nilifanya mtihani wa kumaliza elimu yangu ya sekondari kidato cha sita na kuanza kutafuta kazi ‘tempo’ mtaani. Nikajitahidi nikanunua kamobiteli changu. nikakupa kale ka mama alikokuwa ameacha kukatumia. Tukawa tunawasiliana mpaka usiku wa manane...Kwa hakika penzi letu lilikuwa tamu.
September 2003
Ilifika kipindi nikatakiwa kwenda chuo kuendelea na masomo. Nakumbuka kipindi hicho ndo ulikuwa unamalizia kidato cha nne. Nilitakiwa kwenda kusoma nje ya nchi. Ukataka kujua mstakabali wa uhusiano wetu.
Nakumbuka nilienda kumuuliza mama kwa kutumia mwamvuli wa rafiki yangu, Salva. Nikamwambia mama, “Rafiki yangu Salva ana rafiki yake wa kike anampenda sana ila binti huyo ni muislamu na amesema yuko tayari kubadili dini ili tu wawe wote.”
Mama ni kama alikuwa akiongozwa na roho Mtakatifu kwani alinigeukia na kuniambia, "Mwanangu Mentor! angalia sana hao mabinti. Anaweza kusema lolote leo alimradi tu awe nawe. lakini mkishaoana akarudi kwenye dini yake utafanyaje? Utamuacha? Kumbuka haturuhusiwi kutalikiana!" Mh! maneno yale yaliniingia sana.
Kabla sijaondoka kwenda masomoni tulikutana Haria hotel Moshi pale double road nikamwambia, "Mwanayumba, mimi naenda kusoma lakini ukipata mwingine huku nyuma tafadhali endelea tu nisikuzuie!" Alilia sana Mwanayumba wangu siku ile. Hakujua kwanini nilimwambia vile ila ndo nilikuwa nampoteza Mwanayumba wangu. Sikujua! Alilia nikambembeleza ila sikutaka kumwambia nafanya vile kutokana na ushauri wa mama yangu.
Nilikwenda kusoma. Tuliwasiliana kwa muda mfupi baadaye gharama zikawa nyingi tukapunguza kuwasiliana. Mwanayumba ulinipa anuani yako ya barua pepe ila kila nikikutumia ujumbe haufiki. Huyu mjamaa anaitwa Mailer Daemon ananirudishia ujumbe wangu.
Mwanayumba nakumbuka tulikutana kipindi fulani pale Shoprite Arusha. Tuliongea sana Mwanayumba. Ukaniambia unafundisha sasa. Nadhani ilikuwa 2008. Ukanipa namba za simu. tukawasiliana kwa kipindi kile nilipokuwa nyumbani. Niliporudi shuleni tena nikapoteza line yangu ya Tanzania. Ndo ukawa mwisho wa mimi kukusikia na kuwasiliana na wewe.
Leo, December 10, 2012
Mwanayumba…umeenda wapi Mwanayumba? Mwanayumba ulikuwa binti niliyekupenda kuliko wote niliowahi kuwapenda. Mwanayumba, kila ninapokutana na vicheche vya jiji hili nakukumbuka binti wewe wa Kihabeshi. Popote mnioneapo Mwanayumba wangu mwambieni nampenda! Huenda alishaolewa sasa...ila atabaki kuwa Mwanayumba wangu, binti niliyempenda kuliko wote hadi sasa.
Wasalaam wapendwa,
Mentor.
MWANAYUMBA: PART II
Juni 2015
Ilikuwa siku ya Jumamosi, mwanzoni kabisa mwa mwezi huu wa sita. Nilikuwa nikiendesha gari kutokea baharini kwa kupitia njia hii ya kati ya Ikulu yetu ya Magogoni na Ikulu ndogo ya Zanzibar kama unaelekea hospitali ya Ocean Road. Safari yangu ilikuwa ikielekea Chuo cha Utalii. Nilipofika eneo la round about ile nikitaka kukunja kushoto kuendelea na safari yangu macho – yasiyo na pazia – yalielekea upande wa kulia ambapo kuna lango la kuingilia hospitali hiyo ya Ocean Road.
Niliiona sura ambayo ama kwa hakika haikuwa sura ngeni kabisa machoni pangu.
Itaendelea...
Last edited by a moderator: