figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Heshima kwenu wakuu,
Leo naomba niwashauri wale ambao hawajaoa.
Hii ni siri ya kambi namba mbili.
Usifanye ngono na mwanamke unayetaka kumuoa kama kweli unataka kuwa na familia bora yenye kuheshimiana.
Hii pia inawahusu wanawake, ila mimi nazungumzia wanaume sababu ndo wanaomba mchezo.
Kama hutasikiliza ushauri huu yatakayokupata, usilaumu.
Kuna matatizo yanayotokana na ngono kabla ya ndoa. Yaani hapa namanisha yule unayetaka kuolewa naye au kumuoa.
1. Mkifanya mapenzi, upo uwezekano mkubwa 80% ndoa ikayeyuka, sababu uzuri wa ubora na sifa nzuri za mwanamke zinaisha pale unapotembea naye. Inabaki mazoea tu.
2. Kimungu sisi tunaoamini Mungu ni kwamba ukifanya ngono na mke wako mtarajiwa, unaingiza laana ya uzinzi ndani ya nyumba. Matokeo yake mkishaonana michepuko haiishi sababu ni laana.
Unakuta mtu ana mke lakini anachepuka, mke ana mume lakini anachepuka. Mke au mume ana ndoa lakini wanazaa nje ya ndoa.
Watu hawajui sababu, ya yote haya, sababu ni laana ya uzinzi mliuoingiza ndani ya familia.
3. Wengi wenye migogoro ndani ya ndoa, ni wale walioleta laana ndani nyumba. So hutaishi kwa furaha ndani ya ndoa, iwe mke au mume.
4. Ukianza ngono nje ya ndoa, utatia aibu ndani ya familia kwani utaonywa na kusutwa uache ngono na watoto wako wa kuwazaa. Ndo maana unaona babu mtu mzima 50yrs anatongoza mtoto wa miaka 14. Ni laana
Kikubwa hapa ni kujielewa. Tofautisha rafiki wa ujana na mke mtarajiwa. Mkifanya ngono ni dalili hamheshimu miili yenu na ni sawa na kubikri tabia ya familia itakavyokuwa.
Kama ulifanya hivyo kabla, sasa ni wakati wako wa kujisahihisha. Nendeni kwenye dini zenu mkatubu hiyo dhambi ya laana.
Mimi nikitaka kuoa, siwezi fanya ngono na mke wangu mtarajiwa. Ni kuidhurumu nafsi. Hata siku ya ndoa hamuinjoy sababu kila mtu anamjua mwenzie, hamna msisimko. Matokeo yake mnaanza kula Ugali kwa picha ya samaki, upo na mpenzi wako wa ndoa kitandani kisu kwenye ala lakini mawazo yapo kwa mwanaume/mwanamke mwingine.
Ujumbe huu ni kwa watu wazima na vijana. Hii elimu hutaipata popote bali JF tu.
Leo naomba niwashauri wale ambao hawajaoa.
Hii ni siri ya kambi namba mbili.
Usifanye ngono na mwanamke unayetaka kumuoa kama kweli unataka kuwa na familia bora yenye kuheshimiana.
Hii pia inawahusu wanawake, ila mimi nazungumzia wanaume sababu ndo wanaomba mchezo.
Kama hutasikiliza ushauri huu yatakayokupata, usilaumu.
Kuna matatizo yanayotokana na ngono kabla ya ndoa. Yaani hapa namanisha yule unayetaka kuolewa naye au kumuoa.
1. Mkifanya mapenzi, upo uwezekano mkubwa 80% ndoa ikayeyuka, sababu uzuri wa ubora na sifa nzuri za mwanamke zinaisha pale unapotembea naye. Inabaki mazoea tu.
2. Kimungu sisi tunaoamini Mungu ni kwamba ukifanya ngono na mke wako mtarajiwa, unaingiza laana ya uzinzi ndani ya nyumba. Matokeo yake mkishaonana michepuko haiishi sababu ni laana.
Unakuta mtu ana mke lakini anachepuka, mke ana mume lakini anachepuka. Mke au mume ana ndoa lakini wanazaa nje ya ndoa.
Watu hawajui sababu, ya yote haya, sababu ni laana ya uzinzi mliuoingiza ndani ya familia.
3. Wengi wenye migogoro ndani ya ndoa, ni wale walioleta laana ndani nyumba. So hutaishi kwa furaha ndani ya ndoa, iwe mke au mume.
4. Ukianza ngono nje ya ndoa, utatia aibu ndani ya familia kwani utaonywa na kusutwa uache ngono na watoto wako wa kuwazaa. Ndo maana unaona babu mtu mzima 50yrs anatongoza mtoto wa miaka 14. Ni laana
Kikubwa hapa ni kujielewa. Tofautisha rafiki wa ujana na mke mtarajiwa. Mkifanya ngono ni dalili hamheshimu miili yenu na ni sawa na kubikri tabia ya familia itakavyokuwa.
Kama ulifanya hivyo kabla, sasa ni wakati wako wa kujisahihisha. Nendeni kwenye dini zenu mkatubu hiyo dhambi ya laana.
Mimi nikitaka kuoa, siwezi fanya ngono na mke wangu mtarajiwa. Ni kuidhurumu nafsi. Hata siku ya ndoa hamuinjoy sababu kila mtu anamjua mwenzie, hamna msisimko. Matokeo yake mnaanza kula Ugali kwa picha ya samaki, upo na mpenzi wako wa ndoa kitandani kisu kwenye ala lakini mawazo yapo kwa mwanaume/mwanamke mwingine.
Ujumbe huu ni kwa watu wazima na vijana. Hii elimu hutaipata popote bali JF tu.