Mwanaume Unalichukuliaje hili?

mamanalia

JF-Expert Member
Nov 7, 2009
667
146
Unachukuliaje kumuoa binti aliyekwisha kuzaa labda akiwa O level huko.

Au unamsimamo gani kwa mwanamke aliyekwisha kuzaa, utaweza kumuoa akikwambia ana mtoto baada ya wewe kukaa naye wiki kadhaa kwenye uhusiano?
 
Unachukuliaje kumuoa binti aliyekwisha kuzaa labda akiwa O level huko.

Au unamsimamo gani kwa mwanamke aliyekwisha kuzaa, utaweza kumuoa akikwambia ana mtoto baada ya wewe kukaa naye wiki kadhaa kwenye uhusiano?

Kama kuna uwezekano wa kutumua mbio nitasepa.

mwanamke mwenye mtoto ni noma (sorry kwa wale watakaokwazika)!!

Babu DC (1947)
 
Ukipenda boga .......................................................................!!!!!!!
 
Kama kuna uwezekano wa kutumua mbio nitasepa.

mwanamke mwenye mtoto ni noma (sorry kwa wale watakaokwazika)!!

Babu DC (1947)


UMENIKWAZA.

kwan mwanamke aliyezaa shida yake ninin?
nini kinabadilika?
let say alizaaa olevel . ...as u know that tym utoto mwng so ata kujikinga sio kiivo..kapata mimba kazaa na akaendelea na shule mpk univerdty ...na hana mawasiliano na yule aliyemtia mimba sema ni dent mwenzake na wote walikuwa na miaka 18 kipindi kile...

kumshutumu msichana peke yake na kumuacha yule aliyemtia mimba naona si haki ...au mimba aliipata choon wakat anakojoa?
blame wote basi km ivo na mseme pia MWANAUME ALIYEZAA NA MWANAMKE UKOO NYUMA B4 KUOA ni noma..si husband material...


2me;
utu wa mtu aubadiliki et kisa kazaa..km ni mwema atabak ivo ivo..ever human human being anafanya mistake...sasa kumnnyanyapaa uyu kisa kazaa ahh ist fair

kuna ambao hawajazaaa lakin dahh ni km kazaaa ..kimuonekano na kwa kila kitu

km ni tabia kaka tabia ya mtu aibadilik et kisa kazaa bas ahh afai....


we mchek uyo dada km yaliyomo yamo oa..ni maelewano tu baina yenu...waweza oa asiyezaa na akakuletea sarakas mpk ukamwita mungu shemeji....
 
Kuzaa sio sababu kama unampenda kweli utapenda na kila chake sio watoto2 mpaka nduguzake, na huwezi kujua hao watoto wa mke wanaweza kukuheshimu na kukuthamini kuliko ulio zaa na huyo mwanamke au inawezekana Mungu hakukujalia mtoto na hao watoto wakakustiri.
 
UMENIKWAZA.

kwan mwanamke aliyezaa shida yake ninin?
nini kinabadilika?
let say alizaaa olevel . ...as u know that tym utoto mwng so ata kujikinga sio kiivo..kapata mimba kazaa na akaendelea na shule mpk univerdty ...na hana mawasiliano na yule aliyemtia mimba sema ni dent mwenzake na wote walikuwa na miaka 18 kipindi kile...

kumshutumu msichana peke yake na kumuacha yule aliyemtia mimba naona si haki ...au mimba aliipata choon wakat anakojoa?
blame wote basi km ivo na mseme pia MWANAUME ALIYEZAA NA MWANAMKE UKOO NYUMA B4 KUOA ni noma..si husband material...


2me;
utu wa mtu aubadiliki et kisa kazaa..km ni mwema atabak ivo ivo..ever human human being anafanya mistake...sasa kumnnyanyapaa uyu kisa kazaa ahh ist fair

kuna ambao hawajazaaa lakin dahh ni km kazaaa ..kimuonekano na kwa kila kitu

km ni tabia kaka tabia ya mtu aibadilik et kisa kazaa bas ahh afai....


we mchek uyo dada km yaliyomo yamo oa..ni maelewano tu baina yenu...waweza oa asiyezaa na akakuletea sarakas mpk ukamwita mungu shemeji....

Mpendwa sanaaana Rose,

Nilitegemea feelings za namna hii na ndiyo maana nikaanza kwa kuomba msamaha. Maadam umeshanisamehe...nijariby kueleza niliyomaanisha katika post yangu ya awali.

Sisi (especially wa miaka ya 1947) ni Watanzania na Waafrika, na bado tunaenzi mila zetu ambazo bahati mbaya zina mrengo wa kiume....Naamini hapo tunakubaliana.....Na kwa makunzi yetu (labda mimi binafsi), tumekuwa na imani kuwa mwanamke ni wa mtu mmoja tu (ingawa tunajua kuwa si kweli) hadi hapo tunapo-prove otherwise....Sasa kuwa na mtoto ni ishara kwamba huyo si wako peke yako! Na hilo linawauma wanaume wote hata kama hawasemi!!! ....Mimi babu yao nawasemea kwenye hili (samahani tena kama kuna atakayeguswa)!!

Pia jamii humwona vibaya mtu anayelea mtoto wa mwenzake...Nina office mates kama 3 wana ndoa za namna hiyo ila siku zote hawana amani!

Na jambo jingine ni matatizo yanayojitokeza mara nyingi linapokuja suala la kumlea mtoto (hapa ni nina mifano mingi ila nitaishia hapa)!!

Nitarudi baadaye kidogo,

Babu DC (1947)!!
 
Unachukuliaje kumuoa binti aliyekwisha kuzaa labda akiwa O level huko.

Au unamsimamo gani kwa mwanamke aliyekwisha kuzaa, utaweza kumuoa akikwambia ana mtoto baada ya wewe kukaa naye wiki kadhaa kwenye uhusiano?

Kama kuna uwezekano wa kutumua mbio nitasepa.

mwanamke mwenye mtoto ni noma (sorry kwa wale watakaokwazika)!!

Babu DC (1947)
Unaonaje na wewe ukiwa na mtoto tayari halafu ukataka kumuoa binti ambaye hajazaa?
 
Unaonaje na wewe ukiwa na mtoto tayari halafu ukataka kumuoa binti ambaye hajazaa?

Mkuu J'Bonge,

Hapa kuna mambo mawili ambayo inabidi kuyaangalia.

Kwanza ni mtazamo wa jamii....ambapo inaonekana kwamba mwanamume kuwa na wanawake wengi hata watoto ni sawa ila kinyume chake ni jinai...Unaweza usiamini ila huo ndio ukweli wenyewe!

Pili ni mtazamo wangu binafsi...Kwa vile sina mtoto wa nje, basi siwezi kuwa na mwenzangu (na ki ukweli sina) ambaye ana mtoto wa nje. Kama ingenitokea wakati ule bado natafuta mchumba ningeweza labda kuwa na msimamo huo au tofauti. Kwa sasa nitabaki kusema hayo!!
 
kwangukuwa na mtoto
Mapenzi yako kwake yatajibu swali hili.

Mkuu J'Bonge,

Hapa kuna mambo mawili ambayo inabidi kuyaangalia.

Kwanza ni mtazamo wa jamii....ambapo inaonekana kwamba mwanamume kuwa na wanawake wengi hata watoto ni sawa ila kinyume chake ni jinai...Unaweza usiamini ila huo ndio ukweli wenyewe!

Pili ni mtazamo wangu binafsi...Kwa vile sina mtoto wa nje, basi siwezi kuwa na mwenzangu (na ki ukweli sina) ambaye ana mtoto wa nje. Kama ingenitokea wakati ule bado natafuta mchumba ningeweza labda kuwa na msimamo huo au tofauti. Kwa sasa nitabaki kusema hayo!!
Mkuu Dark City, Majibu na mtizamo wangu ni kama huo hapo juu alioutoa Likwanda. kwangu kuwa na mtoto aukutokuwa naye kwa mwanaume au mwanamke siyo kigezo. kigezo kikubwa ni mapenzi. kama kweli umempenda, mtoto huwa siyo kigezo. Nina mfano hai kabisa ambapo jamaa alioa kwa mara ya kwanza kabisa lakini huyo aliyemuoa alikuwa tayari ana watoto wawili na jamaa mpaka sasa ana watoto wa kuzaa mwenyewe na wale wa kufikia lakini anawatunza wote kama watoto wake na anawasomesha private schools na ndoa yao ina amani kabisa
 
Mpendwa sanaaana Rose,

Nilitegemea feelings za namna hii na ndiyo maana nikaanza kwa kuomba msamaha. Maadam umeshanisamehe...nijariby kueleza niliyomaanisha katika post yangu ya awali.

Sisi (especially wa miaka ya 1947) ni Watanzania na Waafrika, na bado tunaenzi mila zetu ambazo bahati mbaya zina mrengo wa kiume....Naamini hapo tunakubaliana.....Na kwa makunzi yetu (labda mimi binafsi), tumekuwa na imani kuwa mwanamke ni wa mtu mmoja tu (ingawa tunajua kuwa si kweli) hadi hapo tunapo-prove otherwise....Sasa kuwa na mtoto ni ishara kwamba huyo si wako peke yako! Na hilo linawauma wanaume wote hata kama hawasemi!!! ....Mimi babu yao nawasemea kwenye hili (samahani tena kama kuna atakayeguswa)!!

Pia jamii humwona vibaya mtu anayelea mtoto wa mwenzake...Nina office mates kama 3 wana ndoa za namna hiyo ila siku zote hawana amani!

Na jambo jingine ni matatizo yanayojitokeza mara nyingi linapokuja suala la kumlea mtoto (hapa ni nina mifano mingi ila nitaishia hapa)!!

Nitarudi baadaye kidogo,

Babu DC (1947)!!
Jibu lako halijitoshelezi, ongeza point nyingine ili tuone na tujue kosa la mwanamke liko api, coz kumbuka kitendo kafanya na mwanaume
 
Mapenzi yako kwake yatajibu swali hili.

kwangukuwa na mtoto


Mkuu Dark City, Majibu na mtizamo wangu ni kama huo hapo juu alioutoa Likwanda. kwangu kuwa na mtoto aukutokuwa naye kwa mwanaume au mwanamke siyo kigezo. kigezo kikubwa ni mapenzi. kama kweli umempenda, mtoto huwa siyo kigezo. Nina mfano hai kabisa ambapo jamaa alioa kwa mara ya kwanza kabisa lakini huyo aliyemuoa alikuwa tayari ana watoto wawili na jamaa mpaka sasa ana watoto wa kuzaa mwenyewe na wale wa kufikia lakini anawatunza wote kama watoto wake na anawasomesha private schools na ndoa yao ina amani kabisa

Sawa mkuu,

Hakuna jinsi ambayo mambo ya maisha yanaweza kuwa generalized. Kwa hiyo kutakuwa na tofauti kati ya mtu na mtu. Pia sina tatizo na huo msimamo wako.

Ila kwa sababu ya mjadala huu...naomba kukueleza kuwa mila zetu zinaamini kuwa kuna tofauti kubwa kati ya ndoa na mapenzi. Kwa hiyo wapo ambao wameoana wakiwa na watoto na ndoa ikawa nzuri. Pia wapo ambao wana watoto wa nje ya ndoa na maisha ni karaha tupu. Kote kote kuna mifano ya kutosha!

Hata hivyo, neno mapenzi sina hakika kama limo kwenye mambo ya ndoa zetu (kadri ya mila tunazoziishi)...Ndoa inaangaliwa kama kitu independent ambacho kina vigezo vyake tofauti na mambo ya mapenzi ya kisasa. Ndiyo maana wazazi wanaweza kumkataa mchumba wako kwa vigezo ambavyo kwa watu walio wengi huona kama upuuzi!

Itoshe tu kusema kuwa ndoa inaenda mbele zaidi ya mapenzi na matamanio ya ngono...kwa sababu inategemewa kuwa nanyi (mke na mume) hadi muende kwenye makazi yenu ya milele!
 
Jibu lako halijitoshelezi, ongeza point nyingine ili tuone na tujue kosa la mwanamke liko api, coz kumbuka kitendo kafanya na mwanaume

Binafsi sijasema mwanamke ana makosa,

Nimetoa mtazamo wangu na ule wa jamii...Kama hukubaliani nao ni poa tu!
 
Sawa mkuu,
Itoshe tu kusema kuwa ndoa inaenda mbele zaidi ya mapenzi na matamanio ya ngono...kwa sababu inategemewa kuwa nanyi (mke na mume) hadi muende kwenye makazi yenu ya milele!
Mkuu nadhani hapo kwenye red ni suala la lugha tu. maana yangu haikuwa ya kuhusisha mapenzi na matamanio ya ngono nilikuwa na maana ya kupenda
 
Mpendwa sanaaana Rose,

Nilitegemea feelings za namna hii na ndiyo maana nikaanza kwa kuomba msamaha. Maadam umeshanisamehe...nijariby kueleza niliyomaanisha katika post yangu ya awali.

Sisi (especially wa miaka ya 1947) ni Watanzania na Waafrika, na bado tunaenzi mila zetu ambazo bahati mbaya zina mrengo wa kiume....Naamini hapo tunakubaliana.....Na kwa makunzi yetu (labda mimi binafsi), tumekuwa na imani kuwa mwanamke ni wa mtu mmoja tu (ingawa tunajua kuwa si kweli) hadi hapo tunapo-prove otherwise....Sasa kuwa na mtoto ni ishara kwamba huyo si wako peke yako! Na hilo linawauma wanaume wote hata kama hawasemi!!! ....Mimi babu yao nawasemea kwenye hili (samahani tena kama kuna atakayeguswa)!!

Pia jamii humwona vibaya mtu anayelea mtoto wa mwenzake...Nina office mates kama 3 wana ndoa za namna hiyo ila siku zote hawana amani!

Na jambo jingine ni matatizo yanayojitokeza mara nyingi linapokuja suala la kumlea mtoto (hapa ni nina mifano mingi ila nitaishia hapa)!!

Nitarudi baadaye kidogo,

Babu DC (1947)!!
Kama suala la kuzaa ndilo linakufanya kuona kuwa huyo mwanamke si wa peke yako, unalichukuliaje suala la kuoa mwanamke ambaye sio bikra? Hiyo siyo issue, anaweza akawa hana mtoto na akawa si wa peke yako vile vile. Kinacho-matter ni upendo wa kweli - Kama kweli unampenda ......., Na wanawake nao wawachukuliaje wanaume wenye watoto wa zamani.
 
Mradi alomzalisha asiwe anakula chinichini
<br />
<br />
wakikutana tu!.........,kuna jamaa alioa mke ambaye alizalishwa,baada ya muda yule mume akawa anakuja kumchek mtt.cku moja walifumaniwa wanamegana.
 
Mkuu nadhani hapo kwenye red ni suala la lugha tu. maana yangu haikuwa ya kuhusisha mapenzi na matamanio ya ngono nilikuwa na maana ya kupenda

Nakuelewa sana ndugu,

Ila haya mambo tumeshayaongea sana hapa JF na kwingineko. Kupenda ni jambo gumu sana na kuna watu wameishi maisha yao yote blla kujua kama wanawapenda wenzi wao au pia wao wanapendwa. Na ndiyo maana suala la ndoa linahusisha na vigezo vingine tena vile ambavyo siyo vya msimu!

Labda tu pia nikueleze...kwa uzoefu wangu na kwa masimulizi kwamba ni nadra kwa wanaume kupenda kweli kweli...Ndiyo maana wanahanja hanja kama kuku wa kienyeji...Kwao kutamani kunachukua sehemu kubwa katika mambo ya ngono! Bahati mbaya, wenzetu wanawake huwa wanakuwa na mapenzi ya kweli kwenye mahusiano. Ndiyo maana hizi hukumu za jamii na watu binafsi zina waumiza sana.

Ila huo ndio ukweli wenyewe...Wanawake ni wahanga wa mfumo wetu wa maisha...Labda ukibadilika!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom