Baba jayaron
JF-Expert Member
- Jun 29, 2015
- 3,994
- 5,437
Wasalam!
Hii habari ni mwendelezo wa matukio yangu halisi.
Ni muda sasa kama mwaka tangu nitengane na mke wangu kutokana na swala LA uzinzi ambapo aliamua kuondoka kuishi maisha yake na hawara wake.
Muda haukuwa mrefu aliomba kurudi kwangu kienyeji enyeji ila hali swala lilishafika kanisani baada ya kuona mwenzangu ameamua kuishi maisha yangu hivyo na mimi niangalie usawa wangu maana bado kijana na nna nguvu za kutosha kuvutia mrembo yeyote.
Swala langu lilipofika kanisani halikuwa rahisi kwamaana huyo mwanamke alipoitwa alikana na kudai hana mahusiano yoyote isipokuwa nilimfukuza nyumbani baada ya kushawishiwa na ndugu zangu so akaamua aondoke na kuniachia watoto wetu wadogo.
Ilikuwa vuta nikuvute, hakubali na anakataa kwa kilio akiwa na viongozi wa kanisa lakini akiwa na mimi anadai nimsamehe turudiane tuu hivyo wakati bado anawasiliana na hawara wake.
Nilipofanikiwa kunasa sauti zinazothibitisha mahusiano yao ndo ikabidi akubali mbele ya viongozi wa kanisa, lakini sasa anadai anahitaji ndoa yake na si kuachana.
Maajabu ya utaratibu wetu sisi wakristo ni kulazimishana kurudiana watu tulioumizana kiasi kikubwa kwa kigezo cha kusameheana.... Yaani ni lazima nimsamehe turudiane vinginevyo sitoruhusiwa kuoa maisha yangu yoote labda mpaka huyo mwanamke aolewe.
Binafsi kipindi hiki kifupi nimekuwa mzinifu kiani kwakuwa nipo mpweke na ni maisha ambayo naya fake kwakuwa sikuwa na mazoea hayo.
Viongozi wa kanisa wananikazia nimrudie kwakuwa eti kuna watu wanalea watoto si wao ila bado wapo na wake zao, eti ishu yangu ni ndogo tuu.... Yaan hawajui kejeli, dharau na matusi niliyotukanwa mimi na mama yangu kwa mbwembwe na hawara wa huyo mwanamke na mwanamke mwenyewe, hawajui ni magumu kiasi gani nimepitia hata sasa niko hai sababu ya hili swala, woote wapo upande wa mwanamke.
Mwanaume mkristo mwenzangu usikurupuke unapofikia hatua wa kuoa, utamu wa kyuma usikuzibe ufahamu ukashindwa kumng'amua mwanamke unayetarajia kumuoa vinginevyo utajuta.
Hii habari ni mwendelezo wa matukio yangu halisi.
Ni muda sasa kama mwaka tangu nitengane na mke wangu kutokana na swala LA uzinzi ambapo aliamua kuondoka kuishi maisha yake na hawara wake.
Muda haukuwa mrefu aliomba kurudi kwangu kienyeji enyeji ila hali swala lilishafika kanisani baada ya kuona mwenzangu ameamua kuishi maisha yangu hivyo na mimi niangalie usawa wangu maana bado kijana na nna nguvu za kutosha kuvutia mrembo yeyote.
Swala langu lilipofika kanisani halikuwa rahisi kwamaana huyo mwanamke alipoitwa alikana na kudai hana mahusiano yoyote isipokuwa nilimfukuza nyumbani baada ya kushawishiwa na ndugu zangu so akaamua aondoke na kuniachia watoto wetu wadogo.
Ilikuwa vuta nikuvute, hakubali na anakataa kwa kilio akiwa na viongozi wa kanisa lakini akiwa na mimi anadai nimsamehe turudiane tuu hivyo wakati bado anawasiliana na hawara wake.
Nilipofanikiwa kunasa sauti zinazothibitisha mahusiano yao ndo ikabidi akubali mbele ya viongozi wa kanisa, lakini sasa anadai anahitaji ndoa yake na si kuachana.
Maajabu ya utaratibu wetu sisi wakristo ni kulazimishana kurudiana watu tulioumizana kiasi kikubwa kwa kigezo cha kusameheana.... Yaani ni lazima nimsamehe turudiane vinginevyo sitoruhusiwa kuoa maisha yangu yoote labda mpaka huyo mwanamke aolewe.
Binafsi kipindi hiki kifupi nimekuwa mzinifu kiani kwakuwa nipo mpweke na ni maisha ambayo naya fake kwakuwa sikuwa na mazoea hayo.
Viongozi wa kanisa wananikazia nimrudie kwakuwa eti kuna watu wanalea watoto si wao ila bado wapo na wake zao, eti ishu yangu ni ndogo tuu.... Yaan hawajui kejeli, dharau na matusi niliyotukanwa mimi na mama yangu kwa mbwembwe na hawara wa huyo mwanamke na mwanamke mwenyewe, hawajui ni magumu kiasi gani nimepitia hata sasa niko hai sababu ya hili swala, woote wapo upande wa mwanamke.
Mwanaume mkristo mwenzangu usikurupuke unapofikia hatua wa kuoa, utamu wa kyuma usikuzibe ufahamu ukashindwa kumng'amua mwanamke unayetarajia kumuoa vinginevyo utajuta.