Mwanaume Mwenye Aleji na Mke Wake

Dr. Chapa Kiuno

JF-Expert Member
Sep 11, 2009
443
18
</SPAN>


Young hulazimika kuvaa gloves anapokuwa karibu na mke wake.
Tuesday, November 03, 2009 8:33 AM
Mwanaume mmoja nchini Uingereza amedai kuwa na aleji na mke wake na mapigo yake ya moyo huongezeka maradufu na mwili wake kuanza kuvimba kila anapomkaribia.


Darren Young, 45, mkazi wa Yorkshire ana aleji na kemikali ya polyethylene glycol inayotumika kwenye krimu, losheni karibia zote pamoja na kwenye dawa za meno na hupata tabu sana mkewe anapojipaka losheni au krimu.

Mapigo ya moyo wake huongezeka maradufu na wakati mwingine moyo wake hukaribia kusimama, mwili wake huvimba na kutoa vipele kila anapokuwa karibu na vitu hivyo.

Young, ambaye ni dereva wa mabasi ya mji wa Sprotbrough, anasema kuwa huwa hawezi kumsogelea mkewe anapotumia losheni au krimu.

"Unapofika wakati wa kulala, mke wangu Sue huwa hahitaji sababu yoyote ya kunikwepa au kunifukuza kitandani, huwa anatumia losheni", alisema Young alipokuwa akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza.

"Sio Sue peke yake, huwa nadhurika kila ninapoenda baa na kukaa karibu na mwanamke anayetumia losheni".

"Madaktari hawajui nini kimenisibu na kunifanya ghafla niwe na hali kama hii", alisema Young.

Young aligundulika kuwa na aleji hiyo wakati alipochomwa sindano ya steroid iliyokuwa na polyethylene glycol ili kutibu matatizo ya miguu yake.

Uso wake ulivimba baada ya kuchomwa sindano hiyo na moyo wake ulisimama na ilibidi uzinduliwe tena kwa mashine.

Young ametakiwa na madaktari awe makini sana anapogusa kitu chochote na amekuwa akitumia madawa mbali mbali kila siku.



Source: The Sun
 
</SPAN>


Young hulazimika kuvaa gloves anapokuwa karibu na mke wake.
Tuesday, November 03, 2009 8:33 AM
Mwanaume mmoja nchini Uingereza amedai kuwa na aleji na mke wake na mapigo yake ya moyo huongezeka maradufu na mwili wake kuanza kuvimba kila anapomkaribia.

Darren Young, 45, mkazi wa Yorkshire ana aleji na kemikali ya polyethylene glycol inayotumika kwenye krimu, losheni karibia zote pamoja na kwenye dawa za meno na hupata tabu sana mkewe anapojipaka losheni au krimu.

Mapigo ya moyo wake huongezeka maradufu na wakati mwingine moyo wake hukaribia kusimama, mwili wake huvimba na kutoa vipele kila anapokuwa karibu na vitu hivyo.

Young, ambaye ni dereva wa mabasi ya mji wa Sprotbrough, anasema kuwa huwa hawezi kumsogelea mkewe anapotumia losheni au krimu.

"Unapofika wakati wa kulala, mke wangu Sue huwa hahitaji sababu yoyote ya kunikwepa au kunifukuza kitandani, huwa anatumia losheni", alisema Young alipokuwa akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza.

"Sio Sue peke yake, huwa nadhurika kila ninapoenda baa na kukaa karibu na mwanamke anayetumia losheni".

"Madaktari hawajui nini kimenisibu na kunifanya ghafla niwe na hali kama hii", alisema Young.

Young aligundulika kuwa na aleji hiyo wakati alipochomwa sindano ya steroid iliyokuwa na polyethylene glycol ili kutibu matatizo ya miguu yake.

Uso wake ulivimba baada ya kuchomwa sindano hiyo na moyo wake ulisimama na ilibidi uzinduliwe tena kwa mashine.

Young ametakiwa na madaktari awe makini sana anapogusa kitu chochote na amekuwa akitumia madawa mbali mbali kila siku.



Source: The Sun

Hii habari si njema kwangu , maana mabinti wakigundua hiyo kemikali sijui tutawapata wapi tena maana ukimsogelea tu moyo unasimama na mwili kuvimba......
 
...hata mimi na 'Allergy' mbaya na wanawake wanaovuta sigereti na wanaokunywa bia!

Huyo mke si aache tu kutumia hizo lotion na toothpaste kuinusuru ndoa yake?
au ndio anataka kumtoa roho mzee wa watu maisha yaendelee?

Wanawake wengine bana!
 
...hata mimi na 'Allergy' mbaya na wanawake wanaovuta sigereti na wanaokunywa bia!

Huyo mke si aache tu kutumia hizo lotion na toothpaste kuinusuru ndoa yake?
au ndio anataka kumtoa roho mzee wa watu maisha yaendelee?

Wanawake wengine bana!
yaani aache hata kutumia toothpaste, je mdomo na utakuwa na hali gani?
mingine mitihani kwa kweli.
 
Kwa kwel huya mke anamtihan mkubwa. Ila usije kuta jamaa anazunga na kutembea na wadada poa!
 
Back
Top Bottom