ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,649
Kuna hiki kiumbe dhaifu lakini cha ajabu hapa duniani kiitwacho Mwanaume.
Ni cha ajabu kutokana na uwezo wake wa kubadilika kufuatana na mazingira kilichomo kwa wakati husika.
Hakika hata yule bingwa wa kujibadili kinyonga haoni ndani.
Angalia kwa mfano mazungumzo ya simu ya kiumbe huyu
Miaka kumi nyuma wakati kulifahamika kwa sifa ya Mchumba wa mtu
Sweetheart Habari za asubuhi!
Nzuri tu dear, sijui wewe!
Aa, mimi hali yangu sio nzuri kabisa
Ee nini tena Dear!
Nimekumiss mpenzi wangu, hata usiku mzima wa jana nakuota tu!
Jamani pole sana mpenzi
Asante lakini haitoshi darling! Hivi kwanza leo nitakuona saa ngapi?
Sijui wewe labda unifuate wakati wa lanchi!
Ok basi, wife to be endelea na kazi huku ukiendelea kukumbuka ule wimbo wangu ninaoupenda kukuimbia.
Mh? Upi tena huo dear?
Aaah unaniangusha darling! Si ule wa oh my sweet, my sugar, let me love you forever, oh yes umeukumbuka?!
Aaa! Huo! Basi nimeukumbuka! Dear!
Bye, nibusu basi
Baadaye dear, kuna watu hapa!
Ok basi!
Haya basi miaka kumi na mbili na watoto wanne baadaye hiki kiumbe mwanaume sasa kina hadhi ya mume wa mtu na sasa tunakutana nacho kikipiga simu kwa yulee mtu aliyekuwa mchumba wake miaka kumi na mbili nyuma na ambaye sasa anakwenda kwa hadhi ya mkewe. Mazungumzo yao kwenye simu sasa ni makavu kama mtumba wa Manzese ..!
Hujambo?
Sijambo! Za kazi?
Safi , hawajambo hao?
Hawajambo tu!
Huyu aliyekuwa anaharisha vipi!
Anaendelea vizuri, nimempa enthoromycin naona inamsaidia
Sawa, huyo fundi wa TV naye keshafika?
Sijamuona!
Sawa, akija muangalie sana asiibe vitu kwenye hiyo TV!
Sawa, sasa Baba nani .!
Unasemaje?
Kuhusu ile losheni
Umeshaanza Nimesema nitakununulia
Jamani Baba nanii.....! Mwezi wa pili sasa, kila siku unaniambia hivyo hivyo!
Alaa? Tumeshaanza kuhesabiana siku sasa!
Basi yaishe! Mimi nilikuwa nakukumbusha
Haya, mimi nitachelewa kurudi nyumbani kidogo kuna jamaa naenda kumcheki nikitoka kazini
Sawa
Baadaye basi
Sawa
Kiumbe kiitwacho mwanaume kinamaliza kuongea na Mkewe na kukata simu. Bila shaka utapata taabu kukubali kwamba huyo ndiye yule yule aliyekuwa naongea kwenye simu ya kwanza miaka kumi na mbili iliyopita. Bila shaka pia ukajiuliza, yako wapi maneno yale darling, sweetheart, mpenzi na wimbo ooh my sweet, my sugar, sasa yamekuwa ni bidhaa adimu mdomoni mwa mume na masikioni kwa mkewe. Lakini ni kweli kwamba maneno haya yamekuwa bidhaa adimu kwenye mdomo wa kiumbe hiki, mume?
Hebu tusikilize simu hii ya mwisho ya kiumbe huyu dakika chache tu baada ya kuongea na mkewe anaongea na simu hii akiwa amevua ile hadhi ya mume na kujivika mwenyewe bila kushurutishwa na mtu, hadhi ya buzi na anayeongea naye ni kiumbe mwenye hadhi ya mchuna buzi. Patamu hapo, babuyangu!
Haloo, darling
Haloo mambo
Poa! Unafanya nini sasa hivi darling wangu?
Aaa nipo tu natengeneza nywele zangu!
Yees! Zitengeneze vizuri ule mtindo ninaoupenda, jioni nitapitia hapo nikupeleke ukapate vikuku na vikopo viwili vitatu!
Sawa darling! Halafu dear, vipi kuhusu vile vitenge vya Zaire wanavyopitisha wale kinamama niliokuambia?
Darling na wewe! Si nilishakuambia wakipitisha tena we chukua tu pea mbili halafu uniambie tu mimi nitakupa pesa?
Asante ! Na vile viatu je?
Darling sasa unataka kuniudhi nimeshakuambia kuwa sio lazima uniombe ruksa kila kitu we chukua halafu unaniambia mi nakupa hela, sawa?
Sawa mpenzi, nashukuru saana!
Wee endelea kujitayarisha, mi nikimaliza tu kazi hapa nakuja kukupitia, au vipi!
Sawa halafu nakumiss ile mbaya!
Mi pia
Asuu, haayo maumbile yako yananipendeza!
Jamini mpenzi! Hivi wenzako hawakusikilizi kweli hapo!
Watajaza! Asuu roho ingekuwa nguo ningekuazima univae hadi milele eeeee....!
Bwana hebu acha!
Ok basi darling, tutaonana baadaye!
Haya, dear!
Ni cha ajabu kutokana na uwezo wake wa kubadilika kufuatana na mazingira kilichomo kwa wakati husika.
Hakika hata yule bingwa wa kujibadili kinyonga haoni ndani.
Angalia kwa mfano mazungumzo ya simu ya kiumbe huyu
Miaka kumi nyuma wakati kulifahamika kwa sifa ya Mchumba wa mtu
Sweetheart Habari za asubuhi!
Nzuri tu dear, sijui wewe!
Aa, mimi hali yangu sio nzuri kabisa
Ee nini tena Dear!
Nimekumiss mpenzi wangu, hata usiku mzima wa jana nakuota tu!
Jamani pole sana mpenzi
Asante lakini haitoshi darling! Hivi kwanza leo nitakuona saa ngapi?
Sijui wewe labda unifuate wakati wa lanchi!
Ok basi, wife to be endelea na kazi huku ukiendelea kukumbuka ule wimbo wangu ninaoupenda kukuimbia.
Mh? Upi tena huo dear?
Aaah unaniangusha darling! Si ule wa oh my sweet, my sugar, let me love you forever, oh yes umeukumbuka?!
Aaa! Huo! Basi nimeukumbuka! Dear!
Bye, nibusu basi
Baadaye dear, kuna watu hapa!
Ok basi!
Haya basi miaka kumi na mbili na watoto wanne baadaye hiki kiumbe mwanaume sasa kina hadhi ya mume wa mtu na sasa tunakutana nacho kikipiga simu kwa yulee mtu aliyekuwa mchumba wake miaka kumi na mbili nyuma na ambaye sasa anakwenda kwa hadhi ya mkewe. Mazungumzo yao kwenye simu sasa ni makavu kama mtumba wa Manzese ..!
Hujambo?
Sijambo! Za kazi?
Safi , hawajambo hao?
Hawajambo tu!
Huyu aliyekuwa anaharisha vipi!
Anaendelea vizuri, nimempa enthoromycin naona inamsaidia
Sawa, huyo fundi wa TV naye keshafika?
Sijamuona!
Sawa, akija muangalie sana asiibe vitu kwenye hiyo TV!
Sawa, sasa Baba nani .!
Unasemaje?
Kuhusu ile losheni
Umeshaanza Nimesema nitakununulia
Jamani Baba nanii.....! Mwezi wa pili sasa, kila siku unaniambia hivyo hivyo!
Alaa? Tumeshaanza kuhesabiana siku sasa!
Basi yaishe! Mimi nilikuwa nakukumbusha
Haya, mimi nitachelewa kurudi nyumbani kidogo kuna jamaa naenda kumcheki nikitoka kazini
Sawa
Baadaye basi
Sawa
Kiumbe kiitwacho mwanaume kinamaliza kuongea na Mkewe na kukata simu. Bila shaka utapata taabu kukubali kwamba huyo ndiye yule yule aliyekuwa naongea kwenye simu ya kwanza miaka kumi na mbili iliyopita. Bila shaka pia ukajiuliza, yako wapi maneno yale darling, sweetheart, mpenzi na wimbo ooh my sweet, my sugar, sasa yamekuwa ni bidhaa adimu mdomoni mwa mume na masikioni kwa mkewe. Lakini ni kweli kwamba maneno haya yamekuwa bidhaa adimu kwenye mdomo wa kiumbe hiki, mume?
Hebu tusikilize simu hii ya mwisho ya kiumbe huyu dakika chache tu baada ya kuongea na mkewe anaongea na simu hii akiwa amevua ile hadhi ya mume na kujivika mwenyewe bila kushurutishwa na mtu, hadhi ya buzi na anayeongea naye ni kiumbe mwenye hadhi ya mchuna buzi. Patamu hapo, babuyangu!
Haloo, darling
Haloo mambo
Poa! Unafanya nini sasa hivi darling wangu?
Aaa nipo tu natengeneza nywele zangu!
Yees! Zitengeneze vizuri ule mtindo ninaoupenda, jioni nitapitia hapo nikupeleke ukapate vikuku na vikopo viwili vitatu!
Sawa darling! Halafu dear, vipi kuhusu vile vitenge vya Zaire wanavyopitisha wale kinamama niliokuambia?
Darling na wewe! Si nilishakuambia wakipitisha tena we chukua tu pea mbili halafu uniambie tu mimi nitakupa pesa?
Asante ! Na vile viatu je?
Darling sasa unataka kuniudhi nimeshakuambia kuwa sio lazima uniombe ruksa kila kitu we chukua halafu unaniambia mi nakupa hela, sawa?
Sawa mpenzi, nashukuru saana!
Wee endelea kujitayarisha, mi nikimaliza tu kazi hapa nakuja kukupitia, au vipi!
Sawa halafu nakumiss ile mbaya!
Mi pia
Asuu, haayo maumbile yako yananipendeza!
Jamini mpenzi! Hivi wenzako hawakusikilizi kweli hapo!
Watajaza! Asuu roho ingekuwa nguo ningekuazima univae hadi milele eeeee....!
Bwana hebu acha!
Ok basi darling, tutaonana baadaye!
Haya, dear!
(kwa mnaopenda kuzodoa wadesaji, nakiri kabisa hii kitu ni cut n paste)