Mwanaume hakwepi, atakuona tu! sharti utabasamu

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,139
Mwanaume hakwepi, atakuona tu!



Tabasamu hufungua dirisha la Upendo na kujiamini.
Mungu alituumba wanadamu kwa namna ambayo mwanaume huvutiwa na mwanamke kama sumaku hata hivyo kuna wakati mtu hujikuta nguvu ya jinsi tofauti kuvutwa na yeye inakuwa hakuna.Hali huwa mbaya zaidi kwa akina dada hasa wale ambao muda wa kuolewa umefika na hakuna dalili ya mwanaume yeyote kuvutiwa naye.

Wanaume hutafuta mwanamke ambaye anavutia, mrembo, anafurahisha kuwa naye pamoja.
Mwanamke ambaye mwanaume hujisikia proud kuwa naye, anayeongea kirahisi bila kulalamika, ambaye anajiamini, anayejifahamu yeye ni nani bila kuyumbishwa na upepo wa aina yoyote.
Lakini kuna mambo matatu muhimu sana kwa mwanamke na yakiwa sehemu ya maisha yake basi mwanaume atafanya kila analoweza kuhakikisha anakuwa ndani katika maisha yake na kumpa chochote anahitaji.


Lengo ni mwanamke kujizoesha yafuatayo kuwa sehemu ya maisha yake na hatimaye mwanaume kuvutiwa naye.

Mwanamke mwenye tabasamu
Hii ni silaha yenye nguvu na ya uhakika kwa mwanamke.
Mwanamke mwenye tabasamu anarahisisha kwa mwanaume kumuona ni mwenye kujiamini na mchangamfu.
Wanawake wengi huwa na woga jinsi ya kuonekana mbele ya mwanaume na matokeo yake hubania tabasamu, kitu ambacho hupunguza attraction kwa mwanaume.
Pia tabasamu ni alama ya kukubaliwa, wanaume mara nyingi huhitaji message inayompa usalama kwamba mwanamke anaye kutana naye kuna usalama hata kabla hajajitambulisha.

Mwanamke anayeongea na kusikiliza bila kuwa ndo muongeaji (dominate)
Wanaume nao hupenda kusikilizwa, mwanaume huhitaji mwanamke ambaye anachonga sana na yeye kuishia kuwa msilikizaji tu.
Wanaume wengi ni kweli huwa wanategemea mwanamke kuwa mwongeaji pia hawako tayari kuwa wasikilizaji tu.
Mwanamke anayeongea na kusikiliza bila kung’ang’ania kuongea mwenyewe tu wanaume huwafurahia sana na hapo uwezekano wa kuolewa naye huongezeka.

Mwanamke anayevaa kimwanamke
Tunafahamu kwamba wanaume huvutiwa na vile wanaona (visual). Wanawake pia hujisahau kwamba wanaume huvutiwa na wakati mwingine kuchanganyikiwa kabisa na vile mwanamke unaonekana kwa nje kuanzia mavazi.
Kama unataka kuonwa na wanaume Hakikisha unajua na kupanga vizuri utoke vipi kwa pamba zako.
Kwa kadri mwanamke anavyovaa nguo soft (feminine) ndipo wanaume huwezi kumuona, hapa nina maana kuvaa kama​
 
Je wale wanaotembea msitari wa ikweta kule nyuma ukionekana ina maana hawataolewa?
 
Back
Top Bottom