Mwanaume ampe mkewe asilimia ngapi ya mshahara

Inatakiwa mtupe 10% kwa ajili ya matumizi binafsi, halafu inayobaki mtakuwa mnaacha hela ya chakula na matumizi ya watoto kila siku.
 
Jiulize kwanza anajua kutunza hela??

Ana akili ya maendeleo??

Kuna mtu alimuacha mke na mimba ya mwezi 8 na hajamrudia hadi leo????

Alikuwa Ana goli la kuchoma nyama choma Arusha,kila siku Ana mpa mke elfu 20 aweke toka mimba imeanza hadi mimba Ina miezi nane.Kila siku mama tunza hiyo itatusaidia tukipata mtoto hapo na hela ya chakula anatoa na nyama anarudi nayo karibu kila siku...

Miezi nane imefika, mwanamke inabidi aende kujifungulia kwa mama ake maana jamaa Ni yatima, mwanaume anauliza ile pesa iko wapi tujue unaenda na sh ngapi kwa mama, Mwanamke anasema Ana laki na ishirini..miezi 8 *30*20,000=milioni 5 kasoro hiyo.Mara nilimlipia mdogo wangu Ada mara nilinunua sijui mavitu gani.Jamaa alilia kama mtoto.

Baada ya hapo akasusa mtoto na akamwambia mwanamke ukienda kamwe usitie mguu wako kwangu.Kaoa saivi na Ana nyumba tyr.
TULISHAONYWA KUISHI NAO KWA AKILI,KUISHI KWA AKILI NI PAMOJA NA KUJUA AKILI ZA MKEO AU MPENZIO.
 
Wanawake hawajawahi tosheka na hela hata siku moja.
Msome kwanza mkeo yukoje ndio uone anastahili kupewa kiasi gani.
Asije akawa Ni wale akiona hela atamaliza fasheni zote za katani wanazofunga vichwani mwao na familia ikateseka.
Wanawake wengine inakubidi baba ununue kila kitu Cha mwezi mzima ndio Mambo yataenda.

In short hakuna general rule.
Sure, kila baby na baby wake
 
Hivi wanawake wenyewe hawanaga hela, hadi ifikie kwamba eti "umpe sh.ngapi?" sipendi mie hiyo tabia ya kujiona wanaume ndio wenye hela sisi hatuna.
mxewweeew kwani nyie ndio mnaojua kutafuta hela wanawake hawajui.
 
Mwanamke mkalishe chini mwambie apige hesabu ya chakula cha mwezi mzima,kisha chukua fungu lake mpe ,usisahau kumpa na extra money na matumizi yake,ila hakikisha asijue unapata kiasi gani?hapa kwenye mshahara ndio huwa pana mtihani kidogo ila jitahidi umtimizie mahitaji yake lakini asijue mshahara wako ni kiasi gani ,Leo unaweza usinielewe lakini iko siku utanielewa nilikuwa namaanisha nini
 
Gawaneni nusu kwa nusu, kama unapokea M1, MPE laki5 mwambie tutaonana mwezi ujao hapo ikiwa matumizi ya mwezi mzima pamoja mambo mengine yanayohusu jikoni.

Lakini haisiki na bill yoyote ada na gas, mkaa juu yko baba mjengo, hapo mtaishi kwa amani wala hatutawapiga vibomu snaa maisga saaafiii
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom