Ushauri hapa jf ni bure bila gharama. Ila gharama ni kuutekeleza.
Kwanza; Je, umemuoa? Mna muda gani tangu mkae pamoja? Umemsoma vizuri kitabia?? Je ana mipango mizuri ya maendeleo?
Hayo ndiyo yatakupelekea umpe mshahara wako wote au umpe tu hela ya chakula kila siku. Unaweza amua kwenda weka pesa yako kwenye duka la Mangi uwe ukichukua hapo kidogo kidogo kila siku jioni. Umuachie mkeo kwani hata ukimpa ruksa kwenda kuchukua mwenyewe kwa Mangi, atakuibia.
Wapo wanawake yaani ni ngekewa tupu. Ukimwachia elfu 5 kwa siku, mnakula hadi mnashiba. Unga kidogo tu, unaumuka ka kaweka amira. Wapo wengine hata ukileta unga kg 5 hautoshi ugali. Sio kwamba kaumwaga. Hapana. Ni mkono wake tu mbaya.
Hivyo kwamba umwachie kiasi gani, itatokana na hayo hapo juu
Kwanza; Je, umemuoa? Mna muda gani tangu mkae pamoja? Umemsoma vizuri kitabia?? Je ana mipango mizuri ya maendeleo?
Hayo ndiyo yatakupelekea umpe mshahara wako wote au umpe tu hela ya chakula kila siku. Unaweza amua kwenda weka pesa yako kwenye duka la Mangi uwe ukichukua hapo kidogo kidogo kila siku jioni. Umuachie mkeo kwani hata ukimpa ruksa kwenda kuchukua mwenyewe kwa Mangi, atakuibia.
Wapo wanawake yaani ni ngekewa tupu. Ukimwachia elfu 5 kwa siku, mnakula hadi mnashiba. Unga kidogo tu, unaumuka ka kaweka amira. Wapo wengine hata ukileta unga kg 5 hautoshi ugali. Sio kwamba kaumwaga. Hapana. Ni mkono wake tu mbaya.
Hivyo kwamba umwachie kiasi gani, itatokana na hayo hapo juu