Mwanaume ampe mkewe asilimia ngapi ya mshahara

Mung Chris

JF-Expert Member
Sep 12, 2017
3,367
3,778
Mwanaume akishapokea mshahara anatakiwa ampe mkewe asilimia ngapi ya mshahara na asidai pesa nyingine hadi mwezi ujao, pesa hizo ni pamoja na pesa za chakula, matumizi yake na matumizi ya watoto
 
Mpe wote tu hasa kama huyo mwanamke ni mtunza pesa na mpenda maendeleo.
Baadhi ya wanawake huleta maendeleo sana kwenye familia.
Ukiwa na shida anakupa kiasi nawepia kazini unajiongeza unakuwa na OT zako au kazi za ziada, hizo ndio utatoka nazo mara moja moja na kina Arushaone kwenye mambo ya maji ya rangi ya mende.

Jiongeze.
 
Wanawake hawajawahi tosheka na hela hata siku moja.
Msome kwanza mkeo yukoje ndio uone anastahili kupewa kiasi gani.
Asije akawa Ni wale akiona hela atamaliza fasheni zote za katani wanazofunga vichwani mwao na familia ikateseka.
Wanawake wengine inakubidi baba ununue kila kitu Cha mwezi mzima ndio Mambo yataenda.

In short hakuna general rule.
 
Jiulize kwanza anajua kutunza hela??

Ana akili ya maendeleo??

Kuna mtu alimuacha mke na mimba ya mwezi 8 na hajamrudia hadi leo????

Alikuwa Ana goli la kuchoma nyama choma Arusha,kila siku Ana mpa mke elfu 20 aweke toka mimba imeanza hadi mimba Ina miezi nane.Kila siku mama tunza hiyo itatusaidia tukipata mtoto hapo na hela ya chakula anatoa na nyama anarudi nayo karibu kila siku...

Miezi nane imefika, mwanamke inabidi aende kujifungulia kwa mama ake maana jamaa Ni yatima, mwanaume anauliza ile pesa iko wapi tujue unaenda na sh ngapi kwa mama, Mwanamke anasema Ana laki na ishirini..miezi 8 *30*20,000=milioni 5 kasoro hiyo.Mara nilimlipia mdogo wangu Ada mara nilinunua sijui mavitu gani.Jamaa alilia kama mtoto.

Baada ya hapo akasusa mtoto na akamwambia mwanamke ukienda kamwe usitie mguu wako kwangu.Kaoa saivi na Ana nyumba tyr.
 
Back
Top Bottom