Mwanaume aliyempa talaka mke wake na kumuoa mfanyakazi wao wa ndani huko Zambia

Endelea kushupaza shingo. Habari yako kwanza mkuu? Ukoje na hali?

Mke ni mlezi wa familia ninaposema mlezi nazani naeleweka.. baba ni mtafutaji na mtunza familia ndio maana akaitwa kichwa cha familia. Majukumu yote yanayousu nyumba ni ya mke, baba kazi yake ni kutafute mpate kupata maitaji yote muhimu hapo nyumbani.

Kwa mtazamo wako sina hakika kama umeolewa ( niwieradhi kama nitakukwaza) na kama umeolewa kama huna nguvu ya ziada kumzibiti huyo mwanaume jiandae kulimwa taraka, vinginevyo ziwe story za kijiweni tu umeleta hapa
Huyo hawezi kuwa mke wa mtu huyo. Atakuwa single maza tu
 
Mwanamke sio kijakazi na akisahau hukumbushwa yeye ni nani. Amezaa tayari nimtu aliyechoka kukulelea watoto wako.

Hivi wanaume hebu chukueni upande wetu.
Unabeba mtoto miezi tisa hiyo miezi tisa tu kuibeba ni kazi halafu uje uzae ukishampata mtoto umnyonyeshe umfanye alale hadi azoee dunia na mazingira sio kazi rahisi ndio maana mama hueshimiwa huletewa msichana wa kazi ili afue ,apike , aoshe vyombo na ikiwezekana aletwe mwingine kwa ajili ya usaidizi.
Maisha ya kulea sio kazi rahisi ila wa baba kusaidia ni kazi sana .
Wao wanakuja tu wanakulalamikia kama yeye alizaliwa na baba chakula kiko wapi .
Hajui siku nzima ulipitia nini kulea nikazi.

Ila kama uyaya sawa.
Wewe unamakosa maana miezi sita tu ndio unapumzika.
Ila kama huna yaya kulea nikazi .
Huyo bwana hana akili si amesema yule mke wa mwanzo alifanya hayo mwanzoni ukiwa na familia try to understand you are wife mlikuwa wenyewe utatunzwa but if ukiwa na mtoto kwa heri baba.
Ukiwa mwelewa tafuta kipoozeo mke asijue .
 
Alimpenda tu huyo mfanyakazi akaamua kuhalalisha. Mengine yote ni kuhalalisha uhalali wa kukimbia mke.
 
Mimi naona huyo house girl ndio wanaendana na huyo mke wake itakuwa alikuwa anamuogopa hata kumuuliza kushindwa kutandika kitanda Ili ajirekebishe, haya sasa ngoja apambane na house girl na isije kuwa kampendea maisha mazuri akiishiwa anaachwa solemba anakuwa wa kuanza upya mpaka anazeeka.
 
Huyo mfanyakazi amshauri huyo mwanaume wasiishi katika nyumba hiyo maana ni Mali ya mke wa kwanza
Siku zote ndoa ni Amani,upendo,furaha na kushirikiana
Lakini atajirekebisha
Wengi wa hivyo wanapenda vitu na hivyo vitu ndo vimemvuta kwa huyo mwanaume, ifike mahali wanaume wajielewe huwezi kuwa wewe ni wa kuanza upya kila siku maana hapo kuna kulea mimba upya, kulea mzazi upya, kutunza vichanga upya wakati wenzio wanaongoza na watoto wao wakubwa wanapanga maisha.
 
Wengi wa hivyo wanapenda vitu na hivyo vitu ndo vimemvuta kwa huyo mwanaume, ifike mahali wanaume wajielewe huwezi kuwa wewe niwakuanza upya kila siku maana hapo kuna kulea mimba upya, kulea mzazi upya, kutunza vichanga upya wakati wenzio wanaongoza na watoto wao wakubwa wanapanga maisha.
ndio hivyo binadamu tunautofati
 
Hiyo picha ya mwanamke aliye peke yake, ndio Mke au mfanyakazi???

Kama ndio mkeo.. kwangu mimi kama hachepuki, hana dharau, awe ni sifa nyinginezo za mke bora.

Ilo la kazi ningemvumilia .
 
Wanaume wa kiafrika ndo akili zenu zilipoishia..unafikiri ukishaoa mke umejipatia na mfanyakazi wa ndani, yeye huyo mume alikua amekamilika kwa lipi?? Sijaona sababu ya kuacha mke hapo na huyo msichana wa kazi ajiandae baada ya miaka kadhaa na yy atatafutiwa sababu., kama ninkazi wanawake kibao wanafanya kila kitu kwa waume zao bado wanaachwa na kufanyiwa ushenzi..bado tuna safari ndefu sana kwa mtindo huu Africa itabaki kuwa bara la giza milele na milele

Halaf cha ajabu hawa wanaume wanaoongea ongea amevunja ndoa yake na mikono yake mwenyewe anataka yeye apikiwe afuliwe afanyiwe majukumu yote ya mume ajabu muulize yeye kamnunulia lini mkewe hata chupi utasikia maisha ni kusaidiana mara na yeye ana kazi anunue mwenyewe, hapo analalamika hvo si ajabu wote wanafanya kazi na wote wanachoka kwa kiwango kile kile bado mtu ana thubutu kusema hafui mara hatandiki alafu zikija bili mwanaume mzima anaweka mezani agawane na mkewe nyie wanaume weusi mna shida jamani yani sijui mna akili za aina gani
Unaambiwa mama hatimizi majukumu yake, ameyakaimisha kwa mdada wa kazi.....
 
Kuna la kujifunza.


Jambo gani la kujifunza???.

Huyo house girl aliajiriwa awe akifanya nini hapo nyumbani???--- mnamlaumu bure huyo Dada wa watu kwa kosa lisilokuwa lake, isitoshe huyo jamaa atakuwa ni womenizer tu na alikuwa hana utetezi mzuri kuhusu maamuzi yake isipokuwa kujitetea kwamba eti huyo Dada hakuwajibika!!--- awajibike wakati House girl si yupo kwa kazi hizo!!!---- angalisema wajibu wa chumbani hapo kidogo angekuwa na hoja.🤣🤣
 
View attachment 1713163
View attachment 1713185
Mwanaume huyu toka jamii kutoka Ndola aliamua kumuacha mke wake waliyeoana miaka saba iliyopita na kufanikiwa kupata watoto wawili. Mwanamke huyu alienda mahakamani ilikutafuta suluhu ya ndoa yake na maridhiano na mume wake, akiomba mahakama imsaidie kunusuru ndoa yake na kuongeza kuwa hajui kwanini mume wake aliamua kuchukua uamzi wa kumuacha na kuoa mfanya kazi wao wa ndani.

- Mwanamke huyu aliiambia mahakama kuwa anampenda mume wake na haamini kama kweli ameamua kufanya kitu kama kile na kutaka kujua sababu zilizopelekea mume wake afanye hivyo.

- Mahakama ilipomuuliza mwanaume juu ya suala hilo alisema hawezi kubadili msimamo wake na hawezi kumuacha mke wake mpya wala hawezi kumrudia mke wake wa zamani maana maamzi yake ndio yalikuwa yameshafika mwisho na kushukuru kumpata mtu sahihi kwake na kusema mwanzo alifanya makosa kwenye kuchgua mke bila yeye kumjua mwanamke huyo vizuri.
Akaendelea kuaiambia mahakama kuwa mke wake huyo wa zamani alikuwa mzembe kupita kiasi, hakuweza hata kufanya kazi za ndani zinazomhusu kama mama wa familia na badala yake hata yale majukumu yake kwa mumewe aliyaacha mikononi mwa mfanyakazi wao wa ndani ambaye alijikuta kuwa ndio msaada mkubwa kwa mwanaume huyu , mfanyakazi wao wa ndani ndio aliyefua nguo zote za mwanaume huyo huku mke wake akiwa hana habari nae, hakutaka hata kukaa na kuongea na mume wake isipokuwa mfanyakazi wa ndani alikuwa akimuona amerudi toka kazini anampokea na kumuandalia maji ya kuoga, kisha anampa chakula na kukaa na kuongea nae sebuleni huku akimpa pole kwa uchovu na kumtia nguvu pindi anapoonekana kuchoka sana au kuwa na mawazo.

-Kuhusiana na suala hilo wazee walishawakalisha chini na ili kuwapatanisha bila mafanikio yeyote kwa wanandoa hao.

Alichokuwa akikifanya mwanamke huyu nyumbani ni kuwa bize kutoa maelekezo kwa mfanyakazi huyo wa ndani na kumfokea muda wote na kuwa bize na simu huku mfanya kazi wa ndani akiwa bize na mwanaume baba wa familia, hivyo niliona kila mtu abaki na kitu anachopenda kuwa bize nacho muda wote, mfanyakazi wa ndani anapenda kuwa bize na baba wa familia basi ni vyema awe nae aliatimize majukumu yake kwa baba wa familia vizuri, na mke wake kwa sababu yuko bize na simu basi nimuachie nafasi akae na kuchati kwa uhuru ili kila jambo liende sawa pia kwa upande wake.
Mume aliendelea kusema hata siku za mwisho wa juma (weekends) akiwa hayuko kazini mwanamke hakuona umuhimu wa kupika chakula kwa ajili ya mume wake kama alivyokuwa akifanya siku za mwanzo wa ndoa yao,badala yake alikuwa akifanya maandalizi ya kwenda kwenye sherehe za harusi na kamati za Kitchen Party, anarudi amelewa kitu ambacho mwanzo alikuwa hafanyi, na kama angekuwa anafanya nisingemuoa kabisa.

-Mume akaenda mbele zaidi na kuiomba mahakama iangalie kwa makini kucha ndefu za mwanamke huyo kama kweli zinaonesha mwanamke anayeweza kujishughulisha na shughuli za nyumbani kama mke wa mtu, muulizeni ana miaka mingapi hajawahi kupika chakula, kufanya kazi za nyumbani zaidi ya kuagiza, nani amekuwa akitandika kitanda changu kwa muda wa miezi nane sasa ?, Ni lini amejishughulisha hata kutunza na kuangalia watoto kama kweli ni mwanamke anayefaa kuwa mke, hayo yote mfanyakazi wa ndani ambaye ni mke wangu sasa ndio amekuwa akiyafanya siku zote.

Baada ya mahakama kujiridhisha na maneno ya mume ikatengua ndoa hiyo ili sasa mwanamke aendelee kuchat bila kikomo, ahudhurie sherehe za fungate, harusi na kufuga kucha huku mfanyakazi wa ndani akiwa boss ndani ya nyumba mwenye kujua na kujali majukumu yake kwa undani.

Wanaweke wengi huyajua makosa yao na ukimya wa mwanaume humfanya ayaendeleze bila kujua mwanaume muda mwingine yuko kimya akiwaza hatima ya jambo hilo na mwisho anaweza kuja na uamzi mwingine

Kuna la kujifunza.
Sasa huyu mtumishi naye akishazoea tu, ataanza kufanya yaleyale aliyokuwa anafanya huyu mtalikiwa
 
81 Reactions
Reply
Back
Top Bottom