Adrian Stepp
JF-Expert Member
- Jul 1, 2011
- 2,764
- 2,581
Mkuu samahani kama nitakaloongea litakuudhi
Ila napenda sana kukuomba na nanua wewe ni muumini na unajua uwepo wa Mungu katika maisha yako
Najua ni jambo baya sana alilotenda huyo ambaye ni baba yako kutokuwa karibu na wewe au kujua au kushiriki katika malezi yako
Ila naomba nikuombe sana watu wanasema mkono ukinyewa na mtoto huukati ule mkono ila unaufuta na kuuosha na maji na unaendelea na mambo mengine
Limekwishatokea maishani mwako na baba yako kutokuwa karibu na yeye ila nikuombe tena samahani sana msamehe na mpe nafasi ile ya kuwa baba yako japo kumuona na kujua kuwa huyu ndie baba yangu yatosha
Inatosha kumjua ila usimpe nafasi ya kukupangia lolote la maisha yako maana kwa sasa naamini una mipango yako na una mambo yako umekwishajiwekea ya maendeleo yako
Mpe nafasi, msamehe kwa makosa yake na muombee Mungu hata watoto wake wasiwe kama yeye kuwakataa watoto wao
Msamehe na mwachie Mungu ampe kile anachostahili ila usichukue nafasi ya kuweka kisasi moyoni mwako kwa ajili ya yale aliyokutendea
Maandiko yanasema mwachie Mungu kulipa kisasi na usilipize kisasi kwa mtu yoyote
Samahani sana kama nitaharibu siku yako
Nimesha msamehe buree ndo mana sitaki hata kumuona..kwanza nimsamehe ili iweje??