Mwanaume akikataa mimba au kukutelekezea mtoto, usitumie majina yake Kwa mtoto wako

Taikoni umekuwaje siku hizi mkuu??

Yaani usimfundishe mtoto kumchukia baba yake na wakati huohuo cheti chake kina jina la mjomba??

Kama mama kashaanza kuonesha chuki kwa kubadili jina mtoto lazima afate tu..

Na kumbuka kuna muda Me hukataaimba kwasababu za ukata, mambo yakiwanyookea huja kumgomboa mtoto au huonagi hilo la mtoto kugombolewa na familia ya kiumeni!!

Baba kakataa mimba.
Baba kakataa kulea mtoto.

Sasa kwa nini mtoto aitwe kwa Jina lake?
Sio ishu ya chuki ili ni ishu ya Haki na wajibu

Mtoto anaweza kuitwa majina yako na ukaishi naye na ukamhudumia na akakuchukia licha ya kuwa Mama yake hayupo
 
Hayajamkuta ndio maana anaona rahisi tu kuandika nadharia hapa jukwaani
Naam huyu bado huyu.
Unakuta familia inakukalia kikao, uamuzi unapita upotezwe kwa namna yoyote haswa ushirikina.
Aisee sitasahau maisha yangu yoote.
Na mpaka sasa,hata nikitaka kumuhudumia mtoto hawataki maana kuna mazingira wanayatengeneza nionekane nimemkataa na simtunzi mtotoo.
Sio kila familia ni ya kuoa
 
Naam huyu bado huyu.
Unakuta familia inakukalia kikao, uamuzi unapita upotezwe kwa namna yoyote haswa ushirikina.
Aisee sitasahau maisha yangu yoote.
Na mpaka sasa,hata nikitaka kumuhudumia mtoto hawataki maana kuna mazingira wanayatengeneza nionekane nimemkataa na simtunzi mtotoo.
Kuoa familia masikini ni hatari sanaa.
Mkuu io situation yako ndio naipitia wakati huu sasa yani ni matatizo sana adi mtu unawaza kumtelekeza tu akae na lifamilia lake huko kwasababu wanajidai kama wanaweza kulea nk mara ghafla wanalalamika utoe pesa then ghafla wana block namba zako ili ukiwatafuta uonekane mwenye shida na wajisikie raha unavyo hangaika sasa watu kama hawa mwanaume akiwapotezea atalaumiwa kweli yani adi mtu unashindwa kufanya kazi kwa ufanisi kisa wapumbavu wachache
 
Mkuu io situation yako ndio naipitia wakati huu sasa yani ni matatizo sana adi mtu unawaza kumtelekeza tu akae na lifamilia lake huko kwasababu wanajidai kama wanaweza kulea nk mara ghafla wanalalamika utoe pesa then ghafla wana block namba zako ili ukiwatafuta uonekane mwenye shida na wajisikie raha unavyo hangaika sasa watu kama hawa mwanaume akiwapotezea atalaumiwa kweli yani adi mtu unashindwa kufanya kazi kwa ufanisi kila wapumbavu wachache
Sasa mtu kama ww hata mtu akiongea unamuelewa kwa kuwa tayari ushapitia uhalisia.
Ndugu hapo ni kukaa kimya tuu liwalo na liwe mtoto akikua atakutafuta tuu.
Ulimwengu huu wa smartphone uongo unajitenga mapema saana.
Elekeza nguvu kwenye kutafta pesa huku ukihakikisha kile kinachoendelea jamii inakijua.
 
Dah mkuu hii comment yako ni ya 2022 lakini hiki kitu kimenitokea mimi mwaka huu 2024 hakika mwanamke ni kiumbe wa ajabu sana ana block namba zote hataki mawasiliano hapo mtu unatoaje huduma na hataki ata ukue yuko wapi na mtoto aseeee inabidi mtu ukae kimya japo unaumia na mtoto anateseka kwasababu ya tabia za mama yake kujifanya anaweza mambo yote
Ni wazazi wenzetu lakini wengi bado vichwani wanautoto wa hali ya juu. Vumilia tu mkuu kuna siku atarudi kukutafuta. Kuna rafiki yangu imemtokea kisa kama hicho. Kazaa nae mtoto mmoja, mwanamke akakata mawasiliano eti anataka kuwa huru na maisha yake. Baada ya mwezi mmoja. Yule mwanamke akaanza kumtafuta tena jamaa kwamba anashida amsaidie. Sasa unajiuliza mwanamke kama huyu kichwa chake kipo sawa sawa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wazazi wenzetu lakini wengi bado vichwani wanautoto wa hali ya juu. Vumilia tu mkuu kuna siku atarudi kukutafuta. Kuna rafiki yangu imemtokea kisa kama hicho. Kazaa nae mtoto mmoja, mwanamke akakata mawasiliano eti anataka kuwa huru na maisha yake. Baada ya mwezi mmoja. Yule mwanamke akaanza kumtafuta tena jamaa kwamba anashida amsaidie. Sasa unajiuliza mwanamke kama huyu kichwa chake kipo sawa sawa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Inaumiza sana mkuu mara ghafla wanaibuka na kusema kama hutoi pesa za matumizi acha na uyu mtoto usimjue tena yani mambo ya hovyo kabisa mtu anakua kama nakubabaisha mara tuma pesa hapo hapo anasema kama hutaki acha aseeee ni kipengele.
 
Inaumiza sana mkuu mara ghafla wanaibuka na kusema kama hutoi pesa za matumizi acha na uyu mtoto usimjue tena yani mambo ya hovyo kabisa mtu anakua kama nakubabaisha mara tuma pesa hapo hapo anasema kama hutaki acha aseeee ni kipengele.
Nachoweza kukushauri mkuu, usitume chochote mpaka mzazi mwenzako atakapoona umuhimu wako. Kwa sasa wanakuchezea akili yako kwasababu wanakuona hauna msimamo. Kenge hasikii mpaka damu imtoke masikioni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si kila kitu cha kupeleka mahakamani.
Kuna mambo yakupasa unyamaze tuu ukiusoma mchezo.
Kukaa kimya kutakuepusha na mengi saana tena saanaa tuu.
Weka mikono 🙏muda wa ukweli ukifika hujidhihirisha.

Basi msilalamike watoto wakiitwa majina kutoka upande wa Mama zao ikiwa mimba zao zilikataliwa na Mama zao walitelekezwa
 
Baba kakataa mimba.
Baba kakataa kulea mtoto.

Sasa kwa nini mtoto aitwe kwa Jina lake?
Sio ishu ya chuki ili ni ishu ya Haki na wajibu

Mtoto anaweza kuitwa majina yako na ukaishi naye na ukamhudumia na akakuchukia licha ya kuwa Mama yake hayupo
Jina la baba ni kutokana na malezi au sababu za kibailojia??

Mbona kama unataka kupindisha sheria za ulimwengu ndgu??

Vipi mama akitelekeza wanae nae pia asitambiwe?? Kwenye cheti cha kuzaliwa aandikwe dada au mama wa baba yake??

Baba ni baba hata aweje ni baba yako, akukatae, akukubali, akukimbie itabaki hivyo milele, kamwe mjomba hawezi kua baba.

Mnaharibu maadili ndio maana vibinti vinazaa hovyo na kuleta vijukuu nyumbani. Huku kwa jeuri mkijiona mmemkomesha jamaa hamumpi mtoto jina la baba yake.
 
Kwema Wakuu!

Lazima tutende haki, lazima tuseme ukweli.
Wanawake wanamakosa Yao Kama tulivyo Sisi wanaume tunamakosa yetu.
Na mwenye makosa lazima aadhibiwe, na akiomba Msamaha sharti asamehewa lakini adhabu inaweza kubaki palepale.

Taikon huwaga ni mtu wa kuongea mambo magumu yasiyo rahisi, bila kujali yanamgusa Nani, iwe ni Mimi au wewe au Yule. Lengo ni kuweka mambo Sawa Kwa Haki. Ingawaje nafahamu Haki haitawezekana Kwa Asilimia .

Najua wapo wanawake walifanya makosa Kwa kujibebesha mimba kimakusudi Kwa wanaume Kwa malengo Fulani, mathalani
1. Kwa lengo la kuolewa
2. Kwa lengo la Mali
3. Kwa lengo kupendwa

Hata hivyo zipo mimba zilizoingia Kwa bahati mbaya(bila kupanga baina ya mwanaume na Mwanamke).

Makosa ni makosa tuu. Lakini haimaanishi watu waendelee kujilaumu Kwa makosa waliyoyafanya. Lazima maisha yaendelee.

Amekataa mimba!
Amekubali mimba lakini kakataa kumlea mtoto.
Amekubali lakini ameshindwa Kumlea mtoto.

Ikiwa Baba mzazi amekataa au kushindwa kumlea mtoto Kwa sababu yoyote Ile isipokuwa sababu ya kifo au Maradhi basi nakushauri Usimpe mtoto Ubin wa huyo Baba Mzazi.

Amua kumpa jina lolote lile utakalolipenda, aidha ni jina la Wajomba zake wanaokusaidia kumlea, au jina la Baba yako(Babu yake upande wa Mama).

Wala sio dhambi.
Wala hakuna shida yoyote.
Kila mmoja awajibike Kwa makosa yake.

Wakati wewe ukiitwa single Mother, ukitukanwa na kuonekana Malaya, au mwanamke usiyefaa, iwe ni kweli au sio kweli, iwe ni Kwa bahati mbaya au makusudi lakini akakataa na ukazalilishwa na kuyapitia machungu.

Ukamenyeka kumlea mtoto Kwa halali na haramu wakati Baba yake anayetakiwa kutoa matumizi yupo anarandaranda huko, hata Kama Hakuwa na chakutoa lakini hata salamu na kukutia moyo alishindwa, ninachoweza kukushauri ni kubadilisha tuu Ubin WA mtoto.

Hakuna atakayekuuliza,
Na hautaonekana mbaya popote pale.

Hoja ya Msingi hapa ni kuwa, atakayemlea mtoto ndiye mwenye mamlaka naye.
Yeye ndiye ataamua aitwe Nani, ataamua jina la pili na latatu liwe la Nani.

Maana Vijana wa siku hizi tumezidi sasa.

Iwe ni Mimi Taikon au Nani, Kama umezaa na Mimi alafu nikaleta uhuni wa kukataa mimba au kushindwa kuhudumia mtoto, usitumie jina langu. Sistahili.
Na mtoto huyo hastahili kutumia jina langu.

Wanawake msiwafundishe watoto wenu kuwachukia Baba zao, nyie waleeni Kwa maadili ya kimila na Kidini, tumieni majina mtakayopenda ninyi, watoto wanavyokua wanajionea na kujua ni zipi sababu za nyie mama zao kufanya mlio ya fanya.

Lakini jitahidini kuwa wema ili watoto wasijeona kuwa ninyi ndio Wabaya.

Wito Kwa Vijana; msikimbie mimba wala msikimbie Kulea watoto.
Hata Kama huna chochote kitu, angalau mjulie hali mtoto au mzazi mwenza. Mtie moyo, kubali kubeba lawama Kwa maana wanawake ni watu wa lawama hata ungemuoa, lakini wakitulia na kutafakari wenyewe wanaelewa.

Mwanamke ukiwa mwema kwake hata Kama huna kitu anajua, anajali ingawaje atakutolea maneno ya shombo. Lakini haiondoi ukweli kuwa nao wanajisikia vibaya unavyoteseka.

Lakini Kulea mtoto hulei,
Kusalimia husalimii wala kumjulia Hali,
Mwanamke akiwa mkali kwako nawe unajifanya kiburi na jeuri Kwa maneno ya kashfa.
Unafikiri hata ungekuwa wewe ungefanyaje?

Hapo ndipo wanaume tunapokosea.
Saikolojia ya Wanawake ni kuendeshwa na mihemko, kulia upesi na kutoa maneno ya shombo kwao ni ishu ya kawaida lakini haimaanishi hawajali wala haimaanishi hawana akili ya kushindwa kutuelewa.

Mwanamke anahitaji Upendo(kujaliwa, kutiwa moyo, kufarijiwa, kupewa maneno matamu na laini, kushauriwa,)
Ukiyaweza hayo mwanamke kama alikuwa na hisia na wewe hawezi kukuchukia hata Kama humlei mtoto wake. Kwani wanaelewa.

Kitu kingine, wanawake ndio viumbe pekee ambao wanaelewa watu wanaojali hisia zao.

Unaweza kumhudumia Mkeo kila kitu(materials) kamwe hawezi kumnyang'anya mtoto wa Baba mwingine aliyezaa naye akakupa wewe ikiwa Bwana huyo bado anamjali na kumpenda.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Single mama na watoto waliolelewa na single mama wamekuunga mkono.... je baba ambaye mtoto wake amepewa ubin wa mtu mwingine na anatakiwa amuhudumie mtoto hiyo ipo sawa??
 
Back
Top Bottom