Mwanasiasa sharti uwe na wafuasi siyo wapambe. Somo kutoka kwa Hayati Maalim Seif na Hayati Dkt. Magufuli

Imalamawazo

JF-Expert Member
Jul 27, 2021
1,342
3,234
Hawa miamba wawili waliotikisa siasa za Tanzania na Zanzibar kwa miaka ya hivi karibuni. Ulinganisho wao unatokana na ukweli kuwa wote walikuwa viongozi wa juu wa kisiasa na pia muda wao wa kiaga dunia ulikaribiana sana.

Kila mmoja kati ya viongozi hawa walikuwa na misimamo, falsafa na mitazamo iliyowajengea umaarufu mkubwa. Sasa baada ya miezi kadhaa bila uwepo wao tutaweza kutathimini ni nani aliyweza kujijengea wafuasi kwa wingi na wapambe wachache na yupi alijijengea wapambane kwa wingi na wafuasi kwa uchache? Je, ni mbinu zipi kiongozi wa kisiasa anaweza kuzitumia kupata wafuasi wengi badala ya wapambe wengi?

NB: Kwa ajili ya hii post neno wafuasi litamaanisha watu waliojifunza mitazamo na falsafa za kiongozi na kuziishi, lakini wapambe ni watu wanaosifia na kumpamba kiongozi bila kuwa na imani thabiti ya mitazamo na falsafa zake.
 
Pia kuna kundi moja limeshaanzisha wakfu wa kumuenzi kiongozi wao lakini kundi lingine bado linaomboleza kifo cha kiongozi wao lisijue ni nini cha kufanya
 
Magufuli na Seif walikuwa na wafuasi Wengi kuliko wapambe

Nilichogundua ni kuwa Magufuli alikuwa na wafuasi Wengi wanyonge kuliko wapambe wachache waganga njaa na wachumia tumbo Kama Ndugai nk.

Wapambe wengi ni viongozi ambao walikuwa tu wasaka vyeo na wataka kudumu nafasi zao wamo Hadi baadhi ya mawaziri na wabunge na viongozi serikalini na Ndani ya CCM ila wachache hawawazidi wafuasi wa Magufuli

Seif pia alikuwa na wafuasi Wengi na wachumia tumbo wapambe wachache viongozi ndani ya Chama wakiwemo Hamad Rashid , Proffesor Lipumba
 
Lakini kiongozi makini anapaswa kujua kama kazungukwa na wafuasi au amejirimbikizia wapambe wanaojali maslahi binafsi
Uko sahihi kipindi Cha Magufuli au Seif walijitajidi Sana lakini wao sio miungu watu wachumia tumbo Kama Ndugai waliweza kujipenyeza kumzunguka Magufuli pia watu Kama Hamad Rashid na Lipumba waliweza kumzunguka Seif Shariff Hamad

Anyway pamoja na kuzungukwa na wanafiki wachache Hadi wanafariki walikuwa na wafuasi wengi kuliko wapambe
 
Magufuli na Seif walikuwa na wafuasi Wengi kuliko wapambe

Nilichogundua ni kuwa Magufuli alikuwa na wafuasi Wengi wanyonge kuliko wapambe wachache waganga njaa na wachumia tumbo Kama Ndugai na nk. Wapambe wengi ni viongozi ambao walikuwa tu wasaka vyeo na wataka kudumu nafasi zao wamo Hadi baadhi ya mawaziri na wabunge na viongozi serikalini na Ndani ya CCM ila wachache hawawazidi wafuasi wa Magufuli

Seif pia alikuwa na wafuasi Wengi na wachumia tumbo wapambe wachache viongozi ndani ya Chama wakiwemo Hamad Rashid , Proffesor Lipumba
Mkuu umemaliza kila kitu
 
To be specific Mama Samia kwa Sasa kuzungukwa na wapambe sijui atafanyaje kujinasua Ushauri wangu asiongeze Sana Hilo kundi wabaya mno mwisho wa siku watamuweka Kati atake asitake watataka afanye wanayotaka vinginevyo watamkoma Aanze kuwa serious as a president atengeneze wafuasi sio wapambe kwake .Atakuwa toothless president.Aangalie Major kutafuta wafuasi asihangaike kutafuta wapay tu waimba Nani Kama mama ukiwauliza kwa lipi linaloonekana kwa kila mwananchi la umeme? La maji ? Nk unakuta wanatoa mimacho tu utafikiri mjusi kafiwa na mkwewe!!

Mama Samia bila kuwa na wafuasi Wengi kuliko wapambe itakusumbua.Kwa Sasa kwa assessment yangu Mama Samia ana wapambe sio wafuadi
 
Back
Top Bottom