Administer
JF-Expert Member
- Feb 9, 2020
- 930
- 1,408
Ukitaka kujua msimamo wa mwanasiasa au mtu mwingine yeyote apate majaribu kwanza.Hata mimi ninayeandika ukitaka kujua msimamo wangu katika jambo fulani nipe majaribu.
Sijui ni Tanzania tu au na kwingineko haya yanatokea.Unaweza kumsikiliza mwanasiasa fulani kwa misimamo yake,ukajiridhisha kweli huyu ana msimamo. Anaweza kuwa ni mpinga rushwa mkubwa na mnyenyekevu mkubwa katika chama na viongozi wake. Akipata majaribu anashiriki katika rushwa, anahamia kwenye chama ambacho kila siku alikua nahubiri ni chama cha watenda maovu.
Majaribu yenyewe ninayozungumzia hasa fedha au madaraka .Wanasiasa wengi wapo kwenye siasa kwasababu ya matumbo yao. Ukimsikia akisema tupo kwa ajili ya kuwatetea au kulinda maslahi ya watanzania uyue mtanzania wa kwanza ni yeye na familia yake
Sijui ni Tanzania tu au na kwingineko haya yanatokea.Unaweza kumsikiliza mwanasiasa fulani kwa misimamo yake,ukajiridhisha kweli huyu ana msimamo. Anaweza kuwa ni mpinga rushwa mkubwa na mnyenyekevu mkubwa katika chama na viongozi wake. Akipata majaribu anashiriki katika rushwa, anahamia kwenye chama ambacho kila siku alikua nahubiri ni chama cha watenda maovu.
Majaribu yenyewe ninayozungumzia hasa fedha au madaraka .Wanasiasa wengi wapo kwenye siasa kwasababu ya matumbo yao. Ukimsikia akisema tupo kwa ajili ya kuwatetea au kulinda maslahi ya watanzania uyue mtanzania wa kwanza ni yeye na familia yake