Marekani siyo kwamba imeshindwa kumkamata Netanyahu bali haioni sabanu ya kufanya hivyo. Kwani Netanyahu amefanya kosa gani?
Jamii ya kimataifa ilikosea sana. Mara baada ya lile shambulio lila la kigaidi la Hamas, ilitakiwa jamii nzima, hasa nchi za kiarabu, zilaani na zitoe tamko la kushirikiana na Israel kuwaangamiza Hamasi. Hiyo ingetoa nafasi ya kujadili jinsi ya kuwalinda raia, na namna ya kuwakamata Ha.as wote. Lakini kitendo cha baadhi ya nchi za kiarabu na makundi ya kigaidi kuamua kushirikiana na Hamas, ile ilitoa nafasi kwa Israel kutumia nguvu zake zote bila ya kujali magaidi wamejificha katika ya raia au wamekimbilia hospitali au shuleni. Na bila ya hasara kubwa upande wa Hamas, wangekuwa bado wanaishambulia Israel. Kwa kile walichokifanya Hamas dhidi ya Israel, hakuna nchi itakayomkamata Netanyahu, labda kama Israel ingeanza kuwaua wapalestina bila ya lile shambulio la Hamas.