Mwanasheria mkuu wa Serikali:Hakuna haja ya kuwa na katiba mpya,tuboreshe iliyopo

Mwanasheria mkuu wa serikali Werema amesema kuwa Tanzania inahitaji marekebisho tu katika katiba ya sasa na siyo kuandikiwa mpya.

Chanzo:TBC1 Habari saa 2:00 usiku

KWA KAULI HII YA WEREMA, SAED MWEMA AGIZA MABOMU YA KUTOSHA TUFUNGUE MWAKAMPYA UWANJANI MPAKA KIELEWEKE


Kuna kauli kibao zinazojikanganya kanganya kutoka kwenye Serikali ya Mhe Kikwete kuhusu kiu yetu sisi wananchi kujiandikia upya katiba yetu sasa hivi.

1. Makamba; HAKUNA NAFASI YA KUSIKILIZWA MTU HAPA,

2. Chiligati, CHADEMA WASILETE UTANI TUENDA BUNGENI KUWAFUKUZA wote,

3. Chiligati, aaahhh, haya madai ya CHADEMA ni ya msingi na YANAZUNGUMZIKA,

4. Kombani alianza na SUALA LA KATIBA HAPAN, NI GHARAMA NA WALA SI MUHIMU,

5. Mzee Tyson, kuhusu madai ya KATIBA sisi serikali TUNAZO ZILE NJIA ZETU NA WALA HUA HAZITANGAZWI,

6. Alipofika Jaji Mstaafu Mzee Bomani; Suala hili ni halikwepeki na ninashauri Serikali iteue JOPO LA WATAALAM kuliangalia KATIBA na kubaini MAHITAJI yaliomo;

7. Mzee Ruksa; Kwa nini Wa-Tanzania muhitaji KATIBA MPYA SASA HIVI, KUNA NINI???

8. Mwana-JF 'Dar es Salaam' aka JK; Nani kasema Mheshimiwa Kikwete mwenyewe hapendi Kuandikwa KATIBA MPYA???

8. 'Mtoto wa Mkulima' alipofika kwenye kio (TV); Nitamshauri Raisi ateue JOPO LA WATAALAM kuipitia katiba na kushauri HATIMA YAKE NI NINI.

9. Kombani; Leteni rasimu sifuri zenu za KATIBA MPYA kwangu,

10. Jaji Mkuu Augustino Ramadhani; Kwa KATIBA MPYA Tanzania hii kazi tulihitajika kulikamilisha tangu majuzi.

11. Mzee Warioba, CCM Uadilifu lakini masikini, Serikali isicheleweshe zaidi KATIBA MPYA

12. Mzee wa RICHMOND / DOWANS, CCM Ufisadi Mabilionea; Kwa usalama wa nchi yetu KATIBA MPYA haikwepeki.

13. Vuai Nahodha; Wananchi chonde MSILETE VURUGU NA KUANDAMANA kwani vilio vyenu kutaka KATIBA MPYA vinashughulikiwa.

14. Werema; Sasa serikali tumepata jibu sahihi hata bila ya Jopo la Wataalam au bila hata kupeleka popote hizo RASIMU SIFURI zenu za kutaka KATIBA MPYA.

Jibu lenyewe ambalo ni sahihi kabisa na kila mwananchi LAZIMA kuikubali ni kwamba 'WATANZANIA HAMUHITAJI KUANDIKA UPYA KATIBA BALI VIRAKA TU VICHACHE VINATOSHA.

15. Wanaharakati, Asasi za Kiraia, Vyama Vya Wafanyakazi, Vijana, Wana-JF, Vyama vya Siasa, Taasisi za Kidini na Vyuo Vikuu nchini nao wakasema; Saa ya Kuandikwa kwa KATIBA MPYA kwa njia Shirikishi kwa wananchi wote ni sasa.

16. Kesho au keshokutwa; ....

Kwa hayo maelezo yote yanayojikanganya kushoto na kulia sasa tushike lipi? MAFISADI watuambie ya kwamba sasa JIBU RASMI YA SERIKALI NI HILO ALILOLITOA WEREMA.

Na kama kweli ndilo jibu na msimamo rasmi wa serikali juu ya jambo hili la msingi na wa UMUHIMU WA PEKEE HASA KWETU VIJANA na walalahoi tuliowengi nchi hii basi nasi tunaomba kumshauri murua kwenu.

Kwa kuwa HAKI hua hauombwi wala kuletwa bila ya purukushani mivutano ya kujitakia MAFISADI, Saed Mwema tunakuomba ukaagize upesi MA-BOMU YA MACHOZI YA KUTOSHA kabisa na madai sasa yahamie uwanjani kama hata hoja yetu kule Bungeni ndilo hilo mnaelekea kusema ni kupoteza wakati!!!!
 
Werema nimemwona leo ITV sikuamini masikio yangu. Kwa kiburi hasa tena bila kumumunya maneno anadai Watanzania hatutapata Katiba Mpya ila marekebisho tu!!!

Sasa wafahamu hili... Bila ya katiba mpya, serikali CCM itachakachua tena kura zetu 2015 tukiwa makaburini!
A riot is at bottom the language of the unheard.
Martin Luther King, Jr.




Read more: Martin Luther King, Jr. Quotes
 
I think this ass hole called Warema belong behind bars,hawa ni aina ya wapambe ambao kazi yao ni kuchonganisha utawala na wananchi kama ilivyo kwa Gbagbo na Mugabe,yaani wanawashauri Viongozi vibaya ili kulinda maslahi binafsi
 
Aulizwe huyu yeye kama Mwanasheria Mkuu ni kifungu gani cha sheria kinachompa uwezo wa kutuamulia Watanzania zaidi ya milioni 40 kwamba hatustahili kupata katiba mpya ila kuongeza viraka tu? Watu wengine bwana!!!! Wanajisahau sana wanapokuwa madarakani na kudhani wao ni miungu watu.
 

KWA KAULI HII YA WEREMA, SAED MWEMA AGIZA MABOMU YA KUTOSHA TUFUNGUE MWAKAMPYA UWANJANI MPAKA KIELEWEKE


Kuna kauli kibao zinazojikanganya kanganya kutoka kwenye Serikali ya Mhe Kikwete kuhusu kiu yetu sisi wananchi kujiandikia upya katiba yetu sasa hivi.

1. Makamba; HAKUNA NAFASI YA KUSIKILIZWA MTU HAPA,

2. Chiligati, CHADEMA WASILETE UTANI TUENDA BUNGENI KUWAFUKUZA wote,

3. Chiligati, aaahhh, haya madai ya CHADEMA ni ya msingi na YANAZUNGUMZIKA,

4. Kombani alianza na SUALA LA KATIBA HAPAN, NI GHARAMA NA WALA SI MUHIMU,

5. Mzee Tyson, kuhusu madai ya KATIBA sisi serikali TUNAZO ZILE NJIA ZETU NA WALA HUA HAZITANGAZWI,

6. Alipofika Jaji Mstaafu Mzee Bomani; Suala hili ni halikwepeki na ninashauri Serikali iteue JOPO LA WATAALAM kuliangalia KATIBA na kubaini MAHITAJI yaliomo;

7. Mzee Ruksa; Kwa nini Wa-Tanzania muhitaji KATIBA MPYA SASA HIVI, KUNA NINI???

8. Mwana-JF 'Dar es Salaam' aka JK; Nani kasema Mheshimiwa Kikwete mwenyewe hapendi Kuandikwa KATIBA MPYA???

8. 'Mtoto wa Mkulima' alipofika kwenye kio (TV); Nitamshauri Raisi ateue JOPO LA WATAALAM kuipitia katiba na kushauri HATIMA YAKE NI NINI.

9. Kombani; Leteni rasimu sifuri zenu za KATIBA MPYA kwangu,

10. Jaji Mkuu Augustino Ramadhani; Kwa KATIBA MPYA Tanzania hii kazi tulihitajika kulikamilisha tangu majuzi.

11. Mzee Warioba, CCM Uadilifu lakini masikini, Serikali isicheleweshe zaidi KATIBA MPYA

12. Mzee wa RICHMOND / DOWANS, CCM Ufisadi Mabilionea; Kwa usalama wa nchi yetu KATIBA MPYA haikwepeki.

13. Vuai Nahodha; Wananchi chonde MSILETE VURUGU NA KUANDAMANA kwani vilio vyenu kutaka KATIBA MPYA vinashughulikiwa.

14. Werema; Sasa serikali tumepata jibu sahihi hata bila ya Jopo la Wataalam au bila hata kupeleka popote hizo RASIMU SIFURI zenu za kutaka KATIBA MPYA.

Jibu lenyewe ambalo ni sahihi kabisa na kila mwananchi LAZIMA kuikubali ni kwamba 'WATANZANIA HAMUHITAJI KUANDIKA UPYA KATIBA BALI VIRAKA TU VICHACHE VINATOSHA.

15. Wanaharakati, Asasi za Kiraia, Vyama Vya Wafanyakazi, Vijana, Wana-JF, Vyama vya Siasa, Taasisi za Kidini na Vyuo Vikuu nchini nao wakasema; Saa ya Kuandikwa kwa KATIBA MPYA kwa njia Shirikishi kwa wananchi wote ni sasa.

16. Kesho au keshokutwa; ....

Kwa hayo maelezo yote yanayojikanganya kushoto na kulia sasa tushike lipi? MAFISADI watuambie ya kwamba sasa JIBU RASMI YA SERIKALI NI HILO ALILOLITOA WEREMA.

Na kama kweli ndilo jibu na msimamo rasmi wa serikali juu ya jambo hili la msingi na wa UMUHIMU WA PEKEE HASA KWETU VIJANA na walalahoi tuliowengi nchi hii basi nasi tunaomba kumshauri murua kwenu.

Kwa kuwa HAKI hua hauombwi wala kuletwa bila ya purukushani mivutano ya kujitakia MAFISADI, Saed Mwema tunakuomba ukaagize upesi MA-BOMU YA MACHOZI YA KUTOSHA kabisa na madai sasa yahamie uwanjani kama hata hoja yetu kule Bungeni ndilo hilo mnaelekea kusema ni kupoteza wakati!!!!

sio tatizo kusikia misimamo tofauti kutoka vyanzo mbalimbali.na hii inaonyesha kuwa mjadala juu ya katiba unahitajika,pande zote zishiriki,serikali,vyama vya siasa,asasi za kijamii na wananchi kwa ujumla.baada ya hapa tutapata jibu kwa kupiga kura ya maoni hivyo mwisho tutaona kati ya werema na wananchi nani zaidi.naamini maelezo ya werema ni mawazo yake kama mwananchi na haizuii wananchi wengine kupewa fursa ya kutoa maoni yao na sio conclusion kama alivyofanya A.G.Hii ni ishara nyingine ya 'watawala' kutowaheshimu wenyenchi,
"ole wenu nyie mlio juu ni heri mjishushe sasa kwani msipofanya hivyo tutawaporomosha"

DEAR RULERS:
'You'll have to choose OUR WAY or hit the HIGHWAY'
 
Mwanasheria mkuu wa serikali Werema amesema kuwa katiba ya sasa inabidi ifanyiwe marekebishi na siyo kuandikiwa kwa katiba mpya

chanzo TBC1 Habari saa 2:00 usiku

Kuna watu kwasababu ya matumbo yao basi hufungia akili zao makabatini na kuimba nyimbo wasizozijua. Historia inatuonyesha kuwa Mzee Warioba[ Ninamheshimu sana] alipokuwa mwanansheria mkuu aliwahi kupinga katiba mpya. Hivi karibuni amelazimika kumeza matapishi yake. Historia inaonyesha kuwa serikali haikutaka mfumo wa vyama vingi lakini muda ulipofika Tanzania haikuwa kisiwa na busara za mzee Mwinyi zakatumika, licha ya white paper 80% vs 20% in favour of No.
Historia inaonyesha kuwa kuna matatizo ambayo si Werema au Jaji mkuu aliweza kutolea maamuzi kwa mkanganyiko wa katiba. Ni huyu huyu Werema alimpelekea Mh Rais asaini mswaada tofauti na ule ulioafikiwa na bunge.
Asichokijua Werema au anachogoma kukibali ni kuwa Katiba ni mali ya Watanzania, si mali ya Rais au Werema. Wasomi wenye heshima ndani na nje ya nchi wameona tatizo la kuweka viraka, lakini kwa hofu ya madaraka Werema analazimika kutoa kauli zinazosikitisha sana.
Werema, Nguvu ya umma ni kubwa kuliko Nguvu ya madaraka, angalia Kenya na kwingine duniani. Suala la katiba si la mjadala tena, bali lini tuanze kutengeneza mpya ndiyo mjadala. Ipo siku tutakuuliza kwa haya unayoyasema! Usijeona kuwa unadhalilishwa.
 
Si shangai warema lazima atete hiyo hoja katiba mpya si ruksa,mana analinda ugali wa jk na wake , kumbukeni huyo alikuwa hakimu kisutu akapandishwa kuwa jaji na hatimae kuwa mwanasheria mkuu wa gvt kwa hiyo kwa mtiririko huo huyo ni ngumu kutoka hadharani na kusema katiba mpya inatakiwa.
Alafu hii serikali sijui inaongozwa na watu wangapi!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Yani hatuelewi mana kila mtu anakuja la lake. Waziri mkuu pinda kasema katiba mpya inahitajika, kombani anasema hakuna umuhimu, warema nae hivyo hivyo.
Kwa hiyo hao wanampiga waziri mkuu.......................?

Nguvu ya umma ipo na katiba itakuja tu.
 
AG ataka Katiba iwekewa viraka Monday, 27 December 2010 20:16

werema.jpg
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Frederick Werema,

Waandishi Wetu
WAKATI viongozi kadhaa wa nchini akiwamo Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, mawaziri wakuu wa zamani, Joseph Warioba na Frederick Sumaye na Jaji Mkuu Mstaafu Agostino Ramadhan wakitaka iundwe katiba mpya, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Frederick Werema, amepinga wazo hilo na kutaka katiba iliyopo iwekewe viraka zaidi.

Madai ya katiba mpya pia yamewahi kutolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, John Tendwa ambaye alisema bayana kuwa katiba mpya iandikwe mapema kabla ya mambo kuwa mabaya, akitoa mfano wa mapungufu ya katiba ya sasa kuwa ni Rais kupewa madaraka makubwa.

Jana akiwa Ikulu kwenye hafla ya kuapishwa Jaji Mkuu mpya, Mohamed Othman Chande, Werema alisema kuwa haona haja ya kuandikwa katiba mpya badala yake katiba iliyopo iwekewe viraka.

"Kuandika katiba mpya hapana, lakini kufanya marekebisho kwa kuondoa au kuongeza mambo fulani kwenye katiba ruksa," alisema Jaji Werema.

"Suala la kubadilisha ibara zinazoonekana kutokidhi haja na kuingiza mambo mapya kwenye katiba, linakubalika na kwamba hayo yamekuwa yakifanyika," alisisitiza Jaji Werema na kutolea mfano mabadiliko ya katiba yaliyoruhusu kuingizwa kwa haki za binadamu.

Hata hivyo, alisema maoni ya watu yanayotolewa kuhusu katiba mpya ni sahihi kwani kila Mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu wa katiba iliyopo.

"Raha yangu ni kuona Watanzania tunajadili suala hili maana kila mtu ana haki ya kusema na ni sahihi, lakini tunatofautiana tu kama kila maoni ni sawa," alisema Jaji Werema na kuongeza:

"Lakini si kila mtu analolisema lifuatwe. Tukisema kila mtu anachokisema tukifuate haitakuwa sawa. Kwa mfano mimi kule kwetu wafugaji nao watataka mambo ya ng'ombe wao yaingizwe kwenye katiba, na Wahaya pia wanaweza kusema tuingize kwenye katiba ndizi zao, hii si sawa;" alisisitiza Jaji Werema.

Jaji Werema alitoa wito kwa watu wote wanaojadili suala hilo kutochochea watu kuandamana na kuwataka waandishi wa habari pia kuitumia vizuri kalamu yao kuuelimisha umma.

Jaji Werema anakuwa ni kiongozi wa pili wa Serikali kupinga haja ya kuwa na katiba mpya. Kiongozi wa kwanza serikalini kupinga suala hilo alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani.

Hata hivyo, msimamo wa mwanasheria huyo wa Serikali umekuja wakati tayari Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa ameshaweka wazi nia ya kuyafanyia kazi madai hayo yaliyoanzishwa na Chadema na kuungwa mkono na watu wa kada mbalimbali.
Lakini wakati Jaji Werema akitoa msimamo huo, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika amesema Katiba ya Tanzania ina viraka vingi, inahitaji kuandikwa upya na viongozi wa Serikali, hawapaswi kukwepa jambo hilo.
Mnyika alisema hayo jana baada ya kupeleka barua yake kwa Katibu wa Bunge kutoa taarifa ya kusudio la kuwasilisha hoja binafsi bungeni kutaka katiba mpya huku akieleza kuwa katiba iliyopo ina kasoro 90.

Mnyika alisema kuwa katika hoja yake hiyo anayotarajia kuiwasilisha kwenye Bunge la Februari mwakani, pia ametaka katiba itakayoundwa iruhusu mgombea binafsi.

"Kutokana na kanuni za kudumu za Bunge mwaka 2004, 55(1), tunatakiwa kupeleka taarifa kuhusu kuwasilisha taarifa ya hoja binafsi kwa katibu na sio kupeleka hoja binafsi ya katiba,"alisema Mnyika

Alisema taarifa yake ya kusudio la kupeleka hoja binafsi bungeni aliiwasilisha jana kwa Mkurugenzi wa Idara ya taarifa za Bunge, Eliakimu Mrema ambaye alikuwa anakaimu nafasi ya Katibu wa Bunge.

Mnyika alisema baada ya kuwasilishia barua hiyo, atawashirikisha wananchi ili kupata maoni yao kabla hajaipeleka rasmi bungeni.
Alisema kwa sasa Chadema inakaribisha maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo wasomi ,wanasiasa na wananchi wa kawaida ili watoe maoni yao kuhusu mapungufu ya katiba na wapendekeze muundo wa katiba mpya.

Alisema suala la mabadiliko la katiba nchini linamgusa kila mwananchi mwenye uelewa hivyo sio suala la kukurupuka na Chadema ilizingatia hilo ndio maana ikaamua kuwakutanisha wadau mbalimbali kupata maoni yao.
"Tutakutana na wadau wa katiba katika wiki ya kwanza ya Januari jijini Dar es salaam katika uwanja wa wazi ambao tutautangaza baadaye ili tukusanye mawazo yao," alisema Mnyika.

Alitaja baadhi ya mapungufu yaliyomo kwenye katibaya sasa kuwa ni pamoja na suala la madaraka ra Rais ambayo kwa maoni yake, ni makubwa kuliko inavyotakia kuwa.
"Tatizo lingine la katiba yetu ni la kijamii. Katiba hii ni ya muda mrefu na kizazi kipya cha sasa hakikushiriki kuitunga hivyo ni ya kikoloni," alisema Mnyika na kuongeza:

Alisema pia sio sahihi wakurugenzi wa halmashauri kusimamia uchaguzi kwa sababu kura ni za vyama hivyo wanaopaswa kuzisimamia wanatakiwa kutokuwa mashabiki wa kisiasa.

Mnyika alisema pia kuwa katika taarifa yake hiyo amezungumzia suala la Mahakama kwamba haiko huru kwani mtendaji mkuu wa idara hiyo ambayo ni muhimili wa dola Jaji Mkuu, anateuliwa na rais.

Mkurugenzi wa idara ya taarifa za Bunge Eliakimu Mrema aliyepokea barua ya Mnyika alisema kazi ya Ofisi ya Bunge ni kupokea taarifa na kuzifanyia kazi hivyo taarifa hiyo imefika.
Katika hatua nyingine, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, amesema kuwa suala sio kuifanyia marekebisho katiba iliyopo bali kutunga katiba nyingine.

Mukoba aliliambia gazeti hili jana kuwa katiba ya sasa ni ya kikoloni kutokana na kumpa Rais madaraka makubwa hali ambayo inasababisha kuzorotesha maendeleo ya nchi
"Mfano kitendo cha viongozi kuchukua fedha za EPA na rais kuamua kuwasamehe na kusema watarudisha taratibu ni sababu ya katiba kumpa madaraka makubwa; yaani kuwa juu ya sheria maana rais hatakiwi kuwa na mamlaka ya kuwasamehe wezi,"alisema Mukoba.

Alisema kuwa katiba mpya inayohitajika sasa ni ile ambayo haimpi Rais madaraka makubwa kama hayo na kwamba kitendo cha rais kuwa juu ya sheria ni chanzo cha viongozi kuwa na utovu wa nidhamu.

Mukoba alisema kuwa hata majaji hawatakiwi kuteulewa na Rais badala yake wangethibitishwa na Bunge kama ilivyo kwa Waziri Mkuu.

"Ukweli ni kwamba viongozi wote wanaoteuliwa na Rais wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga na kutaka kulinda maslahi yao maana wakisema ukweli wanaweza kupoteza kibarua chao,"alisema Mukoba.

Habari hii imeandaliwa na James Magai, Hussein Issa na Gedius Rwiza
 
<p>
<i><font face="Book Antiqua"><font size="4"><font color="blue">Aulizwe huyu yeye kama Mwanasheria Mkuu ni kifungu gani cha sheria kinachompa uwezo wa kutuamulia Watanzania zaidi ya milioni 40 kwamba hatustahili kupata katiba mpya ila kuongeza viraka tu? Watu wengine bwana!!!! Wanajisahau sana wanapokuwa madarakani na kudhani wao ni miungu watu.</font></font></font></i>
</p>
<p>&nbsp;</p>
Bubu umenena. AG ni mshauri mwandamizi wa sheria wa serikali lakini si mshauri wala mwalimu wa sheria wa wananchi katika suala lolote lile, liwe la Katiba au la Dowans. Pamoja na yote hayo, kwa matamshi yake ya jana, AG wetu si mwanasheria mzuri na makini. Katiba mpya ni haki ya wananchi na malipo kwa Dowans hayana msingi kisheria, ni wizi wa mchana!
 
Mwanasheria mkuu wa serikali Werema amesema kuwa katiba ya sasa inabidi ifanyiwe marekebishi na siyo kuandikiwa kwa katiba mpya

chanzo TBC1 Habari saa 2:00 usiku

Hiyo katiba ni kwa ajili ya wananchi!!! Na si kwa ajili ya Serikali. Wananchi ndiyo tunaamua nini kifanyike kwa katiba hiyo kwa sababu ni yetu!!!! Huyo mwanasheria mkuu ni mwanasheria gani asiyejua hilo????!!!
 
Ama kwa hakika JK aharakishe kutumia kodi ya watanzania kununulia mabomu na risasi kutuliza kiu ya watanzania juu ya katiba mpya. Huyo mshikaji wake atamsababisha JK akatinge mahakama ya kimataifa kama hatengui nafasi ya huyu bwana ya uanasheria mkuu ambao hana uwezo nao. Mwanasheria mkuu hapaswi kuwa mropokaji na mtukana matusi ati watanzania wanaapiga kelele kama mabata wanapodai haki yao ya kimsingi. Hii nchi sio ya Pino Cheet wala Nduli Idd Amini. Nadhani Werema anahitaji kuchunguzwa rekodi yake tangia shuleni, huenda alifaulu kimkakati hadi kufikia hapo alipo. Hawezi hata kusoma nyakati ukutani, ni sheria gani anayoijua? Aliyoyasema ni mawazo yake binafsi na alipaswa kuyasema chumbani kwake kwa mkewe tu, maana akizungumza nje ya hapo imact yake ni kubwa kiasi kwamba nina mashaka kama anao uwezo wa kutafakari kwa kina.

Pole JK, huenda umeipoteza bure nafasi ya mwanasheria mkuu wa serikali, maana anakushauri vibaya mno. Yaani hata majaji maboss wake wanasema bayana umuhimu wa katiba mpya na hata walimu wake waliomfundisha namna ya kutafakari wanamfunza bado hafunziki? Hapo imekula kwetu watanzania. Ndio tutegemee mikataba ya faida kwa nchi itasainiwa hapo??? Nasikia kutapika.....
 
mwanasheria mkuu, mhe werema anayo haki ya kufurahisha nafsi yake lakini si kuamua juu ya hatima ya katiba ya nchi.

Huyu bwana anayo wajibu tu wa kuishauri serikali juu ya katiba ikishapatikana. Lakini pale katiba inapotafutwa, yeye kutoa juu ya hatima ya andiko hili ni to act ultravirously bila ya ulazima. Hatujamsikia akizungumzia mbunge anapopigwa na polisi, kwa nini adandie kazi si yake hapa??

Katiba si mali ya werema, katiba si mali ya kikwete na mwinyi wala katiba si mali ya serikali.

Kama walivyowahi kusema waheshimiwa prof lipumba, dr slaa, duni haji duni, wasomi kibao na wanasheria waliotukuka, katiba ni mali ya mtanzania wa kawaida. Lini akalirekebishe na kwa mtindo gani yote ni juu yake mwenyewe kuamua.

Mwanasheria mkuu ni mwajiriwa wa katiba na hana msingi wa kumamulia mwajiri wake kitu gani akafanye juu ya katiba. Wapinga mabadiliko ya kweli nchini, hebu tukutane bungeni dodoma.

siri kubwa ya kuogopa kuandikwa upya kwa katiba ni wizi ambao werema na wakuu wake wanaendelea kuufanya imewashika pabaya watahangaika saana -nguvu ya umma itawashukia. Uogo huu wa kuandikwa katiba mpya una mshindo mkuu na ni hatari saana kwa maslahi ya taifa hili. Werema anapswa kuambiwa tanzania walioizoea imebadilika sana.
 
Werema hawezi kukubali bila msukumo wa umma kama alivyofanya mnyika, werema ameshachuakua chake mapema na ana kazi alyokabidhiwa kulinda sirikali zilizofichwa ukisema katiba mpya kuna watu wanapata pressure yeye ni mmoja wapo, utasikia wanakwambia wananchi , wnanchi gani hao tofauti na waliokwisha kuongea?? Maaskofu wanataka katiba mpya, cwt wanataka katiba mpya, waislamu wanataka katiba mpya, tucta/wafanyakazi wataka katiba mpya, wanazuoni wanataka katiba mpya, wanasheria na wanaharakati mbalimbali wanataka katiba mpya, jaji samata, jaji warioba, jaji kisanga, jaji manento, jaji ramadhani wanataka katiba mpya , media wanataka katiba mpya, yeye ag ni nani hasa kuzuia katiba mpya na kwa malsahi ya nani hasa??? Anaogopa nini kuandikwa katiba mpya????? Je hofu hii inatoka wapi???
 
Mwanasheria mkuu wa serikali Werema amesema kuwa katiba ya sasa inabidi ifanyiwe marekebishi na siyo kuandikiwa kwa katiba mpya

chanzo TBC1 Habari saa 2:00 usiku


Werema ni Mwanasheria wa CCM. Mwanzoni mwa mwakal walikuwa wamevutana kuhusu kifungu namba 7(3) cha Sheria ya
Gharama za Uchaguzi baada ya Dk Slaa kubaini kuwa kifungu hicho kilikuwa kimechakachuliwa. Huyo ni mpinzani wa sauti ya umma.
 
Who is werema to take this country to hell? Ukisema katiba mpya kuna watu wanapata pressure yeye ni mmoja wapo, utasikia wanakwambia wananchi , wananchi gani hao tofauti na waliokwisha kuongea?? Maaskofu wanataka katiba mpya, cwt wanataka katiba mpya, waislamu wanataka katiba mpya, tucta/wafanyakazi wataka katiba mpya, wanazuoni wanataka katiba mpya, wanasheria na wanaharakati mbalimbali wanataka katiba mpya, jaji samata, jaji warioba, jaji kisanga, jaji manento, jaji bomani,jaji ramadhani wanataka katiba mpya , media wanataka katiba mpya,chadema, cuf, nccr,tlp, udp wote wanataka katiba mpya, yeye ag ni nani hasa kuzuia katiba mpya na kwa malsahi ya nani hasa??? Anaogopa nini kuandikwa katiba mpya????? Je hofu hii inatoka wapi???
 
ag ataka katiba iwekewa viraka monday, 27 december 2010 20:16

werema.jpg
mwanasheria mkuu wa serikali (ag) frederick werema,

waandishi wetu
wakati viongozi kadhaa wa nchini akiwamo rais mstaafu, benjamin mkapa, mawaziri wakuu wa zamani, joseph warioba na frederick sumaye na jaji mkuu mstaafu agostino ramadhan wakitaka iundwe katiba mpya, mwanasheria mkuu wa serikali (ag) frederick werema, amepinga wazo hilo na kutaka katiba iliyopo iwekewe viraka zaidi.

Madai ya katiba mpya pia yamewahi kutolewa na msajili wa vyama vya siasa nchini, john tendwa ambaye alisema bayana kuwa katiba mpya iandikwe mapema kabla ya mambo kuwa mabaya, akitoa mfano wa mapungufu ya katiba ya sasa kuwa ni rais kupewa madaraka makubwa.

Jana akiwa ikulu kwenye hafla ya kuapishwa jaji mkuu mpya, mohamed othman chande, werema alisema kuwa haona haja ya kuandikwa katiba mpya badala yake katiba iliyopo iwekewe viraka.

"kuandika katiba mpya hapana, lakini kufanya marekebisho kwa kuondoa au kuongeza mambo fulani kwenye katiba ruksa," alisema jaji werema.

"suala la kubadilisha ibara zinazoonekana kutokidhi haja na kuingiza mambo mapya kwenye katiba, linakubalika na kwamba hayo yamekuwa yakifanyika," alisisitiza jaji werema na kutolea mfano mabadiliko ya katiba yaliyoruhusu kuingizwa kwa haki za binadamu.

Hata hivyo, alisema maoni ya watu yanayotolewa kuhusu katiba mpya ni sahihi kwani kila mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake kwa mujibu wa katiba iliyopo.

"raha yangu ni kuona watanzania tunajadili suala hili maana kila mtu ana haki ya kusema na ni sahihi, lakini tunatofautiana tu kama kila maoni ni sawa," alisema jaji werema na kuongeza:

"lakini si kila mtu analolisema lifuatwe. Tukisema kila mtu anachokisema tukifuate haitakuwa sawa. Kwa mfano mimi kule kwetu wafugaji nao watataka mambo ya ng'ombe wao yaingizwe kwenye katiba, na wahaya pia wanaweza kusema tuingize kwenye katiba ndizi zao, hii si sawa;" alisisitiza jaji werema.

Jaji werema alitoa wito kwa watu wote wanaojadili suala hilo kutochochea watu kuandamana na kuwataka waandishi wa habari pia kuitumia vizuri kalamu yao kuuelimisha umma.

Jaji werema anakuwa ni kiongozi wa pili wa serikali kupinga haja ya kuwa na katiba mpya. Kiongozi wa kwanza serikalini kupinga suala hilo alikuwa waziri wa katiba na sheria, celina kombani.

Hata hivyo, msimamo wa mwanasheria huyo wa serikali umekuja wakati tayari waziri mkuu, mizengo pinda akiwa ameshaweka wazi nia ya kuyafanyia kazi madai hayo yaliyoanzishwa na chadema na kuungwa mkono na watu wa kada mbalimbali.
Lakini wakati jaji werema akitoa msimamo huo, mbunge wa ubungo, john mnyika amesema katiba ya tanzania ina viraka vingi, inahitaji kuandikwa upya na viongozi wa serikali, hawapaswi kukwepa jambo hilo.
Mnyika alisema hayo jana baada ya kupeleka barua yake kwa katibu wa bunge kutoa taarifa ya kusudio la kuwasilisha hoja binafsi bungeni kutaka katiba mpya huku akieleza kuwa katiba iliyopo ina kasoro 90.

Mnyika alisema kuwa katika hoja yake hiyo anayotarajia kuiwasilisha kwenye bunge la februari mwakani, pia ametaka katiba itakayoundwa iruhusu mgombea binafsi.

"kutokana na kanuni za kudumu za bunge mwaka 2004, 55(1), tunatakiwa kupeleka taarifa kuhusu kuwasilisha taarifa ya hoja binafsi kwa katibu na sio kupeleka hoja binafsi ya katiba,"alisema mnyika

alisema taarifa yake ya kusudio la kupeleka hoja binafsi bungeni aliiwasilisha jana kwa mkurugenzi wa idara ya taarifa za bunge, eliakimu mrema ambaye alikuwa anakaimu nafasi ya katibu wa bunge.

Mnyika alisema baada ya kuwasilishia barua hiyo, atawashirikisha wananchi ili kupata maoni yao kabla hajaipeleka rasmi bungeni.
Alisema kwa sasa chadema inakaribisha maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo wasomi ,wanasiasa na wananchi wa kawaida ili watoe maoni yao kuhusu mapungufu ya katiba na wapendekeze muundo wa katiba mpya.

Alisema suala la mabadiliko la katiba nchini linamgusa kila mwananchi mwenye uelewa hivyo sio suala la kukurupuka na chadema ilizingatia hilo ndio maana ikaamua kuwakutanisha wadau mbalimbali kupata maoni yao.
"tutakutana na wadau wa katiba katika wiki ya kwanza ya januari jijini dar es salaam katika uwanja wa wazi ambao tutautangaza baadaye ili tukusanye mawazo yao," alisema mnyika.

Alitaja baadhi ya mapungufu yaliyomo kwenye katibaya sasa kuwa ni pamoja na suala la madaraka ra rais ambayo kwa maoni yake, ni makubwa kuliko inavyotakia kuwa.
"tatizo lingine la katiba yetu ni la kijamii. Katiba hii ni ya muda mrefu na kizazi kipya cha sasa hakikushiriki kuitunga hivyo ni ya kikoloni," alisema mnyika na kuongeza:

Alisema pia sio sahihi wakurugenzi wa halmashauri kusimamia uchaguzi kwa sababu kura ni za vyama hivyo wanaopaswa kuzisimamia wanatakiwa kutokuwa mashabiki wa kisiasa.

Mnyika alisema pia kuwa katika taarifa yake hiyo amezungumzia suala la mahakama kwamba haiko huru kwani mtendaji mkuu wa idara hiyo ambayo ni muhimili wa dola jaji mkuu, anateuliwa na rais.

Mkurugenzi wa idara ya taarifa za bunge eliakimu mrema aliyepokea barua ya mnyika alisema kazi ya ofisi ya bunge ni kupokea taarifa na kuzifanyia kazi hivyo taarifa hiyo imefika.
Katika hatua nyingine, rais wa chama cha walimu tanzania (cwt), gratian mukoba, amesema kuwa suala sio kuifanyia marekebisho katiba iliyopo bali kutunga katiba nyingine.

Mukoba aliliambia gazeti hili jana kuwa katiba ya sasa ni ya kikoloni kutokana na kumpa rais madaraka makubwa hali ambayo inasababisha kuzorotesha maendeleo ya nchi
"mfano kitendo cha viongozi kuchukua fedha za epa na rais kuamua kuwasamehe na kusema watarudisha taratibu ni sababu ya katiba kumpa madaraka makubwa; yaani kuwa juu ya sheria maana rais hatakiwi kuwa na mamlaka ya kuwasamehe wezi,"alisema mukoba.

Alisema kuwa katiba mpya inayohitajika sasa ni ile ambayo haimpi rais madaraka makubwa kama hayo na kwamba kitendo cha rais kuwa juu ya sheria ni chanzo cha viongozi kuwa na utovu wa nidhamu.

Mukoba alisema kuwa hata majaji hawatakiwi kuteulewa na rais badala yake wangethibitishwa na bunge kama ilivyo kwa waziri mkuu.

"ukweli ni kwamba viongozi wote wanaoteuliwa na rais wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga na kutaka kulinda maslahi yao maana wakisema ukweli wanaweza kupoteza kibarua chao,"alisema mukoba.

Habari hii imeandaliwa na james magai, hussein issa na gedius rwiza

who is werema to take this country to hell? Ukisema katiba mpya kuna watu wanapata pressure yeye ni mmoja wapo, utasikia wanakwambia wananchi , wananchi gani hao tofauti na waliokwisha kuongea?? Maaskofu wanataka katiba mpya, cwt wanataka katiba mpya, waislamu wanataka katiba mpya, tucta/wafanyakazi wataka katiba mpya, wanazuoni wanataka katiba mpya, wanasheria na wanaharakati mbalimbali wanataka katiba mpya, jaji samata, jaji warioba, jaji kisanga, jaji manento, jaji bomani,jaji ramadhani wanataka katiba mpya , media wanataka katiba mpya,chadema, cuf, nccr,tlp, udp wote wanataka katiba mpya, yeye ag ni nani hasa kuzuia katiba mpya na kwa malsahi ya nani hasa??? Anaogopa nini kuandikwa katiba mpya????? Je hofu hii inatoka wapi???
 
Aulizwe huyu yeye kama Mwanasheria Mkuu ni kifungu gani cha sheria kinachompa uwezo wa kutuamulia Watanzania zaidi ya milioni 40 kwamba hatustahili kupata katiba mpya ila kuongeza viraka tu? Watu wengine bwana!!!! Wanajisahau sana wanapokuwa madarakani na kudhani wao ni miungu watu.

Tatizo kubwa sana, kama hii ndio calibre ya AG tuliye naye basi ni balaa tupu. Hivi kuna Nchi gani duniani amabyo ina katiba inayotamka kuwa AG ni Mbunge, nadhani ni Tanzania tu. Ndio maana huyu jamaa anataka katiba isibadilike kwani anamaslahi makubwa sana.

Maoni yake naomba yadharauliwe kwa hali ya juu sana.

Tusonge mbele na tunachotaka kufanya
 
huyu mtu ananishangaza sana mbona anataka kuwa na mamlaka makubwa hivi si ndo alisema amefunga suala la dowans
sasa na la katiba pia anataka kulifunga?? :teeth:hasira kweli kweli
 
Ama kwa hakika JK aharakishe kutumia kodi ya watanzania kununulia mabomu na risasi kutuliza kiu ya watanzania juu ya katiba mpya. Huyo mshikaji wake atamsababisha JK akatinge mahakama ya kimataifa kama hatengui nafasi ya huyu bwana ya uanasheria mkuu ambao hana uwezo nao. Mwanasheria mkuu hapaswi kuwa mropokaji na mtukana matusi ati watanzania wanaapiga kelele kama mabata wanapodai haki yao ya kimsingi. Hii nchi sio ya Pino Cheet wala Nduli Idd Amini. Nadhani Werema anahitaji kuchunguzwa rekodi yake tangia shuleni, huenda alifaulu kimkakati hadi kufikia hapo alipo. Hawezi hata kusoma nyakati ukutani, ni sheria gani anayoijua? Aliyoyasema ni mawazo yake binafsi na alipaswa kuyasema chumbani kwake kwa mkewe tu, maana akizungumza nje ya hapo imact yake ni kubwa kiasi kwamba nina mashaka kama anao uwezo wa kutafakari kwa kina.

Pole JK, huenda umeipoteza bure nafasi ya mwanasheria mkuu wa serikali, maana anakushauri vibaya mno. Yaani hata majaji maboss wake wanasema bayana umuhimu wa katiba mpya na hata walimu wake waliomfundisha namna ya kutafakari wanamfunza bado hafunziki? Hapo imekula kwetu watanzania. Ndio tutegemee mikataba ya faida kwa nchi itasainiwa hapo??? Nasikia kutapika.....
Lekanjobe ujobile ndaga!
 
Back
Top Bottom