TANZIA Mwanasheria Mkuu wa Kwanza Mzalendo na Jaji Mstaafu Mark Bomani afariki dunia

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,792
11,952
bomani.jpg

Habari zilizotufikia ni kwamba Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, Jaji Mark Bomani amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 11, 2020, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Mtoto wake amethibitisha kifo hiki. Shughuli za msiba zipo nyumbani kwa Marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Miaka 50.jpg

Jaji Mstaafu Mark Bomani enzi za uhai wake akiwa na mkewe wakikata keki katika hafla ndogo ya kusherehekea miaka 50 ya ndoa yao mwaka 2017
70FB27C5-AA81-4E1F-9892-72D6E81DF716.jpeg
--
UPDATE 14-09-2020: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aongoza mazishi
--
1.jpg
2.jpg
3.jpg

WASIFU WAKE KWA UFUPI

Mark Danhi Bomani alizaliwa Januari 2 1932, Bunda, mkoani Mara.

Mark alikuwa kati ya watoto kumi wa Mzee Bomani ndugu zake wengine wakiwa Daniel, Paul, Emma, Francis, Martha, Yona, Washington, Phoebe & Neema.

Mark Bomani alisoma shule ya msingi Mwamanyili, Nassa ambapo baba yake mzazi ndiye alikuwa mwalimu wake. Baada ya kumaliza shule ya Msingi, alijiunga na shule ya Bwiru Boys ambapo alisoma mpaka darasa la 10 na baadae alifaulu kuendelea na masomo ya secondary katika shule mashuhuri ya Tabora Boys. Baada ya kufaulu kidato cha 6, Mark alichaguliwa kwenda chuo cha Makerere College nchini Uganda.

ELIMU:

1953 – 1957B.A (Politics, Economics and History), Makerere University, Uganda

1957 – 1958: Diploma in Social Welfare Policy, Institute of Social Studies, The Hague.

1958 – 1961: Bachelor of Laws (LLB), London University

1961: Barrister -at-Law, Lincoln’s Inn, London

KAZI:

1954: Mwakilishi wa Makerere Student’s Guide kwenye Mkutano wa Kimataifa (International Union of Students Conference), Prague, Czechoslovakia.

1959: Kiongozi wa Umoja wa Wanafunzi wote kutoka Tanganyika (Tanganyika Students Association), Makerere University

1962: Wakili wakujitegemea katika mkoa wa Mwanza

1963: Wakili wa Serikali. Akateuliwa na J.K. Nyerere kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu

Katika kazi ya mwanzo aliyoifanya katika cheo chake kipya ilikuwa ni kusaidiana na Mwanasheria Mkuu Roland Brown kutayarisha nyaraka zote za kisheria za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

1963: Alishiriki katika utayarishaji wa Mkataba wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (Charter of the African Development Bank), Casablanca, Morocco.

1963: Mjumbe katika ujumbe wa Tanganyika uliokwenda Addis Ababa, Ethiopia kuandaa mkataba wa nchi huru za Afrika (Charter of the Organization of African Unity)

1964: Mjumbe wa Kamati ya Wajumbe wa Nchi za Afrika ya Mashariki iliyoundwa kwa madhumuni ya kuangalia uwezekano wa kuunda Shirikisho la Afrika ya Mashariki

1964: Mjumbe wa Tume ya Rais iliyoundwa ili ipendekeze mfumo mpya wa Kidemokrasia wa Chama kimoja. Mapendekezo ya Tume hiyo ndiyo yaliyokuwa Msingi wa mfumo wa Chama kimoja cha Siasa

1965– 1976: Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa kwanza mwananchi. Kati ya mambo ya kwanza aliyoshughulikia nikutafuta majaji na mahakimu kutoka nchi za nje ambao waliajiriwa na serikali ya Tanzania katika kipindi ambapo majaji na mahakimu wengi walikuwa wazungu au wahindi. Kati ya watu aliyowachagua ni pamoja na Telford Georges kutoka Trinidad & Tobago aliyekuwa Jaji Mkuu.

1965: Mbunge na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya TANU

1967– 1976: Mjumbe wa Kamati iliyoundwa kwa madhumuni ya kupendekeza mfumo mpya wa ushirikiano kati ya nchi za Afrika ya Mashariki. Hatma yake ilikuwa kuundwa kwa Jumuiya ya Afrka Mashariki (East African Community)

1974: Mshauri wa FRELIMO katika kuandaa Katiba mpya ya Msumbiji na utaratibu wa Serikali yake

1976: Baada ya kuombwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Rais J.K. Nyerere alimruhusu Mark Bomani kujiunga na Utumishi wa Umoja huo kwa madhumuni maalum ya kusaidia katiak matayarisho ya Uhuru wa Namibia.

1976: Naibu Mkurugenzi (Deputy Director), U.N Institute for Namibia, Lusaka, Zambia

1978: Baada ya kuombwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, kuwa mshauri wake wa mambo ya kisheria, Mark Bomani alikwenda Namibia na Afrika ya Kusini kuzungumzia juu ya utaratibu wa kukabidhi madaraka kwa wananchi. Taarifa ya mapendekezo ya ujumbe huo ndiyo iliyowezesha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitisha Azimio Na 435 ya mwaka 1978 ambayo hatimaye yalileta uhuru wa Namibia.

1990: Mark Bomani aliandaa katiba mpya ya Namibia baada ya kupata uhuru

1991: Mark Bomani aliombwa kuwa Jaji Mkuu wa Namibia lakini badala yake akaomba awe mshauri wa masuala ya Sheria na Katiba kwa miaka miwili tuu akiamini kwamba muda huo ungetosha kabisa kutoa mchango wake kwa wana-Namibia.

1992: Bomani aliteuliwa na Rais Mwinyi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Wataalam wa Zanzibar na wa Tanzania Bara iliyoundwa kutoa mapendekezo juu ya namna ya kumchagua Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na mgawanyo wa madaraka kati yao na Bunge. Rais Mwinyi pia alimteua Mark Bomani kuwa Jaji.

1993: Mwenyekiti wa Kamati Maalum (Legal Task Force) iliyopewa jukumu la kukarabati sekta yote ya Sheria nchini, chini ya mradi wa Benki ya Dunia, Wahisani mbalimbali.

1993:1995: Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi

1993: Mwenyekiti wa Tume ya Utangazaji

1995: Bomani ajitosa siasa kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kuwa mgombea Rais.

1995:
Baada Mwalimu Nyerere kuchaguliwa kuwa Mpatanishi wa mgogoro wa Burundi na Umoja wa Mataifa na OAU, Nyerere akamuomba Bomani kuwa msaidizi wake kazi aliyoifanya mpaka Mwalimu Nyerere alipofariki mwaka 1999. Baada ya Nelson Mandela kuchaguliwa kuwa mpatanishi mpya, Bomani akawa msaidizi wake na kwa pamoja wakaweza kufanikisha azma ya kupatanisha pande husika mnamo Agosti 2000.

2007:
Rais Kikwete alimteua Bomani kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya watu 12 kupitia upya sera ya madini.

2018:
Mwenyekiti wa CCM, John J.P. Magufuli alimteua kuwa mmoja wa wajumbe watano wa Bodi ya Kwanza ya Udhamini ya CCM.

Mark Bomani aliendelea na shughuli za uwakili kupitia kampuni yake ya Bomani & Company Advocates. Mark Bomani alikuwa mkurugenzi na muanzilishi wa kampuni ya Serengeti Breweries. Pia alikuwa mkurugenzi wa Bodi ya Benki ya NCBA.


Baadhi ya mada kuhusu Jaji Bomani
> Jaji Mark Bomani: Serekali 2 au 3 zisijadiliwe kwenye Bunge la Katiba!
> Jaji mstaafu Mark Bomani naye atoa mpya..
> Jaji Mstaafu Mark Bomani akataa Tanzania kuitwa Tanzania Bara, ataka iitwe Tanganyika
> Jaji Mark Bomani: Ni vizuri kukawepo kura ya maoni kuhusu Muungano (Referendum)
> Jaji Mstaafu Mark Bomani aunga mkono Serekali 3 asema wasemao ni harama hawana mashiko
> Muungano lazima ujadiliwe kwa Ukweli na Uwazi! - Jaji Mark Bomani
> Jaji Bomani: Wageni wanaimaliza nchi kupitia sekta ya madini
> Jaji Bomani apigilia msumari Katiba Mpya
> Jaji Bomani: ZEC imejipunguzia imani
> Jaji Bomani awachafua wazanzibari
> Bomani: Gamba litapasua CCM
 
Jaji mstaafu wa Tanzania, Mark Bomani amefariki dunia usiku wa kuamkia Leo katika hospital ya taifa Muhimbili.
 
Rest in Peace, tutakukumbuka kwa Yale yote Mema uliyoitendea mama Tanzania na watanzania wote uliowapa haki katika kutekeleza majukumu yako.

Roho yake ipate rehema kwa Mungu apumzike kwa amani.
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) @ccm_tanzania tumepokea kwa huzuni taarifa ya kifo cha Jaji (Mst) Mark Bomani, MwanaCCM & Mwanasheria Mkuu wa kwanza wa Tanzania Uongozi unatoa pole kwa familia, wafiwa & wote walioguswa na msiba huu. Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa Jina lake Lihimidiwe
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) @ccm_tanzania tumepokea kwa huzuni taarifa ya kifo cha Jaji (Mst) Mark Bomani, MwanaCCM & Mwanasheria Mkuu wa kwanza wa Tanzania Uongozi unatoa pole kwa familia, wafiwa & wote walioguswa na msiba huu. Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa Jina lake Lihimidiwe View attachment 1565906View attachment 1565907
Huyu ndio alikuwa tume ya taifa ya kwanza ya uchaguzi lakini akaenda kuchukua fomu kugombea urais kupitia ccm marehemu Nyerere akamwuliza hata wewe jaji
 
Back
Top Bottom