Mwanasheria mkuu wa chuo kikuu cha Dodoma ameandika barua ya kuacha kazi ndani ya masaa 24. Hii imetokana na yeye kushindwa kuendelea kuvumilia kitendo cha uongozi wa chuo hicho kuwa na tabia ya kumshinikiza kufanya mambo ambayo ni kinyume na taratibu za kisheria ambayo humfanya kushindwa kesi nyingi na hivyo kuiweka taaluma yake matatani. Moja kati ya kesi anazoshinikizwa ni pamoja na ile ya kumfukuza kazi mmoja wa tutorial assistant kwa kisingizio kwamba alidisco kwe masomo yake ya masters wakati aliahirisha masomo, pia kesi ya kuwasimamisha masomo wanafunzi kwa kisingizio kuwa wamefanya siasa ndani ya chuo. Kesi zote chuo kimeshindwa vibaya.