Mwanasheria Mkuu awe Huru

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Kati ya vitu ambavyo vimenisumbua binafsi na kunifanya kurudia tena wito wa kuifanyia marekebisho sheria ya Majukumu na Kazi za Mwanasheria Mkuu (Office of the Attorney General - Discharge of Duties - 2005) ni pale niliposikia kuwa Rais anamuagiza Mwanasheria Mkuu kufanya kazi yake ambayo aliapa kuifanya lilipokuja suala la uchunguzi wa EPA.

Binafsi nilikataa kabisa akilini kuwa Mwanasheria Mkuu anahitaji kuambiwa na Rais nini cha kufanya kana kwamba hajui mamlaka yake au hana uwezo wa kupima kitu yeye mwenyewe. Kitendo cha Rais Kikwete kukaa chini na kumuagiza Mwanasheria Mkuu kufanya uchunguzi wa EPA na kuchukua hatua za kisheria kwangu kiliashiria mambo/matatizo makubwa mawili yaliyopo katika kutekeleza utawala wa sheria nchini.

a. Mwanasheria Mkuu hana uwezo wa kuhakikisha sheria zinafuatwa
b. Mwanasheria Mkuu anamtegemea Rais katika kujua nini cha kufanya kesho yake. Kama Rais hatomwambia nini cha kufanya sijui kama anaweza kufikiria yeye mwenyewe pasipo kuuliza tena Ikulu ili kupata baraka.

Hivyo nikalazimika kukaa chini na kuipitia sheria ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu (ambayo nimeiambatanisha hapa). Ndani yake nikaona mambo yafuatayo ambayo naamini ndiyo kiini za uzugaji wa kisheria unaoendelea nchini.

Kwenye Madaraka ya Mwanasheria Mkuu na Kazi za Mwanasheria Mkuu (Ibara ya 6 na ya 8) inaonesha ni nini kiini cha matatizo yetu. Mwanasheria hana madaraka na majukumu ya KUSIMAMIA UTEKELEZWAJI WA SHERIA ZOTE nchini yaani yeye siyo Chief Law Enforcer.

Kwanini hili ni muhimu? Umuhimu wake unakuja na unaonekana pale ambapo kuna watu wanaofanya kana kwamba hakuna sheria nchini au sheria zilizopo ni kama maoni tu au mapendekezo ya aina fulani. Ukiangalia kwa ukaribu sakata la Benki Kuu ni udhihirisho wa mawazo ya namna hii. Mambo yaliyotokea Benki Kuu ni kana kwamba hakuna sheria nchini na hakuna aliyekuwa na majukumu ya kuangalia waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wanafuata sheria.

Ni kwa sababu hiyo basi natoa pendekezo kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu pamoja na majukumu yake mengi, ipewe jukumu la kwanza nalo ni kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa na kila mtu na hasa na kwanza kabisa wale waliopewa dhamana ya kuongoza, kusimamia, au kutekeleza majukumu fulani kwa ajili ya wananchi.

Maana yake ni nini? Manake ni kwamba Gavana wa Benki Kuu atatakiwa kufuata sheria ya fedha na ya Benki na zinazohusiana hadi nukta ya mwisho. IGP hawezi kukurupuka na kwenda kukamata watu na kuwaweka kizuizini kwa muda nje ya sheria vinginevyo Mwanasheria Mkuu anamfungulia mashtaka ya uvunjaji wa sheria.

Inapotokea kiongozi wa kisiasa au mtendaji au mtunga sheria anadaiwa kuvunja sheria Mwanasheria Mkuu anatakiwa kuanzisha uchunguzi mara moja utakaofanywa kwa mtindo wa Grand Jury au kitu kama hicho.

Jambo jingine ambalo linatakiwa kufanyika ni kuweka trigger clauses katika sheria ya Mwanasheria Mkuu ili asisubiri tena kuambiwa au kuitwa na kuelekezwa cha kufanya.

Kwa mfano hivi sasa uchunguzi wa EPA peke yake umechukua miezi sita. Bado hatujaingia kwenye suala la Meremeta, Mwananchi, Deep Green, Tangold, n.k n.k Na huko ni Benki Kuu tu na tena mwaka mmoja tu. Kama Mwanasheria Mkuu atakuwa anasubiri aambiwe na Ikulu nini cha kufanyia uchunguzi kuna dalili kuwa hadi 2010 tutakuwa tumegusa labda mambo manne tu ( kama kila moja litafanywa peke yake litachukua miezi sita kama ya EPA)

Katika kuleta mabadiliko hayo, naamini ofisi zifuatazo ziwekwe chini ya Idara ya Mwanasheria Mkuu.

- Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (anapogundua uvunjaji wa sheria kunakuwa na smooth transition to prosecution badala ya kutoa ripoti ya kila mwaka)
- Ofisi ya Mwenesha Mashtaka Mkuu wa serikali

Na pia kuanzisha kitu ambacho hakipo sasa hivi; Ikulu iwe na Mwanasheria Mkuu wa Ikulu/Rais ambaye atakuwa mshauri mkuu wa kisheria wa Rais au Ikulu. Mwanasheria Mkuu wa Tanzania atakuwa ni mshauri pale tu anapoombwa lakini jukumu lake la kwanza na kubwa zaidi ni kusimamia utekelezaji wa sheria zote nchini. Hivyo wizara na idara mbalimbali za serikali zitakuwa na wanasheria wake ambao si lazima wawe watumishi wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu (nadhani iko hivyo sasa hivi).

Haya ngoja niweke nukta maana naona sitakoma.....
 

Attachments

  • 4-2005.pdf
    984.8 KB · Views: 96
Kati ya vitu ambavyo vimenisumbua binafsi na kunifanya kurudia tena wito wa kuifanyia marekebisho sheria ya Majukumu na Kazi za Mwanasheria Mkuu (Office of the Attorney General - Discharge of Duties - 2005) ni pale niliposikia kuwa Rais anamuagiza Mwanasheria Mkuu kufanya kazi yake ambayo aliapa kuifanya lilipokuja suala la uchunguzi wa EPA.

Binafsi nilikataa kabisa akilini kuwa Mwanasheria Mkuu anahitaji kuambiwa na Rais nini cha kufanya kana kwamba hajui mamlaka yake au hana uwezo wa kupima kitu yeye mwenyewe. Kitendo cha Rais Kikwete kukaa chini na kumuagiza Mwanasheria Mkuu kufanya uchunguzi wa EPA na kuchukua hatua za kisheria kwangu kiliashiria mambo/matatizo makubwa mawili yaliyopo katika kutekeleza utawala wa sheria nchini.

a. Mwanasheria Mkuu hana uwezo wa kuhakikisha sheria zinafuatwa
b. Mwanasheria Mkuu anamtegemea Rais katika kujua nini cha kufanya kesho yake. Kama Rais hatomwambia nini cha kufanya sijui kama anaweza kufikiria yeye mwenyewe pasipo kuuliza tena Ikulu ili kupata baraka.

Hivyo nikalazimika kukaa chini na kuipitia sheria ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu (ambayo nimeiambatanisha hapa). Ndani yake nikaona mambo yafuatayo ambayo naamini ndiyo kiini za uzugaji wa kisheria unaoendelea nchini.

Kwenye Madaraka ya Mwanasheria Mkuu na Kazi za Mwanasheria Mkuu (Ibara ya 6 na ya 8) inaonesha ni nini kiini cha matatizo yetu. Mwanasheria hana madaraka na majukumu ya KUSIMAMIA UTEKELEZWAJI WA SHERIA ZOTE nchini yaani yeye siyo Chief Law Enforcer.

Kwanini hili ni muhimu? Umuhimu wake unakuja na unaonekana pale ambapo kuna watu wanaofanya kana kwamba hakuna sheria nchini au sheria zilizopo ni kama maoni tu au mapendekezo ya aina fulani. Ukiangalia kwa ukaribu sakata la Benki Kuu ni udhihirisho wa mawazo ya namna hii. Mambo yaliyotokea Benki Kuu ni kana kwamba hakuna sheria nchini na hakuna aliyekuwa na majukumu ya kuangalia waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wanafuata sheria.

Ni kwa sababu hiyo basi natoa pendekezo kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu pamoja na majukumu yake mengi, ipewe jukumu la kwanza nalo ni kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa na kila mtu na hasa na kwanza kabisa wale waliopewa dhamana ya kuongoza, kusimamia, au kutekeleza majukumu fulani kwa ajili ya wananchi.

Maana yake ni nini? Manake ni kwamba Gavana wa Benki Kuu atatakiwa kufuata sheria ya fedha na ya Benki na zinazohusiana hadi nukta ya mwisho. IGP hawezi kukurupuka na kwenda kukamata watu na kuwaweka kizuizini kwa muda nje ya sheria vinginevyo Mwanasheria Mkuu anamfungulia mashtaka ya uvunjaji wa sheria.

Inapotokea kiongozi wa kisiasa au mtendaji au mtunga sheria anadaiwa kuvunja sheria Mwanasheria Mkuu anatakiwa kuanzisha uchunguzi mara moja utakaofanywa kwa mtindo wa Grand Jury au kitu kama hicho.

Jambo jingine ambalo linatakiwa kufanyika ni kuweka trigger clauses katika sheria ya Mwanasheria Mkuu ili asisubiri tena kuambiwa au kuitwa na kuelekezwa cha kufanya.

Kwa mfano hivi sasa uchunguzi wa EPA peke yake umechukua miezi sita. Bado hatujaingia kwenye suala la Meremeta, Mwananchi, Deep Green, Tangold, n.k n.k Na huko ni Benki Kuu tu na tena mwaka mmoja tu. Kama Mwanasheria Mkuu atakuwa anasubiri aambiwe na Ikulu nini cha kufanyia uchunguzi kuna dalili kuwa hadi 2010 tutakuwa tumegusa labda mambo manne tu ( kama kila moja litafanywa peke yake litachukua miezi sita kama ya EPA)

Katika kuleta mabadiliko hayo, naamini ofisi zifuatazo ziwekwe chini ya Idara ya Mwanasheria Mkuu.

- Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (anapogundua uvunjaji wa sheria kunakuwa na smooth transition to prosecution badala ya kutoa ripoti ya kila mwaka)
- Ofisi ya Mwenesha Mashtaka Mkuu wa serikali

Na pia kuanzisha kitu ambacho hakipo sasa hivi; Ikulu iwe na Mwanasheria Mkuu wa Ikulu/Rais ambaye atakuwa mshauri mkuu wa kisheria wa Rais au Ikulu. Mwanasheria Mkuu wa Tanzania atakuwa ni mshauri pale tu anapoombwa lakini jukumu lake la kwanza na kubwa zaidi ni kusimamia utekelezaji wa sheria zote nchini. Hivyo wizara na idara mbalimbali za serikali zitakuwa na wanasheria wake ambao si lazima wawe watumishi wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu (nadhani iko hivyo sasa hivi).

Haya ngoja niweke nukta maana naona sitakoma.....

Naona kuna haja ya kuandika katiba mpya na kuachana na hii ya wakoloni tuliyo nayo sasa hivi. Kubadili tu hakutoshi kabisa, wakenya wameamua kuandika katiba mpya na kuanza taifa la wakenya kwa manufaaa ya wakenya wote.
 
Mwanakijiji uko sahihi katika mambo mengi labda tu usahhi wa vitu vichache. Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Mkuu iko chini ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali lakini hana mamlaka ya kumuamru jinsi ya kuendesha kesi za jinai wala jinsi ya kuanzisha upelelezi wa kesi yoyote. Mamlaka ya AG yako limited katika kuishauri serikali kama inavyotamka katiba au sheria ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kuhusu kwamba Rais ndiye anamwagiza AG kufanya uchunguzi, sidhani kama hili ni tatizo maana ni Rais ndiye aliyeunda Timu ya Uchunguzi na anayo mamlaka hayo. AG hana mamlaka ya uchunguzi chini ya katiba au sheria. Uchunguzi hufanywa na vyombo vya uchunguzi kama vile polisi, PCCB nk. Hat DPP anaendesha kesi ambazo zimeshachunguzwa. Hii haina maana kuwa AG hawezi kushauri kuwa upelelzi ufanyike katika suala fulani, atafanya hivyo kama ushauri wa kawaida ambao anaruhusiwa kisheria. Haya ndiyo maoni yangu kwa hili
 
Jobo.. ndio sababu ninasema Mwanasheria Mkuu asiyesimamia utekelezaji wa sheria anakuwaje Mwanasheria Mkuu? Kama Rais ameona kuwa Mwanasheria Mkuu (na siyo IGP, DCI) aongoze uchunguzi wa EPA ina maana Mwanasheria Mkuu anaweza kuongoza uchunguzi wa aina fulani. Kwanini basi tusimpe nguvu ya kufanya uchunguzi badala ya kusubiri kumegewa nguvu na Rais?
 
Jobo.. ndio sababu ninasema Mwanasheria Mkuu asiyesimamia utekelezaji wa sheria anakuwaje Mwanasheria Mkuu? Kama Rais ameona kuwa Mwanasheria Mkuu (na siyo IGP, DCI) aongoze uchunguzi wa EPA ina maana Mwanasheria Mkuu anaweza kuongoza uchunguzi wa aina fulani. Kwanini basi tusimpe nguvu ya kufanya uchunguzi badala ya kusubiri kumegewa nguvu na Rais?

Ni hali ya kustaajabisha kidogo. Umetupa mwanga mkubwa kidogo na kufanya wengi wetu kufikiria mara mbili. Naona ifike mahali tusiwe na ofisi kama hii kabisa. Ukiniuliza kwanini nitajibu haina maana. Ni watu kutafutiana ulaji tu. Kama mtu anasubiri kupewa amri na Rais, au kama mtu ameacha mikataba mibovu kibao ikasainiwa, kuna faida gani ya kuwa na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali? IFUTWE!
 
Jobo.. ndio sababu ninasema Mwanasheria Mkuu asiyesimamia utekelezaji wa sheria anakuwaje Mwanasheria Mkuu? Kama Rais ameona kuwa Mwanasheria Mkuu (na siyo IGP, DCI) aongoze uchunguzi wa EPA ina maana Mwanasheria Mkuu anaweza kuongoza uchunguzi wa aina fulani. Kwanini basi tusimpe nguvu ya kufanya uchunguzi badala ya kusubiri kumegewa nguvu na Rais?

Kwa maelezo haya ninakubaliana na wewe kabisa kuwa Mwanasheria Mkuu kama mshauri mkuu wa sheria wa Serikali anapaswa kuwa na uwezo wa kushauri au hata kuanzisha upelelezi wa masuala nyeti kama haya ya EPA. Kwa kiasi fulani uwezo huu unaweza kuleta kile wazungu wanaita "conflict of interest" or rather "conflict of jurisdiction" kwa sababu Rais ameteua baadhi ya vyombo vya umma na kuvipa madaraka ya upelelezi. Hata katika hii Timu ya sasa wengi walikuwa wanauliza ni kwa nini amepewa yeye kazi ambayo kikatiba ni ya DPP, DCI na DPCCB. Naamini alifanya hivyo kwa kutambua kuwa uwepo wake utasaidia katika kuhakikisha kuwa sheria inafuatwa.
 
Kwa maelezo haya ninakubaliana na wewe kabisa kuwa Mwanasheria Mkuu kama mshauri mkuu wa sheria wa Serikali anapaswa kuwa na uwezo wa kushauri au hata kuanzisha upelelezi wa masuala nyeti kama haya ya EPA. Kwa kiasi fulani uwezo huu unaweza kuleta kile wazungu wanaita "conflict of interest" or rather "conflict of jurisdiction" kwa sababu Rais ameteua baadhi ya vyombo vya umma na kuvipa madaraka ya upelelezi. Hata katika hii Timu ya sasa wengi walikuwa wanauliza ni kwa nini amepewa yeye kazi ambayo kikatiba ni ya DPP, DCI na DPCCB. Naamini alifanya hivyo kwa kutambua kuwa uwepo wake utasaidia katika kuhakikisha kuwa sheria inafuatwa.


sasa katika ninachopendekeza mimi.. ni kuwa AG anakuwa katika utekelezaji wa sheria yuko juu ya hawa wengine wote. HIvyo, DCI au DPCCB anaposhindwa, kuchelewa au kutokufanya uchunguzi basi ofisi ya Mwanasheria Mkuu inaweza kumchunguza na wakiona amevunja sheria wanamfungulia mashtaka. Hivyo kutakuwa hakuna kungojana.

Inapotokea tatizo liko kwa AG basi Bunge linaweza kuanzisha uchunguzi kwa kumuamuaru DCI au Special Investigator au Special Counsel ambaye atakuwa ni mtu mwenye sifa za ujaji kusimamia uchunguzi wa ofisi ya AG.
 
Kati ya vitu ambavyo vimenisumbua binafsi na kunifanya kurudia tena wito wa kuifanyia marekebisho sheria ya Majukumu na Kazi za Mwanasheria Mkuu (Office of the Attorney General - Discharge of Duties - 2005) ni pale niliposikia kuwa Rais anamuagiza Mwanasheria Mkuu kufanya kazi yake ambayo aliapa kuifanya lilipokuja suala la uchunguzi wa EPA.

Binafsi nilikataa kabisa akilini kuwa Mwanasheria Mkuu anahitaji kuambiwa na Rais nini cha kufanya kana kwamba hajui mamlaka yake au hana uwezo wa kupima kitu yeye mwenyewe. Kitendo cha Rais Kikwete kukaa chini na kumuagiza Mwanasheria Mkuu kufanya uchunguzi wa EPA na kuchukua hatua za kisheria kwangu kiliashiria mambo/matatizo makubwa mawili yaliyopo katika kutekeleza utawala wa sheria nchini.

a. Mwanasheria Mkuu hana uwezo wa kuhakikisha sheria zinafuatwa
b. Mwanasheria Mkuu anamtegemea Rais katika kujua nini cha kufanya kesho yake. Kama Rais hatomwambia nini cha kufanya sijui kama anaweza kufikiria yeye mwenyewe pasipo kuuliza tena Ikulu ili kupata baraka.

Hivyo nikalazimika kukaa chini na kuipitia sheria ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu (ambayo nimeiambatanisha hapa). Ndani yake nikaona mambo yafuatayo ambayo naamini ndiyo kiini za uzugaji wa kisheria unaoendelea nchini.

Kwenye Madaraka ya Mwanasheria Mkuu na Kazi za Mwanasheria Mkuu (Ibara ya 6 na ya 8) inaonesha ni nini kiini cha matatizo yetu. Mwanasheria hana madaraka na majukumu ya KUSIMAMIA UTEKELEZWAJI WA SHERIA ZOTE nchini yaani yeye siyo Chief Law Enforcer.

Kwanini hili ni muhimu? Umuhimu wake unakuja na unaonekana pale ambapo kuna watu wanaofanya kana kwamba hakuna sheria nchini au sheria zilizopo ni kama maoni tu au mapendekezo ya aina fulani. Ukiangalia kwa ukaribu sakata la Benki Kuu ni udhihirisho wa mawazo ya namna hii. Mambo yaliyotokea Benki Kuu ni kana kwamba hakuna sheria nchini na hakuna aliyekuwa na majukumu ya kuangalia waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi wanafuata sheria.

Ni kwa sababu hiyo basi natoa pendekezo kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu pamoja na majukumu yake mengi, ipewe jukumu la kwanza nalo ni kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa na kila mtu na hasa na kwanza kabisa wale waliopewa dhamana ya kuongoza, kusimamia, au kutekeleza majukumu fulani kwa ajili ya wananchi.

Maana yake ni nini? Manake ni kwamba Gavana wa Benki Kuu atatakiwa kufuata sheria ya fedha na ya Benki na zinazohusiana hadi nukta ya mwisho. IGP hawezi kukurupuka na kwenda kukamata watu na kuwaweka kizuizini kwa muda nje ya sheria vinginevyo Mwanasheria Mkuu anamfungulia mashtaka ya uvunjaji wa sheria.

Inapotokea kiongozi wa kisiasa au mtendaji au mtunga sheria anadaiwa kuvunja sheria Mwanasheria Mkuu anatakiwa kuanzisha uchunguzi mara moja utakaofanywa kwa mtindo wa Grand Jury au kitu kama hicho.

Jambo jingine ambalo linatakiwa kufanyika ni kuweka trigger clauses katika sheria ya Mwanasheria Mkuu ili asisubiri tena kuambiwa au kuitwa na kuelekezwa cha kufanya.

Kwa mfano hivi sasa uchunguzi wa EPA peke yake umechukua miezi sita. Bado hatujaingia kwenye suala la Meremeta, Mwananchi, Deep Green, Tangold, n.k n.k Na huko ni Benki Kuu tu na tena mwaka mmoja tu. Kama Mwanasheria Mkuu atakuwa anasubiri aambiwe na Ikulu nini cha kufanyia uchunguzi kuna dalili kuwa hadi 2010 tutakuwa tumegusa labda mambo manne tu ( kama kila moja litafanywa peke yake litachukua miezi sita kama ya EPA)

Katika kuleta mabadiliko hayo, naamini ofisi zifuatazo ziwekwe chini ya Idara ya Mwanasheria Mkuu.

- Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (anapogundua uvunjaji wa sheria kunakuwa na smooth transition to prosecution badala ya kutoa ripoti ya kila mwaka)
- Ofisi ya Mwenesha Mashtaka Mkuu wa serikali

Na pia kuanzisha kitu ambacho hakipo sasa hivi; Ikulu iwe na Mwanasheria Mkuu wa Ikulu/Rais ambaye atakuwa mshauri mkuu wa kisheria wa Rais au Ikulu. Mwanasheria Mkuu wa Tanzania atakuwa ni mshauri pale tu anapoombwa lakini jukumu lake la kwanza na kubwa zaidi ni kusimamia utekelezaji wa sheria zote nchini. Hivyo wizara na idara mbalimbali za serikali zitakuwa na wanasheria wake ambao si lazima wawe watumishi wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu (nadhani iko hivyo sasa hivi).

Haya ngoja niweke nukta maana naona sitakoma.....

Mwnkjj,

Hilo ulilolionyesha hapo ni moja ya changa la macho kubwa kuliko yote katika mfumo wa Sheria wa Tanzania.

Lakini kuna tatizo katika suluhisho ulilotoa.

Ukimpa Attorney General nguvu ya kuchunguza uvunjaji sheria mwisho wa siku ni Director of Public Prosecutions ndio ataamua kuleta mashitaka. Hilo bado litakuwa changa la macho! Anatakiwa awepo mtu mwenye nguvu ya kuchunguza, mwenye wajibu wa kuchunguza (umeziita triger clauses) na hapo hapo, nguvu ya kuamua kushitaki. Kufanya hivyo yabidi ufute moja ya hivi vyeo viwili: AG au DPP.

Halafu kuhusu Kikwete kutoa maagizo, nadhani yule mtu hajui cha kuongea hadharani. Mfano, kwenye kesi ya waandishi walipofanyiwa unyama. Kikwete alisema hivi:

"I have ordered the Inspector General of Police to make sure that all those responsible are brought to justice. Jan 8th, 2008

Lakini siku hiyo hiyo Polisi, kupitia RPC Tibaigana, ikasema ilikuwa tayari imeshaanza criminal procedure za uchunguzi.

The Citizens, Jan 1st, 2008
Police have formed a team of detectives, including some from the office of the Director of Criminal Investigations, that would work with their colleagues from the Kinondoni Regional Police Zone to investigate the incident. "Preliminary investigations show that the two items were in possession of the assailants when they carried out the attack," Mr Tibaigana said, adding that police were questioning the suspects.


Sasa, hapa Kikwete alichosema kwa kweli ni kama kuwatia tu presha wa make sure, wafanye kile tayari wanacho takiwa kufanya. (Kama anaagiza watoto vile, if you ask me). Halafu kinaitwa maagizo ya Rais, kana kwamba watu wake kazi yao hawaiwezi au hawaijui bila kukumbushwa na Rais.

Huyo ni Kikwete, hajui jinsi ya kuwaongelesha watu wake. Juzi kasema Waziri wa Madini Ngeleja asipewe Executive Summary ya Ripoti kwa sababu ataingia uvivu na kushindwa kusoma ripoti nzima. Kama una read between the lines huku ni kusema anateua watu wavivu! Hajui jinsi ya kuongea hadharani.
 
Kuhani... tunavyozungumza ndivyo tunavyoliona tatizo kwa mwanga zaidi na ndivyo tunavyoweza kupata suluhisho...
 
Ili mapendekezo yako Mzee Mwanakijiji yaweze kutoa matunda ni vizuri tukaiga mfano wa Kenya. Unajua Kikatiba AG anonekana kuwa ana nguvu lakini hana chochote kwa maana Rais ana uwezo wa kumwondoa anavyotaka. Amosi Wako ambaye ni AG wa Kenya amekuwepo tangu enzi za Moi na sasa Kibaki. Alimrithi Njonjo miaka ya mwanzo ya 80. Huyu analindwa na Katiba maana ni mtumishi wa Umma mwenye mamlaka makubwa ya kusimamia sheria za nchi. Hayuko chini ya Waziri wa Sheria na ana hadhi kubwa. Hapa kwetu, akiingia Rais mpya ana uwezo wa kumwondoa AG na kumweka anayemtaka yeye bila kuangalia uwezo. Kwa kifupi, Katiba ya Tanzania haimlindi AG na ndiyo maana anafanya kazi kwa uoga. Akistaafu AG analipwa kama kiongozi mwingine wa kisiasa wakati yeye ni mtumishi wa umma. Hana mafao ya kustaafu kama majiji au Magenerali wa Jeshi. Kwa kweli a complete overhaul of the law is required.
 
Ili mapendekezo yako Mzee Mwanakijiji yaweze kutoa matunda ni vizuri tukaiga mfano wa Kenya. Unajua Kikatiba AG anonekana kuwa ana nguvu lakini hana chochote kwa maana Rais ana uwezo wa kumwondoa anavyotaka. Amosi Wako ambaye ni AG wa Kenya amekuwepo tangu enzi za Moi na sasa Kibaki. Alimrithi Njonjo miaka ya mwanzo ya 80. Huyu analindwa na Katiba maana ni mtumishi wa Umma mwenye mamlaka makubwa ya kusimamia sheria za nchi. Hayuko chini ya Waziri wa Sheria na ana hadhi kubwa. Hapa kwetu, akiingia Rais mpya ana uwezo wa kumwondoa AG na kumweka anayemtaka yeye bila kuangalia uwezo. Kwa kifupi, Katiba ya Tanzania haimlindi AG na ndiyo maana anafanya kazi kwa uoga. Akistaafu AG analipwa kama kiongozi mwingine wa kisiasa wakati yeye ni mtumishi wa umma. Hana mafao ya kustaafu kama majiji au Magenerali wa Jeshi. Kwa kweli a complete overhaul of the law is required.

Jobo,

Tatizo hapa sio AG kufanya kazi kwa uoga. Tatizo ni kwamba katika majukumu ya kazi za AG hakuna nguvu ya kuanzisha mashitaka kama akiona yafaa. Kwa hiyo hili la kuogopa kuondolewa madarakani sio ishu. Sio kazi yake.

Isitoshe, hiyo model ya Kenya ina matatizo yake pia. Mtu ambae kazi yake inalindwa sana na Katiba anaweza kukosa accountability kwa sababu haogopi kitu. Isitoshe, viongozi siku zote wanatofautiana uwezo. Rais anaweza kushindwa kumteua mtu mwenye uwezo zaidi kwa sababu aliye kuwepo habanduliki. Kuna wakati unahitaji kuleta prosecutor mpya mjini ili mambo fulani yashitakiwe ambayo yule aliyepo haoni ni matatizo. Kwa mfano, kabla hajaja Eliot Spitzer kuwa AG wa jimbo la New York, yule aliye kuwepo hakuona kama Wall Street kuna uvunjaji sheria ulio kithiri. Kuna wakati unahitaji fresh eyes.

Lingine, model ya Kenya nayo ina changa la macho fulani:

Section 26 (3)
The Attorney-General shall have power in any case in which he considers it desirable so to do -

(a) to institute and undertake criminal proceedings against any person before any court (other than a court-martial) in respect of any offence alleged to have been committed by that person;


Halafu inaharibu hapa:


(c) to discontinue at any stage before judgment is delivered any such criminal proceedings instituted or undertaken by himself or another person or authority.

AG anapewa nguvu ya kufuta mashitaka yaliyo anzishwa na mtu mwingine. Hii haitofautiani na model ya Tanzania ambapo mashitaka yeyote lazima yaidhinishwe na Director of Public Prosecutions. Model ya Kenya inafanya kitu kile kile cha Tanzania lakini kwa kujificha. Inatoa nguvu kwa mkono wa kulia halafu inainyopoa kwa mkono wa kushoto. Model zote ni michanga ya macho!
 
As a nation tunahitaji kuwa na Mwanasheria mkuu, cha muhimu ni kubadilishwa kwa katiba yetu ili huyu AG awe huru, na hili litawezekana pale tu bunge letu litakapohusika na process ya appointment ya AG,

Lakini as long as the process inaednelea kuwa chini ya executive branch, kama sasa yes ni vyema kutokuwa na hicho cheo kabisa!
 
Jobo,

Tatizo hapa sio AG kufanya kazi kwa uoga. Tatizo ni kwamba katika majukumu ya kazi za AG hakuna nguvu ya kuanzisha mashitaka kama akiona yafaa. Kwa hiyo hili la kuogopa kuondolewa madarakani sio ishu. Sio kazi yake.

Isitoshe, hiyo model ya Kenya ina matatizo yake pia. Mtu ambae kazi yake inalindwa sana na Katiba anaweza kukosa accountability kwa sababu haogopi kitu. Isitoshe, viongozi siku zote wanatofautiana uwezo. Rais anaweza kushindwa kumteua mtu mwenye uwezo zaidi kwa sababu aliye kuwepo habanduliki. Kuna wakati unahitaji kuleta prosecutor mpya mjini ili mambo fulani yashitakiwe ambayo yule aliyepo haoni ni matatizo. Kwa mfano, kabla hajaja Eliot Spitzer kuwa AG wa jimbo la New York, yule aliye kuwepo hakuona kama Wall Street kuna uvunjaji sheria ulio kithiri. Kuna wakati unahitaji fresh eyes.

Lingine, model ya Kenya nayo ina changa la macho fulani:

Section 26 (3)
The Attorney-General shall have power in any case in which he considers it desirable so to do -

(a) to institute and undertake criminal proceedings against any person before any court (other than a court-martial) in respect of any offence alleged to have been committed by that person;


Halafu inaharibu hapa:


(c) to discontinue at any stage before judgment is delivered any such criminal proceedings instituted or undertaken by himself or another person or authority.

AG anapewa nguvu ya kufuta mashitaka yaliyo anzishwa na mtu mwingine. Hii haitofautiani na model ya Tanzania ambapo mashitaka yeyote lazima yaidhinishwe na Director of Public Prosecutions. Model ya Kenya inafanya kitu kile kile cha Tanzania lakini kwa kujificha. Inatoa nguvu kwa mkono wa kulia halafu inainyopoa kwa mkono wa kushoto. Model zote ni michanga ya macho!

Nadhani tunaongea kitu kimoja ingawa kwa lugha tofauti. Kwa Tanzania unaye AG ambaye anatakiwa kuwa mkuu wa masuala ya sheria lakini hana mamlaka katika mashauri ya jinai. DPP pamoja na kwamba yuko chini ya AG kikatiba na yuko ndani ya ofisi yake inapofika katika masuala ya jinai, AG hana sauti na ndiyo maana hawezi hata siku moja chini ya sheria ya sasa kuanzisha upelelezi wa jambo lolote la kijinai!
 
Naona wote mnakubali kwamba kuna umuhimu wa kuwa na ofisi ya AG. Tatizo ni mfumo wa uteuzi wake, madaraka yake na awajibike kwa nani. Kama uteuzi utaendelea kufanywa na Rais, na Rais akapewa nguvu za kuutengua uteuzi, basi kuna kila sababu ya kuamini kwamba ofisi ya AG haiwezi kuwa na meno, na itakuwa ikifanya kazi kwa uoga mkubwa. Vivyo hivyo kwenye suala la madaraka yake na uwajibikaji kwa ujumla. Kuna kila haja ya kupitia upya katiba yetu na kuona namna ya kurekebisha hili.
 
Naona wote mnakubali kwamba kuna umuhimu wa kuwa na ofisi ya AG. Tatizo ni mfumo wa uteuzi wake, madaraka yake na awajibike kwa nani. Kama uteuzi utaendelea kufanywa na Rais, na Rais akapewa nguvu za kuutengua uteuzi, basi kuna kila sababu ya kuamini kwamba ofisi ya AG haiwezi kuwa na meno, na itakuwa ikifanya kazi kwa uoga mkubwa. Vivyo hivyo kwenye suala la madaraka yake na uwajibikaji kwa ujumla. Kuna kila haja ya kupitia upya katiba yetu na kuona namna ya kurekebisha hili.

Nakuabaliana na wewe. Rais anaweza kumteua lakini asiwe na uwezo wa kumwondoa bial uchunguzi wa kina kama ule unaowahusu majaji haujatumika.
 
Mwnkjj,

Hilo ulilolionyesha hapo ni moja ya changa la macho kubwa kuliko yote katika mfumo wa Sheria wa Tanzania.

Lakini kuna tatizo katika suluhisho ulilotoa.

Ukimpa Attorney General nguvu ya kuchunguza uvunjaji sheria mwisho wa siku ni Director of Public Prosecutions ndio ataamua kuleta mashitaka. Hilo bado litakuwa changa la macho! Anatakiwa awepo mtu mwenye nguvu ya kuchunguza, mwenye wajibu wa kuchunguza (umeziita triger clauses) na hapo hapo, nguvu ya kuamua kushitaki. Kufanya hivyo yabidi ufute moja ya hivi vyeo viwili: AG au DPP.

Sidhani hapa kuna tatizo kubwa. La msingi ni kuhakikisha suala la uhusiano kati ya DPP na AG unawekwa vizuri zaidi. Sasa hivi DPP iko chini ya AG ambacho si kitu kibaya. Hata hivyo mahusiano yao yanaleta matatizo ya msingi ambapo DPP ana nguvu za kufuatilia uchunguzi wowote unaofanywa (Sheria ya Mwanasheria Mkuu Ibara 10, Kifungu cha 1b) na pia ana nguvu ya kuviagiza vyombo vya uchunguzi kuhusu suala fulani la uchunguzi wa kihalifu (Sheria hiyo hiyo kifungu 2d)

Ninapozisoma sheria hizo naweza kuona kuwa DPP ana mamlaka ya kuanzisha au kuamuru kufanyika uchunguzi utaoweza kusababisha mashtaka dhidi ya mtu yeyote yule. Kama DPP angejua hilo, Rais asingetakiwa kuingilia kati na kuamuru uchunguzi wowote ufanyike.

Lakini hiyo ni tafrisi yangu, lakini hakuna mahali ambapo panasema wazi kabisa kuwa AG au DPP ana nguvu ya kuinitiate investigation of a criminal nature kuhusu suala lolote katika Jamhuri yetu. Kama wangekuwa nao hadi sasa hivi tungekuwa na watu wanafuatilia suala la Buhemba, Mwananchi Gold, n.k n.k

Hofu yangu ni kuwa kazi ya DPP imevamiwa na watu wa PCCB ambao wamekuwa wakidandia uchunguzi wowote wa kihalifu ili kuona mambo ya rushwa hasa yale yenye high profile. Badala ya kuangalia uwepo wa rushwa kubwa lilitakiwa ni kama kuangalia kuna what is known as "criminal activity" or "acts of criminal nature". Na hili lilitakiwa kufanywa na DPP.

Kwa hiyo nadhani kimsingi tuko pamoja.


Kuhusu maagizo ya Rais, naamini tukikaa chini na kuuliza sidhani kama yote yanayotolewa majukwaani ni true executive orders. Kuna amri za kisiasa na za majukwaani lakini kuna maagizo ya Rais ambayo yana nguvu ya kisheria. Nimejaribu kuangalia kama tuna "Executive Privileges" au "Executive Orders".
 
Nakuabaliana na wewe. Rais anaweza kumteua lakini asiwe na uwezo wa kumwondoa bial uchunguzi wa kina kama ule unaowahusu majaji haujatumika.

Nadhani wateuliwa wote wa Rais kwa kiwango kikubwa lazima wafanye kazi "at the Pleasure of the President" ukiondoa wale wanaofanya kazi katika mhimili mwingine. Hivyo watu kama Majaji akiwateua hana uwezo wa kuwafuta kazi hadi wawe impeached.

Kwa upande wa Mwanasheria Mkuu ni lazima awe anafanya kazi at the pleasure of the President, lakini lazima apewe nguvu ya kufanya kazi yake na alindwe kufanya hivyo pasipo tishio la kuondolewa na Rais akianza uchunguzi wa aina fulani. Hapa inahitaji kutafakari vizuri.
 
Kwa upande wa Mwanasheria Mkuu ni lazima awe anafanya kazi at the pleasure of the President, lakini lazima apewe nguvu ya kufanya kazi yake na alindwe kufanya hivyo pasipo tishio la kuondolewa na Rais akianza uchunguzi wa aina fulani. Hapa inahitaji kutafakari vizuri.

Akiwa at his pleasure basi anapaswa kufanya anachotaka Rais!
 
ndio manake, Rais atafanya kazi kwa pleasure yake ili mradi havunji sheria yeyote ya nchi. Kama sio kufanya kazi kwa pleasure na maslahi ya chama anachotoka basi leo Tanzania kungekuwa na serikali ya mseto, watu kama kina Slaa, Zitto na wengine wangetakiwa wawe miongoni mwa mawaziri. Mambo ya EPA; Richmond, Kiwira, Buzwagi na mazagazaga yote ya ufisadi Rais angeshayashughulikia zamani mno.
 
Mwanakijiji,Jobo,Mama,Zero,Kuhani Mkuu,

..nilifikiri uchunguzi unafanywa na Director of Criminal Investigation--DCI.

..mashtaka yanafanywa na Director of Public Prosecution -- DPP.

..mwanasheria mkuu is the Chief Legal Counsel wa serikali.

..kazi ya mwanasheria mkuu ni kushauri na kuitetea serikali ktk mashauri ya kisheria.

NB:

..sijui ni mimi tu au, lakini nadhani matatizo yetu na Chenge na Mwanyika yanatukwaza ktk kuwatofautisha wao na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na majukumu yake.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom