kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,887
Baqeri aidha amesema ulipizaji kisasi mkali unawasubiri waliotekeleza ugaidi huo kwani watafuatiliwa na kufikishwa kizimbani.
Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Amri Hatami amesema Shirika la Utafiti na Ubunifu katika Wizara ya Ulinzi ya Iran, ambalo lilikuwa likisimamiwa na Shahidi Fakhirzadeh, lilikuwa mstari wa mbele kuunda vifaa vya kupima ugonjwa wa corona. Amesema pia alikuwa akiongoza jitihada za kuunda chanjo ya corona nchini na matokeo ya jitihada hizo yatatangazwa.
Huku akilaani mauaji hayo, Hatami amesema Fakhirzadeh alikuwa pia naibu waziri wa ulinzi, na mwanasayansi mashuhuri aliyekuwa na historia ndefu ya ubunifu na aliwapa mafunzo wanasayansi wengi kwa ajili ya ustawi wa kisayansi Iran.
Kwa mfano alihusika katika utumizi wa takenolojia ya miale ya laser katika kutambua ndege za adui pasina kutegemea radar.
Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia Jenerali Amri Hatami amesema Shirika la Utafiti na Ubunifu katika Wizara ya Ulinzi ya Iran, ambalo lilikuwa likisimamiwa na Shahidi Fakhirzadeh, lilikuwa mstari wa mbele kuunda vifaa vya kupima ugonjwa wa corona. Amesema pia alikuwa akiongoza jitihada za kuunda chanjo ya corona nchini na matokeo ya jitihada hizo yatatangazwa.
Huku akilaani mauaji hayo, Hatami amesema Fakhirzadeh alikuwa pia naibu waziri wa ulinzi, na mwanasayansi mashuhuri aliyekuwa na historia ndefu ya ubunifu na aliwapa mafunzo wanasayansi wengi kwa ajili ya ustawi wa kisayansi Iran.
Kwa mfano alihusika katika utumizi wa takenolojia ya miale ya laser katika kutambua ndege za adui pasina kutegemea radar.