Augustoons
JF-Expert Member
- Oct 31, 2007
- 409
- 30
Mwananzila: Tulikurupuka sekondari za kata
na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Awamu ya Nne, imekiri kukurupuka katika ujenzi wa sekondari za kata ambazo kwa asilimia kubwa zimekosa sifa za kupokea wanafunzi, upungufu wa walimu na vitabu.
Akizungumza wakati wa mahafali ya tatu ya kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya St Matthews, Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ludovic Mwananzila, alisema uamuzi huo unaigharimu serikali.
Pamoja na hayo, Mwananzila aliweka wazi kwamba kufutwa kwa michepuo ni sababu nyingine inayoendelea kuathiri sekta ya elimu Tanzania.
Alisema, katika kuhakikisha kwamba shule za kata zilizohimizwa kujengwa nchi nzima, zinakuwa na michepuo ya maabara, karakana na kuajiri walimu wa kutosha wenye sifa, serikali pia itatoa mafunzo ya kiwango cha juu kwa walimu wa sekondari hizo.
Haiingii akilini kuona shule ina mwalimu mmoja hili ni jambo lisilowezekana hata kama shule hiyo ingekuwa ina darasa la kwanza tu, alisema naibu waziri huyo.
Katika kuhakikisha kwamba serikali kupitia wizara yake inaboresha kiwango cha elimu nchini, Mwananzila alibainisha kuwa lengo la serikali ya Awamu ya Nne, kwa sasa ni kuangalia jinsi itakavyotoa mikopo kwa wanafunzi wote wanaojiunga na vyuo vya elimu ya juu.
Naibu waziri huyo aliwataka wanafunzi wanaokopa kurejesha mikopo hiyo mara wanapoanza kazi, ili kuwasadia wengine wanaojiunga na vyuo hivyo.
Awali akimkaraibisha mgeni rasmi, Mkurugenzi wa shule hiyo, Thadeus Mtembei, aliitaka serikali kuziboresha shule za kata ili zikidhi sifa sambamba na vyuo vya ufundi kwa lengo la kuajiri wanafunzi wanaomaliza mafunzo mbalimbali.
Naye Mkuu wa Shule hiyo, Charles Mtenga, alimpongeza mkurugenzi huyo, kwa kutenge sh milioni 20 kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki na fedha taslimu kama motisha kwa walimu wanaofaulisha vizuri hali inayochangia ukuaji wa taaluma na ufaulu wa wanafunzi wao.
Jumla ya wanafunzi 219 wa shule hiyo walihitimu na kutunukiwa vyeti huku baadhi yao wakijizolea zawadi mbalimbali na nyingi kati ya hizo zilikwenda kwa wasichana walioongoza kitaaluma.
chanzo:Tanzania daima 14/1/2008
KWAKWELI HII NAYO KALI.
Hawa jamaa sijui wanapopanga mipango yao sijui huwa wanafanya utafiti? au sijui huwa wanaota ndoto tu na kuanza kutekeleza? wana JF hii serikali sometimes nashindwa kuielewa. Wizara ya elimu imekuwa wizara ya majaribio ya sera,kila waziri akija anakuja na msimamo wake matokeao yake ni kuwa na mawaziri karibu kumi na misimamo kumi tofauti.Halafu cha kushangaza mara wanapoanza kutekeleza mikakati hiyo ukiwapinga wanakuwa wakali kama pilipili na wa kwanza kukanusha. Ona sasa aibu inavyowapata hadi wanafikia kukiri hadharani.Hii unatufundisha nini?
na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Awamu ya Nne, imekiri kukurupuka katika ujenzi wa sekondari za kata ambazo kwa asilimia kubwa zimekosa sifa za kupokea wanafunzi, upungufu wa walimu na vitabu.
Akizungumza wakati wa mahafali ya tatu ya kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya St Matthews, Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ludovic Mwananzila, alisema uamuzi huo unaigharimu serikali.
Pamoja na hayo, Mwananzila aliweka wazi kwamba kufutwa kwa michepuo ni sababu nyingine inayoendelea kuathiri sekta ya elimu Tanzania.
Alisema, katika kuhakikisha kwamba shule za kata zilizohimizwa kujengwa nchi nzima, zinakuwa na michepuo ya maabara, karakana na kuajiri walimu wa kutosha wenye sifa, serikali pia itatoa mafunzo ya kiwango cha juu kwa walimu wa sekondari hizo.
Haiingii akilini kuona shule ina mwalimu mmoja hili ni jambo lisilowezekana hata kama shule hiyo ingekuwa ina darasa la kwanza tu, alisema naibu waziri huyo.
Katika kuhakikisha kwamba serikali kupitia wizara yake inaboresha kiwango cha elimu nchini, Mwananzila alibainisha kuwa lengo la serikali ya Awamu ya Nne, kwa sasa ni kuangalia jinsi itakavyotoa mikopo kwa wanafunzi wote wanaojiunga na vyuo vya elimu ya juu.
Naibu waziri huyo aliwataka wanafunzi wanaokopa kurejesha mikopo hiyo mara wanapoanza kazi, ili kuwasadia wengine wanaojiunga na vyuo hivyo.
Awali akimkaraibisha mgeni rasmi, Mkurugenzi wa shule hiyo, Thadeus Mtembei, aliitaka serikali kuziboresha shule za kata ili zikidhi sifa sambamba na vyuo vya ufundi kwa lengo la kuajiri wanafunzi wanaomaliza mafunzo mbalimbali.
Naye Mkuu wa Shule hiyo, Charles Mtenga, alimpongeza mkurugenzi huyo, kwa kutenge sh milioni 20 kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki na fedha taslimu kama motisha kwa walimu wanaofaulisha vizuri hali inayochangia ukuaji wa taaluma na ufaulu wa wanafunzi wao.
Jumla ya wanafunzi 219 wa shule hiyo walihitimu na kutunukiwa vyeti huku baadhi yao wakijizolea zawadi mbalimbali na nyingi kati ya hizo zilikwenda kwa wasichana walioongoza kitaaluma.
chanzo:Tanzania daima 14/1/2008
KWAKWELI HII NAYO KALI.
Hawa jamaa sijui wanapopanga mipango yao sijui huwa wanafanya utafiti? au sijui huwa wanaota ndoto tu na kuanza kutekeleza? wana JF hii serikali sometimes nashindwa kuielewa. Wizara ya elimu imekuwa wizara ya majaribio ya sera,kila waziri akija anakuja na msimamo wake matokeao yake ni kuwa na mawaziri karibu kumi na misimamo kumi tofauti.Halafu cha kushangaza mara wanapoanza kutekeleza mikakati hiyo ukiwapinga wanakuwa wakali kama pilipili na wa kwanza kukanusha. Ona sasa aibu inavyowapata hadi wanafikia kukiri hadharani.Hii unatufundisha nini?