MAPENZI KWA NJIA YA MDOMO, NI CHANZO KIKUU CHA
SARATANI YA MDOMO NA KOO
Saratani imeendelea kuwa tishio hapa nchini huku hofu
ikiendelea kuikumba jamii kutokana na wataalamu wa afya
kushindwa kufahamu tiba halisi ya maradhi hayo hatari.
Takwimu kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road
zinaonyesha ongezeko la saratani ya mdomo na koo kwa
kiasi kikubwa kutoka kesi 167 mwaka 2006 hadi 277 mwaka
2012.
Mkurugenzi wa Idara ya Kinga
Ocean road, Julius Mwaiselage anaeleza kuwa watanzania
wasipende kuiga mambo ambayo si sahihi bila kujua
madhara yake kama kufanya mapenzi kwa njia ya mdomo.
Saratani ya mdomo ipo, na nyingine zinasababishwa na
zinaa anasema Dk Mwaiselage.
Tafiti za saratani
Tafiti mbalimbali zimewahi kufanyika nchini na kubaini
kuwepo kwa ongezeko la saratani ya mdomo.Utafiti
uliofanywa na Dk Innocent Mosha wa Kitengo cha Patholojia
cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), umebaini aina za
saratani 1,594, kati ya hizo 509 zikiwa ni za midomo kwa
mwaka 2003 pekee. Matokeo hayo yanaonyesha kuwa kati ya
saratani 509 za mdomo, saratani 242 zilisababishwa na Virusi
vya Human Papiloma ambavyo hutokana na zinaa.
Ninachojua mimi ni kuwa Virusi vya HPV husababishwa na
magonjwa ya zinaa, hivyo mtu anayeugua saratani ya aina
hiyo, imetokana na zinaa, anasema Dk Mosha.
Wanaume waathirika zaidi wa Saratani
Takwimu hizo ni zile zilizopatikana kwa watu
waliokwenda kufanyiwa uchunguzi katika Mkoa wa Dar es
Salaam pekee. Dk Mosha anasema kuwa wanaume ndiyo
huathiriwa zaidi na saratani ya mdomo ambapo kwa hapa
nchini, asilimia 53 ya wanaume waliofika MNH kwa ajili ya
vipimo, walibainika kuugua saratani hiyo, huku wanawake
wakiwa ni asilimia 47. Utafiti kama huo ulifanywa pia na Dk
Amos Mwakigonja, mkuu wa Idara ya Patholojia katika Chuo
Kikuu cha Tiba cha Muhimbili (MUHAS).
Dk Mwakigonja alifanya utafiti wa saratani ya mdomo
aina ya Kaposis Sarcoma ambapo wagonjwa 78 walibainika
na saratani hiyo kuanzia mwaka 1990 hadi 2003. Saratani
za mdomo zipo za aina nyingi na zimetofautiana kulingana
na visababishi vyake, anasema Dk Mwakigonja. Katika
utafiti wake Dk Mwakigonja alibaini kuwa wanawake wengi
walikuwa na saratani ya mdomo aina ya Kaposis Sarcoma
kuliko wanaume.
Hata hivyo, utafiti huo ulionyesha kuwa asilimia 50 ya
wanaume walikuwa na saratani ya mdomo hatari zaidi
(systemic) kuliko wanawake ambao ni asilimia 37.
Mapenzi kwa mdomo husababisha maradhi
Dk Mwakigonja anasema kuwa mapenzi yoyote kwa njia
ya mdomo lazima yasababishe maradhi ya zinaa iwapo
mmoja ameambukizwa. Pia anasema kwamba sampuli nyingi
za wanaume wanaojihusisha na mapenzi na wanaume
wenzao (mashoga) zilibainika na saratani ya mdomo. Utafiti
huo ni sehemu ya utafiti wa Shahada ya Uzamivu ambao
ulionyesha kuwa wagonjwa wengi wa saratani ya mdomo
walikuwa ni wanaume wenye umri wa miaka kati ya 38 na
kuendelea na wanawake ni 31.
Ufatiti wa WHO Tanzania
Shirika la Afya Duniani (WHO) pia lilifanya utafiti mwaka
2010 nchini kwa kushirikiana na Kituo cha Taarifa za HPV,
ambapo ilibainika kuwa asilimia 20 ya saratani za koo na
mdomo nchini zinasababishwa na ufanyaji wa mapenzi kwa
njia ya mdomo.
Taarifa hizo za WHO zinaeleza kuwa wanaume 747
hugundulika na saratani ya mdomo kila mwaka wakati
wanawake 472 hubainika na saratani hiyo pia. Wakati
huohuo, wanaume wanaopoteza maisha kutokana na saratani
hiyo ni 444, kwa mwaka na wanawake ni 270, kwa mwaka.
Utafiti wa WHO umebaini kuwa saratani ya mdomo inashika
nafasi ya sita katika aina 24 za saratani 24 zinazoisumbua
zaidi Tanzania.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa wanaume wanaoathirika zaidi
ni wenye umri wa kati ya miaka 15 na 55, ambao tayari
wameshaanza kujihusisha na ngono. Kama maradhi mengine
ya kuambukiza, Virusi vya HPV huambukizwa kwa urahisi
zaidi kutoka kwa wanawake kwenda kwa wanaume kuliko
kutoka kwa wanaume kwenda kwa wanawake. Utafiti huo
uliodhaminiwa na mfuko wa Bill na Melinda Gates na Kituo
cha Saratani na Mpango wa Utafiti wa Taasisi ya ICO
unaeleza kuwa mitandao ya kijamii na picha za ngono ndiyo
chanzo cha watu wengi kuiga ufanyaji wa mapenzi ya aina
hiyo.
Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, tafiti
zimefanyika na kubaini kuwa asilimia 70 ya wagonjwa
wanaobainika na saratani ya koo na mdomo duniani,
husababishwa na Virusi vya Human Pappiloma
vinavyotokana na magonjwa ya zinaa.Tafiti hizo zinaonyesha
kuwa wagonjwa wengi wanaogundulika na saratani hiyo ni
wanaume wenye umri wa kati, wenye uwezo wa kifedha,
wasiovuta sigara wala siyo walevi waliokubuhu.
Utafiti huo ulibaini kuwa wanaume wapo hatarini zaidi
kupata saratani ya koo inayosababishwa na Virusi vya HPV.
Miaka ya 80, idadi ndogo ya watu waliougua saratani ya koo
walihusishwa na maambukizi ya Virusi vya HPV. Kihistoria,
watu waliobainika na ugonjwa huo, ni wenye umri wa miaka
70 kwenda juu ambao walikuwa ni wale walevi waliokubuhu
na wavuta sigara.
Ilielezwa kuwa Virusi vya HPV vipo kwa wingi kiasi
ambacho watu wazima wanaojihusisha na ngono ya aina
yeyote ile, huweza kupata maambukizi ya zinaa hata kama
siyo saratani. Hata hivyo ilibainishwa kuwa saratani
isababishwayo na virusi vya HPV ni rahisi kuitibu kuliko
saratani ya koo isababishwayo na tumbaku au pombe kali.
Virusi vya HPV ni nini?
Kwa jina la jumla, saratani ya koo au mdomo huitwa
saratani ya kichwa na shingo. (Neck and Head Cancer) HPV
ni miongoni mwa virusi hatari zaidi duniani
visababishwavyo na magonjwa ya zinaa na vinaweza
kuathiri sehemu mbalimbali za mwili. Zipo aina zaidi ya 120
za HPV, baadhi huweza kuzalisha usugu (warts) ambazo si
saratani katika sehemu za siri, mikononi na miguuni.
Maambukizi ya HPV hufanyika kwa urahisi, hata kwa
kugusana ngozi au majimaji, huku maambukizi mengine
yakisababishwa na ngono.
Virusi hatari na vinavyosababisha saratani ni HPV-16,
HPV-18, HPV-31 na HPV 45. Aina hii ya Virusi vya HPV
husababisha saratani ambapo uvimbe waweza kujitokeza
kwa ndani na unaweza usionekane ukilinganisha na vivimbe
vingine vya saratani. Wataalamu wanasema HPV-16 na
HPV-18 inahusishwa zaidi na saratani ya shingo ya kizazi na
endapo mapenzi kwa njia ya mdomo yatafanywa na mtu
mwenye uambukizo huu ni rahisi kuambukizwa.
SARATANI YA MDOMO NA KOO
Saratani imeendelea kuwa tishio hapa nchini huku hofu
ikiendelea kuikumba jamii kutokana na wataalamu wa afya
kushindwa kufahamu tiba halisi ya maradhi hayo hatari.
Takwimu kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road
zinaonyesha ongezeko la saratani ya mdomo na koo kwa
kiasi kikubwa kutoka kesi 167 mwaka 2006 hadi 277 mwaka
2012.
Mkurugenzi wa Idara ya Kinga
Ocean road, Julius Mwaiselage anaeleza kuwa watanzania
wasipende kuiga mambo ambayo si sahihi bila kujua
madhara yake kama kufanya mapenzi kwa njia ya mdomo.
Saratani ya mdomo ipo, na nyingine zinasababishwa na
zinaa anasema Dk Mwaiselage.
Tafiti za saratani
Tafiti mbalimbali zimewahi kufanyika nchini na kubaini
kuwepo kwa ongezeko la saratani ya mdomo.Utafiti
uliofanywa na Dk Innocent Mosha wa Kitengo cha Patholojia
cha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), umebaini aina za
saratani 1,594, kati ya hizo 509 zikiwa ni za midomo kwa
mwaka 2003 pekee. Matokeo hayo yanaonyesha kuwa kati ya
saratani 509 za mdomo, saratani 242 zilisababishwa na Virusi
vya Human Papiloma ambavyo hutokana na zinaa.
Ninachojua mimi ni kuwa Virusi vya HPV husababishwa na
magonjwa ya zinaa, hivyo mtu anayeugua saratani ya aina
hiyo, imetokana na zinaa, anasema Dk Mosha.
Wanaume waathirika zaidi wa Saratani
Takwimu hizo ni zile zilizopatikana kwa watu
waliokwenda kufanyiwa uchunguzi katika Mkoa wa Dar es
Salaam pekee. Dk Mosha anasema kuwa wanaume ndiyo
huathiriwa zaidi na saratani ya mdomo ambapo kwa hapa
nchini, asilimia 53 ya wanaume waliofika MNH kwa ajili ya
vipimo, walibainika kuugua saratani hiyo, huku wanawake
wakiwa ni asilimia 47. Utafiti kama huo ulifanywa pia na Dk
Amos Mwakigonja, mkuu wa Idara ya Patholojia katika Chuo
Kikuu cha Tiba cha Muhimbili (MUHAS).
Dk Mwakigonja alifanya utafiti wa saratani ya mdomo
aina ya Kaposis Sarcoma ambapo wagonjwa 78 walibainika
na saratani hiyo kuanzia mwaka 1990 hadi 2003. Saratani
za mdomo zipo za aina nyingi na zimetofautiana kulingana
na visababishi vyake, anasema Dk Mwakigonja. Katika
utafiti wake Dk Mwakigonja alibaini kuwa wanawake wengi
walikuwa na saratani ya mdomo aina ya Kaposis Sarcoma
kuliko wanaume.
Hata hivyo, utafiti huo ulionyesha kuwa asilimia 50 ya
wanaume walikuwa na saratani ya mdomo hatari zaidi
(systemic) kuliko wanawake ambao ni asilimia 37.
Mapenzi kwa mdomo husababisha maradhi
Dk Mwakigonja anasema kuwa mapenzi yoyote kwa njia
ya mdomo lazima yasababishe maradhi ya zinaa iwapo
mmoja ameambukizwa. Pia anasema kwamba sampuli nyingi
za wanaume wanaojihusisha na mapenzi na wanaume
wenzao (mashoga) zilibainika na saratani ya mdomo. Utafiti
huo ni sehemu ya utafiti wa Shahada ya Uzamivu ambao
ulionyesha kuwa wagonjwa wengi wa saratani ya mdomo
walikuwa ni wanaume wenye umri wa miaka kati ya 38 na
kuendelea na wanawake ni 31.
Ufatiti wa WHO Tanzania
Shirika la Afya Duniani (WHO) pia lilifanya utafiti mwaka
2010 nchini kwa kushirikiana na Kituo cha Taarifa za HPV,
ambapo ilibainika kuwa asilimia 20 ya saratani za koo na
mdomo nchini zinasababishwa na ufanyaji wa mapenzi kwa
njia ya mdomo.
Taarifa hizo za WHO zinaeleza kuwa wanaume 747
hugundulika na saratani ya mdomo kila mwaka wakati
wanawake 472 hubainika na saratani hiyo pia. Wakati
huohuo, wanaume wanaopoteza maisha kutokana na saratani
hiyo ni 444, kwa mwaka na wanawake ni 270, kwa mwaka.
Utafiti wa WHO umebaini kuwa saratani ya mdomo inashika
nafasi ya sita katika aina 24 za saratani 24 zinazoisumbua
zaidi Tanzania.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa wanaume wanaoathirika zaidi
ni wenye umri wa kati ya miaka 15 na 55, ambao tayari
wameshaanza kujihusisha na ngono. Kama maradhi mengine
ya kuambukiza, Virusi vya HPV huambukizwa kwa urahisi
zaidi kutoka kwa wanawake kwenda kwa wanaume kuliko
kutoka kwa wanaume kwenda kwa wanawake. Utafiti huo
uliodhaminiwa na mfuko wa Bill na Melinda Gates na Kituo
cha Saratani na Mpango wa Utafiti wa Taasisi ya ICO
unaeleza kuwa mitandao ya kijamii na picha za ngono ndiyo
chanzo cha watu wengi kuiga ufanyaji wa mapenzi ya aina
hiyo.
Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, tafiti
zimefanyika na kubaini kuwa asilimia 70 ya wagonjwa
wanaobainika na saratani ya koo na mdomo duniani,
husababishwa na Virusi vya Human Pappiloma
vinavyotokana na magonjwa ya zinaa.Tafiti hizo zinaonyesha
kuwa wagonjwa wengi wanaogundulika na saratani hiyo ni
wanaume wenye umri wa kati, wenye uwezo wa kifedha,
wasiovuta sigara wala siyo walevi waliokubuhu.
Utafiti huo ulibaini kuwa wanaume wapo hatarini zaidi
kupata saratani ya koo inayosababishwa na Virusi vya HPV.
Miaka ya 80, idadi ndogo ya watu waliougua saratani ya koo
walihusishwa na maambukizi ya Virusi vya HPV. Kihistoria,
watu waliobainika na ugonjwa huo, ni wenye umri wa miaka
70 kwenda juu ambao walikuwa ni wale walevi waliokubuhu
na wavuta sigara.
Ilielezwa kuwa Virusi vya HPV vipo kwa wingi kiasi
ambacho watu wazima wanaojihusisha na ngono ya aina
yeyote ile, huweza kupata maambukizi ya zinaa hata kama
siyo saratani. Hata hivyo ilibainishwa kuwa saratani
isababishwayo na virusi vya HPV ni rahisi kuitibu kuliko
saratani ya koo isababishwayo na tumbaku au pombe kali.
Virusi vya HPV ni nini?
Kwa jina la jumla, saratani ya koo au mdomo huitwa
saratani ya kichwa na shingo. (Neck and Head Cancer) HPV
ni miongoni mwa virusi hatari zaidi duniani
visababishwavyo na magonjwa ya zinaa na vinaweza
kuathiri sehemu mbalimbali za mwili. Zipo aina zaidi ya 120
za HPV, baadhi huweza kuzalisha usugu (warts) ambazo si
saratani katika sehemu za siri, mikononi na miguuni.
Maambukizi ya HPV hufanyika kwa urahisi, hata kwa
kugusana ngozi au majimaji, huku maambukizi mengine
yakisababishwa na ngono.
Virusi hatari na vinavyosababisha saratani ni HPV-16,
HPV-18, HPV-31 na HPV 45. Aina hii ya Virusi vya HPV
husababisha saratani ambapo uvimbe waweza kujitokeza
kwa ndani na unaweza usionekane ukilinganisha na vivimbe
vingine vya saratani. Wataalamu wanasema HPV-16 na
HPV-18 inahusishwa zaidi na saratani ya shingo ya kizazi na
endapo mapenzi kwa njia ya mdomo yatafanywa na mtu
mwenye uambukizo huu ni rahisi kuambukizwa.