Mwananchi communications kupitia gazeti la The Citizens wanavyoshindwa kusimamia maslahi ya nchi (national interests)

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Moja katika habari kubwa kwenye medani ya siasa za Kimataifa inayomhusisha Mtanzania ni habari ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson kuteuliwa kuwania Urais wa Umoja wa Mabunge ya Dunia (IPU) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2023.

Taarifa za kuteuliwa zilitangazwa Mei 11, 2023 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax baada ya kikao na mabalozi wa nchi mbalimbali kuhusu Tanzania kuwania nafasi hiyo.

Kama inavyofahamika kwa kuwania nafasi kubwa kama hii ni lazima apate baraka za Mheshimiwa Rais wa nchi na bila shaka kama ambavyo Rais Samia aliridhia Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Liberata Mulamula kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola ni wazi pia aliridhia ("endorsement") Spika Tulia kugombea nafasi ya hiyo ya Urais wa Mabunge ya Dunia (IPU).

Serikali imesimama na Dkt Tulia na kwa kupitia Wizara wa Mambo ya Nje, Waziri Dkt Tax amekutana na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini ili kuomba kuunga mkono jitihada za Dkt Tulia ambaye sasa anawakilisha Tanzania. Vyombo vya habari vimeandika habari hii yenye maslahi mapana kwa Taifa lakini Mwananchi Communications Ltd kupitia gazeti la The Citizen (nadhani wameandika kwa lugha ya Kiingereza kwa makusudi kabisa) wameamua kupingana na juhudi zote hizi na kupingana na maslahi ya Taifa.

Tunafahamu maamuzi ya juu kabisa ya Gazeti hili yanatoka makao makuu yaliyoko nchi jirani ambayo ni mpinzani mkubwa na mshindani wa nchi yetu katika kila suala hivyo pengine hiyo ndio sababu ya kuandika makala yenye kichwa
"WHY I THINK TULIA IS UNSUITABLE TO LEAD IPU". Yaani The Citizen wanaamua kwa makusudi kuchafua taswira ya Mtanzania anayewania nafasi kimataifa tena wakichapisha katika lugha ambayo ni rahisi kueleweka na wapinzania wa DKt Tulia, HII SIO SAWA NA NI JAMBO LA KUKEMEWA NA WOTE WANAOWEKA MASLAHI YA TAIFA MBELE

Tunapaswa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari lakini pia tunapaswa kusema na kukemea pale ambapo vyombo hivi vinashindwa kusimamia maslahi ya nchi na pengine vinatumika kubeba agenda za nchi nyingine bila kujua au kwa kujua.

Lakini hapa ndipo tulipo The Citizen wamewaomba wajumbe kutomuunga mkono Dkt Tulia na wameshauri wajumbe wamuunge mkono Spika wa Bunge la Afrika Kusini.

IMG_4632.jpg
 
Uzalendo maana yake sio kukubali tu kila jambo hata kama lina mapungufu, hao The Citizens wametumia uhuru wao wa kutoa maoni kusema walichosema.

Ningekuona wa maana kama ungeonesha mapungufu ya hoja zao walizotoa kumkataa Dr. Tulia, lakini kuwapinga tu kisa wanafanyia shughuli zao Tanzania, na Dr. Tulia ni Spika wa Bunge la Tanzania sio sahihi.

Binafsi hata mimi kama ningepewa nafasi ya kupiga kura yangu huko IPU, nisingemchagua Dr. Tulia, kwasababu ameshindwa kuli handle bunge, anachojua yeye ni kulinda maslahi ya serikali bungeni, issue ya kina Mdee na uchambuzi wa ripoti ya CAG ni mifano michache.
 
Moja katika habari kubwa kwenye medani ya siasa za Kimataifa inayomhusisha Mtanzania ni habari ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson kuteuliwa kuwania Urais wa Umoja wa Mabunge ya Dunia (IPU) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2023.

Taarifa za kuteuliwa zilitangazwa Mei 11, 2023 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax baada ya kikao na mabalozi wa nchi mbalimbali kuhusu Tanzania kuwania nafasi hiyo.

Kama inavyofahamika kwa kuwania nafasi kubwa kama hii ni lazima apate baraka za Mheshimiwa Rais wa nchi na bila shaka kama ambavyo Rais Samia aliridhia Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Liberata Mulamula kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola ni wazi pia aliridhia ("endorsement") Spika Tulia kugombea nafasi ya hiyo ya Urais wa Mabunge ya Dunia (IPU).

Serikali imesimama na Dkt Tulia na kwa kupitia Wizara wa Mambo ya Nje, Waziri Dkt Tax amekutana na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini ili kuomba kuunga mkono jitihada za Dkt Tulia ambaye sasa anawakilisha Tanzania. Vyombo vya habari vimeandika habari hii yenye maslahi mapana kwa Taifa lakini Mwananchi Communications Ltd kupitia gazeti la The Citizen (nadhani wameandika kwa lugha ya Kiingereza kwa makusudi kabisa) wameamua kupingana na juhudi zote hizi na kupingana na maslahi ya Taifa.

Tunafahamu maamuzi ya juu kabisa ya Gazeti hili yanatoka makao makuu yaliyoko nchi jirani ambayo ni mpinzani mkubwa na mshindani wa nchi yetu katika kila suala hivyo pengine hiyo ndio sababu ya kuandika makala yenye kichwa
"WHY I THINK TULIA IS UNSUITABLE TO LEAD IPU". Yaani The Citizen wanaamua kwa makusudi kuchafua taswira ya Mtanzania anayewania nafasi kimataifa tena wakichapisha katika lugha ambayo ni rahisi kueleweka na wapinzania wa DKt Tulia, HII SIO SAWA NA NI JAMBO LA KUKEMEWA NA WOTE WANAOWEKA MASLAHI YA TAIFA MBELE

Tunapaswa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari lakini pia tunapaswa kusema na kukemea pale ambapo vyombo hivi vinashindwa kusimamia maslahi ya nchi na pengine vinatumika kubeba agenda za nchi nyingine bila kujua au kwa kujua.

Lakini hapa ndipo tulipo The Citizen wamewaomba wajumbe kutomuunga mkono Dkt Tulia na wameshauri wajumbe wamuunge mkono Spika wa Bunge la Afrika Kusini.

View attachment 2635373
Uteuzi wake una impact gan kwa maisha ya Bibi na babu zetu kule kijijini?
 
Moja katika habari kubwa kwenye medani ya siasa za Kimataifa inayomhusisha Mtanzania ni habari ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson kuteuliwa kuwania Urais wa Umoja wa Mabunge ya Dunia (IPU) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2023.

Taarifa za kuteuliwa zilitangazwa Mei 11, 2023 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax baada ya kikao na mabalozi wa nchi mbalimbali kuhusu Tanzania kuwania nafasi hiyo.

Kama inavyofahamika kwa kuwania nafasi kubwa kama hii ni lazima apate baraka za Mheshimiwa Rais wa nchi na bila shaka kama ambavyo Rais Samia aliridhia Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Liberata Mulamula kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola ni wazi pia aliridhia ("endorsement") Spika Tulia kugombea nafasi ya hiyo ya Urais wa Mabunge ya Dunia (IPU).

Serikali imesimama na Dkt Tulia na kwa kupitia Wizara wa Mambo ya Nje, Waziri Dkt Tax amekutana na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini ili kuomba kuunga mkono jitihada za Dkt Tulia ambaye sasa anawakilisha Tanzania. Vyombo vya habari vimeandika habari hii yenye maslahi mapana kwa Taifa lakini Mwananchi Communications Ltd kupitia gazeti la The Citizen (nadhani wameandika kwa lugha ya Kiingereza kwa makusudi kabisa) wameamua kupingana na juhudi zote hizi na kupingana na maslahi ya Taifa.

Tunafahamu maamuzi ya juu kabisa ya Gazeti hili yanatoka makao makuu yaliyoko nchi jirani ambayo ni mpinzani mkubwa na mshindani wa nchi yetu katika kila suala hivyo pengine hiyo ndio sababu ya kuandika makala yenye kichwa
"WHY I THINK TULIA IS UNSUITABLE TO LEAD IPU". Yaani The Citizen wanaamua kwa makusudi kuchafua taswira ya Mtanzania anayewania nafasi kimataifa tena wakichapisha katika lugha ambayo ni rahisi kueleweka na wapinzania wa DKt Tulia, HII SIO SAWA NA NI JAMBO LA KUKEMEWA NA WOTE WANAOWEKA MASLAHI YA TAIFA MBELE

Tunapaswa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari lakini pia tunapaswa kusema na kukemea pale ambapo vyombo hivi vinashindwa kusimamia maslahi ya nchi na pengine vinatumika kubeba agenda za nchi nyingine bila kujua au kwa kujua.

Lakini hapa ndipo tulipo The Citizen wamewaomba wajumbe kutomuunga mkono Dkt Tulia na wameshauri wajumbe wamuunge mkono Spika wa Bunge la Afrika Kusini.

View attachment 2635373
We ni mjinga sana bro,kama unaamini Mmoja wa wezi wa ccm akiteuliwa kushika cheo kwenye taasisi ya kimataifa,Kuna leta tija kwa kwa nchi,na wananchi,utakuwa upo kwenye usingizi wa pono,
Hizi ni akili za hovyo sana,kule Kenya,Fisadi Mkikuyu au mruo,akishitakiwa,anaenda kwenye kqbila lake,anasema wananionea,na wananchi wa kabila lake walivyo mazuzu,watamtetea,sawa ni mwizi,Fisadi kaiba Mali ya umma,lakini ni mwizi wa kqbila letu!
False sense of comfort and satisfaction.
Wewe ni mkaguru,mkaguru akiwa makamu wa Raisi,unajisikia vzr,Richa ya kwamba hakuna unachofaidika kutoka kwake!!,ni kwa vile ni kabila lako tu
 
We ni mjinga sana bro,kama unaamini Mmoja wa wezi wa ccm akiteuliwa kushika cheo kwenye taasisi ya kimataifa,Kuna leta tija kwa kwa nchi,na wananchi,utakuwa upo kwenye usingizi wa pono,
Hizi ni akili za hovyo sana,kule Kenya,Fisadi Mkikuyu au mruo,akishitakiwa,anaenda kwenye kqbila lake,anasema wananionea,na wananchi wa kabila lake walivyo mazuzu,watamtetea,sawa ni mwizi,Fisadi kaiba Mali ya umma,lakini ni mwizi wa kqbila letu!
False sense of comfort and satisfaction.
Wewe ni mkaguru,mkaguru akiwa makamu wa Raisi,unajisikia vzr,Richa ya kwamba hakuna unachofaidika kutoka kwake!!,ni kwa vile ni kabila lako tu
Wewe ni mjinga zaidi kama unaangalia suala hili kwa lens ya CCM,
Una uwezo finyu wa kufikiri kuliko wa mende.
Kama hutambui faida za Stergomena Tax alipokuwa Boss pale SADC
Kama hutambui faida za Asharose Migiro alipokuwa Naibu Katibu Mkuu pale UN

WEWE NI PUNGUANI KAA KIMYA, PUNGUANI
 
Uzalendo maana yake sio kukubali tu kila jambo hata kama lina mapungufu, hao The Citizens wametumia uhuru wao wa kutoa maoni kusema walichosema.

Ningekuona wa maana kama ungeonesha mapungufu ya hoja zao walizotoa kumkataa Dr. Tulia, lakini kuwapinga tu kisa wanafanyia shughuli zao Tanzania, na Dr. Tulia ni Spika wa Bunge la Tanzania sio sahihi.

Binafsi hata mimi kama ningepewa nafasi ya kupiga kura yangu huko IPU, nisingemchagua Dr. Tulia, kwasababu ameshindwa kuli handle bunge, anachojua yeye ni kulinda maslahi ya serikali bungeni, issue ya kina Mdee na uchambuzi wa ripoti ya CAG ni mifano michache.
Huwezi kupewa nafasi wewe endelea kupigana vita vyako nyuma ya Keyboard
 
Tena ashukuru hakuna kura za wazi kutoka kwa wananchi kwenye nchi husika. Maana kungekuwa na kura za wazi, huyo Tulia angepata kura chache mno kutoka Tanzania. Yeye aende na vyombo vya dola vikampe kura, maana hana uwezo wa kushinda kwa ushawishi wa hoja. Isitoshe hakuna maslahi yoyote kwetu wananchi hata akipata hiyo nafasi.
 
Wewe ni mjinga zaidi kama unaangalia suala hili kwa lens ya CCM,
Una uwezo finyu wa kufikiri kuliko wa mende.
Kama hutambui faida za Stergomena Tax alipokuwa Boss pale SADC
Kama hutambui faida za Asharose Migiro alipokuwa Naibu Katibu Mkuu pale UN

WEWE NI PUNGUANI KAA KIMYA, PUNGUANI
Makasiriko 🙄 😅🙏🙏
 
Wewe ni mjinga zaidi kama unaangalia suala hili kwa lens ya CCM,
Una uwezo finyu wa kufikiri kuliko wa mende.
Kama hutambui faida za Stergomena Tax alipokuwa Boss pale SADC
Kama hutambui faida za Asharose Migiro alipokuwa Naibu Katibu Mkuu pale UN

WEWE NI PUNGUANI KAA KIMYA, PUNGUANI
Kulikuwa na faida gani kwetu wananchi? Hizo ni sifa zao binafsi, labda sana sana kwa tabaka la watawala. Usitake kulazimisha tuone kuna lolote la maana kwa hizo taasisi ceremonial.
 
The Citizen wanatumika. Tulia ni spika bora kuwahi kutokea bongo na anafaa kuwa Spika IPU.
 
Tena ashukuru hakuna kura za wazi kutoka kwa wananchi kwenye nchi husika. Maana kungekuwa na kura za wazi, huyo Tulia angepata kura chache mno kutoka Tanzania. Yeye aende na vyombo vya dola vikampe kura, maana hana uwezo wa kushinda kwa ushawishi wa hoja. Isitoshe hakuna maslahi yoyote kwetu wananchi hata akipata hiyo nafasi.

Na hapo ndo mnapozidiwa na nchi zote mnazozisifia kila siku. Mitanganyika mna safari ndefu sana.
 
Na hapo ndo mnapozidiwa na nchi zote mnazozisifia kila siku. Mitanganyika mna safari ndefu sana.
Kwani ni kipi tunawazidi ambacho ww unadhani tunawazidi? Yaani tumuunge mkono mtu ambaye tunajua kabisa yuko kwenye nafasi aliyopo kwa siasa chafu, ili tuwazidi nchi nyingine?
 
Moja katika habari kubwa kwenye medani ya siasa za Kimataifa inayomhusisha Mtanzania ni habari ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson kuteuliwa kuwania Urais wa Umoja wa Mabunge ya Dunia (IPU) katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2023.

Taarifa za kuteuliwa zilitangazwa Mei 11, 2023 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax baada ya kikao na mabalozi wa nchi mbalimbali kuhusu Tanzania kuwania nafasi hiyo.

Kama inavyofahamika kwa kuwania nafasi kubwa kama hii ni lazima apate baraka za Mheshimiwa Rais wa nchi na bila shaka kama ambavyo Rais Samia aliridhia Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje Liberata Mulamula kugombea nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola ni wazi pia aliridhia ("endorsement") Spika Tulia kugombea nafasi ya hiyo ya Urais wa Mabunge ya Dunia (IPU).

Serikali imesimama na Dkt Tulia na kwa kupitia Wizara wa Mambo ya Nje, Waziri Dkt Tax amekutana na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini ili kuomba kuunga mkono jitihada za Dkt Tulia ambaye sasa anawakilisha Tanzania. Vyombo vya habari vimeandika habari hii yenye maslahi mapana kwa Taifa lakini Mwananchi Communications Ltd kupitia gazeti la The Citizen (nadhani wameandika kwa lugha ya Kiingereza kwa makusudi kabisa) wameamua kupingana na juhudi zote hizi na kupingana na maslahi ya Taifa.

Tunafahamu maamuzi ya juu kabisa ya Gazeti hili yanatoka makao makuu yaliyoko nchi jirani ambayo ni mpinzani mkubwa na mshindani wa nchi yetu katika kila suala hivyo pengine hiyo ndio sababu ya kuandika makala yenye kichwa
"WHY I THINK TULIA IS UNSUITABLE TO LEAD IPU". Yaani The Citizen wanaamua kwa makusudi kuchafua taswira ya Mtanzania anayewania nafasi kimataifa tena wakichapisha katika lugha ambayo ni rahisi kueleweka na wapinzania wa DKt Tulia, HII SIO SAWA NA NI JAMBO LA KUKEMEWA NA WOTE WANAOWEKA MASLAHI YA TAIFA MBELE

Tunapaswa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari lakini pia tunapaswa kusema na kukemea pale ambapo vyombo hivi vinashindwa kusimamia maslahi ya nchi na pengine vinatumika kubeba agenda za nchi nyingine bila kujua au kwa kujua.

Lakini hapa ndipo tulipo The Citizen wamewaomba wajumbe kutomuunga mkono Dkt Tulia na wameshauri wajumbe wamuunge mkono Spika wa Bunge la Afrika Kusini.

View attachment 2635373
Achaguliwe mwingine,over
 
Tena ashukuru hakuna kura za wazi kutoka kwa wananchi kwenye nchi husika. Maana kungekuwa na kura za wazi, huyo Tulia angepata kura chache mno kutoka Tanzania. Yeye aende na vyombo vya dola vikampe kura, maana hana uwezo wa kushinda kwa ushawishi wa hoja. Isitoshe hakuna maslahi yoyote kwetu wananchi hata akipata hiyo nafasi.
Naunga mkono hoja. Hivi hizo nchi zingine wangetambua kuwa hata hili bunge la nyumbani kwao limemshinda wangetupia kapuni tuu.
 
Kwani ni kipi tunawazidi ambacho ww unadhani tunawazidi? Yaani tumuunge mkono mtu ambaye tunajua kabisa yuko kwenye nafasi aliyopo kwa siasa chafu, ili tuwazidi nchi nyingine?

Na hapo ndo mnapozidiwa kudhani mmezidiwa na kukubali kuzidiwa. Mitanganyika mna safari ndefu. Wakenya na ukabila wao can't spit such nonsense.
 
Naunga mkono hoja. Hivi hizo nchi zingine wangetambua kuwa hata hili bunge la nyumbani kwao limemshinda wangetupia kapuni tuu.
Kabisa mkuu, halafu watu wanataka tujivike uzalendo wa kinafiki kwa mtu tunayejua kabisa sio. Hatuna muda wa kuunga mkono wazandiki. Huwa nawashangaa hawa watu wenye sifa mbovu hivi za uongozi ni kigezo gani huwa kinatumika kuwapata?
 
Na hapo ndo mnapozidiwa kudhani mmezidiwa na kukubali kuzidiwa. Mitanganyika mna safari ndefu. Wakenya na ukabila wao can't spit such nonsense.
Katika watu hawaendekezi unafiki ni hao Wakenya.
 
Back
Top Bottom