Mwananchi: Agizo la Makalla stendi ya Magufuli Lazua mjadala

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,735
6,281
Dar es Salaam. Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kuagiza wenye mabasi kuyaingiza ndani ya kituo cha mabasi cha Magufuli wakati wa kupakia na kushusha abiria, baadhi ya wananchi wamekuwa na maoni tofauti kuhusiana na uamuzi huo.

Makalla alitoa agizo hilo jana Ijumaa Julai 9,2021 wakati akisikiliza kero za wafanyabiashara katika stendi hiyo, ambao walisema miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo ni pamoja na kukosa wateja kwa kuwa baadhi ya mabasi hupakia na kushusha abiria maeneo mengine.

Hata hivyo, mchambuzi wa masuala ya siasa, Richard Mabala kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika: Sijui kwanini watu wa mipango wanapenda kuangalia urahisi kwao badala ya kuangalia urahisi kwa ajili ya wateja, wamejenga barabara nzuri hadi Ubungo kwanini mabasi yasiwafikishe abiria karibu zaidi na nyumbani”.

Naye Hajia Soza katika ukurasa wake wa Instagram ameandika: Sahihi sana mkuu Amos Makala, na Dodoma tusione aibu kulisimamia hili kwani mabasi mengi yatokayo safari siku hizi huingia stendi kuu Dodoma wanapojisikia, sasa hizi stendi zilijengwa za nini? Halafu uongozi unalichukuliaje suala hili?”

Kwa upande wake Tanzania Bound Buses Flag of Tanzania wameandika: “Fikiria gari limetoka Mwanza limefika stendi ya Magufuli saa 7 usiku, na wewe kama abiria unaishi Ilala, unalazimishwa ushuke hapo hapo stendi wakati basi linaelekea kupaki maeneo ya Shekilango”.

Hata hivyo, akizungumza na Mwananchi, Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), Joseph Priscus amesema watatekeleza agizo hilo lakini, changamoto iliyopo ni baadhi ya stendi kuwa mbali na makazi ya watu.

Amesema kumekuwa na kilio cha muda mrefu kutokana na stendi nyingine kuhamishiwa nje ya mji, na kusababisha usumbufu kwa abiria ikiwemo kuwagharimu fedha nyingi kwa ajili kupanda bajaji au bodaboda.

Awali, kituo cha mabasi Ubungo kilihamishiwa hadi eneo la Mbezi ambako ndio kumejengwa stendi mpya ya Magufuli ikiwa ni umbali wa kilomita 11.7 (Ubungo-Mbezi) huku kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam kwenda Mbezi ni umbali wa kilomita 20.

Tangu kuzinduliwa na kuanza kazi kwa stendi ya Magufuli ambayo inatajwa kuwa na ubora nay a kisasa kwa nchi za Afrika Mashariki, baadhi ya wamiliki na abiria wamekuwa wakilalamikia umbali hasa kwa safari za masafa ya mbali ambazo nyingi huanza saa 12:00 alfajiri.

Mwananchi Gazeti.
 
Hata hayo mabasi yanafanya biashara ndio maana urafiki pamekuwa kama stand kwa sababu ya urahisi wa abiria kufika. Mimi nashauri hiyo stand ya Magufuli ivunjwe 🍻🍻🍻
 
Yafaa watambue anayekaa mkuranga leo hii anaweza kuhitaji kwenda Arusha au moshi na sii tu Kwenda ntwara,kama shida ni kuingia kituoni ili kukusanya kodi Bila kuangalia hao watoa kodi,yote hayo ni juu, mteja anatafutwa na atakuwa mteja kwa huduma bora atakayopatiwa,kama magari yote yanaweza kuwachukua wateja kutoka maeneo ya manyumbani kwao,halafu wakaja kulipa ushuru hapo kwenye kituo kikuu,ni vyema.
 
Mkuu suala hili ni jepesi sana, ni sisi wenyewe ndio tunazalisha tatizo na usumbufu usiokuwa wa lazima kwa wananchi. Mabasi yanaanza safari zake 12 asubuhi kila stand nchi mzima, mfano; Mbezi stand kwa magari yaendayo Arusha, Tanga, Dodoma, Singida, Babati, Iringa ect hulazimika kuondoka muda huo, mwendo wa mabasi, hayatakiwi kuzidi 80km/h.

Barabara zetu zina miji midogo na vijiji karibu karibu sana ambavyo kisheria vinamtaka dereva apunguze mwendo hadi 30km/h; wakati barabara yenyewe ni highway, hivyo inapelekea mabasi kupoteza muda mwingi barabara kwa kutii sheria hizi. Aidha askari wa barabara nao ni chanzo cha upotevu wa muda wa mabasi barabarani.

Kwa jinsi ambavyo miji midogo na vijiji inavyoota/kujengwa kandokando ya barabara na tukaendelea kukumbatia sheria hizi za 30km/h, ni dhahiri mabasi yataendelea kupoteza muda mwingi barabara. Huko mbeleni safari ya Dar - Arusha itachukua masaa zaidi ya 12 badala ya masaa7, Mwanza inaweza kuwa masaa 24.

Kama tunamtazamo wa treni ya mwendo kasi 120km/ kwa nini tunafunga mabasi yetu speed gavana? Kituo kama cha Mbezi kwa nini kisiwe na hoteli yake yenye bei rafiki kwa ajiri ya abiria/wasafiri, ambao wanaotarajia kusafiri siku inayofuata saa 12 asubuhi na wale ambao mabasi yao yamefika usiku sana kutoka mikoani, tiketi za kusafiria ndizo zitumike kupata huduma hiyo ya malazi. Leo wengi wa wanao lala pale ni vibaka. EBU TUJARIBU YOTE HAYA TUONE.
 
Hata hayo mabasi yanafanya biashara ndio maana urafiki pamekuwa kama stand kwa sababu ya urahisi wa abiria kufika. Mimi nashauri hiyo stand ya Magufuli ivunjwe
Wewe! Ivunjwe Tena? Si Magufuli atagarauka kaburini?!
 
Hakika ni kusumbuana...

Ila kwa upande mwingine mbona kuifuata Airport hatulalamiki kwamba ipo mbali...
 
Hakika ni kusumbuana...

Ila kwa upande mwingine mbona kuifuata Airport hatulalamiki kwamba ipo mbali...
Mkuu, hakika wakati mwingine ni kusumbuana. Ila kwa upande mwingine abiria wa airport na abiria wa bus stand wanatofautiana kwenye UKWASI, ndio maana airport hakunaga WAMACHINGA wakati bus stand wamejaa tele hadi vibaka
 
Nimeamini Viongozi wakiwa ndani ya Ma V8 tena tinted hawana huruma kwa Wananchi kabisa..
 
Hakika ni kusumbuana...

Ila kwa upande mwingine mbona kuifuata Airport hatulalamiki kwamba ipo mbali...
Mtu anaepanda ndege anajimudu,kama nauli Ni kuanzia laki kulanda juu sidhani km atashindwa elfu 10 ya kulipia Uber au bodaboda

Nadhani ndugu Amos alitakiwa alazimishe Gari ziingie ila zisilazimishwe kushusha stendi

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
Mtu anaepanda ndege anajimudu,kama nauli Ni kuanzia laki kulanda juu sidhani km atashindwa elfu 10 ya kulipia Uber au bodaboda

Nadhani ndugu Amos alitakiwa alazimishe Gari ziingie ila zisilazimishwe kushusha stendi

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
Wanyonge wanazidi kudidimizwa kimtindo, wanapokonywa hata kile kidogo walichookoa safarini
 
Hakika ni kusumbuana...

Ila kwa upande mwingine mbona kuifuata Airport hatulalamiki kwamba ipo mbali...
Mtu anaepanda ndege anajimudu,kama nauli Ni kuanzia laki kulanda juu sidhani km atashindwa elfu 10 ya kulipia Uber au bodaboda

Nadhani ndugu Amos alitakiwa alazimishe Gari ziingie ila zisilazimishwe kushusha stendi

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
Mkuu Makala ana mawakala humu wala usiumize kichwa
 
Mkuu suala hili ni jepesi sana, ni sisi wenyewe ndio tunazalisha tatizo na usumbufu usiokuwa wa lazima kwa wananchi. Mabasi yanaanza safari zake 12 asubuhi kila stand nchi mzima, mfano; Mbezi stand kwa magari yaendayo Arusha, Tanga, Dodoma, Singida, Babati, Iringa ect hulazimika kuondoka muda huo, mwendo wa mabasi, hayatakiwi kuzidi 80km/h.

Barabara zetu zina miji midogo na vijiji karibu karibu sana ambavyo kisheria vinamtaka dereva apunguze mwendo hadi 30km/h; wakati barabara yenyewe ni highway, hivyo inapelekea mabasi kupoteza muda mwingi barabara kwa kutii sheria hizi. Aidha askari wa barabara nao ni chanzo cha upotevu wa muda wa mabasi barabarani.

Kwa jinsi ambavyo miji midogo na vijiji inavyoota/kujengwa kandokando ya barabara na tukaendelea kukumbatia sheria hizi za 30km/h, ni dhahiri mabasi yataendelea kupoteza muda mwingi barabara. Huko mbeleni safari ya Dar - Arusha itachukua masaa zaidi ya 12 badala ya masaa7, Mwanza inaweza kuwa masaa 24.

Kama tunamtazamo wa treni ya mwendo kasi 120km/ kwa nini tunafunga mabasi yetu speed gavana? Kituo kama cha Mbezi kwa nini kisiwe na hoteli yake yenye bei rafiki kwa ajiri ya abiria/wasafiri, ambao wanaotarajia kusafiri siku inayofuata saa 12 asubuhi na wale ambao mabasi yao yamefika usiku sana kutoka mikoani, tiketi za kusafiria ndizo zitumike kupata huduma hiyo ya malazi. Leo wengi wa wanao lala pale ni vibaka. EBU TUJARIBU YOTE HAYA TUONE.
Suala la speed sio la ku compromise kabisa tuamgaie hizo changamoto nyengine kama za usumbufu wa askari wa barabarani.

La pili juu ya ushauri wako wa kuwa kuwe na guests houses za bei rafiki, pia kuwe na usafiri wa mwendo kasi ( transfer shuttle style) kwa masaa 24 Mbezi-Ubungo kwa ajili ya kubebea abiria.
 
Mwaka miaka ya 90's mwishoni wakati kituo cha mabasi kinahama kutoka Kisutu kuja Ubungo. Kulikuwa na makelele kuzidi haya. Maana upinzani ulikuwa mkubwa sana mwanzoni, lkn baadaye tukazoea na mambo yakaenda shwaari. Hapa ni suala la muda tu. Baada ya hapo wadau wote watakubaliana na hali.
 
Suala la speed sio la ku compromise kabisa tuamgaie hizo changamoto nyengine kama za usumbufu wa askari wa barabarani.

La pili juu ya ushauri wako wa kuwa kuwe na guests houses za bei rafiki, pia kuwe na usafiri wa mwendo kasi ( transfer shuttle style) kwa masaa 24 Mbezi-Ubungo kwa ajili ya kubebea abiria.
Mkuu kuhusu angalizo la kuwa na transfer shuttle kwa masaa 24 Mbezi - Ubungo halitaweza kukidhi mahitaji kwa abiria wote. Kituo cha mabasi Mbezi (Magufuli) na kituo cha daladala Mbezi ambacho kwa sasa kinahudumia madaladala kutoka sehemu zote za Jiji ndicho ninacho kizungumzia.
 
Back
Top Bottom