Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,806
- 15,379
Kwa wanawake kupenda kunawachanganganya sana, tofauti na wanaume. kwa mwanamke kupenda kunahusisha mambo mengi na kila mmoja anazo sifa zake anazozipa kipaumnbele ingawa hazitofautiani sana.
Kuna wakati mwanamke anaweza kumpata mwanaume mwenye sifa muafaka, wenyewe wanaita husband material. Mwanaume mwenye muonekano mzuri yaani handsome, mtanashati, msikivu, mwenye kujitoa pale mpenzi wake anapomuhitaji, asiye na makuu, mwenye kupenda familia hususan watoto na mcha Mungu. Huyu kwa wanawake wengi ndiye mwanaume wa ndoto zao.
Lakini baada ya muda mrefu wa kufahamiana na mwanamke anapoamua kujinasibu na kuukabidhi moyo wake kwa huyu mpenzi wake mpya kwa kuugawa utukufu wake kunako 6x6 anajikuta hafikishwi popote halafu mwanaume anageukia ukutani na kukoroma na yeye akibaki kukodolea macho dari akiwa na msongo wa mawazo.
Hata baada ya kujaribu tena na tena mpaka kujitahidi kutoa msaada wakiwa ndani ya uwanja wa 6x6 lakini mambo hayaelekei kuwa kama alivyotarajia. kwa kifupi ni kwamba mwanaume huyu hawezi utundu wakitandani zaidi ya yeye kujiridhisha peke yake, lakini pia hatoi ushirikiano kama inavyotakiwa, na jogoo wake hawiki ipasavyo.
Ikumbukwe kwamba kila mwanamke anapopata mpenzi mpya kabla ya tendo anakuwa na ndoto nyingi jinsi siku hiyo ya kukutana kimwili itakavyokuwa. Mwanamke atajitahidi kujenga picha nzuri nzuri jinsi busu lake la kwanza litakavyokuwa, jinsi atakavyofikishwa kileleni na mpenzi wake mpya, ilimradi atakuwa na ndoto tamu tamu zisizoisha hamu. Sasa mambo yatakapokuwa tofauti na matarajio yake, lazima atapata msongo wa mawazo.
Inakuwaje mambo haya..........!
Lakini yupo mpenzi wa zamani, huyu hana sifa za kuitwa husband material, ni mwanaume mnyanyasaji na mkatili kwa wanawake. Ni mwanaume mbinafsi na asiyejua majukumu yake kama mwanaume zaidi ya ubinafsi na ulevi kupindukia, ila kunako uwanja wa 6x6 ni hodari kweli kweli, anayajua mambo ya kitandani usipime. Ni mwanaume ambaye ukiwa naye kitandani unahisi kama uko peponi kwa jinsi anavyoyajua mambo.
Hapo ndipo mwanamke anapobaki njia panda ampende yupi?
Wapo baadhi ya wanawake hufanya maamuzi magumu, kukubali kuolewa na mwanaume mwenye muafaka lakini linapokuja swala la kutimiziwa yale ya kitandani analazimika kutoka nje ya ndoa kwa kwenda kwa mpenzi wa zamani ambaye anayajua ya kitandani.
Uamuzi huo ni wa hatari sana na hauwezi kuwa na mwisho mwema kwani mwisho wa siku ndoa hiyo inaweza kuingia katika vurugu na hata kuvunjika na watoto wakabaki wakipata shida.
Je mwanamke, iwapo utakutana na mtihani kama huu, utachukua hatua gani?