Mwanamke ukimfanyia hili anakuwa na furaha sana, hatakuja kugombana na wewe

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Sep 22, 2016
4,580
7,938
Waungwana natumaini kuwa mu wazima!

Twende kwenye mada, familia nyingi Afrika ziko kwenye mgogoro au kamgogoro, na migogoro hii husababishwa hasa na mambo ya fedha au mapenzi nje ya mahusiano(cheating).

Sasa hapa ninatoa tiba ya mgogoro unaosababishwa na mambo ya kifedha.

Kulingana na kipato chako ewe mwanaume unaweza kuitafuta fedha ambayo kwa level yenu ya maisha itaonekana ni kubwa. Ichukue mpe mkewe atunze, mwambie itunze ninà kazi nayo.

Ukimpa kama milioni 5, 4,3 au hata laki tano akutunzie moyo wake unakuwa mweupe.

Hii style ina faida zake, ikumbukwe wanawake wana forecast nzuri ya kuona jambo zuri ambalo akikushauri ufanye utapata faida kubwa.

Usiwe dictator kwenye masuala ya fedha, kuwa muwazi ingawa usiwe muwazi kupitiliza.
 
Aiseee ahsante sana mdau, sijawahi fikiria hivyo. Huwa naficha asijue nina balance kiasi gani bank. Umenipa wazo zuri sana ngoja nilifanyie kazi..


Kwa moyo mweupe nasema Mungu akubariki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na sasa ukute ni mwanamke anaependa maendeleo utafurahia nakuambia unampa tu, utaona yani dunia yote ni yako yani utaona you are the luckiest dude in the planet , alichosema mdau i rate 100%,
 
Back
Top Bottom