Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,393
Wengi wetu tumekulia kwenye mazingira ambapo mijisifu na majidai yetu tukiwa vijana na balehe ikiwa imeshika kasi, sifa mojawapo ya kuonesha ushababi wetu ilikuwa ni jinsi tulivyoweza kumshikisha adabu mtoto wa kike. Tumekulia kwenye mazingira ambayo mwanamke hapaswi kujibu wakati mwanaume anaongea. Na pia tumekulia kwenye mazingira ambapo kusikia mwanamke kapigwa au kubakwa kwa staili ya "niangusage" au "chagulaga" ni jambo la kawaida na pengine sifa kwa aliyemfanyia hivyo mwanamke huyo.
Kwa bahati mbaya kuna wale ambao wamelelewa na kukulia kwenye maeneo ambapo tangu kale mwanamke ni kama bidhaa, akishalipiwa ng'ombe kadhaa anakuwa amenunuliwa. Huko mwanamke hatakiwi kumjibu mume, hatakiwi kujitetea kwa lolote. Kwa bahati mbaya na mwanamke naye amelelewa na kukulia kwenye mazingira yenye kumwambia kwamba, hatakiwi kumjibu mume na pengine kupigwa ni dalili ya upendo.
Uwezekano ni mkubwa sana kwamba, kuna watu wa idadi ya kutosha hapa nchini ambao wanaamini kwamba mke ni lazima apigwe kila anapokosea. Watu hawa huwapiga kweli wake zao na pia wako tayari kuwapiga hata wasio wake zao, mradi ni wanawake. Vilevile ingawa siyo kwa idadi kubwa, wapo wanawake wanaoamini kwamba kupigwa na mume ni muhimu au lazima na siyo jambo la kuudhi sana.
Hawa walizoea kuwaona mama zao wakipigwa na baba zao na kusema, "hewala mume wangu," hivyo wakaamini kwamba, kupigwa ni sehemu muhimu katika kukamilisha ndoa bora na imara. Wengine walizoea kuwaona mama zao wakilalamika kila siku kwamba, ni afadhali kupigwa kuliko ghubu. Walipokuwa wakubwa wakaamini kwamba, kupigwa ni adhabu bora na nyepesi zaidi kutoka kwa mume.
Lakini ukweli utaendelea kubaki kwamba kama kuna wanaoamini kuwa mapenzi au uhusiano wao utanona kwa mwanamke kukubali kupigwa kila akikosa, mimi nadhani wanahitaji kutembea safari ndefu sana kabla hawajaufikia ustaarabu.
Na labda wengine wako humu humu JF.
Kwa bahati mbaya kuna wale ambao wamelelewa na kukulia kwenye maeneo ambapo tangu kale mwanamke ni kama bidhaa, akishalipiwa ng'ombe kadhaa anakuwa amenunuliwa. Huko mwanamke hatakiwi kumjibu mume, hatakiwi kujitetea kwa lolote. Kwa bahati mbaya na mwanamke naye amelelewa na kukulia kwenye mazingira yenye kumwambia kwamba, hatakiwi kumjibu mume na pengine kupigwa ni dalili ya upendo.
Uwezekano ni mkubwa sana kwamba, kuna watu wa idadi ya kutosha hapa nchini ambao wanaamini kwamba mke ni lazima apigwe kila anapokosea. Watu hawa huwapiga kweli wake zao na pia wako tayari kuwapiga hata wasio wake zao, mradi ni wanawake. Vilevile ingawa siyo kwa idadi kubwa, wapo wanawake wanaoamini kwamba kupigwa na mume ni muhimu au lazima na siyo jambo la kuudhi sana.
Hawa walizoea kuwaona mama zao wakipigwa na baba zao na kusema, "hewala mume wangu," hivyo wakaamini kwamba, kupigwa ni sehemu muhimu katika kukamilisha ndoa bora na imara. Wengine walizoea kuwaona mama zao wakilalamika kila siku kwamba, ni afadhali kupigwa kuliko ghubu. Walipokuwa wakubwa wakaamini kwamba, kupigwa ni adhabu bora na nyepesi zaidi kutoka kwa mume.
Lakini ukweli utaendelea kubaki kwamba kama kuna wanaoamini kuwa mapenzi au uhusiano wao utanona kwa mwanamke kukubali kupigwa kila akikosa, mimi nadhani wanahitaji kutembea safari ndefu sana kabla hawajaufikia ustaarabu.
Na labda wengine wako humu humu JF.