Mwanamke mwenye zaidi ya miaka 35

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Sep 29, 2012
3,401
1,604
Natafuta mwanamke mwenye miaka 35 na kuendelea kwaajili ya mawasiliano ya kirafiki na kubadilishana mawazo. Mi ni mwanafunzi wa chuo, nasoma mlimani nipo mwaka wa 3. Kutokana na ugumu wa ajira uliopo mbele yangu naamini kufahamiana na watu wengi kuna faida zake. Kwa aliye tayar tuwasiliane(PM) au tumia email yangu ambayo ni; tonyhaule@hotmail.com. Busara zitumike katika uchangiaji, asanteni sana.
 
Kwanini mwanamke tu??
Does it mean kuwa unatafuta mwanamke wa kukulea?
 
Mmh? Sikuelewi. Unatafuta maisha au mwanamke? Ebu soma kwanza hayo mengine utayakuta duniani.
 
Kwanini mwanamke tu??
Does it mean kuwa unatafuta mwanamke wa kukulea?

Binafsi naamini kuwa mwanamke ana huruma sana zaidi ya mwanaume hivyo mwanamke anauwezo wa kunisaidia kwa haraka tofauti na mwanaume mwenzangu. Mwanaume atasema "mwache akomae, Si wenyewe tulihangaika bwana". Kikubwa ni hicho rafiki sifikirii kulelewa kikubwa natengeza channel ya kufahamiana na watu wengi zaidi
 
Mmh? Sikuelewi. Unatafuta maisha au mwanamke? Ebu soma kwanza hayo mengine utayakuta duniani.

chuoni kwetu kuna wanawake wengi sana mkuu, njian ninapo pita kuna wanawakw wengi sana, supermarket pia, Kanisani, sokoni hata kwenye daladala so siwezi kutafuta wanawake kupitia internet maana hiyo nidalili ya uoga
 
Binafsi naamini kuwa mwanamke ana huruma sana zaidi ya mwanaume hivyo mwanamke anauwezo wa kunisaidia kwa haraka tofauti na mwanaume mwenzangu. Mwanaume atasema "mwache akomae, Si wenyewe tulihangaika bwana". Kikubwa ni hicho rafiki sifikirii kulelewa kikubwa natengeza channel ya kufahamiana na watu wengi zaidi
unahitaji kuhurumiwa!!!kuhurumiwa si ni sawa na kubebwa!!!
na kama ni kwa mema tu kwa nini u-specify umri!kama unaamini wanawake wanaweza kukusaidia zaidi kwa nini usipanue wigo!!kuna wenye kuona huruma hata chini ya 35 year!
 
We unadanganya eti unasoma. Unasoma nini kama hujitambui na kutambua kuwa huyo unayemtafuta kukufuga anaweza kuwa tatizo kuliko hayo matatizo madogo yanayotaka kukuingiza mtoni? Jitegemee badala ya kutafuta kula na kulala bure.
 
We unadanganya eti unasoma. Unasoma nini kama hujitambui na kutambua kuwa huyo unayemtafuta kukufuga anaweza kuwa tatizo kuliko hayo matatizo madogo yanayotaka kukuingiza mtoni? Jitegemee badala ya kutafuta kula na kulala bure.

soma elewa kisha andika maoni yako, usiandike maoni kwa mazoea.
 
unahitaji kuhurumiwa!!!kuhurumiwa si ni sawa na kubebwa!!!
na kama ni kwa mema tu kwa nini u-specify umri!kama unaamini wanawake wanaweza kukusaidia zaidi kwa nini usipanue wigo!!kuna wenye kuona huruma hata chini ya 35 year!

kwanaza, hakuna mtu asiyependa kuhurumiwa. Pili, nimechagua umri huo kwakuwa naamini wenye umri huo wengi wao tayar wanakuwa wameshakaa kwenye system na wanajua mambo yanavyoendeshwa japo chini ya hapo wanaweza wakawepo pia
 
Mie kwa uelewa wangu unahitaji kupanua wigo na marafiki wa wanawake wa miaka 35 na kuendelea. Lakini kuna faida na hasara. Faida ni kwamba mipango yako itaenda vyema. Lakini ukifanikiwa wewe katika maisha yako utakuja na kusema "SITAKI MWANAMKE WA MIAKA 35 NA KUENDELEA..."
Kaka FRANCIS njia moja wapo ya kupata kazi jiangalie upo katika Faculty gani? Na ongeza ku compete na watu wengne hapo chuo ili GPA iwe yakuwafanya watu wakupe kazi fasta. Mie nimepata kazi lakini jitahidi upate kazi.
 
Binafsi naamini kuwa mwanamke ana huruma sana zaidi ya mwanaume hivyo mwanamke anauwezo wa kunisaidia kwa haraka tofauti na mwanaume mwenzangu. Mwanaume atasema "mwache akomae, Si wenyewe tulihangaika bwana". Kikubwa ni hicho rafiki sifikirii kulelewa kikubwa natengeza channel ya kufahamiana na watu wengi zaidi
Siku zote mwanaume ni lazima ugangamae. Hizi tabia unazoonyesha za kutaka kuonewa onewa huruma siyo za kiume!!
Hebu acha kutuaibisha wanaume wenzako!!
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom