Mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe.

mbalisana

Member
Dec 15, 2011
46
42
"Mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake kwa mikono yake mweyewe" huu ujumbe nimekutana nao mara nyingi ila kwa siku hizi unanichanganya. Ni upumbavu upi hasa unaotajwa hapa?na je kuna wanaume wanaopelekea nyumba zao kuvunjika? hawa wapo katika kundi gani? inanitatiza nimekutana nayo mazingira mengi mfano mume kasafiri kakutana na mwanamke mwingine kazaa nae,mwaka unaofuata kasafiri tena kikazi kazaa na mwingine mwanamke akitaka kuondoka jamii inamwambia acha upumbavu usiondoke utavunja nyumba yako kisa mahawala wa nje.na hizo safari sio za miaka ikizidi sana miezi miwili. na amekuacha unalea watoto na kutunza nyumba hamuwezi kufuatana kila mahali. hii imekaaje jamani. mwanamke tu ndo wakujenga nyumba na kuvumilia yote?
 
kwa mwanamume inakuwa ''mwanamume mpumbavu huvunja nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe''
 
"Mwanamke mpumbavu huvunja nyumba yake kwa mikono yake mweyewe" huu ujumbe nimekutana nao mara nyingi ila kwa siku hizi unanichanganya. Ni upumbavu upi hasa unaotajwa hapa?na je kuna wanaume wanaopelekea nyumba zao kuvunjika? hawa wapo katika kundi gani? inanitatiza nimekutana nayo mazingira mengi mfano mume kasafiri kakutana na mwanamke mwingine kazaa nae,mwaka unaofuata kasafiri tena kikazi kazaa na mwingine mwanamke akitaka kuondoka jamii inamwambia acha upumbavu usiondoke utavunja nyumba yako kisa mahawala wa nje.na hizo safari sio za miaka ikizidi sana miezi miwili. na amekuacha unalea watoto na kutunza nyumba hamuwezi kufuatana kila mahali. hii imekaaje jamani. mwanamke tu ndo wakujenga nyumba na kuvumilia yote?

Nafikiri hii nakuu imetoka kwenye vitabu vya dini ambavyo kimsingi binafsi sipendi kuongezea neno kwenye maneno matakatifu.
Ila ninachoweza kusema nje ya hiyo nukuu ni kuwa kuna BAADHI ya wanawake ambao tabia zao husababisha waume zao kuzichoka nyumba zao. Sababu kama Ukali, ugomvi, kutokuwajibika nyumbani, kutoa siri za ndani, kukosa ukarimu, kuchukia na kununa bila sababu, kutokujishughulisha, unyanyasaji kwa ndugu na wengine, kukosa unyenyekevu, choyo, uwongo nk ni baadhi ya mambo yanayochangia wanawake kuvunja nyumba zao. Yanaweza kuitwa ya kipumbavu kwa sababu ni mambo madogo madogo ambayo kimsingi mtu anaweza kuyaacha na kujikuta ameidumisha nyumba yake.

Zipo tabia zingine ambazo ni common kwa wote, vitu kama kuwa na nyumba ndogo, uhuni nk zinaweza pia kusababisha na hizo hatuwezi kuzijadili kwa sasa.
 
Mkuu hilo ni somo refu sana...uzuri ni kwamba huo mstari hata ukisimama alone bado unaeleweka.
Kwa urahisi tu ni kwamba wanawake wasiwe WAPUMBAVU wawapo kwenye ndoa.
 
Mithali 14:1 "Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe" MSEMO HUU UNA MAANA KUBWA SANA KATIKA MAANDISHI MATAKATIFU, Kila binadamu anahusika moja kwa moja katika hili' na TAFAKARI YA INA MAANA PANA ZAIDI KULIKO TUNAVYO FIKIRI.
 
Katika ulimwengu wa roha na nafasi: Mungu amempa nafasi zifuatazo mwanamke; 1. Ni MSAIDIZI wa mume. 2. MLINZI wa mwanaume. 3. MJENZI wa nyumba yake. 4. MSHAURI wa mumewe. 5. MLETA KIBALI kwa mumewe
 
Back
Top Bottom