Ahahahaaaa....Mwanne Othman kiboko yao aisee! Hivi bado ana-host kipindi cha rusha roho C2C?
Hilo la mwanamke mmbea kuwa na midomo myeusi kaa kunguru nadhani lilikuwa dongo kwa Baby J. Si unajua kuna beef kati ya Offside Trick na AT. Sasa Offside Trick walimshirikisha Baby J kwenye wimbo wao wa Kidudu mtu. Baby J ana midomo myeusi ndiyo maana nahisi kuwa hilo dongo lilirushwa kwake.
AT alipojibu naye ndo akamshirikisha Mwanne. Huyu mdada ni noumer! Kuna mstari anakwambia "mnajua kuchumu lakini mnanuka midomo". Madongo yake hunichekesha sana.
Sasa mtu ukitaka uuelewe vizuri Vifuu Tundu sikiliza kwanza Kidudu Mtu ya Offside Trick. Ukimaliza ndo usikilize na Vifuu Tundu. Ukimaliza kusikiliza Vifuu Tundu sikiliza Dege ya hao hao Offside Trick safari hii wakimshirikisha Hammer Q. Nadhani Dege ni jibu la Vifuu Tundu. Namsubiri AT naye aijibu Dege.
Haya mambo ya mduara, chakacha, na taarab hapa ndo mwake bana. Penda sana mimi hizo genres!
Kama hii ni kweli hawa wafuatao ambao nimeshawahi kuwaona ni wambeya wa kutupwa.
MwanajamiiOne
Nyamayao
Blaki womani
Lizzy
Askofu
...mtm na nyani ngabu mmenipeleka deep, big up!!! hahaha...
Mbu na wewe wapenda haya mambo ya Kiswahili swahili? Mi nilidhani wewe una mambo ya kizungu zungu bana? Lol
mwanaume watasema anavuta sigara....
Mkuu mirindimo ya pwani ina messages usizoweza kuzipata mahala popote...
mbona wanawake wa kidhungu wambea kama nini na wana midomo myeupe?lol!
basi nilijikuta naangalia tbc1 kila asubuhi ya j1 ndo nikaanza kuskiza hizi,zina raha yake.
GMie mpenzi wa hizi nyimbo lakini Dege imetia fora too much ......kisha mbaya yenyewe mziki full kukolea, bila ya kujijua unaimba dege ...aggggrrrrr
Za zamani zilikuwa nzuri .......
kuna hii moja ya Mzee Yussuf na Dj.Chuchu (RIP)
Mzee Yusuf - Unanyodo - YouTube
Wabeba box kina NN mtajijuuuuu
Btw: Naskia Ahmada walikuwa wanampiga dongo Rais Karume wa Zanzibar!
Ahahahaaaa....Mwanne Othman kiboko yao aisee! Hivi bado ana-host kipindi cha rusha roho C2C?
Hilo la mwanamke mmbea kuwa na midomo myeusi kaa kunguru nadhani lilikuwa dongo kwa Baby J. Si unajua kuna beef kati ya Offside Trick na AT. Sasa Offside Trick walimshirikisha Baby J kwenye wimbo wao wa Kidudu mtu. Baby J ana midomo myeusi ndiyo maana nahisi kuwa hilo dongo lilirushwa kwake.
AT alipojibu naye ndo akamshirikisha Mwanne. Huyu mdada ni noumer! Kuna mstari anakwambia "mnajua kuchumu lakini mnanuka midomo". Madongo yake hunichekesha sana.
Sasa mtu ukitaka uuelewe vizuri Vifuu Tundu sikiliza kwanza Kidudu Mtu ya Offside Trick. Ukimaliza ndo usikilize na Vifuu Tundu. Ukimaliza kusikiliza Vifuu Tundu sikiliza Dege ya hao hao Offside Trick safari hii wakimshirikisha Hammer Q. Nadhani Dege ni jibu la Vifuu Tundu. Namsubiri AT naye aijibu Dege.
Haya mambo ya mduara, chakacha, na taarab hapa ndo mwake bana. Penda sana mimi hizo genres!