Mwanamke mmbeya....

...mtm na nyani ngabu mmenipeleka deep, big up!!! hahaha...





 
Last edited by a moderator:
Ahahahaaaa....Mwanne Othman kiboko yao aisee! Hivi bado ana-host kipindi cha rusha roho C2C?

Hilo la mwanamke mmbea kuwa na midomo myeusi kaa kunguru nadhani lilikuwa dongo kwa Baby J. Si unajua kuna beef kati ya Offside Trick na AT. Sasa Offside Trick walimshirikisha Baby J kwenye wimbo wao wa Kidudu mtu. Baby J ana midomo myeusi ndiyo maana nahisi kuwa hilo dongo lilirushwa kwake.

AT alipojibu naye ndo akamshirikisha Mwanne. Huyu mdada ni noumer! Kuna mstari anakwambia "mnajua kuchumu lakini mnanuka midomo". Madongo yake hunichekesha sana.

Sasa mtu ukitaka uuelewe vizuri Vifuu Tundu sikiliza kwanza Kidudu Mtu ya Offside Trick. Ukimaliza ndo usikilize na Vifuu Tundu. Ukimaliza kusikiliza Vifuu Tundu sikiliza Dege ya hao hao Offside Trick safari hii wakimshirikisha Hammer Q. Nadhani Dege ni jibu la Vifuu Tundu. Namsubiri AT naye aijibu Dege.

Haya mambo ya mduara, chakacha, na taarab hapa ndo mwake bana. Penda sana mimi hizo genres!

Monkey Ngabu, Umetisha Mkuu Kwa Kumbusha tu ni kwamba AT alikuwa mshirika mkubwa wa Offside Trick na aliwang'arisha sana ktk nyimbo za Samaki na Mduara Kutoka Zanzibar( Intro ya Offside Trick) ndipo bifu lilipoanzia baada yakutoelewana.
 
Kama hii ni kweli hawa wafuatao ambao nimeshawahi kuwaona ni wambeya wa kutupwa.

MwanajamiiOne
Nyamayao
Blaki womani
Lizzy
Askofu
 
...mtm na nyani ngabu mmenipeleka deep, big up!!! hahaha...








Mbu na wewe wapenda haya mambo ya Kiswahili swahili? Mi nilidhani wewe una mambo ya kizungu zungu bana? Lol
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mbu na wewe wapenda haya mambo ya Kiswahili swahili? Mi nilidhani wewe una mambo ya kizungu zungu bana? Lol

...aaah, mja haachi asili yakhe pwani ndio kwetu hata kama sio 100% lakini kuzaliwa na kukulia mzizima-- 'bandari ya salama' pekee ni cheti cha mzaliwa wa mwambao, nitaachaje uswahili swahili bana?...msikize binti koba mstari kwa mstari ati "...kwanini hawalali...!"---samaki anarudi reverse!!!
 
Last edited by a moderator:
Mambo ya pwani we acha tu mtu mzima anaimbiwa "kindumbwe-dumbwe"

Halo-halooooo

Hivi wangapi wamewahi kucheza "akosae mfinye ukucha" utotoni?
 
mbona wanawake wa kidhungu wambea kama nini na wana midomo myeupe?lol!
basi nilijikuta naangalia tbc1 kila asubuhi ya j1 ndo nikaanza kuskiza hizi,zina raha yake.
mwanaume watasema anavuta sigara....

Mkuu mirindimo ya pwani ina messages usizoweza kuzipata mahala popote...
 
mbona wanawake wa kidhungu wambea kama nini na wana midomo myeupe?lol!
basi nilijikuta naangalia tbc1 kila asubuhi ya j1 ndo nikaanza kuskiza hizi,zina raha yake.

Kumbe nawe wazipenda hizi eeh? Swaaafi sana. Napenda sana mimi watu wazipendao.
 
Mie mpenzi wa hizi nyimbo lakini Dege imetia fora too much ......kisha mbaya yenyewe mziki full kukolea, bila ya kujijua unaimba dege ...aggggrrrrr
 
Za zamani zilikuwa nzuri .......

kuna hii moja ya Mzee Yussuf na Dj.Chuchu (RIP)

Mzee Yusuf - Unanyodo - YouTube

Wabeba box kina NN mtajijuuuuu :p

Btw: Naskia Ahmada walikuwa wanampiga dongo Rais Karume wa Zanzibar!

Hebu pata hiki kitu cha mduara toka kwa Mfalme Mzee Yusuf akimshirikisha Baby J! Ushawahi kukisikia hiki wewe? Chezeya Mzee Yusuf utatungiwa wimbo hiv hivi....jamaa ana maneno balaa!!

Na hili kaseme-Mfalme - YouTube
 
ah aha Mange wa uturn amewachamba huko wabongo wa majuu wanapenda majungu na kusikiliza taarab, lol! ila mambo ya pwani yana raha yake, am a big fun too!
 
Ahahahaaaa....Mwanne Othman kiboko yao aisee! Hivi bado ana-host kipindi cha rusha roho C2C?

Hilo la mwanamke mmbea kuwa na midomo myeusi kaa kunguru nadhani lilikuwa dongo kwa Baby J. Si unajua kuna beef kati ya Offside Trick na AT. Sasa Offside Trick walimshirikisha Baby J kwenye wimbo wao wa Kidudu mtu. Baby J ana midomo myeusi ndiyo maana nahisi kuwa hilo dongo lilirushwa kwake.

AT alipojibu naye ndo akamshirikisha Mwanne. Huyu mdada ni noumer! Kuna mstari anakwambia "mnajua kuchumu lakini mnanuka midomo". Madongo yake hunichekesha sana.

Sasa mtu ukitaka uuelewe vizuri Vifuu Tundu sikiliza kwanza Kidudu Mtu ya Offside Trick. Ukimaliza ndo usikilize na Vifuu Tundu. Ukimaliza kusikiliza Vifuu Tundu sikiliza Dege ya hao hao Offside Trick safari hii wakimshirikisha Hammer Q. Nadhani Dege ni jibu la Vifuu Tundu. Namsubiri AT naye aijibu Dege.

Haya mambo ya mduara, chakacha, na taarab hapa ndo mwake bana. Penda sana mimi hizo genres!

Ngosha, kumbe unapenda hivi taarabu
 
Back
Top Bottom