Mwanamke matunzo babu Eeh!

mwengeso

JF-Expert Member
Nov 27, 2014
9,219
6,650
Nimesoma makala yenye kichwa cha habari hapo juu katika gazeti la 'Nipashe Jumapili Julai 17, 2016' iliyoandikwa na Mwanahabari 'Mary Geofrey'.

Mwandishi naamini amewakilisha mtazamo, hisia na matarajio ya wanawake wengi. Kama ni hivyo basi, katika mwono, mawazo na maswali mengi, je, hili halipingani na hitaji la wanawake la usawa kwa kila jambo isipokuwa maumbile!

Baadhi ya hoja zake kuhusu matunzo nanukuu:
1) Kuna baadhi ya wanaume ni wabahili sana, yaani kutoa fedha kwa wapenzi wao wanaona shida, wengine wanatoa lakini shingo upande.
2) Baadhi wanatoa visingizio kwamba kumpa pesa mwanamke kwa ajili ya kujikimu na kununulia mavazi ni sawa na kupoteza.
3) Siyo lazima mwanamke akuambie naomba kitu fulani, ni jukumu lako kufahamu aina ya vitu anavyopenda na unapaswa kumnunulia nk.

Anahitimisha na "kama hautoi matunzo kwa mpenzi wako basi jua umemuruhusu atoke nje ili apate kile anachotaka". Hili linakumbusha sakata lilijitokeza, katika kikao cha bunge kilichokwisha, pale Mbunge mmoja alipowaambia wabunge wanawake ni baadhi ya "babies" za watu kupata ubunge.

Mh wanajammvi, hilo nalo WAZO!
 
Kama haki sawa kwa wote hamna haja kumtunza mwanamke bali tutatunzana.
Nikiwa na buku tugawane na yeye akiwa na buku tugawane.

Kila mwisho wa mwezi tujue kila mmoja ameingiza sh ngapi.
 
Wanawake wamepoteza mwelekeo sikuiz hawafahaam tena wanachopigania kama ni usawa au matunzo. Ila wengi wamesalimu amri wameona bora kupigania matunzo tu manake kwenye usawa game ya ajira iko tyt
 
Kama haki sawa kwa wote hamna haja kumtunza mwanamke bali tutatunzana.
Nikiwa na buku tugawane na yeye akiwa na buku tugawane.

Kila mwisho wa mwezi tujue kila mmoja amein
giza sh ngapi.
Dah.... Hakuna kitu Kama hicho HAKI SAWA kwenye dunia ya UHALISIA. Wanawake hawapambani na wanaume ila wanapambana na ASILI ya mwanadamu na watashindwa tu :)
 
Siku hizi wanapenda sana na wao wawe wanakuwa juu ili ionekane na yeye anakudinya, tena unakuta anasukuma utafikri wewe mwanaume ndiyo unakunwa wakati yeye ndiyo anakunwa
 
Dah.... Hakuna kitu Kama hicho HAKI SAWA kwenye dunia ya UHALISIA. Wanawake hawapambani na wanaume ila wanapambana na ASILI ya mwanadamu na watashindwa tu :)
hakuna kitu kama hicho, kushindwa ni mwiko, hapa ni kubadili fikra tu! mwanamke akisha gundua ndani ya fikra yake kwamba yeye ni tegemezi na aichukie hiyo hali ndani ya moyo wake; nakwambia sky is not a limit! society imemfanya awe dependent na sio nature yake... time will tell, remain blessed my friend!
 
Hata ukimtunza kama ni wa kugegedwa atagegedwa tu hata kwa jelo
 
hakuna kitu kama hicho, kushindwa ni mwiko, hapa ni kubadili fikra tu! mwanamke akisha gundua ndani ya fikra yake kwamba yeye ni tegemezi na aichukie hiyo hali ndani ya moyo wake; nakwambia sky is not a limit! society imemfanya awe dependent na sio nature yake... time will tell, remain blessed my friend!
Dah... Madhara yake mabaya ni makubwa kuliko yale mazuri katika jamii. Mwanamke ni wa kuhudumiwa hili halihitaji hata akili nyingi. Fanya utafiti kidogo tu kwa vinara wa haki sawa ... Wanafanya hivyo kwenye familia zao? Au wanaishia kupiga kelele majukwaani ili wapate Pesa ya saluni? Wanaotekeleza kwa dhati je wamefanikiwa kiasi gani katika sehemu nyanja kuu 4 za maisha yao binafsi??
 
Dah... Madhara yake mabaya ni makubwa kuliko yale mazuri katika jamii. Mwanamke ni wa kuhudumiwa hili halihitaji hata akili nyingi. Fanya utafiti kidogo tu kwa vinara wa haki sawa ... Wanafanya hivyo kwenye familia zao? Au wanaishia kupiga kelele majukwaani ili wapate Pesa ya saluni? Wanaotekeleza kwa dhati je wamefanikiwa kiasi gani katika sehemu nyanja kuu 4 za maisha yao binafsi??
wala tusihangaike kubishana...angalia nchi zilizoendele kwani kuna uzembe kama huu kwa wanawake? sasa hilo ni wimbi la fikra kuamka... na upende usipende litafika nchini kwetu pia. mpaka sasa wasichana wenye uwezo wao wameamua kupata watoto wao wenyewe au kuolewa na wanaume ambao kipato chao sio cha juu sana au sawa, na wengi wao hawachukui hata senti kwa wapenzi wao! HIYO NDIYO DUNIA YA SASA!
 
Safi kabisa!
Ipi safi! Ni halali na haki kabisa mwanamke atunzwe na mwanaume (kama mwanahabari anavyotaka jamii ifanye)na wakati uleule adai usawa.

Lakini yawezekana ikawa sawa kwa kuwa mwanamke ndiye, kimaumbile, amepewa majukumu mengi.

NANI KAMA MAMA!
 
Dah hilo pepo la kuombwa pesa lilinidondokea leo, ila kwakuwa nilishamgegeda nilijibu dry tu na ametulia tuli.
 
Ipi safi! Ni halali na haki kabisa mwanamke atunzwe na mwanaume (kama mwanahabari anavyotaka jamii ifanye)na wakati uleule adai usawa.

Lakini yawezekana ikawa sawa kwa kuwa mwanamke ndiye, kimaumbile, amepewa majukumu mengi.

NANI KAMA MAMA!


Rejea maandiko! Tafakari neno la Mungu
 
wala tusihangaike kubishana...angalia nchi zilizoendele kwani kuna uzembe kama huu kwa wanawake? sasa hilo ni wimbi la fikra kuamka... na upende usipende litafika nchini kwetu pia. mpaka sasa wasichana wenye uwezo wao wameamua kupata watoto wao wenyewe au kuolewa na wanaume ambao kipato chao sio cha juu sana au sawa, na wengi wao hawachukui hata senti kwa wapenzi wao! HIYO NDIYO DUNIA YA SASA!
Dah... Ndiyo mnavyopotea..DUNIA YA SASA... single mothers wa kumwaga, watoto kwenye akili nzito ( kapukuz), ndoa za jinsia moja.... Mbona hampiganii sheria ya kujamiana ikawa sawa kwa sawa???...sheria za ndoa nayo,...Hivi hamuwezi mkajiongeza kidogo mkachukua mazuri ya DUNIA YA SASA kisha mkayatupa mbali Yale ya AMRI ILE.... Labda Kama nawe ni mmoja wao, lakini bado nakwambia hii vita mwanaume haimuhusu kabisa ni vita Kati ya mwanamke dhidi ya asili ya dunia... Na kamwe mwanamke hawezi kushinda zaidi ya kupata majeruhi wengi ambao ni mparaganyiko wa mfumo wa kibinadamu na mazingira yake
 
Dah... Ndiyo mnavyopotea..DUNIA YA SASA... single mothers wa kumwaga, watoto kwenye akili nzito ( kapukuz), ndoa za jinsia moja.... Mbona hampiganii sheria ya kujamiana ikawa sawa kwa sawa???...sheria za ndoa nayo,...Hivi hamuwezi mkajiongeza kidogo mkachukua mazuri ya DUNIA YA SASA kisha mkayatupa mbali Yale ya AMRI ILE.... Labda Kama nawe ni mmoja wao, lakini bado nakwambia hii vita mwanaume haimuhusu kabisa ni vita Kati ya mwanamke dhidi ya asili ya dunia... Na kamwe mwanamke hawezi kushinda zaidi ya kupata majeruhi wengi ambao ni mparaganyiko wa mfumo wa kibinadamu na mazingira yake
Mimi na laani ndoa ya jinsia moja na pia na laani uonevu. ... kijijini kwetu wanawake wajane wako wengi sana na hata mijini pia, bado fumbuzi hujalijua ni kwa sababu ya uonevu? Mwanamke na mwanamume ni viumbe sawa. ...lakini wanawake tuna roho ya MOLA, ya huruma, hapo sasa ndipo mlipotuzidi akili na kuja na kila aina ya mila zinazo mpendelea mwanamume. ...sasa tumeshtuka, kumbe ni upuuzi mtupu. ..kama sisi wanawake tunaweza kuleta kiumbe duniani kwa nini tugeuke omba omba? Kumbuka The weaker are oppressing the stronger, na giant ameamka! barikiwa my friend
 
ISIS anasema "the weaker are oppressing the stronger, na giant ameamka!". Du, ni hitimisho linalozua maswali kuhusu mahusiano kijinsia!

'Weaker' dhidi ya 'stronger', shindano la nini na mwamuzi ni nani!

"Giant" aliyeamka ni yupi! Ni yule anayeomba matunzo!
 
Back
Top Bottom