Mwanamke kuchukua vitu vya ndani kupeleka kwao.

What an idiot? Umekimbilia JF kupata ushauri. Mbona husemi kama ulimuuliza mkeo anachofanya na kutuambia hadithi aliyokueleza unaleta habari nusu nusu. Ndio umbeya wenyewe huo, kama unampenda mkeo ungeleta hilo jambo hapa kwenye mkeka? Tena unasema anamtuma dreva yaani wewe ni tajiri sana asubuhi subuhi tu una dreva wa kukufanyia maswala yako binafsi? Watanzania hawawezi kuendelea kutokana na kasumba ya kujifanya wana pesa wakati ni masikini wa kutupwa, ati una gari na kuajiri dreva then unalalamika na pesa za peremende stupid kabisa. Grow up!

huwez kumshauri mtu bila matusi?(IDIOT,STUPID) au unafikiri mm sijui matusi ya kiingereza ?
Dereva sijamajiri mm ameajiriwa na shirika mm ananiendesha tu na nilifanya vile kwakuwa natambua yule ni mzazi wangu pia.halafu hapa mm si lalamikii pesa na lalamikia tabia ya mke wangu siku nyingine usome kwa makini kama hujaelewa acha usichangie had unatukana ningekurudishia matusi pia lakin basi haina maan
 
asante kwa ushauri wako nakaa sasa chini nitafakari nn cha kumsaidia,katika namna nyingine nlimpa mtaji miezi sita sasa lakin kila nikimuuliza ansema alikopesha walokopa hawajamlipa hadi sasa
Amefikia wapi kielimu?
Some people just need a little push. Ulivyompa mtaji, jaribu kumshauri na kumfwatilia maendeleo yake. Ndio nikazi ya ziada sio utani. But its for ur own good.
Lakini cha msingi ongea nae. I believe in every marriage communication nikila kitu. Jaribu kumuelewa as a person and her reasons for doing what she does. Then from there ndo utajua jinsi ya kumsaidia.
She is ur wife. Ur better half. Not just a person u live with. I hope umenielewa. Kwa sasa jf cant help u. Talk to her kwanza. Ukishamuelewa then njoo omba ushauri how to help her.
 
........Sasa kama wazazi wake hawana mlo, na yeye ana uwezo wa kuwalisha kuna tatizo gani?

Acha kulalamika, je mkeo yeye hana kipato?

hata kama alipaswa kumwambia mmewe mtu anavyonunua mahitaji ya nymban ananunua kwa malengo na budget sasa inapokata kabla ya muda aliokusudia kwa kweli unakuwa unampa wakati mgumu.
 
huwez kumshauri mtu bila matusi?(IDIOT,STUPID) au unafikiri mm sijui matusi ya kiingereza ?
Dereva sijamajiri mm ameajiriwa na shirika mm ananiendesha tu na nilifanya vile kwakuwa natambua yule ni mzazi wangu pia.halafu hapa mm si lalamikii pesa na lalamikia tabia ya mke wangu siku nyingine usome kwa makini kama hujaelewa acha usichangie had unatukana ningekurudishia matusi pia lakin basi haina maan

Weka full story basi sio kutupa viporo kama unataka ushauri.
 
pole mkuu ndio tabu za ndoa hhzio vumilia ukisema umwache utakuta wengine wanashida kuliko hizo.!! cha msingi ongea nae
 
naamini huyu mwanamke ana akili kuliko wewe,

mpaka amefikia hatua ya kuikumbuka kwao, that means wewe umeshajisahau sana!

kaka, familia za kiafrika in most cases ni extended family,

kumbuka wazazi wa pande zote mbili.. upande wa baba yako na kwa mkeo pia!

ukifanya hivi, mkeo hatofanya anayofanya tena.
 
Ndugu ndoa yako ina tatizo tena tatizo kubwa

Kwanza mna tatizo la mawasiliano

Pili inawezekana wewe humhudumii mkeo ipasavyo, umesema mkeo hana kazi, unajua kutokuwa na kazi hakuna maana kuwa asisaidie kwao? Unategemea atasaidia vipi?

Au wewe neno lako ni sheria hauna majadiliano hujali hisia za wenzio

Pia inawezekana mkeo ana tatizo kama umesema umemwanzishia biashara huoni faida inawezekana ni mvivu au hana kipawa cha biashara au biashara haikulipa(still mna tatizo la mawasiliano / au mnasimangana ndo maana mmeshindwa kuzungumza)

Au mke ndo zile design za mwanamke ambaye kila fashion anaitaka? Anajua kutumia tu na si kutafuta?

Maswala ya kipato ndo yanayoongoza kuvunja ndoa, ila jua ndoa yako ina tatizo kubwa ambalo wote wawili mnahitaji kulisolve



nashukuru kwa ushauri mke wangu hana kazi ya mshahara,nilimpa mtaji wa kutosha kabisa ni miezi sita sasa sioni pesa ya mtaji wala faida zaidi ya madeni ya nguo ambazo kimsingi si lazima kwa sababu zilizopo zinatosha,kama haitoshi kuna wakti ametoa pesa kwenye account yangu ya Mpesa nimemuuliza anakataa wakti mm nimpata ushahidi wote toka voda
 
........Sasa kama wazazi wake hawana mlo, na yeye ana uwezo wa kuwalisha kuna tatizo gani?

Acha kulalamika, je mkeo yeye hana kipato?

Yani mijamaa mingine nuuuunda kwelikweli sasa wakweze kusaidiwa vitu vidogo kama misosi ni mpaka mkae kamati kuu kwani ulipooa hukujua unaoa toka familia gani? wakwezo kupita mtaani pekupeku wakati wewe unapita na mwanae kwenye vx unaona fresh? wazazi ni sawa na watoto wenu bhana mwanao akilala na njaa wewe utapata usingizi?
 
Wapendaw salaam na heri kwa sikukuu.
Naomba ushauri wa nini cha kufanya hapa niko kwenye ndoa mwaka mmoja sasa,hivi karibuni nimegundua kuwa mke wangu anachukua vitu vya ndani madhalani vyakula na kuvipeleka kwa wazazi wake kisiri bila hata kunambia, nimeona mwenyewe asubuhi akimtuma dereva yebo . Alijua mm bado nimelala kumbe niko chumba kingine ambacho dirisha halikufungwa na kila kinachofanyika nje kinaonekana.nimekuwa na tatizo la vitu kuisha ndani kabla muda wake kwa mfanoo na nunua consumables kwa ajili ya mwezi mzima matokeo yake kabla ya mwezi utaambiwa vimeisha.
Nampenda mke wangu ila kwaa hili amenikwaza kwan ndo kwanza tumeanza maisha sasa kama kila hela itaishia kwenye vyakula tutafanya cha maana kweli?
Yani mijamaa mingine nuuuunda kwelikweli sasa wakwezo kusaidiwa vitu vidogo kama misosi ni mpaka mkae kamati kuu kwani ulipooa hukujua unaoa toka familia gani? wakwezo kupita mtaani pekupeku wakati wewe unapita na mwanae kwenye vx unaona fresh? wazazi ni sawa na watoto wenu bhana mwanao akilala na njaa wewe utapata usingizi?
 
ndugu tatizo ni kwa nini afanye kwa kujificha. Hana kipato I have to take care of her A to Z,
.......Dahh!! Unafikiria nini future ya mkeo? Kama hana kipato inabidi ufanye kitu.Kama mtaji umegoma,biashara hawezi, je shule itamfaa?
Hebu jaribu kukaa na kuzungumza hili jambo.
Kwa upendo mwambie mkeo anapotaka kusaidia kwao, awe na uhuru
asifanye kwa siri. Kwa sababu wewe unapenda jinsi anavyosaidia family yake.
 
Wapendaw salaam na heri kwa sikukuu.
Naomba ushauri wa nini cha kufanya hapa niko kwenye ndoa mwaka mmoja sasa,hivi karibuni nimegundua kuwa mke wangu anachukua vitu vya ndani madhalani vyakula na kuvipeleka kwa wazazi wake kisiri bila hata kunambia, nimeona mwenyewe asubuhi akimtuma dereva yebo . Alijua mm bado nimelala kumbe niko chumba kingine ambacho dirisha halikufungwa na kila kinachofanyika nje kinaonekana.nimekuwa na tatizo la vitu kuisha ndani kabla muda wake kwa mfanoo na nunua consumables kwa ajili ya mwezi mzima matokeo yake kabla ya mwezi utaambiwa vimeisha.
Nampenda mke wangu ila kwaa hili amenikwaza kwan ndo kwanza tumeanza maisha sasa kama kila hela itaishia kwenye vyakula tutafanya cha maana kweli?


Simpo punguza bajeti ya nyumbani! mpango wa kununua jumla kwishney! Kila tatizo lina solution yake, solution ya hilo si kumuacha possibly mwenzio hajazoea kuwa na vitu vingi! so anaona haina shida!

Punguza bajeti then muweke wazi, kuwa vitu vinatumika bila mpango so unapunguza bajeti! ila muweke wazi pia kama ana shida akueleze 9Just any shida)
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom